Saa 3 usiku mpaka saa 11 asubuhi simu inatumika

mimi nlkua nachat na mwanamke wangu tunafanya kazi sehemu moja na tumetoka kuinana muda si mrefu mara ghafla akawa kimya sms hajibu nkapiga simu ikapokelewa na mwanaume like anamwambia bibie ongea..Hakuongea kitu nilijarbu kumpgia simu mara kadhaa haikupokelewa tena hadi baada ya kupita saa moja kasoro.
Akanitafuta yeye akidai kuwa alichomolewa simu kwenye daladala ikabd nmuelekezi mahali nilipo akanifuata nikachukua ile simu na kukaa nayo kwa muda wa siku mbili sikupata majibu nlotarajia kwamba may be kuna mtu atamtafuta.
still tupo kweny mahusiano lkn now namega kisela tu sina future nae coz kuna alert imeshagonga akilin mwangu
 
Unajua mambo ya mapenzi hayashauriki. Hapa tunaweza muambia aachane nae kumbe usiku halali. Ataamua yeye afanyaje.
Bora achukue maamuzi magumu now, kuna manzi ashawahi nitesa kwa ujinga huu wa hivhiv mind games za kipuuzi.
 
Hongera,jiepushe kutengeneza single maza
 
Na usijaribu kuwaza tofauti, ukweli tyr umeshauhisi na ndivyo ilivyo
 
Abbort mission, over
 
sasa akikwambia amelala na mwanaume mwingine itakusaidia nini 🐒

amekublock bahati mbaya umekubali na umeridhika...

pia atakwambia amelala na mwanaume mwingine bahati mbaya tena inaonekana utakubali na utaridhika....

sasa si afadhali ukae kimya tu kama huoni, wala huhisi chochote katika hali hiyo 🐒
 
Na usijaribu kuwaza tofauti, ukweli tyr umeshauhisi na ndivyo ilivyo
Hivi una mahusiano ambayo yamedumu walau kidogo? Inaonesha toka uumizwe na huyo mwanamke wako umeingia sumu. Utakua ndio wale ukituma sms haijajibiwa kwa wakati basi unapiga chini. Kama jibu ni ndio basi usipokua makini utakua na chain ndefuu ya mahusiano.
 
Hapana, ila napenda kuwa alert watu kuhusu hii michezo, nikiwa muhanga mojawapo, wanawake wengi sana wanachezea watu kisaikolojia and it's seen normal. Mm sipendi watu feki.. kuna utofauti wa bahati mbaya na hizi scenario za kipuuzi.
 
Pole sana Juma, nimewahi kupitia mazingira kama yako kwa mwanamke mmoja hivi, alinipitisha kwa awamu tatu.

Nilimpenda sana yule mwanamke na nilikuwa nagharamia, kitu ambacho mpaka sasa nikikaa na najilaumu ni kwamba, nilishaona dalili zote za tamaa za maisha zinazopelekea yeye awe malaya lakini nikajipa moyo atabadilika nikawa nasamehe na kuendelea na maisha.

Brother, huyo mwanamke hayo ndo maisha yake, hapo sana sana kuna muda atajifanya kubadilika ili upate imani kwamba amebadilika na amekuwa mtu mwema, na hapo kuna mawili, yamkini ameachana na huyo bwana wake au kuna kitu anatafuta kwako mfano ndoa, fedha n.k

Kuna mdau amekushauri hapo juu kwamba ni vyema ukaachana nae sasa hivi sababu huko mbeleni utakuja kupata maumivu makali zaidi kuliko hivi sasa. Jamaa amesema ukweli sababu hata mimi ndicho kilichokuwa kimenitokea. Ukimsamehe mwanamke inamjengea imani kwamba wewe ni dhaifu kwake ameshakuweza, hapo atajipa uhakika wa kufanya lolote lile kwako, achana na huyo mwanamke mapema ila nakuahidi kuna nyakati atakukumbuka, anaweza akakutafuta kukwambia ukweli kwamba anakukumbuka kwa mazuri yako au akapiga kimya ila ipo siku atakukumbuka.

Achana naye.
 
Hawa wanawake ni pasua kichwa sana. Nachoshangaa ni mtu kufanya kosa halafu haonekani kujutia
 
Ushauri wa nini tena mkuu? Hapo nini hujaelewa? Alafu nyie vijana wa siku izi sijui mpo namna gani yani sasa hivi kila kijana anataka ushauri wa mapenzi hivi mnakuwa mpo serious au mnachangamsha jukwaa?
 
Ukiendelea nae, usitusumbue tena, huna akili.
 
Ahsante sana Bro. Sasa nimemwambia abaki kuwa rafiki yangu. Naona amekuwa mkali hivi eti ni kwa sababu alishanivulia nguo ndio maana nimeamua hivi. Kwamba alipanga aje tuonane anipe ushahidi. Hivi unablock namba za watu, ghafla unashangaa mtu ambaye kila siku lazima akutafute hajakutafuta. Haifikishi?

Amesema kwa kuwa nimeamua tuwe marafiki SAWA na anaonekana hajajutia. Anajutia kwa jicho la mbali kwa kuwa nimemgonga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…