Ripoti ya CAG imefichua madudu mengi ya awamu ya tano, kulikuwa na ufisadi wa kutisha

Ripoti ya CAG imefichua madudu mengi ya awamu ya tano, kulikuwa na ufisadi wa kutisha

Huu ni muondelezo wa lile liloanza pale Chamwino siku ya tatu baada ya JPM kuzikwa. Wakaitisha hii ripoti jamanyemzo ya kupoza yatokanayo na mchakato wa mazishi. Ndio mafuta waliyo enda kumpaka marehemu haya. Hakuna jipya hapa.
 
Naomba kuuliza hivi hii ni tofauti na ule uchunguzi wa January to March?
 
1. Natamani taarifa ile ungeichambua ukaweka hayo madudu moja baada ya lingine tukayajadili hapa.

2. Masuala mengine ni wahusika kuwa wazembe kushindwa kurejesha majibu kwa wakati kwa CAG (kujibu hoja)

3. Nina imani kubwa Bunge litakapojadili mengi yatatolewa ufafanuzi na yataondoka!

4. Tunamshukuru sana CAG ametekeleza maagizo ya mzee marehemu Hayati JPM na Rais wa sasa Mhe. Samia Sukuhu Hassan kama alivyomwambia ukaandike report ya kina ili tuisaidie serikali na kukomesha ufisadi na wizi. Hivyo CAG amefanya kazi yake kwa weledi kama mwalimu wetu Prof. Assad

Tuwe na akiba ya maneno ndg zangu. Tusubiri Bunge lipitie taarifa hiyo kwa kina tujue mbivu na mbichi.

Namshauri Rais wetu mama yetu Mhe. Samia. Kama kuna mtendaji yoyote yupo madarakani na itathibitika kuiletea Serikali hasara na pia uzembe wa kutokujibu hoja za CAG, basi amtoe haraka sana kabla hajamuharibia kazi.
Hebu nitajie wabunge watatu watakaoweza kupitia hii ripoti kwa kina!

Tunafurahia siasa za kijinga matokeo ndo haya! Tunasubiri Babu Tale achambue!
 
Siku ya leo sijui tuuiteje huko; Mbaya? Au nzuri sana?

Ripoti ya mkaguzi mkuu wa serikali inayoendelea kusomwa muda huu si kwamba tu inawaweka CCM na watetezi wa mwendazake kwenye wakati mgumu sana, lakini tayari imechefua wananchi wengi kwa kiwango kisichomithilika.

Madudu ya SHUJAA WA AFRIKA yanatisha na kutia kinyaa.

Madudu ya MTETEZI WA WANYONGE Yanatia hasira sana.

Chukulia hili moja BILIONI 3.9 kwenye matengenezo ya ndege moja ambayo HAIKUFAA![emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064]

Upinzani uliwahi kusema upigaji wa awamu hii utavunja rekodi, watu wakabeza sana. Lakini wakati ni hakimu mzuri. Uongo hupanda lift lakini ukweli hukwea ngazi. Mahakama ya mafisadi inaweza kuanzia pale kwenye nyumba ya milele ya mwendaAzakwe marehemu hayati.

Huu uozo uliendelea kuwekwa wazi peupe hivi tusishangae kuona siku moja marehemu akalikimbia kaburi lake. N itokee kuna kitu kinaitwa maandamano kifanyike[emoji848][emoji848][emoji848] Bila udhibiti imara si ajabu kuwakuta waandamanaji wakilicharaza bakora kaburi la shujaa wa Afrika na kuipopoa mawe picha yake.

Baada ya kusomwa hii ripoti, masikio yote yako kwa Bimkubwa. Je, atasemaje? Watu wamefura kwa hasira. I hope hatawazingua
Mahabusu ziandaliwe za kutosha sasa. Ni zamu ya kubadilisha wapangaji. Karibia kila wizara ina vimeo vya kutisha.
Kaka Mshana wewe ni mzoefu, nadhani unakumbuka ripoti ya 2014 ambapo hoja karibu zote zilipanguliwa! Nadhani hata hizi ngoja ziende Bungeni. Nina mdogo wangu mahali ananiambia watu wanakimbizana kujibu hizi hoja.

Najiuliza walikuwa wapi kabla? Huu ni uzembe wa hali ya juu. Tunaimani na Bi Mkubwa kuwachukulia hatua wahusika kabla hawajaichafua serikali ya awamu ya sita.
  • Ikithibitika wizi na ufisadi fukuzaa
  • waliichelewa kujibu hoja fukuzaaa
  • waliohonga hela pale OR TAMISEMI wakapata hati safi na kwenye ma taasisi ya umma fukuzaaaa! Wakiwemo hao watumishi wa CAG

Wanadamu ni wabaya sana jamani wasimzingue mama!
 
Kaka Mshana wewe ni mzoefu, nadhani unakumbuka ripoti ya 2014 ambapo hoja karibu zote zilipanguliwa! Nadhani hata hizi ngoja ziende Bungeni. Nina mdogo wangu mahali ananiambia watu wanakimbizana kujibu hizi hoja.

Najiuliza walikuwa wapi kabla? Huu ni uzembe wa hali ya juu. Tunaimani na Bi Mkubwa kuwachukulia hatua wahusika kabla hawajaichafua serikali ya awamu ya sita.
  • Ikithibitika wizi na ufisadi fukuzaa
  • waliichelewa kujibu hoja fukuzaaa
  • waliohonga hela pale OR TAMISEMI wakapata hati safi na kwenye ma taasisi ya umma fukuzaaaa! Wakiwemo hao watumishi wa CAG

Wanadamu ni wabaya sana jamani wasimzingue mama!

Wawajibike na kuwajishwa
 
Shida yetu kubwa ni kwamba tunapojadili haya mambo hatuji na masuluhisho. Na kila mwaka ni yale yale. Upigaji wa kutisha!

Kama jamii tufanye nini ili kuikomesha hali hii? Tunawezaje kuukomesha ufisadi? Kwa nini viongozi wetu wanakuwa hivi? Tufanye nini?

Mwendazake keshalala. Hata tukipopoa mawe na kucharaza bakora kaburi lake hatatusikia. Kimbembe ni kwetu tuliobakia. Ni kweli hatuwezi kuikomesha hali hii?
Wamesema tuandike Katiba yenye taasisi huru mumekataa sasa kwa nini kila mtu asipigwe

Afu watumishi ndio tumebebeshwa zigo bovu mbwa kabisa hao wapuuzi na marehemu wao

Yaani maccm ni laana ya nchi hii
 
Siku ya leo sijui tuuiteje huko; Mbaya? Au nzuri sana?

Ripoti ya mkaguzi mkuu wa serikali inayoendelea kusomwa muda huu si kwamba tu inawaweka CCM na watetezi wa mwendazake kwenye wakati mgumu sana, lakini tayari imechefua wananchi wengi kwa kiwango kisichomithilika.

Madudu ya SHUJAA WA AFRIKA yanatisha na kutia kinyaa.

Madudu ya MTETEZI WA WANYONGE Yanatia hasira sana.

Chukulia hili moja BILIONI 3.9 kwenye matengenezo ya ndege moja ambayo HAIKUFAA![emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064]

Upinzani uliwahi kusema upigaji wa awamu hii utavunja rekodi, watu wakabeza sana. Lakini wakati ni hakimu mzuri. Uongo hupanda lift lakini ukweli hukwea ngazi. Mahakama ya mafisadi inaweza kuanzia pale kwenye nyumba ya milele ya mwendaAzakwe marehemu hayati.

Huu uozo uliendelea kuwekwa wazi peupe hivi tusishangae kuona siku moja marehemu akalikimbia kaburi lake. N itokee kuna kitu kinaitwa maandamano kifanyike[emoji848][emoji848][emoji848] Bila udhibiti imara si ajabu kuwakuta waandamanaji wakilicharaza bakora kaburi la shujaa wa Afrika na kuipopoa mawe picha yake.

Baada ya kusomwa hii ripoti, masikio yote yako kwa Bimkubwa. Je, atasemaje? Watu wamefura kwa hasira. I hope hatawazingua
Mahabusu ziandaliwe za kutosha sasa. Ni zamu ya kubadilisha wapangaji. Karibia kila wizara ina vimeo vya kutisha.
Ilani ya ccm 2020 - 2025 inasema tutaendelea kupambana na rushwa na ufisadi kwa nguvu zote.


Haisemi ufisadi umeisha.

Hata Ulaya kina Morinyo, Messi, Ronaldo mara kwa mara tunasikia aamepelekwa mahakamani kwa kukwepa kodi.

Hata Chadema wabunge wengi walihama mwaka jana sababu ya ufisadi michango yao. Kinachotakiwa ni kuendelea kupambana na ufisadi
 
Ukweli ni kwamba madhambi mengi yanafanyika kwenye giza. Na ukiona kiongozi anataka giza litawale ujue ana nia ya kuficha madhambi.

Na kwa wale wanaosema Marehemu alikuwa sio mwizi, let's assume ni kweli hakuiba. Lakini kama nchi tulimpa pia kazi ya kulinda rasilimali zetu.
 
Back
Top Bottom