Rais Samia unajiandalia majuto ambayo hutayasahahau kwenye maisha yako ya kisiasa

Umetumwa ama?
 
Heheheh adui yako kaa karibu naye... End. Hali ilivyo there is no way kuendelea na yale ya baba. Kiufupi mambo yamebadilika sana na siasa za dunia zimebadilika. Una budged deficits unahitaji misaada kuendesha serikali. Amekuta tayari kuna mabaruwa mengi yakukata misaada kwa sababu ya ubabe kwa upinzani. Tunahitaji pesa na tunahitaji huduma za afya zote hizi nchi hisani wanatupa support. Baba alipiga rungu matajiri wengi hawapumui vizuri ajira zikawa hamna maana muajiri mkubwa ni serikali na secta binafsi. Sasa akaze tuzidi kupandisha bei ya petroleum mpaka ifike book 3 ama? Mm nadhani tumuache afanye vile anaona ni vyema kwa masilahi mapana ya Taifa. Siasa zipo ila siasa na chuki nijanga kubwa zaidi kwa ustawi wa taifa na usalama pia.
 
Mleta mada!!mwanaccm uliejeruhiwa na siasa za chuki zilizo asisiwa na serikali hii KWA MUDA mrefu!!!ndio madhara yanayokuumiza Hadi leo Ndugu!!!
 
Siasa sio chuki au kuonea upande wa pili, usimdanganye mheshimiwa Rais ! Siasa zifanywe kistaarabu na anayekwenda tofauti na sheria, Sheria ichukue mkondo wake !! That's it !
 
Kwani nchi hii ni ya nani? Tanzania si mali ya CCM na baba yako, ni mali ya watanzania wote. Wewe unadhani wananchi wasio wanaccm wakinyimwa haki ya ustawi basi watanyamaza milele, kuna siku watakuja na manati mpaka kieleweke.
 
Ili Rais Samia aonekane Ni mwema saaana kwa kina Mbowe inabidi awaachie hicho kiti Cha Urais wake.

Bila hivyo kelele haziwezi kuisha, kila siku litakuja jipya.
Ndio maana ya siasa za vyama vingi kila chama kinawania kuongoza nchi ! Ili mradi tu iwe ni siasa za kistaarabu na vyama vyote vina haki sawa kwa mujibu wa sheria za nchi !! Ndio maana kunakuwepo na uchaguzi mkuu ! Anayeshinda ataongoza nchi !! Kila chama kinajaribu kuwaonyesha wapiga kura kwamba wao ndio wanaofaa kuongoza nchi ! Na kila muwamba ngozi huvutia upande wake bandugu !! Wala hakuna cha ajabu ! Mradi tu siasa zifanywe kistaarabu !!
 
Tatizo kubwa la watu wa aina kama yako huwa mna hisia mbaya za "sadistic mentality" ambazo bila shaka zilijengeka ndani ya mioyo yenu kutokana na uongozi wa JPM. Pengine wewe ni mmoja wa wanufaika wa matendo ya kidhalimu yaliyofanyika, kwa hiyo kwa sasa una hofu juu ya hatima ya maisha yako.

Wakati Rais SSH akizidi kutafuta mapatano, utengamano na mshikamano wa kitaifa ili kuponya vidonda vilivyotokana na siasa za kiharamia zilizofanywa katika kipindi cha kati ya 2016 mpaka 2021, wewe unakuja na tahadhari ya kibwege kabisa. Hivi unatambua kiasi ambacho watu waliumizwa kutokana na siasa ambazo unazishabikia na kutaka kuzihalalisha?

Ficha aibu ya ujinga wako aisee. Siasa za aina hiyo zimekwisha anza kusahaulika, Watanzania walio wengi wanafurahishwa na kuunga mkono kile ambacho Rais wetu anakifanya ili kujenga umoja wetu wa kitaifa.
 
Ulitaka Mbowe na Lissu waunge mkono juhudi kisa wamepewa passport na kutolewa jela?
 
Angewafungia vioo angelaaniwa na jamii ya kimataifa. Anawapa uhuru na tambua urais ni taasisi, usione SSH kafanya kitu gani ukadhani nyuma yake hakuna kundi kubwa la washauri.

Kapokea misaada mingi sana siku za karibuni, hivyo wigo wa wanaofuatilia siasa zetu kwa sasa ni mpana.
 
Yeah. Kabla hujaanza kushughulikia hiyo “reform” ya upinzani, bila shaka umeshajitambua kuwa na wewe ni mpinzani wa utawala kiaina - yaani mtu hatari sana kuchekewa na Mama Samia - kwa mawazo yako mwenyewe!

Kama sivyo, basi hii hoja imejaa kizunguzungu tu.
 
kilaza ktk ubora wako.
 
Mumiani mkubwa wewe.....
 
Ni maana ya uhuru,upo kwenye katiba, uhuru wa maoni, Uhuru wa kufanya mikutano ya kisiasa Kwa vyama vya siasa.Wewe nani hata utake uhuru huo kupokwa.Au ni mmoja wa sukuma gang 🤔.
 
Ukishaingia kwenye siasa ni sawa na mchezo wa ngumi huwezi kusema usipingwe za uso kikubwa ni kufuata sheria na taratibu ,Raisi asitake kushangiliwa na wapinzani hilo haliwezi kutokea hata siku moja ,yeye anachotakiwa kukifanya asimamie sheria na katiba ya nchi na ndivyo anavyofanya wala hampendezeshi mtu yoyote yeye anafanya wajibu wake,Mbowe na Tundu Lisu ni watanzania hana sababu yakuwabagua.hii nchi ni yetu sote na wala hakuna chama chenye hati miliki na nchi hii.CCM kipo madarakani leo lakini kuna siku moja kitaondoka.kisipo jenga misingi mazuri leo kesho yake itakuwa mbaya sana.Nani aliye Amini Rais Albashiri wa Sudani leo hii Angekuwa Jela.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…