Safari za Rais Jakaya Kikwete tangu aingie madarakani 2005

Safari za Rais Jakaya Kikwete tangu aingie madarakani 2005

sasa kama amesafiri mara 313 tukiweka zilsafari ambazo alikua anakaa zaid ya siku3 si lazima itafika na kuzidi 365, manake kapoteza zaidi ya mwaka
kataika safari.
 
Nchi hutafunwa na wenye Meno, Safari nyingi, zinagharimu pesa Nyingi pia, tena hizo pesa ni zetu sisi walalahoi na wavuja jasho. Tanzania ni nchi Masikini sana, kama kweli hizo safari zingepunguzwa jamanii, hizo pesa sizingesaidia hata kununulia Madawa mahospitalini au Vitabu mashuleni?
 
Kesho tar 9/9/2011 rais atasafiri kuelekea Kenya kwa ziara ya kikazi!
Hiyo ni safari ya 316 tangu rais aingie madarakani mwaka 2005!
 
Tunaomba mtuwekee na siku alizokaa uko nje ya nchi!
 
Tatizo siyo safari kinachotakiwa ni kuoanisha gharama zinazotumika kufanya safari hizo na hali ya uchumi wa nchi . Takwimu zinaonyesha mzee wa magogoni amesafiri safari nyingi sana kweanda maeneo mbalimbali nje ya nchi kwa shughuli za kakazi na mausino . lakini mpaka sasa hakuna chochote ambacho watanzania wamenufaika kutokana na safari hizo'' ikiwa ni pamoja na kuona hali ya uchumi wa nchi ikizidi kuwa mbaya sambamba na kushuka kwa thamani ya shilingi ya tanzania ukilinganisha na kenya katika soko la dunia hivyo kuruhusu mifuko ya bei za bidhaa kuwa juu na kusababisha kuzolotesha hali za maisha ya watanzania '' penginepo anapashwa kukaa chini na kubuni njia mbadala ya kutatua matatizo kuliko kusafiri kwenda nje ya nchi bila mafanikio na feha hizo zikaelekezwa kuboreshwa secta yeyote muhimu kutokana na vipaumbele vilivyopo.
 
Kesho tar 9/9/2011 rais atasafiri kuelekea Kenya kwa ziara ya kikazi!<br />
Hiyo ni safari ya 316 tangu rais aingie madarakani mwaka 2005!
<br />
<br />
Mkuu record yako haipo sahihi, nadhan hii safari ya 319, ile ya canada ambayo imekuwa postponed kutokana na huu msiba uliotokea zenji itakuwa ya 320, sa7a fanyeni juu chini tupata idadi kamili ya siku zilizotumila katika safari zote, ni muhimu kwa kumbukumbu na kwa faida ya kizazi kijacho! Yeah ni muhimu coz kila rais anatalent yake!
 
Pamoja na data hizo za nguvu bado mstaafu Mkapa jana amemtetea huko kwenye kufungua kampeni za uchaguzi mdogo Igunga. Kwa kweli fani ya siasa inadhalilishwa na wasio na soni!
 
...Jakaya Khalfan Mrisho (Kikwete); alikuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Mheshimiwa Ben Mkapa kwa miaka kumi (10 yrs), 1995 hadi 2005! Tamaa ya kusafiri huku, kule na pale ilkuwa kwenye "ndoto pevu" ya Mheshimiwa Jakaya Kikwete kwa muda mrefu...! Hata kama ni mtu wa matanuzi; hawezi kutanua akiwa Bongoland, ni lazima aruke na au aelee hewani na atembelee kwenye "vioja" vya dunia...aende akaone kile asichokiona; na akatembelee sehemu maarufu kwa "matanuzi".

Wakati wengine wanakuna "vichwa" katika kutafuta suluhisho la matatizo ya uchumi, jamii na siasa ya wananchi wao; Mheshimiwa JK anapasua anga za kimataifa...! Kama amefikisha safari kama 313 hivi, kuna uwezekano hadi anamaliza kipindi chake (2015) anaweza kusafiri zaidi ya 350+...Hii inaweza kuingizwa kwenye Guinness Book of Records (ya Tanzania) kwa kuwa hakuna Rais kuanzia Awamu ya Kwanza hadi ya Tatu aliyewahi kufanya safari kama mh. JK!

Nadhani sasa kuna kila sababu kurejea kauli ya Prof. Lipumba aliyesema wakati wa kampeni za 2005 kwamba, "Kikwete ni msanii; anafaa apewe wizara ya utamaduni na michezo kwa kuwa anapenda starehe." Inawezekana wakati ule Prof. Lipumba alionekana "msanii" au zilionekana ni "chuki za kisiasa" na alipuuzwa! Leo watu wanashangaa kwa trip za Mheshimiwa JK ambazo zinatia fora...! Tusubiri tuone; miaka mine iliyobakia si mingi tuendelee kuhesabu safari na tupeane taarifa juu yake!
 
hivi wakubwa nifafanulieni kidogo, hizo Nisafari au idadi ya siku alizokaa nje? na kama ni safari tu, je wastani wa siku alizokaa huko kwa kila safari ni ngapi?
 
Mmh! We mchokozi. Mie simo.
Mheshimiwa wa magogoni alisafiri kinyemela bila kutuaga waajili wake na kwenda Juba South Sudani kwenye birthday ya taifa hilo!&amp;amp;lt;br /&amp;amp;gt;&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Hiyo ni safari ya 313 ta awe rais wa tz mwaka 2005!&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Mpaka leo tarehe 23/8/2011 tayari amesha safiri safari 315 tangu aingie magogoni octoba mwaka 2005!&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Hii ni rekodi ya kipekee duniani ambayo watz tunatakiwa kujivunia na kutembea kifua mbele maatako nyuma!!!<br />
<br />

UDATEs!

Kesho tar 9/9/2011 rais atasafiri kuelekea Kenya kwa ziara ya kikazi!<br />
Hiyo ni safari ya 316 tangu rais aingie madarakani mwaka 2005!
 
Mheshimiwa wa magogoni alisafiri kinyemela bila kutuaga waajili wake na kwenda Juba South Sudani kwenye birthday ya taifa hilo!&amp;amp;lt;br /&amp;amp;gt;&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Hiyo ni safari ya 313 ta awe rais wa tz mwaka 2005!&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Mpaka leo tarehe 23/8/2011 tayari amesha safiri safari 315 tangu aingie magogoni octoba mwaka 2005!&amp;lt;br /&amp;gt;&lt;br /&gt;<br />
Hii ni rekodi ya kipekee duniani ambayo watz tunatakiwa kujivunia na kutembea kifua mbele maatako nyuma!!!<br />
<br />

UDATEs!

Kesho tar 9/9/2011 rais atasafiri kuelekea Kenya kwa ziara ya kikazi!<br />
Hiyo ni safari ya 316 tangu rais aingie madarakani mwaka 2005!

Ni muhimu kwa Rais kufanya safari nyingi kwa kipindi hiki alichokuwepo madarakani ili kuiunganisha Tanzania na mataifa. Taifa limegundua kwamba Katka East Africa na Afrika kwa ujumla Tanzania ni miongoni mwa nchi za mwisho kwa kutofahamika kimataifa. Kwa mfano Tanzania ni miongoni mwa nchi kubwa (Eneo, idadi ya watu, maliasili n.k) lakini huwezi kuamini kuwa utafiti ulipofanyika katika nchi za Ufaransa, Uingereza, Ujerumani, Marekani, Saudi Arabia, India, China na New Zealand, Tanzania ilishika mkia kwa wananchi wa nchi hizo kuifahamu (miongoni mwa Kenya, Uganda, Somali, Burundi, Rwanda, Zambia, Msumbiji, Sudan, Ethiopia, Eritrea, na djibout.) ispokuwa huko China na India ambako ilishika nafasi ya Tatu.

Uhusiano wa kimataifa ni muhimu sana katika kukuza uchumi wa nchi hasa katika kipindi hiki cha utandawazi. Uchumi na Siasa ni vitu vinavyoenda pamoja na nyakati za Ujamaa tulielekeza macho yetu sana katika nchi za Kikomunist kama Rusia , Korea ya Kaskazini, kuba na China. Leo nchi hizo zote zenyewe zipo katika hali ngumu na kimsingi hatufaidiki sana na nchi hizo pengine China tu. Na si vizuri katika kipindi hiki kwa nchi moja kuwa na monopoli katika nchi nyingine, kwa sababu nchi zinozopenda kufanya biashara nasi lazima ziwe katika ushindani. Na mtazamo wa Tanzania kwa muda huu ni kuzichanganya kati ya nchi zilizoendelea na nchi na zile za kati kama Turky, Iran, Brazil, Mexico, Venuzuela, korea ya kusini, uhispania, Poland. Uzuri wa nchi hizi za kati ni kwamba, ziko tayari zaidi kuuza Teknlojia yaondogo waliyokuwa nayo kuliko nchi zilizoendelea. Leo hii Turky, Korea kaskazini, Brazil na Iran ndio wauzaji wakubwa wa Teknolojia ya kati kuliko nchi zilizoendelea. Na demand yake katika nchi za Afrika ni kubwa sana, na ni lazima kuifuata huko huko iliko.

Tatizo la Thread hii haijazingatia ni nini kinachopatikana katika safari za Rais bali imezingatia Idadi ya safari alizozifanya kwa kipindi alichokuwepo madarakani. Hili ni Tatizo la kutokuona mbali, na ni moja kati ya tatizo kubwa la Wana JF. Hii inanikumbusha filamu ya Senior Bachelor pale mke wa Erick alipomlaumu kwa kutokaa nyumbani. Erick alimuomba achague moja kati ya mawili, Au yeye akae siku nzima nyumbani na waishi katika umasikini ule wa zamani au amruhusu akachachalike huko nje na kurudi nyumbani na chochote. Mke wake hakuwa mjinga, alikaa kimya ndipo Erick alipopata jibu kuwa umasikini hautaki, na akaendelea kuchachalika nje. Na wanaJF wanamawili ya kuchagua kati ya... na ....

Populist Thread hazitatusaidia hapa JF wala kwa maendeleo ya nchi yetu. Kwa sababu watanzania wengi hapa JF WAMELALAMIKA KUWA TANZANIA HAIFAHAMIKI HUKO NJE. Leo juhudi mbali mbali zinafanyika ikiwa pamoja na kuisuka timu yetu ya Taifa ya mpira wa miguu, Kukuza Viwango vya Filamu zetu, leo zinaangaliwa na nchi nyingi Afrika n.k. Zote hizi ni katika juhudi za za kuipandisha chati Tanzania.

Kwa machache haya na kwa tathmini ya yale tuliyoyapata kwa safari za Rais, ninaziunga mkono safari zake zote na rais ajaye mwaka 2015 aendeleze uhusiano na nchi hizo na ikibidi naye asafiri.
 
Ni muhimu kwa Rais kufanya safari nyingi kwa kipindi hiki alichokuwepo madarakani ili kuiunganisha Tanzania na mataifa. Taifa limegundua kwamba Katka East Africa na Afrika kwa ujumla Tanzania ni miongoni mwa nchi za mwisho kwa kutofahamika kimataifa. Kwa mfano Tanzania ni miongoni mwa nchi kubwa (Eneo, idadi ya watu, maliasili n.k) lakini huwezi kuamini kuwa utafiti ulipofanyika katika nchi za Ufaransa, Uingereza, Ujerumani, Marekani, Saudi Arabia, India, China na New Zealand, Tanzania ilishika mkia kwa wananchi wa nchi hizo kuifahamu (miongoni mwa Kenya, Uganda, Somali, Burundi, Rwanda, Zambia, Msumbiji, Sudan, Ethiopia, Eritrea, na djibout.) ispokuwa huko China na India ambako ilishika nafasi ya Tatu.

Uhusiano wa kimataifa ni muhimu sana katika kukuza uchumi wa nchi hasa katika kipindi hiki cha utandawazi. Uchumi na Siasa ni vitu vinavyoenda pamoja na nyakati za Ujamaa tulielekeza macho yetu sana katika nchi za Kikomunist kama Rusia , Korea ya Kaskazini, kuba na China. Leo nchi hizo zote zenyewe zipo katika hali ngumu na kimsingi hatufaidiki sana na nchi hizo pengine China tu. Na si vizuri katika kipindi hiki kwa nchi moja kuwa na monopoli katika nchi nyingine, kwa sababu nchi zinozopenda kufanya biashara nasi lazima ziwe katika ushindani. Na mtazamo wa Tanzania kwa muda huu ni kuzichanganya kati ya nchi zilizoendelea na nchi na zile za kati kama Turky, Iran, Brazil, Mexico, Venuzuela, korea ya kusini, uhispania, Poland. Uzuri wa nchi hizi za kati ni kwamba, ziko tayari zaidi kuuza Teknlojia yaondogo waliyokuwa nayo kuliko nchi zilizoendelea. Leo hii Turky, Korea kaskazini, Brazil na Iran ndio wauzaji wakubwa wa Teknolojia ya kati kuliko nchi zilizoendelea. Na demand yake katika nchi za Afrika ni kubwa sana, na ni lazima kuifuata huko huko iliko.

Tatizo la Thread hii haijazingatia ni nini kinachopatikana katika safari za Rais bali imezingatia Idadi ya safari alizozifanya kwa kipindi alichokuwepo madarakani. Hili ni Tatizo la kutokuona mbali, na ni moja kati ya tatizo kubwa la Wana JF. Hii inanikumbusha filamu ya Senior Bachelor pale mke wa Erick alipomlaumu kwa kutokaa nyumbani. Erick alimuomba achague moja kati ya mawili, Au yeye akae siku nzima nyumbani na waishi katika umasikini ule wa zamani au amruhusu akachachalike huko nje na kurudi nyumbani na chochote. Mke wake hakuwa mjinga, alikaa kimya ndipo Erick alipopata jibu kuwa umasikini hautaki, na akaendelea kuchachalika nje. Na wanaJF wanamawili ya kuchagua kati ya... na ....

Populist Thread hazitatusaidia hapa JF wala kwa maendeleo ya nchi yetu. Kwa sababu watanzania wengi hapa JF WAMELALAMIKA KUWA TANZANIA HAIFAHAMIKI HUKO NJE. Leo juhudi mbali mbali zinafanyika ikiwa pamoja na kuisuka timu yetu ya Taifa ya mpira wa miguu, Kukuza Viwango vya Filamu zetu, leo zinaangaliwa na nchi nyingi Afrika n.k. Zote hizi ni katika juhudi za za kuipandisha chati Tanzania.

Kwa machache haya na kwa tathmini ya yale tuliyoyapata kwa safari za Rais, ninaziunga mkono safari zake zote na rais ajaye mwaka 2015 aendeleze uhusiano na nchi hizo na ikibidi naye asafiri.

Kujulikana kwa nchi hakufanywi kwa Rais kusafiri sana bali ni kazi ya balozi zetu zilizoko nchi za nje; hata hivyo hoja yako haina nguvu kwasababu Mkweree yeye anapenda safari za Kwenda United States na Europe kwa sana tu[ ingefaa iorozeshwe ili tujue toka aingie marakani amekwenda mara ngapi marekani na Ulaya] hivyo hoja sio kuitangaza nchi bali ni kustarehe yaani usharobaro!! Kwavile safari zenyewe hazina tija nchi itafaidika zaidi kama huyu Mkweree asingekuwa anasafiri, kwani zile fedha lukuki anazozitumia na wapambe wake zingetumika kwa mambo mengine ya msingi huko nyumbani kama vile kuwanunulia madawati wanafunzi badala ya kungoja mpaka Mwanaidi Sinare Maajar aanzishe foundation ya kuwanunulia madawati watoto!!
 
me nadhani mkuu wa kaya huwa hajisikii vizuri bila kupaa angani.
 
Kujulikana kwa nchi hakufanywi kwa Rais kusafiri sana bali ni kazi ya balozi zetu zilizoko nchi za nje; hata hivyo hoja yako haina nguvu kwasababu Mkweree yeye anapenda safari za Kwenda United States na Europe kwa sana tu[ ingefaa iorozeshwe ili tujue toka aingie marakani amekwenda mara ngapi marekani na Ulaya] hivyo hoja sio kuitangaza nchi bali ni kustarehe yaani usharobaro!! Kwavile safari zenyewe hazina tija nchi itafaidika zaidi kama huyu Mkweree asingekuwa anasafiri, kwani zile fedha lukuki anazozitumia na wapambe wake zingetumika kwa mambo mengine ya msingi huko nyumbani kama vile kuwanunulia madawati wanafunzi badala ya kungoja mpaka Mwanaidi Sinare Maajar aanzishe foundation ya kuwanunulia madawati watoto!!

Marekani na Ulaya ndio Dunia, ukiwaweka sawa hawa ndio nchi yako ina uhakika wa kaamani unakojivuniana na kuuiweka sawa uchumi wetu. Jamani tuache kuandikia mawe wakati kalamu zipo kwani unapolia kuwa MIKATABA YA UCHIMBAJI WA DHAHABU TUMELIWA, unazungumzia Ulaya, Marekani na marafiki zao, LADA (BAE), ununuaji wa silaha, unapozungumzia kumtoa Gadaffi unazungumzia Ulaya na Marekani, Mgogoro wa Israel na Palestina ni hao hao, Just name it. Sasa mnahitaji aende wapi kama sio shinani.

Hizi nchi za kati wao wenyewe wanatafuta marafiki kwa hiyo hakuna haja ya kukimbia sana kwenda Turky,Brazil na Iran kwa sababu wenyewe ndio wanakuja kwetu. Unajua Marais wa Marekani na Uchina walikuwa hawana kawaida ya kuitembelea Afrika, lakini kwa kipindi cha miaka 15 tumeona safari za akina Bill Klinton, Bush na Zao Jintao wa China kuja Afrika ikiwa pamoja na Tanzania. Napenda kukueleza kitu kimoja kila kitu huenda kwa wakati wake na pale kwenye Demand. Kama Marais wa Nchi kubwa kama hizo wanakuja Tanzania sasa unatarajia Rais wa Tanzania aende mara ngapi huko.

Unasema safari hazina Tija, Hebu nieleze angalau safari 5 tu za JK na madhumuni yake na alifanya nini huko ili nami nikujibu. Usifanye kama wengi hapa JF kukurupuka na kutafuta maneno ayapendaye tu bila uthibitisho na kuyaweaka hadharani kama hilo neno ' Haina Tija'. Nasema hivi kwa vile mimi ninavithibitisho vya maandishi juu ya safari zake Marekani na ulaya amefanya nini, na nini alichobakiza Kilicomfanya arudi tena na tana.

Umetamka juu ya Mabalozi, ni vyeme na sahihi kabisa Lakini ujue kwamba Balozi huanzisha na kuendeleza mazungunzo husika mpaka kikomo chake. Panapobaki ni sehemu ya kiongozi wa nchi. Kwa mfano Balozi hawezi kutia saini ya mkataba wa nchi na nchi, hapo huhitajika KIONGOZI WA JUU. Pengine uchakachuaji wa mikataba ya LDA, MADINI, MINARA MIWILI n.k ndiko kulikomfanya Raisi kutowaamini aliokuwa akiwaamini. kWA SABABU HATA HIYO MIKATABA MIBOVU YA MADINI INAYOIPATIA tz 3% kuna waliosaini na wana 10% mpaka leo.

Kifupi hujui kwa hatua aliyoichukua Raisi amaokoa sh ngapi za uchakachuaji wa mikataba. Kwa taarifa yako kwa mikataba tu ambayo Tanzania imeingia wakati wa kipindi cha miaka 10 ya mkapa inaiingizia Taifa hasara ya $2 bilioni kila mwaka. Na hiyo ndio gharama ya kusamehewa deni la $8 bilioni. Kwa lugha nyepesi ya kibiashara ni kwamba kama tusingekubali kufutiwa deni na kutoingizwa katika mikataba hii ya Kalpeters, tungeweza kulipa deni la $8 bil kwa miaka 4. Haya ni mahesabu rahisi.

Tulilojifunza katika ile ya kusamehewa deni ni kwamba, Mzungu hafanyi biashara ya hasara. Nilikuwa na mashaka toka mwanzo juu ya hii deal pale ambapo INDIA ilikataa ofa hiyo na kusema watalipa deni lao pole pole. Ukiona wajanja wanakataa OFA jiulize sana kama hiyo OFA inalipa au la. Ama kweli Mkapa alikuwa YELTSIN WA Tanzania.
 
Back
Top Bottom