Ripoti ya CAG 2021-2022: Rais Samia ataka baadhi ya mashirika yasiyo na tija kufutwa

Ripoti ya CAG 2021-2022: Rais Samia ataka baadhi ya mashirika yasiyo na tija kufutwa

Watoa maamuzi wa TRC iendeshweje, ndio wenye malori ya kusafirisha mizigo na mabasi ya kubeba abiria nchi nzima. Usione basi limeandikwa SUMRY ukadhani ni la yule mkinga pekee..!!! Usikute hata akina Jeni Mhagama womo au Selous, akina Makinda ya ndege nao wamo
Kumbe kweliiii, aseeeh bas hatareee mnoo.
 
TTCL ni kampuni ya umma, naiona hatari simu nyeti kama za ikulu na Usalama zikipitia kampuni binafsi, ambazo wanahisa ni wale mabeberu.

TTCL wabaki na land line na miundombinu wezeshi ya mawasiliano
Mabeberu mnawaonea sana wakati Kazi yao ni kutafta tu faida, software nyingi za mawasiliano wao ndio wanakuuzia sema sisi watanzania hatuma mawazo ya pamoja kila mmoja na Lake hivyo kuleta ushabiki na ujinga kwenye vitu vya msingi.
 
Umeshaondoka kwenye point, Mimi sio mtumishi mimi napambana na box. Shirika kufanya vibaya solution yake sio kulifuta.

Shirika kufanya vibaya tafsiri yake ni uongozi mbaya. Ndio maana nikasema kama shirika ambalo lipo ndani ya wizara linafanya vibaya vipi kuhusu wizara?

Kuna wizara mara nyingi amekua akilalamika kufanya vibaya, mbona hatuzifuti?
Hayo mashirika anaposema yafutwe sio kama hayatokuwepo mbadala hapana .... kwa huku bongo tunakasumba kama shirika likishajijenge kwenye upigaji hata aje nan mwema kama hatojiunga nao basi atapigwa kitu kizito aondolewe, akimbie ama arogwe afe... so bora yafutwe tuu
 
Hayo mashirika anaposema yafutwe sio kama hayatokuwepo mbadala hapana .... kwa huku bongo tunakasumba kama shirika likishajijenge kwenye upigaji hata aje nan mwema kama hatojiunga nao basi atapigwa kitu kizito aondolewe, akimbie ama arogwe afe... so bora yafutwe tuu
Sijakuelewa, yaani shirika linafutwa alafu linaletwa mbadala? Hilo mbadala litakaloletwa litakua halina upigaji?
 
Kwanini Wakurugenzi, Bodi za Mashirika 14 yanayojiendesha kwa hasara waendelee na kazi zao?

Mashirika haya yamepata hasara kubwa sana
Mashirika haya yana Wakurugenzi na Bodi ambazo kazi yake ni kuweka malengo ili mashirika yafanikiwe, je kwanini waendelee kuwepo ofisini?

Rais Samia kama una uchungu wa nchi anza na hizo bodi, Wakurugenzi na Wasaidizi wao wote waondolewe kazini

Mashirika yafutwe

ATCL
NDC
TRC
TIB
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu leo amepokea ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) pamoja na TAKUKURU. Katika ripoti hiyo CAG aliyataja mashirika 14 yanayoendeshwa kwa hasara ikiwemo TRC, ATCL na NDC. Rais Samia alisema kwa muda baadhi ya makampuni yamekuwa yakiendeshwa kwa hasara lakini hayaingizii serikali chochote ni bora yakafutwa ili kutoendelea kuleta hasara.

"Kuna haja ya kufanya tathimini kama baadhi ya mashirika ya umma yanafaa kuendelea kuwa nayo, yale yanayofaa yaendelee na yasiyo na tija yafutwe. Mashirika mengi yanachuma fedha kutoka serikalini lakini yenyewe haileti fedha serikalini" - Rais Samia Suluhu.

Lakini kwa upande wa TTCL, Rais Samia Suluhu anasema "TTCL na biashara ya simu kusema kweli imewashinda, tujiulize hivi kweli wanaweza kuendelea kufanya biashara ya sekta ya simu, kwanza wao wana mkongo, kwa kufanya biashara ya simu hakuleti mazingira sawa ya ushindani katika biashara hiyo na kampuni nyingine."

FsYZILXXoAE0pLd

ATCL, TRC na NDC ni mashirika muhimu kwa uchumi wa nchi.

Kuyavunja kutarudisha nyuma maendeleo ya nchi.

Pia kufanya hivyo kwamfanya raisi Samia nae aonekane ni sehemu ya tatizo kwa kukubali kushindwa kuwa ameshindwa kusimamia ukuaji wa mashirika hayo na uendeshaji wake.
 
Lina binafsishwa
Hayo mashirika ni mali ya taifa yaani assets hivyo huwezi kuyabinafsisha kwa watu binafsi.

Serikali yaweza tu kutafuta management ambayo ina utaalam wa uendeshaji na ikaingia nayo mkataba maalum.

India shirika lao la ndege Air India laongozwa na muingereza na ana ujuzi wa kusimamia mashirika mbalimbali ya ndege ya kimataifa.

Tukubali sisi baadhi ya waafrika akili zetu tumeziweka rehani.
 
Hayo mashirika anaposema yafutwe sio kama hayatokuwepo mbadala hapana .... kwa huku bongo tunakasumba kama shirika likishajijenge kwenye upigaji hata aje nan mwema kama hatojiunga nao basi atapigwa kitu kizito aondolewe, akimbie ama arogwe afe... so bora yafutwe tuu
Ukisema yafutwe unakuwa wajishusha sana kifikra.

Toa wazo la kuleta tija.
 
TTCL ni kampuni ya umma, naiona hatari simu nyeti kama za ikulu na Usalama zikipitia kampuni binafsi, ambazo wanahisa ni wale mabeberu.

TTCL wabaki na land line na miundombinu wezeshi ya mawasiliano
Mawazo ya kijima kutoka kwa wale wanaitwa BBC (Born Before Computers). Dunia hii kama hacker/Intruder anaweza kiingilia mawasiliano ya Vodacom kutaka kujua siri za Serikali basi hashindwi kuingia hata hizo za TTCL.

Nobody needs TTC, let them be euthanized right now
 
Wakurugenzi wa hayo makampuni yote wameteuliwa. Hakukua na interview Wala nini.
Tangaza kazi hizo watu wenye sifa wajitokeze.
Mfano mzuri, Maharage alifanyishwa na Nani interview? Sidhani Kama anajua kwamba Power =| squared R ama V=IR
 
Wakurugenzi wa hayo makampuni yote wameteuliwa. Hakukua na interview Wala nini.
Tangaza kazi hizo watu wenye sifa wajitokeze.
Mfano mzuri, Maharage alifanyishwa na Nani interview? Sidhani Kama anajua kwamba Power =| squared R ama V=IR
Kuna wakati wala huhitaji kujua hivyo vitu ili kuwa kiongozi mzuri, management skills, uzalendo na kuweka mbele maslahi ya nchi..
 
Back
Top Bottom