Rais Samia: Waliopokea ongezeko la gharama za ununuzi wa ndege ya mizigo waachie nafasi zao watupishe

Rais Samia: Waliopokea ongezeko la gharama za ununuzi wa ndege ya mizigo waachie nafasi zao watupishe

Kuna watu wameongezeka 10% kwenye gharama za Ununuzi wa Ndege ya Mizigo.

Nadhani Sasa mh.Rais ameanza kuwafahamu Watanzania.

Hawa watu msiishie kuwafuta kazi waende mahakamani.

Hii Nchi watu Kuiba ni sehemu ya maisha Yao so kuwasimamia Kwa kuwabembeleza watakutafuna Hadi ukome..

Watanzania wanatakiwa kuendeshwa kama punda ndio wanaleta..

Mwisho waboresheeni maslahi Yao pia vinginevyo Kuna syndicate kubwa sana ya wizi.

----
Rais Samia Suluhu Hassan ameonesha kuchukizwa na kitendo cha ongezeko la fedha za manunuzi ya Ndege mpya ya mizigo kinyume na fedha ambazo zilikuwepo kwenye mkataba wa awali huku akiwataka Watumishi wa Serikali waliokubali ongezeko hilo bila kuhoji waachie nafasi zao kwakuwa hawana uchungu na fedha za Watanzania.

“Kuna mradi hapa tumetengeneza Ndege ya mizigo ambayo tunakaribia kuipokea, last Installments ilikuwa tulipe dola milioni 37, invoice imekuja dola milioni 86….. unauliza mkataba ulisemaje? hii imetokana na wapi?, ooh vifaa vimepanda bei, vipi? mkataba wetu ulisemaje”

“Na bado aliyepokea anakuletea Serikalini hii ilipwe ndio invoice tumepokea….. stupid, ulipopokea umechukua hatua gani? umeuliza nini? umefanya nini? ukilitazama kwa undani hili ongezeko limeanzia huku ndani kuna Watu wameongea huko”

“Hatuwezi kwenda hivyo na nadhani hawa wanaopokea hizo invoice wakazileta kwa raha zao kabisa Serikalini watupishe, hawafai kuwa kwenye hizo nafasi, kama wanafaa angepokea huko akalihoji”

“Baada ya kuhoji akasema nilipokea hivi, nimeambiwa hivi lakini bado nimeoka tufanye hivi, huyu unamuelewa lakini Mtu anapokea kwa raha zake tu analeta Serikali ‘Kuna hiyo invoice imekuja, vifaa vimeongezeka baada ya covid, pumbavu haiwezekani….. Mawaziri tusaidieni over-invoicing zipo nyingi sana” ——— Rais Samia.

 
Mama usicheke na kima, fukuza wote ujenge heshima na kuaminiwa zaidi na Watanzania.
Huyo hata afukuze wote mpaka mumewe hamna mwenye akili atamuelewa.

Kiongozi mkuu wa nchi kusimama hadharani na kuelekeza walio chini yake namna wanapaswa kula (kuiba) ulikuwa udhaifu mkubwa sana kiutendaji na kupitia udhaifu huo nchi itaumia sana.
 
Maana yake Invoice imejidouble 🤣🤣🤣

Ongezeko la $ 49 Million. Zaidi ya Billion 112 za Kitanzania.

Kuwaondoa kazini ni kuwapa nafasi ya kuzitumia hela zao kwa uwazi na uhuru. Hakuna mtumishi wa Umma atastaafu na ukwasi wa walau Billion 3.

Kama Mh Rais ana nia basi waondolewe na moja kwa moja mahakamani.
 
Mzee alimwachia watendaji wazuri, yeye akawafukuza, hao watamla hela mpaka basi, kufikia 2025, kapu halina kitu.
Rais atafanya mabadiliko ya msingi kwenye mfumo wa Usimamizi wa Mali.

Mwendazake na kufura watu walioiga za kutosha sembuse saizi..

Hapa inatakiwa mfumo wa Usimamizi uhusishe wengine bila kusubiria Central government walau inaweza saidia..
 
Maana yake Invoice imejidouble [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ongezeko la $ 49 Million. Zaidi ya Billion 112 za Kitanzania.

Kuwaondoa kazini ni kuwapa nafasi ya kuzitumia hela zao kwa uwazi na uhuru. Hakuna mtumishi wa Umma atastaafu na ukwasi wa walau Billion 3.

Kama Mh Rais ana nia basi waondolewe na moja kwa moja mahakamani.
Alafu kuna takataka humu zimekomaa na plea bagain ya bilion 3
 
Kuna watu wameongezeka 10% kwenye gharama za Ununuzi wa Ndege ya Mizigo.

Nadhani Sasa mh.Rais ameanza kuwafahamu Watanzania.

Hawa watu msiishie kuwafuta kazi waende mahakamani.

Hii Nchi watu Kuiba ni sehemu ya maisha Yao so kuwasimamia Kwa kuwabembeleza watakutafuna Hadi ukome..

Watanzania wanatakiwa kuendeshwa kama punda ndio wanaleta..

Mwisho waboresheeni maslahi Yao pia vinginevyo Kuna syndicate kubwa sana ya wizi.

----
Rais Samia Suluhu Hassan ameonesha kuchukizwa na kitendo cha ongezeko la fedha za manunuzi ya Ndege mpya ya mizigo kinyume na fedha ambazo zilikuwepo kwenye mkataba wa awali huku akiwataka Watumishi wa Serikali waliokubali ongezeko hilo bila kuhoji waachie nafasi zao kwakuwa hawana uchungu na fedha za Watanzania.

“Kuna mradi hapa tumetengeneza Ndege ya mizigo ambayo tunakaribia kuipokea, last Installments ilikuwa tulipe dola milioni 37, invoice imekuja dola milioni 86….. unauliza mkataba ulisemaje? hii imetokana na wapi?, ooh vifaa vimepanda bei, vipi? mkataba wetu ulisemaje”

“Na bado aliyepokea anakuletea Serikalini hii ilipwe ndio invoice tumepokea….. stupid, ulipopokea umechukua hatua gani? umeuliza nini? umefanya nini? ukilitazama kwa undani hili ongezeko limeanzia huku ndani kuna Watu wameongea huko”

“Hatuwezi kwenda hivyo na nadhani hawa wanaopokea hizo invoice wakazileta kwa raha zao kabisa Serikalini watupishe, hawafai kuwa kwenye hizo nafasi, kama wanafaa angepokea huko akalihoji”

“Baada ya kuhoji akasema nilipokea hivi, nimeambiwa hivi lakini bado nimeoka tufanye hivi, huyu unamuelewa lakini Mtu anapokea kwa raha zake tu analeta Serikali ‘Kuna hiyo invoice imekuja, vifaa vimeongezeka baada ya covid, pumbavu haiwezekani….. Mawaziri tusaidieni over-invoicing zipo nyingi sana” ——— Rais Samia.

Rais aliwapa ruksa wale kwa urefu wa kamba yao ila wasivimbiwe. Sasa analalamika nini wakati wamefata maagizo kutoka juu??
 
Huyo hata afukuze wote mpaka mumewe hamna mwenye akili atamuelewa.

Kiongozi mkuu wa nchi kusimama hadharani na kuelekeza walio chini yake namna wanapaswa kula (kuiba) ulikuwa udhaifu mkubwa sana kiutendaji na kupitia udhaifu huo nchi itaumia sana.
Mbona kama mna akili ndogo sana ,hivi kula Kwa urefu wa kamba Yako Kuna shida kwenye hiyo Kauli?

Kwamba Ile methali ya Kila mbuzi hula Kwa urefu wa kamba yake Ina walakini?

Wewe Ukiwa muajikiwa hujui urefu wa kamba Yako? Kuiba si ndio kuvuka kamba? Hapo Kuna tatizo gani mbona mna shida mahala kwenye uwezo wenu wa kufikiri?
 
Mbona kama mna akili ndogo sana ,hivi kula Kwa urefu wa kamba Yako Kuna shida kwenye hiyo Kauli?

Kwamba Ile methali ya Kila mbuzi hula Kwa urefu wa kamba yake Ina walakini?

Wewe Ukiwa muajikiwa hujui urefu wa kamba Yako? Kuiba si ndio kuvuka kamba? Hapo Kuna tatizo gani mbona mna shida mahala kwenye uwezo wenu wa kufikiri?
USITUZINGUE. Wizi na CCM unawezaje kuvitenganisha??
 
Back
Top Bottom