TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

Status
Not open for further replies.
Nilivyoamka saa saba usiku nakutana na meseji ya mpenzi wangu kuwa magufuli amefariki.nikaingia instagram nakuta na hizi habari. Nikaingia JamiiForums.
Nikalog out kwanza.
Nikawa naingia kama guest user .
Sikukoment kitu mpaka asubuh ndo nimeanza kukoment.
Binafsi kama siamini vile.
 
"Heri sifa njema kuliko marashi mazuri; Na siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa. Heri kuienndea nyumba ya matanga, kuliko kuiendea nyumba ya karamu. Kwa maana huo ndio mwisho wa Wanadamu wote, naye aliye hai atautia moyoni mwake.

Huzuni ni afadhali ya kuliko kicheko, maana simanzi ya uso ni faida ya moyo". MHUBIRI 7:1-3
 
Hata mimi nilimkubali kama wewe, na hata Jana baada ya kupata taarifa niliumia sana mpaka nikashindwa kulala , usingizi uligoma kuja, Yani nilikuwa na maumivu yaliyochanganyikana na furaha kwa mbali.

Ila alifanya mazuri mengi sana na nimemkubali sana, pia mapungufu nayo yalikuwepo yameumiza wengi sana.

Naomba tupage kiongozi ambaye atakuwa na maono Kama Magufuli na mixture Kikwete, JKN .

Pengo la raisi linazibika ila kwa fimilia ndio halitazibika, Mungu aipe faraja familia yake. Katika kipindi hichi kigumu.
 
Hakika taifa letu limempoteza Mtu ambaye si rahisi kumpata, kwakweli ni mshituko mkubwa ndani ya Taifa letu.
naona kiza kinene kimetanda kila kona lkn Tunamuomba Mungu atuvushe salama ktk kipindi hiki kigumu.
Mungu ana watu wengi wewe katika taifa hili hayo ndo yaleyale makufuru tunayoyasema kila siku hamjifunzi tu.
 
Sasa si wawe wanasema ukweli lini alikuwa ameshafariki.

Kwani wakisema trh 9.3 lkn trb za kiserikali zilikuwa zinafanyika kuna dhambi gani.

Serikali za uongo uongo hazipati mafanikio.
 
Kweli kabisa, wema unalipa
 
Hii ni kweli?
Mbona hawakutuambia kuwa anaumwa? Kwa hakika hapa serikiali imechemsha. Kuumwa ni ubinadamu. Wangetueleza tu ili tuanze kujiandaa kisaikolojia. Badala ya kutwambia ukweli wanasema oh yuko mzima kabisa anachapa kazi (Majaliwa) au amenipigia simu leo na ametuletea pesa (RC Chalamila). Wakati huo huo watu wanakamatwa kwa kusema tu kuwa Rais ni mgonjwa. Mama Samia, tunakuombea ufungue ukurasa mpya!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…