Rais Samia Suluhu anakwenda kuzoa kura zote uchaguzi ujao


Anawaheshimu wapi?. Kama angekuwa anawaheshimu angefuta katazo la siasa.
 
Nishaona kuna magenge yameshaandaliwa kuongea PUMBA na yametapakaa sana mitandaoni. Topic zao zinajulikana sana, ukiona heading tu lazima unaweza kubashiri mleta mada ni flani. Hivi lini mtaleta uzi wenye kujadili changamoto za nchi kuliko haya mapambio ya kila siku? Nchi inavuliwa nguo na vijana watafuta teuzi, si ajabu wengi ni uvccm. Unaweza kusema ukienda huko akili zinabaki kwenye kabati linatembea dude wazi kichwani. Unaweza kukuta mnatoka semina ya sensa na kuona maisha mmeyamaliza 2025 wanastahili kura 100%
 
Embu leta hizo unazosema changamoto ili ujibiwe na kupewa majibu
 
Mh mama Samia suluhu Hassani 2025 usidanganyike kuchukua fomu utaaibika.

CCM viongozi wanakundanganya , CCM wanachama wanakusema vibaya mno.

Sabuni ya Kufulia nguo kipande ni Tsh 1,200 /=
Kama huwezi ku afford kununua sabuni kipande Tsh 1,200 then wewe ni mvivu. Fanya kazi acha mjungu na utoto
 
Kama huwezi ku afford kununua sabuni kipande Tsh 1,200 then wewe ni mvivu. Fanya kazi acha mjungu na utoto

Mwenzako anaongelea mfumuko wa Bei wewe unaleta dharau. Usifikirie kila mtu anaishi Maisha unayoishi wewe. Tuwafikirie na wengine.
 
Ndugu yangu,wewe kama ni mwanachama na unadhanikia kwakuwa huko upande huo, nami nikili wazi tuko pamoja upande huo lakini sikubaliani na hoja zako dhaifu, yaani maisha yalivyopanda, kila uchwao watanzania wanabebeshwa misalaba ya ugumu wa maisha,katika tozo za muamala ya simu, leo tozo kwenye mabenki, gharama za usafiri juu, vyakula juu,mafuta ya kula juu, kila sehu juu, unakuja kushabikia na kupongeza serikali kwa stahi hiyo, basi wa utakuwa mlamba asali pia.
Narudia niko upande huo unaoshabikia,naheshimu mawazo yako lakini binafsi serikali imewafanya watanzania kuishi kwa kubahatisha huku fedha za umma zikitafunwa hovyo na huduma za huduma zikishuka mwelekeo wako ktk utendaji wake.
Note: 2025 namuona mheshimiwa kutogombea nafasi hiyo ya juu tena na sina imani iliyotumilika kama chama kitampitisha nafasi hiyo ya juu nchini kwakuwa amerithi kikatiba hadi kufika hapo alipo. Muda utaongea vinginevyo upinzani ukishindwa hapo,basi wafanye kazi nyingine.
 
Hata wapinzani wapewe nafasi yakuwa na wajumbe kutoka kamati kui yao kuwa katika tume ya uchaguzi bado hawawezi kumtikisa mh Rais, maana wanaopiga kura Ni wananchi na wananchi ndio hao ambao kwa Sasa wanamuunga mkono mh Rais
Talk for yourself....... Ni wananchi gani hao unaowasemea. Wapinzani pia ni wananchi. Kama una mahaba na Maza baki na mahaba yako.
 
Watanzania wengi Sana wameguswa na utendaji kazi wa mh Rais, embu niambie hapo ulipo Kama mh Rais hajakufikia, au hujaona shule , zahanati,vituo vya Afya, zikijengwa hapo mtaani kwako, vipi wewe siyo mkulima, Kama Ni mkulima hujasikia habari za mbolea za Ruzuku
Talk for yourself....... Ni wananchi gani hao unaowasemea. Wapinzani pia ni wananchi. Kama una mahaba na Maza baki na mahaba yako.
 
Nyie recruits wa Shaka .... mnatuharibia jukwaa letu kwa vipropaganda vyenu uchwara.
 
Wivu utakuua Mzee..😬😬

.Wewe unadhani kwa nini asizoe kura zote Kwa mambo makubwa anayofanya?

Atazoa Lisu au Mbowe au? Ni hivi hata Mbowe awe Chibukati,Benson Kigaila awe IGP na mgombea awe Lisu ,Rais Samia atashinda saa tatu asubuhi..

Kazi inaendelea kila Kona ya Tanzania πŸ‘‡
 

Attachments

  • Screenshot_20220818-073531.png
    170.4 KB · Views: 4
  • Screenshot_20220818-091905.png
    157.7 KB · Views: 4
  • Screenshot_20220818-091739.png
    116.8 KB · Views: 4
  • Screenshot_20220817-214809.png
    113.1 KB · Views: 5
  • Screenshot_20220817-171225.png
    240.6 KB · Views: 4
Sidhani kama kuna mtanzania yupo tayari kuleta vurugu kwenye nchi yake kwa ajili ya kupigania maslahi ya wanasiasa labda wenyewe ndio wajitetee wenyewe. Mwanasiasa huwa hataki kutawaliwa anataka yeye ndio atawale ndio maana leo watasema kiongozi huyu mbaya akija mwingine naye mbaya ukimuuliza yupi ndio mzuri atasema yeye chama chake na wapambe wake
 
Watanzania wote tunaonekana hovyo kwasababu ya wapumbavu wachache
 
Labda atapata kura yako tu. Rais gani wa tz badala kutoa hela kwa matajiri kuendesha na kuendeleza nchi anatoza mitozo kwa watu wa chini huku taifa halielezwi kama zile kodi za madini zimeenda wapi. Kawasamehe barrick ile hela waliyoepa kodi ya makinikia utadhani ni wajomba zake.
Tumezoea mjamaa kuongoza nchi sio kuachia sekta binafsi kudhibiti serikali.
 
Kiongozi wa watu vs MapakaπŸ‘‡πŸ˜πŸ˜πŸ˜
Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…