Ripoti ya CAG imefichua madudu mengi ya awamu ya tano, kulikuwa na ufisadi wa kutisha

Ripoti ya CAG imefichua madudu mengi ya awamu ya tano, kulikuwa na ufisadi wa kutisha

Nakulinganishia hivi...
1. Miaka 10 ya JK, kulikuwa na makashfa ya kutosha (eg EPA, ESCROW, RICHMOND, RADA etc). Makashfa hayo yote yalisababisha zipigwe 784 Bilioni kwa miaka 10....!!!

2. Lakini kwa awamu ya tano, 1.5T hazikujulikana ziliko NA NI KWA MWAKA MMOJA tuuuuuuuuuuuuu wallah...!!!! Hebu Sikitika kidogo kwakwanza.. @%#$&()*&%#^@...!!!!!

Sasa embu jumlisha na hizi zilizosemwa na CAG wa sasa kwa taarifa ya leo...!!! Zitafika ngapi?

Hivi angepewa mitano tena ingekuwaje?

Wale wa atake asitake, wanaweza wakasimama na kusema lolote?

Hiyo namba 2 ndio report ya CAG au ndio unabashiri
 
Mada ya 2018

Awamu ya tano imetupa pembeni utaratibu wa zabuni na sasa inaamua na kufanya manunuzi au kuingia mikataba wenyewe kwa amri toka juu...

Rejea hii itatukumbusha siku za usoni na hasa kwa Miradi hii.

1. Uwanja wa ndege chato
2. Vitambulisho vya utaifa
3. Fly overs
4. Bombadier
5. Tenda za ujenzi za TBA n.k
6. SGR
7. Bwawa la umeme

Kwa kumalizia tuu.... nimeandika hayo nikiwa full detailed. Kuna vitu duniani havichiki navyo ni Jua mwezi na ukweli.

MUDA NI HAKIMU WA YOTE!!

Credit kwako Lusungo
Wewe hebu acha maneno mengi,fichua,fichua,fichua bana.
Serikali hi ndio iliyokuja na mahakama ya mafisadi sisi tunataka kuweka historia ya kushitaki na kupeleka jela Skeleton.kwa sababu najua mpaka kesi iishe nyama zotakua zimeisha imebaki skeleton tu.
 
hukutakiwa kudhani awamu ya nne ni ya wapigaji,ilikuwa ni ya wapigaji kweli kweli.na ndio wako mbioni kurudi sasa.
Mkuu, hapa sioni tofauti. Hiyo ni report ya mwaka moja. Tofauti inawezekana kuwa awamu ya 4 kila mtu alikula kivyake, ila ya 5 walaji walikuwa ni wateule wachache tu. Imagine wakitoa ile report iliyomfukuzisha Assad in detail na kuchambua zile 1.5 Trillion .... mbona hata EPA ni cha mtoto!!
 
Na
Ni kweli kabisa kuwa ufisadi uliofanyika kipindi hiki cha mwendazake kinavunja rekodi ya tawala za awamu zote tokea nchi ipate Uhuru wake toka kwa mkoloni.
Na baada ya kugundua kavurunda akaanza njama kutaka atawale milele.
Kwa sababu alijua akiondoka baada ya miaka mitano tutamkamata na kumtupa ndani.namaanisha jela.
 
Spika wa Bunge Job Ndugai amewaasa wbunge kuchangia kwa uwazi bila kuogopa mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022 na sio kusubiri serikali ifeli kisha walaumu

Spika amesemakwa mfano Taarifa ya CAG imeonyesha ATCL imepata hasara ya bilioni 60 na kuuliza je ni sahihi kuendelea kununua ndege nyingine?

Pia ameshauri sekta binafsi kuhusishwa kwenye uwekezaji wa miradi mikubwa kama kununua mabehewa ya treni za kisasa zitakazokuja na sio kila kitu kufanya Serikali huku akisema wabunge nao inabidi washiriki na sio kuwaachia wawekezaji wa kutoka nje pekee japo nayo ni vizuri
Hii siku ilikuwa nzito sana hadi amefunguka hayo
IMG_20210328_135011.jpg
 
Wa mwenendo huu Dikteta magufuli keshakula F
Ripoti ya CAG ni sawa na repoti ya matokeo ya final exams
Sio wote wanapata A, B, C wapo pia wa D, E....... na yote hayo ni matokeo

Tusubiri hati safi na chafu tujue wale walioPass na walioDisco
 
Report za CAG zilianzia kwa Assad???? Before hapakuwa na reports?
Weka hayo madudu ya siku za nyuma... Nimekuwekea kiduchu ya wakati wa JK... BY THE WAY, WIZI WOTE, HUO UMEFANYIAKA WAKATI RAIS ANATOKA CCM... tangu awamu ya kwanza hadi kwa JPM...

Nakwambia bado ripoti ya fedha zilizotoka BoT toka January 2021 hadi machi 2021... hakuna rangi tutaacha ona safari hii
 
mama D mwaka huu yamezidi. Hata ukiangalia mh angekuwepo yasingewekwa hadharani kama hivi inavyofanyika sasa. Mwaka jana tu alituambia ATCL imefanya faida ya bil 28. Mwaka huu angekubali CAG aseme hasara ni 60bil kwa miaka 5?
Hujaelewa vizuri.. hasara ya Bilioni 60 sio ya miaka mitano, Ni ya mwaka mmoja uliopita. Hasara ya miaka mitano Ni Bilion 690 iliyosababishwa na ndege tu. Mkuu kuwa makini fuatilia vizuri ripoti ya CAG utaona ninachokuambia.
 
Weka hayo madudu ya siku za nyuma... Nimekuwekea kiduchu ya wakati wa JK... BY THE WAY, WIZI WOTE, HUO UMEFANYIAKA WAKATI RAIS ANATOKA CCM... tangu awamu ya kwanza hadi kwa JPM...

Nakwambia bado ripoti ya fedha zilizotoka BoT toka January 2021 hadi machi 2021... hakuna rangi tutaacha ona safari hii
Kama huyajui yote unalinganishaje unachokijua na usvyovijua🤣🤣🤣🤣🤣
Acha kutumia nguvu bila faida
 
Kama huyajui yote unalinganishaje unachokijua na usvyovijua🤣🤣🤣🤣🤣
Acha kutumia nguvu bila faida
Kheee... unaposema sijui kwani kuna nilichodanganya? Nimelinganisha awamu ya nne na awamu ya tano....
 
Back
Top Bottom