Ripoti ya CAG imefichua madudu mengi ya awamu ya tano, kulikuwa na ufisadi wa kutisha

Ripoti ya CAG imefichua madudu mengi ya awamu ya tano, kulikuwa na ufisadi wa kutisha

Yaan hapa ndipo ninapowanyooshea CCM wanaharibu then wanatwambia walichoharibu kwa kujiegemeza kwa Rais(mtu) ili kutengeneza Imani kwa chama na aliyepo madarakani. Nae ataharibu watakuja kusema ili tumwamini aliyesema n.k na wananchi tunakubali tu. Nyerere alifanya, wakaja kumbeza kupitia mwinyi, nae akaharibu, mkapa akaharibu, kikwete usiseme, magu nae Kama mnavyosikia. Na ujanja wa CCM ni kuhakikisha wao ndio wanaibua madudu mengi ili kumpa credibility aliyepo madarakani. Kwa kifupi CCM anajigeuza kwa wananchi kwa kuwa mpinzani wa aliyoyafanya anavyoona kuna faida ya kufanya hivyo kwa wananchi na wananchi nao wanajaa. Wakijaa anarudi kuwa mtawala na anaharibu tena yaan ni mwendelezo. So everything is f*ucked.
 
Jifunze Break Even Point utajua faida inavyoliwa na running cost kwenye biashara mpya...

Angalia mchoro wa BEP

View attachment 1746810
IMG-20210408-WA0113.jpg
 
Hakuna kitu hapo. Hizi ni mbinu za kuwafanya watu wamsahau SHUJAA.
Wanaona Power yake bado imejaa mioyoni mwa watu, kwa hiyo njia pekee ni kuonesha kana kwamba SHUJAA hakuiweza kazi.
Kwa kutumia akili ndogo kabisa, kama kulikuwa na ubadhirifu huo, aliwezaje:-
(1)Kujenga Ikulu na kuhamia Dodoma ndani ya miaka 5?
(2)Kuifikisha Nchi uchumi wa kati ndani ya miaka 5?
(3)Kuanza kujenga Bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere ndani ya miaka 5?
(4)Kuanza Kujenga SGR ndani ya miaka 5?
(5) Kujenga Flyovers kwa miaka 5?
(6)Kununua ndege hizo kwa miaka 5?
Hayo ni machache tu kati ya mengi aliyoyafanya kwa muda mfupi kabisa na ikumbukwe kuwa, Watangulizi wake wote hawakuweza kufanya hata moja kati ya hayo kwa miaka yote 10 waliyokaa madarakani. Kwa sababu hayupo, ndo yanaibuka hayo. Kwa vyovyote vile ilivyo au itakavyokuwa,
Ukweli utabaki pale pale kuwa, JPM alikuwa SHUJAA.
 
Tatizo lipo kwa wakuu wa Idara husika, na viongozi wenye wajibu wa kusimamia Matumizi ya fedha za serikali.
wahusika ktk ubadhirifu au matumizi mabaya ya fedha za serikali wachukuliwe hatua bila kuoneana aibu.

kuleana na kuoneana aibu ndio kutaiangamiza taifa letu, hatua kali zichukuliwe.

Hata Hayati JPM ange kuwa haki ange chukua hatua kali vivo hivyo tunategemea kwa Rais wetu Mama Samia atachukua hatua kali kwa kila idara na viongozi wake.
 
Humu 80% ni blabla tu hakuna facts ya maana, ATCL ni loss ya bil 60 kwa miaka mitano, ni loss sio wizi, uendeshaji wa shirika lenyewe, takribani mashirika yote yamekula loss, suali lingekuwa je pamoja na loss ya mashirika yote haya mbona bado wanaendelea na biashara hiyo?.
hiyo bil 60 ni 2019/2020. miaka mitano back ina loss kubwa kuliko hiyo
 
Nafahamu
Kwani hizi report si huwakilishwa hivi kila mwaka?
Mkuu usipoteze muda kujadiliana na watu ambao hawana uelewa mpana wa na masuala ya auditing ,wengi wao humu ndani hawana uelewa mpana na masula ukaguzi, hawawezi kutofautisha kati ya hoja za ukaguzi na wizi, hawajui kwamba CAG ana mamlaka ya kuagiza mtuhumiwa kukamatwa endapo Kuna ubadhilifu umetokea vinginevyo zinabaki kuwa hoja Kama hoja nyingine.
 
Hakuna kitu hapo. Hizi ni mbinu za kuwafanya watu wamsahau SHUJAA.
Wanaona Power yake bado imejaa mioyoni mwa watu, kwa hiyo njia pekee ni kuonesha kana kwamba SHUJAA hakuiweza kazi.
Kwa kutumia akili ndogo kabisa, kama kulikuwa na ubadhirifu huo, aliwezaje:-
(1)Kujenga Ikulu na kuhamia Dodoma ndani ya miaka 5?
(2)Kuifikisha Nchi uchumi wa kati ndani ya miaka 5?
(3)Kuanza kujenga Bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere ndani ya miaka 5?
(4)Kuanza Kujenga SGR ndani ya miaka 5?
(5) Kujenga Flyovers kwa miaka 5?
(6)Kununua ndege hizo kwa miaka 5?
Hayo ni machache tu kati ya mengi aliyoyafanya kwa muda mfupi kabisa na ikumbukwe kuwa, Watangulizi wake wote hawakuweza kufanya hata moja kati ya hayo kwa miaka yote 10 waliyokaa madarakani. Kwa sababu hayupo, ndo yanaibuka hayo. Kwa vyovyote vile ilivyo au itakavyokuwa,
Ukweli utabaki pale pale kuwa, JPM alikuwa SHUJAA.
No body anataka kuchafua image yake.
and to be honestly kila mtu anajua kazi alio ifanya. yanaonekana kwa macho.

lakin lila shilling ina pande mbili. upande mwingine ndio huo kama report ya CAG inavyosema.

JPM hakuwa mkamilifu.
 
Wengi wanaopiga debe kudai "madudu" yamefichuliwa hawajawahi kusoma ripoti za CAG, wanadakia ya kusikia tu. Kopi za hii ripoti ya mwaka huu mimi sijaiona, lakini nilishasoma za kila mwaka kwa miaka 11 iliyopita tangu waanze kuziweka mtandani. Utashangaa ukija kusoma hii ukakuta ni sawa kabisa na zile za zamani. Hati chafu ni kama 5% au chini ya hapo kwa nchi nzima.
Mkuu wasamehe bure hawana wanashindwa kutofautisha kati ya hoja za ukaguzi na wizi.

Hoja hizi huibuliwa na CAG huzifuta zile ambazo hukosa majibu kwa miaka 3 mfululizo CAG au bunge huagiza vyombo vingine vya Serikali Kama vile TISS ,PCCB POLICE kuchukua hatua .
 
Shida yetu kubwa ni kwamba tunapojadili haya mambo hatuji na masuluhisho. Na kila mwaka ni yale yale. Upigaji wa kutisha!

Kama jamii tufanye nini ili kuikomesha hali hii? Tunawezaje kuukomesha ufisadi? Kwa nini viongozi wetu wanakuwa hivi? Tufanye nini?

Mwendazake keshalala. Hata tukipopoa mawe na kucharaza bakora kaburi lake hatatusikia. Kimbembe ni kwetu tuliobakia. Ni kweli hatuwezi

Tatizo letu ni mfumo wa uendeshaji serikali na uwajibikaji, kudhibiti mapato na matumizi

Suluhu ni katiba mpya, ile ilopita kwa raia na kuithibitisha.

Kama tunataka mabadiliko tuanzie hapo.
 
viongozi wa hii nchi hata siwaelewagi Kama kweli wamesoma au laa,maana hata wao wanajishangaa.
Ni wapuuzi tu
Siku ya leo sijui tuuiteje huko; Mbaya? Au nzuri sana?

Ripoti ya mkaguzi mkuu wa serikali inayoendelea kusomwa muda huu si kwamba tu inawaweka CCM na watetezi wa mwendazake kwenye wakati mgumu sana, lakini tayari imechefua wananchi wengi kwa kiwango kisichomithilika.

Madudu ya SHUJAA WA AFRIKA yanatisha na kutia kinyaa.

Madudu ya MTETEZI WA WANYONGE Yanatia hasira sana.

Chukulia hili moja BILIONI 3.9 kwenye matengenezo ya ndege moja ambayo HAIKUFAA![emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064]

Upinzani uliwahi kusema upigaji wa awamu hii utavunja rekodi, watu wakabeza sana. Lakini wakati ni hakimu mzuri. Uongo hupanda lift lakini ukweli hukwea ngazi. Mahakama ya mafisadi inaweza kuanzia pale kwenye nyumba ya milele ya mwendaAzakwe marehemu hayati.

Huu uozo uliendelea kuwekwa wazi peupe hivi tusishangae kuona siku moja marehemu akalikimbia kaburi lake. N itokee kuna kitu kinaitwa maandamano kifanyike[emoji848][emoji848][emoji848] Bila udhibiti imara si ajabu kuwakuta waandamanaji wakilicharaza bakora kaburi la shujaa wa Afrika na kuipopoa mawe picha yake.

Baada ya kusomwa hii ripoti, masikio yote yako kwa Bimkubwa. Je, atasemaje? Watu wamefura kwa hasira. I hope hatawazingua
Mahabusu ziandaliwe za kutosha sasa. Ni zamu ya kubadilisha wapangaji. Karibia kila wizara ina vimeo vya kutisha.
 
Humu 80% ni blabla tu hakuna facts ya maana, ATCL ni loss ya bil 60 kwa miaka mitano, ni loss sio wizi, uendeshaji wa shirika lenyewe, takribani mashirika yote yamekula loss, suali lingekuwa je pamoja na loss ya mashirika yote haya mbona bado wanaendelea na biashara hiyo?.
Io ni loss ya mwaka mmoja acha kupotosha
 
Back
Top Bottom