TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

Status
Not open for further replies.
Kuna hoja zingine hazina kichwa wala miguu. Kama watu wangekuwa wanakufa kwa sababu ya laana kutoka kwa watu fulani kwa mabaya waliyowahi kuyatenda, hii dunia ingekuwa imeshaishiwa watu wabaya!

Wewe sherehekea kifo cha mmoja wa majemedari hodari kupata kutokea katika taifa hili, lakini tambua kwamba ipo siku nafsi yako itakusuta kwa bad judgment yako hii.
 
Wale wanafiki hawatapoteza muda... utasikia mama Samia ni mpango wa Mungu...

Ni swala la muda tu utashangaa
EeenHee!

Huenda wengi wao wakabadili hata majina humu!

Ni vigumu kukaa nje ya JF..., kama alivyofanya Paskali Njaa?

Hata huu msiba haumstuwi? Atakuwa yupo mahala pagumu sana!

Inawezekana naye anahitaji maombi maalum.

Mwanzo nilidhani ni uteuzi ndio umemnyamazisha, lakini ni nafasi gani hiyo ya uteule inayoweza kumnyima nafasi ya kuja msibani JF?
 
Tarehe 17 ndio tarehe aliyofariki Maalim Seif Sharif Hamad ,duniani kuna mambo.
RIP Magu tumepoteza kiongozi aliejaa utani na wananchi wake.
 
JK mtu wa maneno maneno atatuharibia nchi tena; labda kama Mkapa angekuwa hai angekuwa ni nguzo nzuri lakini siyo huyu JK! Watu wanamkumbuka JK kwa meneno maneno ya kujisikia vizuri, hela kutoka njia za mkatomkato na mishen town lakini siyo kwa mambo thabiti ya kitaifa.
Mmhhh! Mkapa tena? Ngoja nisiseme sana maana jamaa ni marehemu
 
Apumzike kwa amani .President John Pombe Magufuli will be remembered for his determination and commitments. He was steadfast in his leadership. I know we shall all miss the devotion and integrity he has brought to the country. His contribution deserves the continued congratulations of us all.
 
Innallillahi Wainna Illaihi Raj Un. Nchi imepoteza jembe. Mwenyezimungu amlaze mahali pema peponi.
 
Wanafiki wachache na wachumia tumbo lazima mumkumbuke mungu wenu.

Mimi siyo mnafiki wala mchumia tumbo, lakini nitamkumbuka. Alikosea sana katika kusimamia janga la korona ambalo huenda ndilo limechukua uhai wake ingawa hatujaambiwa hivyo, nilimlaumu sana hapa JF. Lakini alisimamia sana discipline serikalini na matumizi ya raslimali za nchi, jambo ambalo ndilo nililopenda sana kuliko viongozi waliomtangulia. Kwa vile mimi siyo mwanasiasa, misuguano ya kisasa na pressure alizokuwa anaweka kwa wapinzani wake kisiasa ili kutogawanya taifa halikuwa jambo la muhimu sana kwangu ingawaje kulikuwa na elements nzuri na mbaya ndani yake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom