Riwaya: Mwanamke Uliyekula Pesa Zangu Nakutafuta

Riwaya: Mwanamke Uliyekula Pesa Zangu Nakutafuta

Msisitizo

Kwa sababu ya mtindo wangu wa uandishi, ukubwa wa riwaya na mengine niyajuayo mimi, sitaweza kuleta kipande chenye zaidi ya maneno 500 kwa siku.

Malalamiko kuwa riwaya ni fupi yanapoteza ladha ya riwaya yenyewe, kwani badala ya kujadili yale yanayojiri kwenye riwaya, sasa tunajadili urefu wake.

Kama mimi nisivyowakera kwa kuwaomba hela ili niwape simulizi hii, basi nanyi acheni kunikera kwa kunihamasisha niongeze urefu wa simulizi badala yake turidhike na kidogo kilichotumwa huku tukisubiri mwendelezo.

mtaacha au niache?
Mmh
 
Msisitizo

Kwa sababu ya mtindo wangu wa uandishi, ukubwa wa riwaya na mengine niyajuayo mimi, sitaweza kuleta kipande chenye zaidi ya maneno 500 kwa siku.

Malalamiko kuwa riwaya ni fupi yanapoteza ladha ya riwaya yenyewe, kwani badala ya kujadili yale yanayojiri kwenye riwaya, sasa tunajadili urefu wake.

Kama mimi nisivyowakera kwa kuwaomba hela ili niwape simulizi hii, basi nanyi acheni kunikera kwa kunihamasisha niongeze urefu wa simulizi badala yake turidhike na kidogo kilichotumwa huku tukisubiri mwendelezo.

mtaacha au niache?
Tumeacha baba, tusamehe
 
Sehemu ya 18

Wakiwa wamebakiza hatua themanini na tano kulifikia gari, niliachia risasi mfululizo, risasi zikawapiga miguu yao wakadondoka chini wanaolia kwa maumivu. Lakini kumbe hawakuwa peke yao, ilikuja gari ndogo iliyokuwa wazi kwa nyuma, wakashuka wengine watano, kama wenzao, nao wamevaa viremba vyeusi. Wakamimina risasi mfululizo hata nikashindwa kufanya maamuzi, vioo vya basi letu vikapukutika vyote na nikasikia sauti ya vilio. Haraka sana, wale jamaa waliwaokota wale wenzao kisha wakapanda katika gari ambalo liligeuza haraka na kuanza kurudi walikotoka, nikazimimina risasi kadhaa ili kuwasimamisha, lakini sikuwapata.

Baada ya kuona hali ipo shwari, nilirudi ndani ya basi, nikapokelewa kama shujaa, tukashangilia pamoja. Tulikaguana wote ili tuone kama tupo salama, watu wote walikuwa salama isipokuwa dereva bonge ambaye alilala muda wote kutokana na kupoteza fahamu kwa sababu ya ule mshituko wa risasi. Nilibaini mawazo ya watu na hofu waliyokuwa nayo, dereva ndiyo huyo kapoteza fahamu, nani angeendesha basi ile?

Ukiachilia mbali hofu, palitokea jambo moja la kutisha. Abiria walianza kuwasema vibaya wale askari waoga. Palitokea mzozano mkubwa, askari mmoja akapigwa kofi, mwingine akakimbia akachukua ile silaha aliyoitupa chini, akapiga risasi tano juu halafu akaamrisha watu wote wakae chini. ukimya ukatawala. Halafu akaninyooshea bunduki yake, akanitaka nirudishe silaha ile niliyokuwa nayo nimpe yule askari mwingine. Nikakataa, huku nasogea karibu yake, akaniamrisha nisisogee zaidi lakini alishachelewa. Nilishafika karibu yake, nikaishika bunduka na kuielekeza juu halafu nikampiga teke kali la kifua, akadondoka kama furushi la dhambi. Nikazikamata bunduki zote mbili kisha nikaagiza askari wale wafungwe kamba. Abiria waliwafunga kamba huku wakiwapiga makofi, sikuwazuia, lakini jamaa waliumizwa kidogo japo si kwa kiasi cha kutisha, kilikuwa kiasi cha kuadhibu tu.

Kama nilivyosema awali palikuwa na hofu ya nani angeendesha gari, hata nyuso za abiria zilionyesha wasiwasi huo, naye Dereva Bonge hakuwa na dalili yoyote ya kuamka.

Nilikaa katika kiti cha dereva, nikapiga honi, abiria wakashangilia, askari waoga wakanuna. Basi lenyewe lilikuwa ‘automatic’, nikaliwasha, halafu nikakanyaga breki, nikatia gia, nikakanyaga mafuta, gari likaenda.

Abiria aliyegeuka dereva, niliendesha basi lile nikielekezwa njia za kupita na mhudumu wa basi, kijana huyu kabla hayajatufika maafa, alituhudumia kwa soda moja na biskuti, sasa alikuwa akinielekeza kona za kupita hasa tulipokuwa tunafika eneo lenye njia tatu au nne.

“Asante sana, umetuokoa,” sauti ilisikika, hata bila kugeuza shingo, niliitambua, alikuwa Kijana Msomi. “Tuko pamoja,” nilijibu, nikapiga honi kwa mbwembwe, kijana akarudi kukaa katika nafasi yake.

Baada ya kimbiakimbia nyingi humo njiani, hatimaye tulifika Kolkata, askari walishauri kuwa, badala ya kwenda stendi ya mabasi, tupitie kituo cha polisi ili kutoa taarifa za uhalifu. Sikukaidi, na abiria wengine waliunga mkono, basi nikaliendesha mpaka katika kituo cha polisi, ilikuwa yapata saa nne usiku.

Dereva bonge alirudiwa na fahamu tulipofika kituo cha polisi, mhudumu wa basi akamsimulia ilivyokuwa. Tulishuka, askari waoga wakafunguliwa na kuungana na wenzao kituoni pale, kisha kijana msomi akishirikiana na abiria wengine, akasimulia namna ilivyokuwa.

Baadae watu waliruhusiwa kuondoka, kila mmoja na mzigo wake. Nami nikazipiga hatua nikitafuta mahali pa kulala usiku huo, lakini kabla sijazimaliza hatua tatu, niliitwa na askari, akaniomba niingie ndani.

Tulifika ndani ya kituo, nikakuta askari watatu wengine waliokuwa wananisubiri. Wawili kati yao, walikuwa ni wale askari waoga.

“Ndugu, kwa nini ulipora silaha za askari na kuzitumia kushambulia wahalifu?” aliniuliza askari niliyemkuta kakaa tulivu, kwa kuwa nilikuwa sijakaa, ikabidi nikae kwanza.

“Sikupora silaha za askari, askari walitupa silaha kwa uoga wao wenyewe.”

“Vipi kuhusu kuhamasisha abiria wawashambulie askari hawa?”

“Sikufanya hivyo!”

Askari hakuendelea kunihoji, aliamrisha niwekwe rumande, dakika moja iliyofuata, nilikuwa ndani ya chumba cha rumande, chumba kidogo, kichafu tena kilichokuwa na wahalifu saba.

Ndani ya mahabusu hiyo sikutaka kuzungumza na mtu, kwa vyovyote tusingeelewana. Nilifika nikajiweka katika kona moja, kisha nikaanza kuzipiga hesabu, kitendo cha kuwekwa ndani mule kingetosha kunichelewesha kutoka. Vipi kama mahakamani ningeshindwa kesi na kufungwa? Halafu hiyo kesi yenyewe ingetumia siku ngapi? Niliona siwezi kuchomoka katika mtego ule, ushujaa wote niliofanya haukuthaminiwa, nikaishia kuwekwa rumande!

Inaendelea...

Kuwa wa Kwanza Kupokea mwendelezo wa Riwaya hii Kwa kujiunga katika Group la bure WhatsApp, Gusa Hapa Kujiunga

Tupate Wadhamini:

Kwa Mahitaji ya kuandikiwa CV, Barua ya Maombi ya Kazi na Masomo kwa Wanafunzi wanaorudia mitihani, Gusa Hapa Tuwasiliane Whatsapp.
Twasubili bwana mako
 
Sehemu ya 19

Ilifika saa nane usiku nikiwa rumande, wahalifu niliokuwa nao, walikuwa wamelala, nikasogea mpaka katika mlango wa chuma uliotengenezwa kwa nondo kiasi cha kuweza kuona yanayofanywa na askari. Niliona askari mmoja aliyekuwa katika kiti, bila shaka alikuwa zamu, naye alikuwa amelala. Nilitambua nje lazima kungekuwa na askari wawili au watatu. Nilijitahidi kuchungulia lakini sikuwaona.

“Polisi, polisi kuna tatizo,” nilisema kwa nguvu nikiwa nimesimama mlangoni lakini nikinyoosha mkono kuelekea ndoo iliyokuwa ndani ya mahabusu.

“Kuna nini?” aliuliza askari aliyetoka usingizini, nami nikautumia mwanya huo wa akili yake kuzubaa.

“Kuna kitu cha ajabu ndani ya ndoo ile, nahofia kinaweza kutudhuru wote humu!”

Askari alifungua lango lile ama tuliite geti la mahabusu, mimi nikasogea nyuma kidogo kumpisha, halafu nikamwambia, “Fungua taratibu afande, ni kitu kisichoeleweka.”

Aliifikia ndoo, akaanza kuifungua taratibu kuona kilichokuwa ndani, ghafla, nikatoka ndani ya mahabusu, halafu nikalifunga geti kwa komeo lake la chuma, askari akapiga kelele, “We mshenzi umenidanganya… fungua ama sivyo wenzangu watakupiga risasi ufe.” Halafu akaanza kupiga kelele kuwaita wenzake akizisukuma nondo za geti asiyeweza kutoka.

Nilitoka kwa tahadhari kwani nilifahamu lazima kelele za askari yule zingewaamsha wenzake katika maficho yao. Sikunyoosha njia, niliruka kajiukuta kadogo kalikokuwa pale, kisha nikaviingia vichochoro ninayetembea kwa tahadhari kubwa.

Nilitembea katika mitaa mingi ya Kolkata, kila eneo lililokuwa na danguro nilifika lakini sikumpata Asi.

Leo hii nimeamka salama, nakwenda tena kumtafuta Asi katika madanguro ambayo sikuyafikia. Nilipokuwa katika mitaa fulani, niliona benki ambayo mtu mmoja alinieleza hiyo ni benki ambayo hutumika kuweka pesa za watu wanaofanya biashara ya kujiuza, yaani makahaba. Mbele ya benki hiyo niliona mwandishi wa habari akimhoji mwanamume fulani, baada ya kumalizana na yule mwanamume akahojiwa mwanamke. Nilimfuata mtu mmoja niliyehisi anaelewa kiingereza, nikamuomba anifasirie kilichokuwa kinaendelea hapo. Akaniambia yule mwanamume ni Meneja wa benki na anaeleza kwamba, kiasi cha uwekaji wa pesa katika benki hiyo ya makahaba kimepungua, pia biashara ya kondomu imeshuka kupita kiasi. Yule mwanamke ni kiongozi wa makahaba hapa Kolkata, analalamika kuwa, kwa sababu ya ‘lockdown’ biashara yao imedorora na hivyo wanaiomba serikali iwape pesa kwani wao ni walipa kodi wazuri.

Sikuendelea kufuatilia, sasa niliamua kwenda Sonagachi, sehemu iliyosifika kwa biashara ya ukahaba hapa Kolkata.

Nikiwa natafuta usafiri kuelekea Sonagachi, niliona gari la askari likipita, nao waliniona, niliwatambua, ni askari wa kile kituo nilichotoroka. Askari wanne walikuwa na silaha za kivita, wakashuka, wawili walikuwa mikono mitupu tena wenye vyeo, nao wakashuka, nikaanza kufukuzwa na askari sita.

Nilikimbia kama mwanariadha Usain Bolt, nao walinikimbiza bila kuchoka, hata ikawa kama Usain Bolt anakimbizwa na Mkenya Kipchoge. Nilikunja kona, nao wakakunja. Nikafika eneo la wazi, sikulipenda eneo hili, ingekuwa rahisi kwao kunipiga risasi, nikakimbia haraka na kutafuta kichochoro, kisha mbio. Uchochoro ulikuwa mrefu, kabla sijaumaliza askari wakawa nao wameingia na kuniona, halafu mbele nikakutana na ukuta, basi ikawa kama ningeishia katika ukuta ule na kukamatwa. Hata hivyo, nilikimbia kwa kasi kisha mguu wa kushoto ukakanyaga juu ya ukuta, mguu wa kulia ukakanyaga juu zaidi halafu kushoto ukakanyaga juu kidogo ya kulia kisha mikono ikashika juu halafu nikajivuta na kutua chini kwa kishindo hafifu, ‘puuuuh.’

Nilitembea kwa kujificha mpaka nilipofikia usafiri, gari likawashwa, nami nikaelekea Sonagachi kumtafuta Asi, Mwanamke aliyekula pesa zangu. Shilingi za Kitanzania, elfu kumi na tisa.

Nilifika Sonagachi saa kumi jioni. Sonagachi inafanana na Kariakoo kwa wakazi wa Dar es Salaam, kwa wakazi wa maeneo mengine, mji huu unafanana na sehemu ya mnada. Nilishangazwa sana kuona wanawake wakijiuza wakati hata jua halijazama.

Nikiwa natembea kwa kuangaza huku na kule, mara nyingi niliombwa kununua wanawake wa Kihindi kwa bei ndogo ya dola moja yaani shilingi elfu mbili na mia tatu! Nilishangaa, Wahindi hawa wanaosemekana kwamba huwa hawataki kuolewa ama kuwa na mahusiano na watu wa mataifa mengine, leo wanapatikana kwa gharama ya shilingi elfu mbili na mia tatu za Kitanzania, tena katika nchi yao! Isingekuwa hofu ya maradhi na yale mahusiano yangu mapya na msichana mrembo Deepa Akshay, ningenunua mmoja. Lakini laaah!

Inaendelea...

Kuwa wa Kwanza Kupokea mwendelezo wa Riwaya hii Kwa kujiunga katika Group la bure WhatsApp, Gusa Hapa Kujiunga

Tupate Wadhamini:

Kwa Mahitaji ya kuandikiwa CV, Barua ya Maombi ya Kazi na Masomo kwa Wanafunzi wanaorudia mitihani, Gusa Hapa Tuwasiliane Whatsapp.
mambo yamekua mambo
 
Jina moja kama mbwa anajifanya sterling katika nchi ya watu haha, pili mbona muda unazidi kwenda tu huko uhindini au amesahau kuwa yupo likizo na Dar pande za mwananyamala alishakaa muda mrefu zaidi ya wiki 3?!
ltakuwa likizo yenye majukumu bila shaka,haendi ofisini tu lakini kila kila alipo yupo kikazi zaidi...!
 
Sehemu ya 20

Niliendelea kuzurura nikikutana na makahaba kila baada ya hatua tatu. Sikumuona Asi, hata dalili haikuwepo na kiza kilianza kuingia, hata hivyo, hakikuwa tishio kwa uwepo wa taa zilizomeremeta kwa nguvu.

Saa nne usiku nilichoka, nikaamua kutafuta sehemu ya kulala. Nikaipata Hotel Hafsha, bei ndogo tu, Shilingi za Kitanzania elfu ishirini na nne, nikalala kwa amani, lakini nikiwa na vurumai moyoni, nirejee nyumbani au niendelee na msako huu usio na dalili za mafanikio! Katikati ya mtu anayesinzia na kuwa macho, nikapata njia moja. Nikaamua kuijaribu njia hiyo.

** ** **​

Kulikucha asubuhi, nikaenda msalani kutoa haja ndogo, kisha nikarejea na kutaka kusoma kitabu, lakini nikakumbuka sikuwa na kitabu, vyote niliviacha nyumbani. Nikakaa kwa muda wa dakika kumi, nikanywa bilauri moja ya maji, halafu nikachukua simu yangu, nikaweka ‘application’ ya kupima umbali nikimbiapo, nikavaa mavazi ya mazoezi nikatoka nje na kuanza kukimbia barabarani.

Lengo langu ilikuwa kukimbia kiasi cha kilomita tano. Japo nilikuwa na uwezo wa kumaliza mbio hizo ndani ya dakika kumi na mbili sawa na Mganda Cheptegei, nilipanga kutumia dakika ishirini na tano ili mwili upate joto.

Joshua Cheptegei ni Mganda anayeshikilia rekodi ya Dunia ya kumaliza mbio za kilomita tano kwa dakika kumi na mbili tu. Aliweka rekodi hiyo huko Monaco Ufaransa. Msomaji, mimi ninao uwezo wa kukimbia mbio hizo kwa dakika hizo kama Cheptegei, lakini sitaki kwenda kushiriki kwa sababu sipendi sifa wala kumfedhehesha ndugu yangu Cheptegei, wana Afrika Mashariki ni wamoja, sisi ni ndugu.

Wakati ninakimbia, nilipitwa na mwanamume aliyekuwa anakimbia kama mimi, lakini yeye akiwa kasi zaidi, akiwa mbele yangu, niliweza kumtambua, mtu huyu alikuwa Akshay, baba yake Deepa. Nilifurahi kugundua kuwa hakuweza kunitambua.

Nilikimbia kwa mwendo kadri nikimfuata mwanamume huyo. Baada ya mbio za kilomita tatu, alikunja kushoto, akavuka barabara kisha akasimama katika geti kubwa lililoandikwa kihindi na likiwa na picha za wanawake warembo. Geti dogo sehemu ya lile kubwa, lilisukumwa na mwanamume mfanya mazoezi, akaingia ndani. Nami nikavuka barabara haraka na kuzunguka upande wa nyuma, nikaruka na kujivuta juu ya ukuta kwa kiwango cha kuwezesha macho yangu kuona. Nikaona kuna nyumba mbili, moja ilikuwa upande wa kulia na nyingine ilikuwa mbele. Ile ya upande wa kulia ilikuwa ndogo kwa makadilio, pengine ilitosha kuwa na vyumba viwili na sebule. Humo aliingia Akshay. Niliitazama ile nyumba kubwa, nikagundua ilikuwa ni sehemu iliyofanya biashara fulani, hata hivyo sikuweza kutambua ilikuwa biashara ya aina gani. Nilishuka nikaendelea na mazoezi ya kukimbia nikirejea katika makazi yangu ya muda.

** ** **​

Ilikuwa jioni yenye makelele mengi. Nikiwa nimevalia suti nyeusi, nilionekana bonge la bwana. Nilikaa katika kiti cha nyuma ndani ya gari dogo nililolikodi linipeleke mahali pale alipoishia Akshay asubuhi.

Dereva alinifikisha, nikamlipa pesa yake kisha nikashuka. Sasa nikawa natazamana na geti kubwa lililoandikwa Kihindi na kupambwa kwa picha za warembo. Nikiwa natafakari kama nitafute mtu anipe tafsiri ya maneno yale, alikuja jamaa mmoja mhindi, akasukuma lile geti dogo na kuingia ndani mle, nami nikafanya hivyohivyo tukawa tumeongozana. Japo palikuwa na walinzi kando, jamaa aliwapita bila kuwasabahi, nami nikafanya hivyo. Alitembea mpaka katika ile nyumba kubwa, akasukuma mlango wa kioo na kuingia ndani. Nami nilifanya hivyo nikawa ndani ya jumba lile.

Nilishangazwa na nilichokiona katika chumba cha kwanza, kilikuwa chumba cha vioo hivyo aliyekuwamo ndani alionekana. Alikaa binti mrembo sana Mhindi. Alikaa katika sofa akitabasamu sana, nyuma yake palikuwa na kitanda kilichotandikwa vizuri. Nikasogea chumba cha pili, nacho hivyohivyo, alikaa msichana mwenye asili ya Ufilipino sifa za muonekano wa chumba kama kile cha kwanza!

Nilitembea nikitazama warembo wale chumba kwa chumba. Mpaka sasa niliona wasichana wahindi wengi zaidi, wafilipino kiasi na dada zangu kutoka Afrika, niliwaona wanne. Nikaendelea kuzunguka nikitazama hapa na pale, huyu na yule.

Lakini sasa ukafika wakati ambao niliusubiri kwa muda mrefu. Kumuona tena mtu niliyemtafuta, mbele ya kioo, nilimuona Asi, kakaa katika sofa, kavaa mavazi ya kahaba, lakini tofauti na wenzake wote, Asi hakutabasamu, dalili za msichana aliyelazimishwa kufanya kazi ya kuukejeli utu wake. Kwa kuwa nilivaa barakoa, hakuweza kunifahamu, pia, hakuwa na muda wa kutazama watazamaji, alijiinamia mwenye mengi mawazo.

Inaendelea...

Kuwa wa Kwanza Kupokea mwendelezo wa Riwaya hii Kwa kujiunga katika Group la bure WhatsApp, Gusa Hapa Kujiunga

Tupate Wadhamini:

Kwa Mahitaji ya kuandikiwa CV, Barua ya Maombi ya Kazi na Masomo kwa Wanafunzi wanaorudia mitihani, Gusa Hapa Tuwasiliane Whatsapp.
Mambo yananoga bwana
 
Back
Top Bottom