Rais Samia Suluhu: Kusanyeni kodi kwa kutumia akili, sio nguvu

Rais Samia Suluhu: Kusanyeni kodi kwa kutumia akili, sio nguvu

Tuna mfumo wa kodi ambao ulibuniwa kipindi Taifa linajenga uchumi wa Kijamaa. Kutumia mfumo huo huo kipindi hiki tukiwa katika mfumo wa Soko huria, ni kama kuingiza "a square peg in a round hole". Tunahitaji kufumua mfumo huu wa kodi na kubuni ambao unafanana na malengo yetu ya kiuchumi kwa sasa.
 
Sisi wananchi wenyewe kulipa kodi bila kusukumwa ni mtihani!! Ukisema leo waje kwa kulemba kwenye kodi aaah hawapati ata bilion 1 kwa mwezi. Wakwepa kodi wengi wanajua kama wanakwepa kodi na wanafanya hivo ili faida ipige maradufu.
Mimi sikubaliani na wewe Mkuu. Wananchi wenye utashi wa kulipa kodi bila kusukumwa ni wengi. Bali kinachokera ni namna TRA wanavyoshughulikia zoezi la kulipa kodi. Hii ikiwa ni pamoja na makadirio ya kodi, maswali wanayoulizwa walipa kodi ni kama wapo kituo cha polisi. Ukimaliza makadirio, Kuna milolongo kibao isiyokuwa na msingi. Unazungushwa kwenye vyumba utadhani uko Hospital. Hivyo, Wananchi wengi kuepuka adha hiyo wanaacha kulipa kodi. Kwa ujumla TRA sio wabunifu wa kupunguza kero za walipa kodi.
 
Kweli...

Ndio maana TRA wakiwa around na center flani..kila mtu Nduki.

Kuna mambo ukibembeleza bembeleza hayaendi kamwe!
Tra walipaswa kuwatembelea wateja wao na kuwapa elimu na kutengeneza mahusiano mazuri na wafanyabiashara, tatizo kubwa hapa limetokana na mfumo wetu wa ujamaa uliomtambulisha mfanyabiashara mbele ya jamii kama mnyonyaji na hali hiyo imekaa kwa watendaji wengi wa serikali. Majina kama kabaila na mengineyo yaliimbwa sana enzi za ujamaa, pia mazingira gani yanayotengeneza wafanyabiashara? Kumbukeni pia nchi yetu inatambulishwa kwa jembe na nyundo.
 
Kweli...

Ndio maana TRA wakiwa around na center flani..kila mtu Nduki.

Kuna mambo ukibembeleza bembeleza hayaendi kamwe!
Kutokubembeleza ni kupora hela za wanaume kwenye a/c? Jiwe alikuwa ni kiongozi jizi na muovu, ndio maana huyo mama anajitenga na uovu wake.
 
Mama amenikosha sana.

Kumbe walikuwa wanatumia mabavu hadi kukwapua hela za watu kwenye account zao za benki.

Kama analoongea ndo alilokusudia kulisimamia basi sekta hii ya biashara na uwekezaji itaanza kustawi tena.
Nimemwelewa sana rais. Inaelekea alikuwa akipumua pumzi ikawa haitoki sasa inatoka vizuri na tutafaidi, hongera.
 
natamani hii mentality iwe induced kwetu.
sijui wazungu wamewezaji kuzishawish jamii zao zilipe kodi.
imefika mahali wanaona aibu hata wasipo lipa kodi. yaani kwao wanasikia msukumo toka moyoni kabisa.

lini tutafika huko?
Kuna mambo mengi ikiwemo; Matumizi sahihi ya kodi na vipaumbele vya matumizi ya kodi, watumishi kutokukwapua pesa za umma, Uzalendo kwa vitendo, Kodi zinazokusanyika (rafiki) kutokana na kipato cha wananchi husika,Sheria kali za ukwepaji wa kodi zisizo na double standards, Watumishi wa Umma kuwa watumishi wa wananchi, sio unawafokea wananchi na kuwavimbia wakati kodi zao ndizo zinazolipa mpaka mafuta ya gari lako, Nidhamu za wananchi wakawaida (walipa kodi) . Mengine wadau wataongeza, Nchi zingine mtu kukwepa kodi anaona kama dhambi na Mungu anamuona 😀

Inawezekana kabisa watu kuacha kukwepa kodi, turudi kwenye sheria za kodi za madini, Kwa kiasi kikubwa Hayati aliwaita na kuwasililiza wafanya biashara ya madini, Mapendekezo yao yamefanyiwa kazi na kwa kiasi kikubwa sana ukwepaji kodi kwenye madini umepungua.

Nchi hii kuna watu wajinga sana, utasikia kodi za nchi hii ni dogo sana, mnazijua kodi za UK, US unaanza kuwauliza mnajua kipato cha wananchi wa hizo nchi kwanza ili tupate cha kujadili?
 
Ni suala la upinzani ama ni kutofautiana mtizamo![emoji16]

Magufuli aliifikisha nchi hii kwenye mahali ukipishana naye mitazamo unakuwa mpinzani, na mpinzani kwake alikuwa adui. Ndio maana huyo mama anayoongea hivi sasa inaonekana kabisa alikuwa haridhiki na tabia za kikatili za boss wake.
 
Mimi naona mfumo wote ufumriwe,sio lafiki,mfano,unatoa mzigo china,bandarini unalipa Kodi,ukiuzia mteja wa jumla unaweka vat 18% na uliye muuzia anaweka Tena 18%,mzigo mmoja unakuwa na kodi za 100%,kwanini wasi deal na bandarini na viwandani? ulipe Kodi na vat 18%huku madokoni biashara iwe sawa kwa wote?
 
Wanapoambiwa watumie akili maana yake watoe elimu nzuri kwenye ulipaji kodi, kuna wengine hata hiyo % ya kodi hawajui inalatwa namna gani

Lazima kuwa na vipeperushi vinavyoelezea kwa undani kodi ni nini na nani anayelipa
Bidhaa ambazo hazina kodi zijulikane kama zipo
Elimu inatakiwa sana kwani unakuta mtu ananunua bidhaa jumla halafu anaweka faida yake tu badala ya kuongeza na ya kodi

Matokeo yake akija daiwa kodi anaona kama anaonewa wakati hakuongeza hiyo VAT
Najua wengi wanaangukia hapo ila nao wakusanyaji ndio wanaona pa kuwapigia bila kuwapa elimu ya ukusanyaji
 
Mimi sikubaliani na wewe Mkuu. Wananchi wenye utashi wa kulipa kodi bila kusukumwa ni wengi. Bali kinachokera ni namna TRA wanavyoshughulikia zoezi la kulipa kodi. Hii ikiwa ni pamoja na makadirio ya kodi, maswali wanayoulizwa walipa kodi ni kama wapo kituo cha polisi. Ukimaliza makadirio, Kuna milolongo kibao isiyokuwa na msingi. Unazungushwa kwenye vyumba utadhani uko Hospital. Hivyo, Wananchi wengi kuepuka adha hiyo wanaacha kulipa kodi. Kwa ujumla TRA sio wabunifu wa kupunguza kero za walipa kodi.
Ni kweli, mtu unafungua biashara mwenyewe unajipeleka TRA, ukifika tu unakuwa kama uko polisi. Afisa anakuhoji akishamaliza anajipigia mahesabu ya uongo na kweli anakubandika likodi paah, hakupi hata room ya kumuuliza kwanini umenikadiria hiyo kodi na hayo mahesabu yako umeyapataje pataje, wanaact kama maaskari wa usalama wakimkamata gaidi. 😀

It's high time watumishi wa umma wajue wao ni watumishi wa watu na wapo hapo kuwasaidia wananchi. Haya mambo mbona hayapo sekta binafsi mfano mabank etc. Client unahudumiwa na unaridhika kuwa umepata huduma.
 
Mimi sikubaliani na wewe Mkuu. Wananchi wenye utashi wa kulipa kodi bila kusukumwa ni wengi. Bali kinachokera ni namna TRA wanavyoshughulikia zoezi la kulipa kodi. Hii ikiwa ni pamoja na makadirio ya kodi, maswali wanayoulizwa walipa kodi ni kama wapo kituo cha polisi. Ukimaliza makadirio, Kuna milolongo kibao isiyokuwa na msingi. Unazungushwa kwenye vyumba utadhani uko Hospital. Hivyo, Wananchi wengi kuepuka adha hiyo wanaacha kulipa kodi. Kwa ujumla TRA sio wabunifu wa kupunguza kero za walipa kodi.
Ni lini ulihisi wanaotaka kulipa kodi ni wengi? Mi nakuambia hivi ukiona mtu anasikia TRA wanakuja anafunga kizimba chake anasepa anarudi jion au ndo mpaka kesho hiyo sababu hana chochote kitakacho mponyesha wakipita TRA, hili suala nenda mpaka posta utakuta hivi sababu wengi hatupendi kulipa kodi, ata tuambiwe kwa mwaka tulipe laki 1 bado tutakwepa tu. Kama Machinga waliambiwa 20,000 kwa mwaka na bado wanasiasa wakaona eti machinga wanaibiwa wanalipa hela nyingi sasa utakadiliwa Tsh ngapi uone chache..??

Kipindi cha nyuma NGO zilikuwa hapeleki Hesabu kwa msajili wala kulipa ada ya kila mwaka Tsh 150,000/= walikuwa hawalipi.. si kama walikuwa hawajui wakijua vizuri tu ila walikuwa hawafanyi mpaka washinikizwe! Alipokija John naona Wizara ikalivakia njuga NGO zisizo peleka Hesabu na Ada kwa Mwaka zikaanza kufungiwa hapo walikimbizana kutimiza wajibu wao.

Waafrica sisi ni mizigo hatupendi kulipa kodi ila tunataka maendeleo kwa kulalamikaaa.
 
Aliyekuwa kinara wa kupora watu ndio huyo kapewa umakamu.

Na kuonyesha kwamba bado ana uchu ameagiza zikusanywe trilioni mbili....hivi zinakusanywa vipi hizo pesa? Kama sio sisi Wanyonge wa huku chini kukamuliwa mapaka tone la mwisho?.

Kati ya mbinu alizokuwa anatumia yeye ndio hayo mabavu na kupora akina Ramadhani Ntuzwe pesa zao zipelekwe HAZINA.

Kuna usemi "Shona Koti kulingana na kitambaa ulichonacho"

Serikali ifanye utafiti kujiridhisha kama Wananchi wake wana huo uwezo wa kulipa Serikalini hizo Trilioni mbili kabla tu ya kutamani zikusanywe.
 
Kujitetea kuwa bila kutimia nguvu Watu hawalipi kodi ni utetezi wa kitoto sana....haina tofauti na akili za kuchoma nyumba ili kuuwa siafu.

Na wakati mnaomba ridhaa ya kupewa uongozi huwa mnajinadi kuwa mnajua cha kufanya, yaani nyie ni GREAT THINKERS, mkishaingia madarakani na akili zikigoma mnakimbilia kutumia mabavu.
 
Back
Top Bottom