Rais Samia Suluhu: Kusanyeni kodi kwa kutumia akili, sio nguvu

Rais Samia Suluhu: Kusanyeni kodi kwa kutumia akili, sio nguvu

Mheshimiwa Rais anaposema TRA watumie akili ni kwamba wapaswa kubuni njia rafiki za kukusanya kodi ikiwemo njia ya kumruhusu mfanyabiashara alipe kwa awamu endapo atagundulika alikwepa kulipa kodi.

Sheria ya uhujumu uchumi ni kweli yahitaji mabadiliko lakini sheria hii ni dawa ya wahujumu uchumi.

Mtu hawezi kuingiza nchini bidhaa zilokwisha muda wake kisha atake kuuza na kupata faida kubwa.

Kama mteja amegundulika alikuwa akiepa kulipa kodi TRA wapaswa kuandaa utaratibu wa kulipa kwa awamu au "Instalments" mpaka amalize.

Hii ya TRA kuingia kuchungulia akaunti ipo katika nchi nyingi tu na imeruhusiwa kisheria ila pale wanapogundua una fedha za kutosha kwenye akaunti hawachukui bali wanakujulisha halafu mnaandaa utaratibu wa kulipa kwa awamu.

Suala la raisi kusema wizara ya fedha na TRA watumie akili katika kuhakikisha wanakusanya kodi ni pamoja na kuhakikisha kila raia ambae apaswa kulipa kodi yumo kwenye mfumo na analipa kodi.

Pia ukusanyaji kodi kwenye halmashauri zote nchini wapaswa kuwa ni wa kuhakikisha kodi ya maendeleo yalipwa na kila mlipakodi na hakuna wizi unaofanywa ama kupitia mashine za OPS au maofisa wa halmashauri ambao hukusanya kodi na kukimbia na fedha.

Hivyo kila mlipa kodi ni lazima atumie njia rasmi ya muamala kulipa kodi nikimaanisha kwamba lazima TRA iendeshwe kisasa kwa kuwa na mifumo ya kielektroniki yaani automated system ambapo hata wawekezaji wa nje wataridhika na njia hizo rahisi na rafiki za ulipaji kodi.

Mwisho, Wizara ya fedha na TRA wawekeze zaidi kwenye mifumo ya kisasa ya kieletroniki ambapo mashine kama za EFD ni kwa ajili ya utoaji stakabadhi na kuwekeza katika mfumo wa EDS yaani Electronic Data System ambapo shughuli hizi zinakuwa "outsourced" kwa makandarasi wa nje.

Shughuli hizi zikiwa outsourced inakuwa rahisi kwa vijana kupata ajira kupitia makampuni hayo ambayo mengi ni ya nje na pia huweza kuleta teknolojia mpya khasa kampuni kama MphasIS ya Bangarole India ni mojawapo.

Hivyo basi, utozaji kodi aina zote ni lazima uwe ni rafiki ambapo kila mlipa kodi atawajibika bilashuruti na pia elimu zaidi kupitia vipeperushi na matangazo redioni na njia zingine vitasaidia kupanua mfuko wa trillioni 2 na zaidi.
 
Mama amenikosha sana.

Kumbe walikuwa wanatumia mabavu hadi kukwapua hela za watu kwenye account zao za benki.

Kama analoongea ndo alilokusudia kulisimamia basi sekta hii ya biashara na uwekezaji itaanza kustawi tena.
Changamoto sio kuongea kazi ni kutenda sasa unamkuta mzee wa watu anakwambia yupo TRA mwaka wa 50 huu na anakusanya kodi kwa staili ya mabavu utamfanya nini?? Ameshatengeneza network za polisi na kila kitu utampeleka wapi??
 
Mpango itabidi abadilike....naona hajamuelewa mama. Anataka kuendelea na utaratibu wa kukusanya kodi bila weledi ambao umeua biashara.

Bahati nzuri mama ni very intelligent,ameliweka vizuri suala hili mapema.

Yani Mh VP nahisi bado yuko awamu ya tano. Hivi hajamsoma tu Mama muelekeo wake anaoutaka? Jamani tumeshatoka kwenye mabavu. Asome alama za nyakati. Hivi kulazimisha zipatikane trilioni 2, si ndio yale yale yaliyotufikisha hapa? Huyu si tunaambiwa ni mchumi mzuri? Naogopa Mama atakuja kuwa disappointed nae. Namuona bado yuko awamu ya tano ya kutaka masifa yasiyonamsingi. Mama inabidi ajitahidi sana kuwaelewesha watu wake kila mara —serikali yake anataka iweje. Wengine hawawezi kusoma alama za nyakati.
 
Mama amenikosha sana.

Kumbe walikuwa wanatumia mabavu hadi kukwapua hela za watu kwenye account zao za benki.

Kama analoongea ndo alilokusudia kulisimamia basi sekta hii ya biashara na uwekezaji itaanza kustawi tena.
Kweli kabisa mkuu
 
Sisi wananchi wenyewe kulipa kodi bila kusukumwa ni mtihani!! Ukisema leo waje kwa kulemba kwenye kodi aaah hawapati ata bilion 1 kwa mwezi. Wakwepa kodi wengi wanajua kama wanakwepa kodi na wanafanya hivo ili faida ipige maradufu.
Ndio maana amesema wakusanye kodi kwa Akili.
 
Kuna nchi watu hawakwepi kodi mbona, walau watu walio wengi isipokuwa wachache sana walioshindikana. watu wanaona fahari kulipa kodi.

Kitengo cha elimu kwa mlipa kodi hapo TRA mnakunywa chai tu badala msambae mitaani kutoa hii elimu adimu ya kizalendo, kodi zikiwa rafiki na haki watu watalipa bila msukumo, ni suala la muda mrefu kujenga nchi na kuwaelimisha walipa kodi sambamba na sheria kali za kodi, ukikwepa kodi sahihi uliyopangiwa yakupate tu yakukupata.

Rushwa kwa maafisa pia ni jipu, mtu kakwepa kodi 3M, afisa anamwambia nipe 1M tumalizane, hili jambo lina mzizi mrefu sana. Maafisa wa TRA wana mishahara ya kawaida kabisa, huo ukwasi wa ghafla ghalfa wachunguzwe wanakoutoa, Nchi hii tuwe waadilifu jamani.
Mfanyabiashara Ukikwepa kulipa kodi ya kubambikwa sawasawa tu! Maana wamezidi.
 
Mama Samia ameonya tabia ya Watendaji wa Serikali kutumia nguvu kukusanya kodi, kufungia biashara zao, kunyang'anya fedha kwenye akaunti kisa Sheria inawaruhusu[emoji1752][emoji1752][emoji1752][emoji1752] Mungu akubariki Bi mkubwa
TRA inakiuka sheria kwa kubambika na rushwa na baadhi ya wafanyabiashara wanakwepa kodi je nani mbaya zaidi?
 
Naunga mkono hoja lakini kwa tanzania hii walipa kodi kwa hiari ni wafanyakazi wa Umma pekee! Walio baki ni lazima nguvu na akili zitumike lasivyo hakuna kodi wanatoa!

Swala la kufunga biashara limeshasemwa sana na kila mtu na kila Rais!
Pia TRA wanabebeshwa lawama za bure bali wao wanafata sheria zilizo wekwa na ndizo zinawapa nguvu!


CCM mbele mbele
Wabongo wapo radhi wafunge duka siku nzima ma afisa mapato wakiwa on duty, ila sio walipe kodi ni asili tu ya watanzania hata kodi ikiwa buku!
 
Kwenye kupanua wigo wa walipa kodi, napendekeza mshahara wa Rais utozwe PAYE ali awe mfano ingawa anaweza kuongezwa marupurupu mengine. Ni suala tu la ku demonstrate kuwa Yuko mstari wa mbele wa kulipa kodi
 
Mama amenikosha sana.

Kumbe walikuwa wanatumia mabavu hadi kukwapua hela za watu kwenye account zao za benki.

Kama analoongea ndo alilokusudia kulisimamia basi sekta hii ya biashara na uwekezaji itaanza kustawi tena.
Yaani kapiga mulemule, inavyoelekea atakuwa na speed ya 5g sikutegemea kama yuko strong namna hii, aacha tumpe muda.
 
Wabongo wapo radhi wafunge duka siku nzima ma afisa mapato wakiwa on duty, ila sio walipe kodi ni asili tu ya watanzania hata kodi ikiwa buku!
Hhahahah.. Mkuu yani wabongo noma, huwaga wana peana signal wakisikia jamaa wapo karibu ndani ya dakika 2 mtaa mzima fremu zote zimefungwa

[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sisi wananchi wenyewe kulipa kodi bila kusukumwa ni mtihani!! Ukisema leo waje kwa kulemba kwenye kodi aaah hawapati ata bilion 1 kwa mwezi. Wakwepa kodi wengi wanajua kama wanakwepa kodi na wanafanya hivo ili faida ipige maradufu.
Aliposema tumieni akili kukusanya mapato hapo unatakiwa kupaelewa vizuri, wasipotumia akili itabidi watumie nguvu kukusanya kodi, sasa wewe hutaki TRA utumie akili? Angalia watao huduma wengine mfno kuna mtu anakatiwa maji sikuhizi au kuna mtu anakatiwa umeme sikuhizi ? jiulize kwa nini? je hapo nyuma ilikuwaje? je mashirika hayo yanatumia nguvu kukusanya mapato? Mhe. Rais yuko sahihi sana na Mungu ambarki
 
Mama sio mtu mzuri anakwambia macho yangu yanarembua lakini naona vizuri tu
Huyo ni Mama inabidi umuzoehe, vidole sasa wakati wa speech zake huwa nacheka mpaka bhaasi! naona furaha ya watanzania inarudi.
 
Huenda baada ya miezi 6 kukawa na Hali ya utulivu kwenye nchi yetu haswa kwenye uchumi.
Hatuwezi kuwa na uhakika na kauli hizi moja kwa moja kwa sababu Ni kauli za Wanasiasa.
Na mwanasisa haaminiki kwa kauli zake hata Kama Ni Nani na anatoka wapi.

Lakini Kama ikiwa hivyo hakika tutaanza tena kupiga hatua za kusonga mbele kama taifa.
 
Hhahahah.. Mkuu yani wabongo noma, huwaga wana peana signal wakisikia jamaa wapo karibu ndani ya dakika 2 mtaa mzima fremu zote zimefungwa

[emoji23][emoji23][emoji23]
Hahahah kwenye swala la kodi wafanya biashara wa kibongo sio watu wa kuwabembeleza kabisaa...Yani hata kodi ikiwa buku kwa mwezi wataikwepa tu kwa namna yeyote
 
Back
Top Bottom