Rais Samia: Vita ya Urusi, Tanzania hatutanusurika, bidhaa zote zitapanda bei

Rais Samia: Vita ya Urusi, Tanzania hatutanusurika, bidhaa zote zitapanda bei

Bei ya mafuta inatengenezwa kwenye soko la dunia, Rais hawezi kufanya lolote labda kama unataka awadanganye kama watoto wadogo ili muweze kupata usingizi usiku. Na bei ya mafuta ikipanda, bei za kusafirisha bidhaa na vyakula zitapanda na kila mtu zitamgusa. Maana meli, ndege, malori, magari, mabasi yote yanatumia mafuta kufanya kazi.
Kuna hali mbaya mno kiuchumi ipo mlangoni ndani ya kipindi cha miaka mitatu hali itakuwa mbaya sana na hii ni ulimwengu mzima. Athari za korona na hii vita zimeharibu sana uchumi wa dunia na unaedelea kuharibika. Kampuni kubwa ya uzalishaji wa mbolea YARA washasema gharama za uzalishanj wa mbolea zimepanda maradufu, uzalishaji wa ngano umeathirika tayari, mafuta na gesi ndiyo bei zinazidi kupanda. Sasa wenye nguvu kiuchumi wana ahueni wana uwezo wa kutoa ruzuku kwenye hizo bidhaa ili wananchi wao wanunue kwa bei ambayo siyo kali sana, na wana uwezo wa kununua kwa bei kubwa iliyopo sokoni maana wana misuli ya kiuchumi sasa shida ni hizi nchi zisizo na akiba na wala hazina nguvu za kiuchumi kwa kuwa mafuta na gesi ishakuwa bidhaa adimu na zinazidi kuwa gharama ina maana haziwezi tena nunua kwa kiwango kikubwa hata wafanyabiashara waliopo wanaoleta mafuta wanapoenda sokoni na wao wanakutana na ushindani na bei ikiwa kubwa maana yanahitajika kwa wingi kuliko stock iliyopo. demand kubwa supply kidogo.

So bi Tozo hapo kaongea ukweli, na ni mtihani mkubwa kwa washauri wake je watashauri nini kifanyike ili angalau makali ya maisha japo yameshaanza but yasilete athari kubwa kupindukia.

Kipindi kama hiki dunia nzima ndipo washauri wa serikali na viongozi wakuu huwa na wakati mgumu sana maana inabidi watoe suluhu ya changamoto zilizopo na hapa ndipo washauri wengi wanapoonekana wa maana au si wa maana kipimo chao ni sasa.
 
Na wewe utakuwa mwehu,bei lazima zitapanda,hatua zinazoqeza kuchukuliwa ni za kupunguza makali tuu.

..matusi hayasaidii.

..serikali inatakiwa kuchukua hatua zitakazopunguza makali kwa kiwango kikubwa, kama sio kuyadhibiti kabisa.

..Raisi na watendaji wake wanalipwa kutatua matatizo ya nchi, sio kuja kutulalamikia.
 
..matusi hayasaidii.

..serikali inatakiwa kuchukua hatua zitakazopunguza makali kwa kiwango kikubwa, kama sio kuyadhibiti kabisa.

..Raisi na watendaji wake wanalipwa kutatua matatizo ya nchi, sio kuja kutulalamikia.
Ndicho inachofanya lakini pia haiwezi ku compromise mapato yake Sana
 
Bei ya mafuta inatengenezwa kwenye soko la dunia, Rais hawezi kufanya lolote labda kama unataka awadanganye kama watoto wadogo ili muweze kupata usingizi usiku. Na bei ya mafuta ikipanda, bei za kusafirisha bidhaa na vyakula zitapanda na kila mtu zitamgusa. Maana meli, ndege, malori, magari, mabasi yote yanatumia mafuta kufanya kazi.
Tunataka sababu za kupanda kwa bei ya mafuta na bidhaa nyingine kabla ya vita

Kabla ya vita nini kilisababisha bei ya nondo, bati, Cement, mafuta ya kula, petrol kupanda?

Jibu swali.

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Rais Samia Suluhu Hassan ameelezea kupanda kwa bei ya mafuta kwa kiasi inasababishwa na mgogoro unaoendelea kati ya Urusi na Ukraine.

“Mabadiliko ya kupanda kwa bei ya mafuta kiasi kidogo yamesababishwa na vita ya Ukraine na Urusi, yanapanda bei mno. Tanzania hatutanusurika, bidhaa zote zitapanda bei, nauli zitapanda bei kila kitu kitapanda, thamani ya kila kitu itapanda juu.

“Tumesikia minong’ono kuwa maisha yanakuwa magumu, ‘kila kitu kinapanda bei, wanasema ni hao viongozi wetu tulionao hawana baraka’.

"Si baraka ya kiongozi ni hali ya ulimwengu inavyokwenda,” amesema Rais Samia katika maadhimisho ya 'Siku ya Wanawake Duniani', Zanzibar, leo Machi 8, 2022.
Tulijua yatafika, it was Corona and now Russia. Hata Ukraine hawaja lalamika sisi ndiyo twaona sifa kuwa ni chaka la kujificha wavivu!
 
Tunataka sababu za kupanda kwa bei ya mafuta na bidhaa nyingine kabla ya vita

Kabla ya vita nini kilisababisha bei ya nondo, bati, Cement, mafuta ya kula, petrol kupanda?

Jibu swali.

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
Hapo unatoka nje ya mada. Mada hii inaongelea vita ya urusi na bidhaa kupanda bei. Huo ni ukweli haupingiki.
 
Hapo unatoka nje ya mada. Mada hii inaongelea vita ya urusi na bidhaa kupanda bei. Huo ni ukweli haupingiki.
Niko ndani ya mada

1.Hapa tunamlaumu Rais kwa kushindwa kudhibiti mfumuko wa bei na kuja na visingizio ndio maana nikakuuliza kama kweli sababu ni vita
Kabla ya vita bidhaa za ujenzi kama nondo zimepanda bei kwa zaidi ya mara mbili sababu ilikuwa nini na kwanini alishindwa kutoa suluhu?
Kwanini hakuwahi kutolea ufafanuzi hili kama Rais wa nchi au alikuwa anasubiri kisingizio?

2. Wakati huu Rais ametoa suluhu gani badala ya kulalamika?
Kutuambia ukweli pekee haitoshi kwasababu kila mwenye akili anaujua ukweli hatumlipi alalamike tunamlipa atatue changamoto za Taifa.
What's the solution?



Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Niko ndani ya mada

1.Hapa tunamlaumu Rais kwa kushindwa kudhibiti mfumuko wa bei na kuja na visingizio ndio maana nikakuuliza kama kweli sababu ni vita
Kabla ya vita bidhaa za ujenzi kama nondo zimepanda bei kwa zaidi ya mara mbili sababu ilikuwa nini na kwanini alishindwa kutoa suluhu?
Kwanini hakuwahi kutolea ufafanuzi hili kama Rais wa nchi au alikuwa anasubiri kisingizio?

2. Wakati huu Rais ametoa suluhu gani badala ya kulalamika?
Kutuambia ukweli pekee haitoshi kwasababu kila mwenye akili anaujua ukweli hatumlipi alalamike tunamlipa atatue changamoto za Taifa.
What's the solution?



Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
Kupanda bei kabla ya vita ya Urusi na kupanda bei baada ya vita ya Urusi vinahusiana vipi? Kama havihusiana badi unatoka nje ya mada. Rudi kwenye mada tujadili. Vita ya Urusi imepandisha bei ya mafuta dunia nzima na bei ya mafuta ikipanda bidhaa zingine zinapanda bei.
 
Nchi haijengwi kwa kusafiri..ndio mana imeanza kumshinda..sasa anatafuta machaka ya kujificha kila ikitokea shida ya kiuchumi.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee! Hiyo hotuba alikuwa anaisoma ama alikuwa anazungumza tu bila kusoma?

Kumbuka Rais anajua mengi kuliko yeyote mambo yanayowahusu wananchi.Hili ni jambo la msingi kulijua.
 
Bei ya mafuta inatengenezwa kwenye soko la dunia, Rais hawezi kufanya lolote labda kama unataka awadanganye kama watoto wadogo ili muweze kupata usingizi usiku. Na bei ya mafuta ikipanda, bei za kusafirisha bidhaa na vyakula zitapanda na kila mtu zitamgusa. Maana meli, ndege, malori, magari, mabasi yote yanatumia mafuta kufanya kazi.
Kwanini Serikali yake isipunguze Kodi ili mwananchi apate unafuu wa garama? Sasa huyu rais anamsaada gani kama nae analalamika? Nchi hii Ina kila aina ya vito na madini ya kila aina, kwanini Serikali isiwe na akiba kwa ajili ya majanga kama haya? kwani Urusi ndio wanazalisha mafuta peke yao, mpaka tuanze kipiga miayo sasahivi? Vita yenyewe ndio ina wiki moja,je ikija kimaliza mwaka,? Rais huyu ni hopeless
 
Rais Samia Suluhu Hassan ameelezea kupanda kwa bei ya mafuta kwa kiasi inasababishwa na mgogoro unaoendelea kati ya Urusi na Ukraine.

“Mabadiliko ya kupanda kwa bei ya mafuta kiasi kidogo yamesababishwa na vita ya Ukraine na Urusi, yanapanda bei mno. Tanzania hatutanusurika, bidhaa zote zitapanda bei, nauli zitapanda bei kila kitu kitapanda, thamani ya kila kitu itapanda juu.

“Tumesikia minong’ono kuwa maisha yanakuwa magumu, ‘kila kitu kinapanda bei, wanasema ni hao viongozi wetu tulionao hawana baraka’.

"Si baraka ya kiongozi ni hali ya ulimwengu inavyokwenda,” amesema Rais Samia katika maadhimisho ya 'Siku ya Wanawake Duniani', Zanzibar, leo Machi 8, 2022.

Rais kuongea haya ni kutoa baraka kwa watu kupandisha bei za bidhaa na bahati mbaya zaidi nao watajua pakujifichia!

Bidhaa ni lazima zipande na wafanyabiashara lazima wapandishe bei ya kila kitu maana wamepewa baraka zote....

Rais hakutakiwa kutamka haya mambo ya kupanda bei za vitu labda kama angelikuwa na suluhu ya tatizo husika bali kinyume chake ni kuhalalisha upandishaji wa bei kiholela.

Bidhaa nyingi zimepanda bei toka mwezi wa tatu mwaka jana sasa sijui vita ilisha anza au lah?
 
Amepata pakujificha, mbona Kenya hawalalamiki? Bidhaa zimeanza kupaa bei kabla hata ya vita
Weeee kijana tulia hivo hivo, Kenya saa hii kwenye social medius kuna trending hashtag ya #lowerfoodprices, vitu Kenya vimepanda sana bei asikwambie mtu, ila tofauti ya kenya na TZ ni sasa unaona wakenya wameanza kuchukua reaction ya kugomea bidhaa flani wanarudi kwenye masoko ya mtaani hali inayosababisha bidhaa flani hasa za food zisipande sana bei, na soon watu wataanza ku organise maandamano na wanawachana viongozi live, sasa hivi gas ya 6kg ni 1550 ksh, na before ilikua 850, ikapanda January to 1300, now ni 1550 na hapo hii ndio ya bei ndogo, zingine zimefika hadi 1700 per 6kg hali ni mbaya, mafuta yamepanda, bidhaa zote zimepanda bei hadi mayai, soon mtaskia jambo manake wakenya hawana mchezo, umeme tu kukatika bila maelezo yakutosha sku hiyo viongozi watakula matusi hadi wasiingie online. Kenya gharama ya maisha imepanda sana hasa kwa wanachi wa hali ya chini.

Sent from my vivo X6D using JamiiForums mobile app
 
Kwanini Serikali yake isipunguze Kodi ili mwananchi apate unafuu wa garama? Sasa huyu rais anamsaada gani kama nae analalamika? Nchi hii Ina kila aina ya vito na madini ya kila aina, kwanini Serikali isiwe na akiba kwa ajili ya majanga kama haya? kwani Urusi ndio wanazalisha mafuta peke yao, mpaka tuanze kipiga miayo sasahivi? Vita yenyewe ndio ina wiki moja,je ikija kimaliza mwaka,? Rais huyu ni hopeless
Marais wengine nao ni hopeless pia maana nao nchi zao zinaathirika na kupanda bei ya mafuta baada ya vita ya Urusi. Joe Biden mmoja wao pia.
 
Mmmhhh kwa hii statement, Mkuu kakosea kutamka wazi wazi, indirectly vitu sasa ndio itakuwa vimepanda rasmi. Hapa kapata pa kujificha sbb bidhaa kibao zilishapanda bei na alikuwa kimya
 
Back
Top Bottom