Rwanda wamepiga marufuku "Adhana" Alfajiri

Rwanda wamepiga marufuku "Adhana" Alfajiri

Rwanda wamepiga marufuku vyote hivyo. Ukute hata masuala ya mashindano ya dini au matamasha ya kwaya uwanjani kama kwa mkapa isingewezekana huko
Hawachelewi kusema hio Ni mikusanyiko isiyo na kibali na yenye malengo ya kuchochea uvunjifu wa amani Hahah.
 
Kwa hili Rwanda nawapongeza sana, zile kelele za alfajiri zinakera sana.

Hii ni Taharifa ya BBC...

Waislamu wanaoadhimisha mwezi mtukufu wa Ramadhani nchini Rwanda hawasikii adhana wakati wa swala ya asubuhi, na huenda wasisikie tena, kutokana na marufuku iliyowekwa na mamlaka nchi humo.

-

Mwezi uliopita mamlaka ilipiga marufuku matumizi ya vipaza sauti kwenye misikiti asubuhi na mapema, ikisema kuwa ilikiuka sheria za uchafuzi wa kelele ambazo zinakataza kelele zaidi ya decibel 55 wakati wa mchana na decibel 45 usiku katika maeneo ya makazi.

-

Mamlaka ya Rwanda inasema kuwa wakaazi walilalamika kuhusu mwito wa mapema wa maombi - ambao hufanyika majira ya alfajiri na huchukua kama dakika mbili au tatu. View attachment 2188599

Sent from my Redmi Note 9S using JamiiForums mobile app
Rwanda si Tanzania....

Wala Rwanda si kigezo cha kuigizwa na kila mtu.....

Tuwaige watu waliomwagana danu kisa ya PUA NDEFU na PUA PANA FUPI ?!!!

Nakukumbusha baba wa taifa alileta UJAMAA WA KIAFRIKA akasema hawezi kusimamisha UKOMUNISTI kwa kuwa UKOMUNISTI unapinga DINI...naye ni mkatoliki....na akina AbdulWahid Sykes ,Mshume Kiate ,Mashado Plantan ,Ally Sykes ,Mzee Rehani ,John Rupia na wazee wale wenye kupenda DINI ZAO walipambana naye bega kwa bega......

#siempre JMT🙏
 
Mengine yana-record maombezi Yao ya mchana kutwa na kwaya zao halafu wakisepa Ile usiku wanaachia Yale maombezi Yao kwa hewa kwny Yale maspika yao, zinapigwa usiku kucha huku wamefunga kanisa Lao na kufuli.Asubuhi wanakuja kufungua kanisa na Maisha yanaendelea 😄😄😄.
Yani tanzania tunavumiliana sana watu hawajali kama usku watu wanataka kulala yani hawajali. We unaachaje maspka yamapga kelele usku kucha
 
Huu msimamo ungekuja na hapa bongo

Sema CCM hawatalikubali maana wao na hao wenye dini lao ni moja
Hahah Hilo halitawezekanika chief,kumbuka kwny kampeni zetu Hawa viongozi wa dini hua wanakua na 'kazi maalumu'.
 
Yaani wale wazee waliopambana Vita vya majimaji kutoka UNGINDONI ,UMATUMBINI ,UNDENGEREKONI,LIWALE ,KILWA MASOKO walipambana ili siku moja TANZANIA imuige KAGAME...huyu Kagame huyu?!!! kupiga marufuku wito wa swala ya alfajr ?!!! 😳😳😳

What a joke 🤣🤣🤣

#Siempre JMT🙏
 
Tuache mambo ya Wakristo ama Waislamu. Point ni kwamba, unapofanya kazi zako, fikiria watu wanaokuzinguka pia. Usijifikirie wewe mwenyewe. Kazi zako zisisumbue watu wengine. Uwe na baa ama club, uwe Mbudha, uwe Mkristo ama uwe Muislam ama mpagani. Umeelewa?
Una uhakika huyo Kagame amezuia kelele zote au unaunga tu mkono Uhuru wa kuabudu kuminywa? Hao wanasiasa, wakati wa kampeni hawatafunga speaker mitaani? Ambulance zitatembea bila sauti? Misafara Yao itaendeshwa kimya kimya? Ndege zao hazina kelele? Hazishuki alfajiri?

Ni upuuzi kufurahia Uhuru wa namna yeyote ile kuminywa, iwe unakugusa au haukugusi.
 
Yani tanzania tunavumiliana sana watu hawajali kama usku watu wanataka kulala yani hawajali. We unaachaje maspka yamapga kelele usku kucha
Na ukienda kulalamika inaonekana wewe Ni atheist.
 
Mungu hawezi kujilipua

Maana hayupo

Ndiyo hujawahi "kumuona" Mungu akijipigania

Ni binadamu,wafuasi wa dini ndiyo hupumbana kumpigania wakati yupo "mbinguni"

Mimi siyo mfia dini kaka.
Na siamini katika Mungu.
 
Safi sana. Nafikiri hii pia ifatwe huku kwetu wasisahau na makanisa pia. Kila kitu kufanyikie ndani ya nyumba ya ibada kwa utulivu.

Makongamano na miadhara ya dini zote ipigwe marufuku. Wahubiri kwenye vyombo vya usafiri wa uma na maeneo ya uma pia piga marufuku
 
Back
Top Bottom