Ripoti ya CAG 2021-2022: Rais Samia ataka baadhi ya mashirika yasiyo na tija kufutwa

Ripoti ya CAG 2021-2022: Rais Samia ataka baadhi ya mashirika yasiyo na tija kufutwa

Kwanini Wakurugenzi, Bodi za Mashirika 14 yanayojiendesha kwa hasara waendelee na kazi zao?

Mashirika haya yamepata hasara kubwa sana
Mashirika haya yana Wakurugenzi na Bodi ambazo kazi yake ni kuweka malengo ili mashirika yafanikiwe, je kwanini waendelee kuwepo ofisini?

Rais Samia kama una uchungu wa nchi anza na hizo bodi, Wakurugenzi na Wasaidizi wao wote waondolewe kazini

Mashirika yafutwe

ATCL
NDC
TRC
TIB
Dah maza Hana hata meno maskini anaongea kama mtu aliyejikatia tamaa,eti mtu ana mikopo mi5 afu kasepa,kwani Maafisa waloshuhulikia hiyo mikopo si wapo?haya hili nalo wakalitazame 🤣🏃
 
TRC isifutwe bali atafutwe mwendeshaji, ikiwezekana kampuni ya nje ya nchi. Watumishi wa Serikali jawana kabisa weledi wa biashara au uchumi.
Hatujakoma kwa yaliyotokea kwa wahindi? Mwekezaji aliklchukua spare part hadi vichwa vya tremi akapeleka kwao
 
Hayo mashirika ni mali ya taifa yaani assets hivyo huwezi kuyabinafsisha kwa watu binafsi.

Serikali yaweza tu kutafuta management ambayo ina utaalam wa uendeshaji na ikaingia nayo mkataba maalum.

India shirika lao la ndege Air India laongozwa na muingereza na ana ujuzi wa kusimamia mashirika mbalimbali ya ndege ya kimataifa.

Tukubali sisi baadhi ya waafrika akili zetu tumeziweka rehani.
Hata hivyo ni sawa maana kama ATCl haijawahi kua na faidi lakini private companies wanapambana ivo ivo, so tatizi ni ile kasumba ya mali ya serikali ndo inafanya watu wawe wazembe na wapigaji.... na hatabkuwapa wazungu waendeshe bado watabanwa tuu na wahuni kwakua watajua nanmna ya kuwawajibisha wasipotekeleza intrest zao
 
Baada ya ripoti ya CAG Kutolewa na kueleza madudu ya GPSA, Rais Samia Hassan amependekeza taasisi hiyo ya umma ifutwe au iundwe upya.

Kwa kauli hii ya Rais bila shaka huu ni uamuzi kamili wa kuizika rasmi GPSA .
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu leo amepokea ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) pamoja na TAKUKURU. Katika ripoti hiyo CAG aliyataja mashirika 14 yanayoendeshwa kwa hasara ikiwemo TRC, ATCL na NDC. Rais Samia alisema kwa muda baadhi ya makampuni yamekuwa yakiendeshwa kwa hasara lakini hayaingizii serikali chochote ni bora yakafutwa ili kutoendelea kuleta hasara.

"Kuna haja ya kufanya tathimini kama baadhi ya mashirika ya umma yanafaa kuendelea kuwa nayo, yale yanayofaa yaendelee na yasiyo na tija yafutwe. Mashirika mengi yanachuma fedha kutoka serikalini lakini yenyewe haileti fedha serikalini" - Rais Samia Suluhu.

Lakini kwa upande wa TTCL, Rais Samia Suluhu anasema "TTCL na biashara ya simu kusema kweli imewashinda, tujiulize hivi kweli wanaweza kuendelea kufanya biashara ya sekta ya simu, kwanza wao wana mkongo, kwa kufanya biashara ya simu hakuleti mazingira sawa ya ushindani katika biashara hiyo na kampuni nyingine."

FsYZILXXoAE0pLd

Wamemtuma kijana wao neppie ili kuua ttcl wameona haitoshi. Hivi kusema ttcl wana mkongo eti hakuna ushindani sawa, hapo ni suala la hasara kwa shirika la ttcl au ni kukingia kampuni binafsi ushindani. Kwani serikali kukusanya kodi toka raia ni biashara? Kazi ya kodi ni nini kama sio pia kuendesha mashirika ya huduma muhimu kwa faida ya jamii. Kwa nini waone uchungu shirika kama ttcl likitoa huduma kwa bei nafuu kwa raia. Halafu ujue huyu mama hakuna kitu anajua. NDC ni shirika la biashara? Au hajui kazi ya NDC? Wanaacha kusimamia uadilifu na tija badala yake wanalihujumu ttcl kwa maslahi yao kwenye mashirika binafsi. Mtu kama magufuli asiye na mawaa alitoa nguvu yake kuimarisha ttcl sasa wahuni wameingia kutaka kuliua shirika.
 
Ifike muda mheshimiwa rais aruhusu mchakato wa katiba mpya uendelee ili tupate viongozi kutoka vyama vyote vya siasa.
Viongozi wengi wa CCM ndio wezi wa mali za watanzania maskini.
Halafu utasikia waziri fulani anasema "tuwe wazalendo".
Na wengine wanavaa tai na suti zenye rangi ya bendera ya Taifa.

Inauma sana.
 
Hata serikali ikiwemo Ikulu ikifanyiwa tathmini tunaweza kuja na pendekezo ivunjwe kwa kukosa tija.
Nataka kufanya comment kama ya kwako .naona hata ikulu ibinafsishwe tu jamani maana hatuwezi kuwa na rais asiyekuwa na tija wala kuumiza kichwa kujua changamoto ni ipi kitu kikiienda ndivyo si vyo tunakimbilia ubinafsishaji kama shortcut
 
Mambo mengine Serikali yetu iwe inajifikiria,hivi unawezaje kukuza uchumi bila njia za Reli.wewe kama Serikali kwa nini usisimamie mpaka hiyo TRC itengeneze faida.
Watawala wanapenda sana shortcut yaani kitu kikishindikana na kikaaenda ndivyo sivyo solution ni ubinafsishaji
 
Back
Top Bottom