Rais Samia unajiandalia majuto ambayo hutayasahahau kwenye maisha yako ya kisiasa

Rais Samia unajiandalia majuto ambayo hutayasahahau kwenye maisha yako ya kisiasa

Yaani kwa ufupi wapinzani hawana akili za uzalendo. Wanachowaza wao ni madaraka na siyo mbinu mbadala wa maendeleo ya nchi yetu, kila kitu wanapinga. Mama karuhusu mpaka kitabu kinachomtukana Dkt Magufuli kichapishwe kile cha mdude, maana yake ana seek sympathy kwenye kundi ambalo watanzani hawataki kulisikia maana hawana jipya.
Correct! Mama anaamini anajenga ustaarabu lakin wapinzani hawana ustaarabu always.
 
Mhe. Rais wewe ni mzoefu kwenye siasa za Tanzania. Kwa sasa ni kama unatafuta huruma ya wapinzani na unafanya vya kuwafurahisha lakin jua hii kitu itakugharimu

Kuachiwa kwa Mbowe, kukutana na Lisu ubeligiji, kujipanga kuruhusu mikutano ya kisiasa nk yote unatafuta kuonekana unajali ila ujue wapinzani hawaonagi jema.

Lisu sasa anademand utoe kauli ya kumkaribisha nyumbani na kwamba atakuwa salama, ni kama anakuamuru vile

Mbowe iko siku atasimama jukwaani na kukutukana live

Stay tuned hutaamini kama ni wao. Ule msemo wa shukrani ya punda unatimizwa vizuri na hao jamaa
Mbowe hanaga matusi kabisa, Ni mkristo yule tusimsingizie!
 
Mie nilisema mapema, Mh. Rais wangu SSH achana na wapinzani, piga kazi, hao watukuzodoa, watakudharau, watakutukana, watakuona huna maana hata uwafanyie nini, Mh. Rais akianza kutaka kuwadhirisha wapinzani ni sawa na kujaza maji gunia.

Umeona Lissu alivyogeuka, umeenda kumuona, umempatia passport, umeahidi uso kwa uso kushughulikia maslahi yake aliyokuwa analilia kutwa, bado anasema ww sio alivyokufikuria, kasema vibaya sana juzi kati ulivyokutana na ile tume ya kutoa maoni ya vyama vya siasa.

Lissu au Mbowe hata ufanye nini, ni bure kabisa, huwezi kuwaridhisha. Achana nao. Umeona juzi Mbowe kwenye jukwaa akikunanga.
Mama anatakiwa ashauriwe, vinginevyo atatengeneza fujo kama ile ya zamani kabla ya utawala wa JPM
 
Kuachiwa kwa Mbowe, kukutana na Lisu ubeligiji, kujipanga kuruhusu mikutano ya kisiasa nk yote unatafuta kuonekana unajali ila ujue wapinzani hawaonagi jema.
Petrol kwenye moto hii

Yule wa kijali aliye mpiga mwenye kombati na jiwe Dodoma alifanya jema?
Yule wa kijani aliyemuua mwenye kombati kule kanda ya ziwa alifanya jema?
 
Petrol kwenye moto hii

Yule wa kijali aliye mpiga mwenye kombati na jiwe Dodoma alifanya jema?
Yule wa kijani aliyemuua mwenye kombati kule kanda ya ziwa alifanya jema?
Ongea fact sio udhanifu
 
Tatizo lenu TEAM MWENDAZAKE, mnahisi zile siasa za kishamba ndio zenye manufaa!!kitu gani cha maana sana ambacho jiwe alikifanya kwa kupitia njia yake hiyo, ukilinganisha na jk ktk awamu yake?eti shukrani ya punda, kwani kuruhusu demokrasia na uhuru ni takwa la rais?!!Angalia siasa za KENYA, na jinsi Kenyata alivyo fair, tunawazidi nini?!kutokana na siasa zao za kuruhusu matakwa ya katiba ndio yawaongoze?!
Mkuu siasa zile muasisi wenu ndio hivyo tena, Muacheni mama aliponye taifa, na huko zanzibar mwinyi anapata upinzani mkubwa sana kutoka kwa maa consevatives, kwani bado wanataka siasa zile za mguu wa shingo, mguu wa roho!!na yeye siasa hizo hazitaki!!kwani muasisi wake jiwe hayupo.
Mojawapo ya vichwa adimu humu jf.
 
Dah... Hii nchi kuna vijana wa hovyo sana! Hivi ni kweli Anayofanya huyu mama anakosea..?
Mkuu kuna watu wanaona wao na familia zao ndiyo wenye right ya kuishi na nchi ni yao, anachokifanya Samia ni threat kwa survival yao however good it will be. Kuna mtu alisema siasa siyo uadui hawakumuelewa
 
Yaani kwa ufupi wapinzani hawana akili za uzalendo. Wanachowaza wao ni madaraka na siyo mbinu mbadala wa maendeleo ya nchi yetu, kila kitu wanapinga. Mama karuhusu mpaka kitabu kinachomtukana Dkt Magufuli kichapishwe kile cha mdude, maana yake ana seek sympathy kwenye kundi ambalo watanzani hawataki kulisikia maana hawana jipya.
Huna akili wana chama wa ccm sio Tanzania? Wengi wenu hamjitambui mnatumiwa kwa manufaa ya watawala huku familia zenu zinateseka!
 
Umeongea ukweli..
Huyu mama anajichimbia kaburi..
Mwalimu ni muda..siku zinahesabika.
Ili Rais Samia aonekane Ni mwema saaana kwa kina Mbowe inabidi awaachie hicho kiti Cha Urais wake.

Bila hivyo kelele haziwezi kuisha, kila siku litakuja jipya.
 
Naunga mkono hoja, Upinzania wa Tanzania ni wakipumbavu sana... Ni bora tuupotezee tufanye mambo mengine..

Viongozi wengi wa upinzani ni bure na hata ufanye nini huwezi kuwaridhisha zaidi zaidi mwisho wa siku watakuzodoa na kukudhalilisha tu..hawa sio wakuchekea kabisa... Siasa zenyewe wanazoziita za upinzani zimejaa wapumbavu ambao wanaamini Serikali au nchi ina chakuwafanyia au kuwalipa baadala ya wao ndio tuone faida yao kwa Taifa..

Kuna jamaa amemtaja eti JK hapo juu, anasahau JK alichezanao fair sana lakini wakaishia kumdhalilisha na kumuita majina meengi ya kijinga na madai yasiyo na kichwa wala miguu..

Hawa wazee wa deko mama asipokuwa makini watamdekea kweli na madai lukuki yasiyo na maana..
 
Tanzania hakuna wanasiasa wa upinzani bali kuna kikundi cha wasaka maslahi kwa mgongo wa upinzani....kama wengi tuonavyo CCM haina watu sahihi kwenye mifumo ndio hivyo hivyo pia tunaona upinzani hakuna watu sahihi wakuendesha siasa za upinzania....kifupi siasa za upinzani zinahitaji reform..
 
Nyerere alisema kuna watu walimwambia akiachia madaraka nchi haitaendelea, baadaye akagundua kuwa walitaka aendelee kuongoza kwakuwa hawakuwa na uhakika wa kuwepo kwenye nafasi zao iwapo angekuja mtu mwingine kuongoza nchi
 
Watu waelewe mama ni mcha Mungu hapendi kuendeleza siasa za chuki ambazo kwa namna moja au nyingine zilidhoofisha sana umoja wa kitaifa ilifika mahali watu walianza kufurahia nchi yetu inapopata majanga na hali hiyo haileti afya kwa taifa letu maconservatives wamuache mama afanye mambo yenye tija kwa nchi yetu nadhani kinachowatia mchecheto ni kuhofia vyeo ambavyo walikuwa wanavipata through weak competition .2025 wajiandae kupambana kweli kweli
 
Viongozi wengi wa upinzani ni bure na hata ufanye nini huwezi kuwaridhisha zaidi zaidi mwisho wa siku watakuzodoa na kukudhalilisha tu..hawa sio wakuchekea kabisa... Siasa zenyewe wanazoziita za upinzani zimejaa wapumbavu ambao wanaamini Serikali au nchi ina chakuwafanyia au kuwalipa baadala ya wao ndio tuone faida yao kwa Taifa..
Pande zote mbili zina mazuri na mapungufu, bila kuliona hilo mtatumia muda mwingi na gharama kubwa kuumizana badala ya kujenga nchi
 
Back
Top Bottom