Rais wetu Samia acha hotuba za kujitetea juu ya jinsia yako, wewe ni Rais siyo Rais mwanamke

Rais wetu Samia acha hotuba za kujitetea juu ya jinsia yako, wewe ni Rais siyo Rais mwanamke

Unajua kwanza haya maswala ya jinsia ni aina ya ubaguzi ambao mimi kwa namna nautazama hauna tofauti na ubaguzi wa rangi.

Hivi kuna haja gani ya kutaka kuonekana ni mwanamke au mwanaume katika kazi au sehemu yoyote tukiachia chooni.

Nadhani bado jamii yetu haijaweza kuelewa maana ya jinsia katika swala maendeleo. Na ndio maana wanawake wa sasa mbali na kupata fursa tofauti na wenzao wa miaka ya 1980's kurudi nyuma, bado Wanajiona wao ni underprivileged minority kumbe ni upuuzi mtupu.

Mimi huwa nachukia sana kampeni za kijinsia maana kwa Tanzania ukizungumzia maswala ya changamoto za jinsia then automatically watu wanahisi unawazungumzia wanawake. As if neno jinsia ni sawa na kusema mwanamke.

Ushamba ni mwingi sana eneo hilo, huwa sipendi hata kujihusisha mazungumzo yake....
 
Mkuu upo sahihi kabisa na kingine aangalie asije akafanya mambo ili aonekane bora kuliko wanaume,afanye kwa kadri ya ilani yao na utashi alojaliwa ,Hapo alipo amezungukwa na wanafiki ambao wanamuingiza mkenge
siku hadi siku
 
Tatizo, huko pia atakwenda kupewa support kama mwanamke. Nchi kama US siyo mfano mzuri maana nao bado wanaona ni ajabu m'ke kuwa kiongozi wa nchi. Ndo maana hata makamu wao alituma salamu maalumu, 'za kike.'
Nadhani wanafahamu weaknesses za mwanamke na hii kitu huwa nawaambia sana watu watazame.

Ukiona kuna jambo mzungu anakusisitiza sana ufanye ila yeye kwake hakitilii mkazo then jiandae siku za mbeleni huko kupata majanga.
 
Mkuu Zygot kuna tofauti kati ya jinsi na jinsia miongoni mwa watu. Jinsia ama "gender" kwa lugha ya Kingereza ni mahusiano ya kijamii na kiutamaduni yenye kuhusisha mgawanyo wa majukumu muhimu kwa kuangilia jinsi ya mtu, yaani Mume (Me[emoji124]) au Kike (Ke[emoji126]). Kwa hiyo basi jinsi ya Rais wetu au "sex category" kwa lugha ya kigeni ni ya Kike (Ke) [emoji126].
Nijuavyo mambo ya sex yameshaleta taabu dunia hii. Siyo tu M and F siku hizi wapo akina transexual/transgender, gay.... nao wanataka watambuliwe siyo kwa mahusiano ya gender bali ya sex. Tusipoteze muda kujadili mambo ambayo hayajawa na nafasi ktk jamii yetu.
 
Wewe ni mwanadamu wa jinsia ya kike. Kila mtu anafahamu juu ya matatizo ya jinsia ktk dunia hii na kila nchi inajitahidi kuondoa matatizo hayo. Njia mojawapo ni kuachana na hali ya kulinganisha jinsia hizi ktk kazi, ili tuzifunike tofauti hizo.

Tangu Samia uliposhika nafasi ya urais, kila hotuba yako imekuwa ni kama nafasi ya kujitetea kwamba unaweza nafasi hiyo, na kuwatetea wanawake wenzako. Ombi langu kwako, achana na kujitetea.

Angalia unavyoshangiliwa na wanawake wenzako, wakiona kama ni mafanikio yao kumbe wengine hawawezi kama wanaume wengine wasivyoweza.

Mfano mzuri dunia hii ni Margret Thatcher na sasa ni yule ‘binti’ mdogo anayeiongoza serikali ya Finland, Sanna Marin kama alivyokuwa Thatcher hataki kabisa kukaribisha jambo hilo la kuonesha wanawake wanaweza au hawawezi. Kwake yeye ni kiongozi na siyo kiongozi mwanamke.

Mkuu umesema jambo la maana sana! Kama hakuna mtu amemwambia kuwa jinsia yake ni tatizo, hana haja ya kuzungumzia jinsia yake!! Ameonesha kuwa sexist na sasa ndio anaweza kuanzisha tatizo kwa kufikiria tu kuna tatizo. Nchi hii imekuwa na madiwani, wabunge, mawaziri na hata makamu wa Rais wanawake - hatuna ubaguzi wa kijinsia kiasi cha kuzungumzwa na kushadidiwa kiasi hiki.

Ninahisi ni yule Rais atasumbua wanaume kwa maneno kama “usinione mwanamke ukanidharau”! Hajui hata atakaposhindwa au kuweza hatapimwa kwa mzani wa jinsia bali utu/imani/tabia na taasisi yake tu!!
 
Rais kupewa support na mwanamke mwenzake siyo jambo baya maana kumbuka tupo kwenye mission ya Beijing.

Muhimu ni kuprove kuwa anaweza kufanya vizuri zaidi.
Udhaifu wa kupeana support kimakundi tunaujua na hauna msaada. Ndo maana hata mashuleni sasa hakuna haja ya kuwatenga wenye ulemavu, wanajichanganya na wengine. Kujitenga inawanyima nafasi ya kujiona wako sawa, wanaendelea kujiona wako tofauti. Ndo maana hata viti maaalumu Bungeni wengi wansubilia kupendelewa eti wana changamoto kumbe uzembe tu. Kuna watu wana PhD bado wanatafuta viti maalumu. Shit!
 
Nadhani anatuma ujumbe kwa kundi fulani huko huko juu. [emoji144]‍♀️[emoji144]‍♀️
 
Mkuu umesema jambo la maana sana! Kama hakuna mtu amemwambia kuwa jinsia yake ni tatizo, hana haja ya kuzungumzia jinsia yake!! Ameonesha kuwa sexist na sasa ndio anaweza kuanzisha tatizo kwa kufikiria tu kuna tatizo. Nchi hii imekuwa na madiwani, wabunge, mawaziri na hata makamu wa Rais wanawake - hatuna ubaguzi wa kijinsia kiasi cha kuzungumzwa na kushadidiwa kiasi hiki.

Ninahisi ni yule Rais atasumbua wanaume kwa maneno kama “usinione mwanamke ukanidharau”! Hajui hata atakaposhindwa au kuweza hatapimwa kwa mzani wa jinsia bali utu/imani/tabia na taasisi yake tu!!
Nimeanza kuona eti wanawake sasa wanataka kila nafasi idadi iwe sawa, badala ya kutafuta uwezo wao kama yeye Samia, sasa wanataka hata nafasi wasizokuwa na uwezo nazo. wanapigiana vigelegele; Yaani wapewe vitengo kwa kuwa tu kuna mwanamke ameweza kuwa rais. Wengine ndo hata tabia hazieleweki.

Tunataka mwanamke na mwanaume au kwa ujumla m-TZ anayeweza kuwa kiongozi na awe na tabia ya uongozi. siyo kupiga kelele ndo ajione yuko strong.
 
Wewe ni mwanadamu wa jinsia ya kike. Kila mtu anafahamu juu ya matatizo ya jinsia katika dunia hii na kila nchi inajitahidi kuondoa matatizo hayo. Njia mojawapo ni kuachana na hali ya kulinganisha jinsia hizi ktk kazi, ili tuzifunike tofauti hizo.

Tangu Samia uliposhika nafasi ya urais, kila hotuba yako imekuwa ni kama nafasi ya kujitetea kwamba unaweza nafasi hiyo, na kuwatetea wanawake wenzako. Ombi langu kwako, achana na kujitetea.

Angalia unavyoshangiliwa na wanawake wenzako, wakiona kama ni mafanikio yao kumbe wengine hawawezi kama wanaume wengine wasivyoweza.

Mfano mzuri dunia hii ni Margret Thatcher na sasa ni yule ‘binti’ mdogo anayeiongoza serikali ya Finland, Sanna Marin kama alivyokuwa Thatcher hataki kabisa kukaribisha jambo hilo la kuonesha wanawake wanaweza au hawawezi. Kwake yeye ni kiongozi na siyo kiongozi mwanamke.
Bado hajiamini.
 
Mimi naona apate ziara moja aende Ughaibuni (official visit) akapigiwe mizinga 21 na heshima zote ili aongeze kujiamini na ajue kabisa ndani ya dunia hii yeye siyo wa Rais kwanza mwanamke.

Kina Queen Elizabeth wametawala dunia miaka na miaka. Majukumu mazito kuliko aliyonayo.
Nakubalina nawe katika hoja ya kwanza, lakini napingana nawe katika suala la Malkia Elizabeth, yule ni ceremonial leader hana majukumu makubwa ya kiserikali, mwenye majukumu ya kuongoza serikali ni waziri mkuu...so Malkia hana stress za kiongozi!
 
Nakubalina nawe katika hoja ya kwanza, lakini napingana nawe katika suala la Malkia Elizabeth, yule ni ceremonial leader hana majukumu makubwa ya kiserikali, mwenye majukumu ya kuongoza serikali ni waziri mkuu...so Malkia hana stress za kiongozi!
Ceremonial leadership siyo title ya muda mrefu sana
 
Hata mimi hili jambo jana lilinifikirisha, nikajisemea moyoni inawezekana ndani ya Chama chake au watu walio karibu naye wanazungusha maneno kwamba hataweza kuongoza hii Nchi, nionavyo ndani ya chama kuna kila zana inainuliwa kumponda Mh. Rais, watu wa Jiwe wapo vitani muda wote, hawataki kuamini kwamba sasa keki imevunda wakae kwa kutulia.

Mama akae kwa kujiamini, aunde timu anayoiamini bila shaka yoyote, atoe takataka na chawa wote wa aliyepita, tayari anaye Mabeyo wasiwasi wa nini?
Hii nchi ni ngumu sana kuongozwa na mwanamke wa kariba yake.... Ataendeshwa sana na hii itamfanya aendelee kufanya maamuzi ya hovyo kama alivyofanya uteuzi wa DG wa Tume ya madini kumteua Janeth Reuben former Barrick HR Manager .. ndio maana JK anaonekana master mind. Kaacha manguli anaenda kuweka mtu wa rasilimali watu ...yetu macho sijui kama Buzwagi itafungwa.
 
Yeye sio Rais wa kwanza mwanamke hapa Duniani na hata kuwa wa mwisho,ajiamini japo najua ni kiwewe bado cha kuzoea madaraka makubwa confidence yake bado maana imekuwa ghafla
 
Ndo imeshatokea tu lakin kuna changamoto nyingi rais mwanamke., wakati akienda kujifungua nchi itakuwa kwenye likizo mpaka amalize siku 40, akiwa mja mzito nako pia ni changamoto kuna miezi fulani pale hataweza kuwajibika sawa sawa.
Ujauzito gani kwa umri wake ule mkuu
 
Mimi naona apate ziara moja aende Ughaibuni (official visit) akapigiwe mizinga 21 na heshima zote ili aongeze kujiamini na ajue kabisa ndani ya dunia hii yeye siyo wa Rais kwanza mwanamke.

Kina Queen Elizabeth wametawala dunia miaka na miaka. Majukumu mazito kuliko aliyonayo.
Au yule Makel (kama sijakosea) wa Ujerumani
 
Anachukua tahadhari juu ya mfumo dume!

PENGINE BAADA YA TAREHE 30/4 TUNAWEZA ONA MABADILIKO BAADA YA KUWA MWENYEKITI. HIVI SASA ANACHUKUA TAHADHARI NDIO MAANA ANAFICHA MAKUCHA!! PIA HUU NI MWEZI WA RAMADHANI KUHUTUBIA MCHANA NA SWAUMU SIO MCHEZO!!!
MAMA SAMIA HUU MWEZI MTUKUFU APUNGUZE KAZI ZENYE SHURUBA WAFANYE WASAIDIZI ZAIDI!
 
Back
Top Bottom