Sahihi kusema Arusha ndio Jiji bora Tanzania?

Sahihi kusema Arusha ndio Jiji bora Tanzania?

Ni kweli Arusha ni pazuri ila mimi kusema kweli palinikataa lile vumbi na baridi la pale! Hapana Dar ndo naona nikikaa nakaa vizuri!
wamepaboresha mno sasa hivi barabara nyingi ni lami tu
kuanzia mjini hadi ngusero
mjini hadi njiro atomic
chekereni hadi usa
barabara zote za levolosi ngarenaro na makao mapya sasa ni lami tu
karibu tena Arusha hakika utapapenda sana
 
Ukiondoa hali nzuri ya hewa, Arusha ni jiji la ovyo kabisa. Nyumba za ovyo zipo hadi ndani ya CBD, barabara ni nyembamba na hazina hadhi. Barabara nyingi hazina lami nenda makao mapya uone vumbi la ugoro. Arusha ndani ya miaka 60 ya uhuru inafaa kuitwa squalor of Africa
ukienda makao mapya barabara zote zile sasa ni lami mkuu na zinawaka taa usiku
karibu tena
 
ngoja tu utaskia mtu anasema hapa Arusha mara wachagga
kuna kikundi flan aka gang sitaki kukitaja wana inferiority Complex ajabu wakiskia Arusha wanawashwa balaa 🤣🤣
ngoja tuwasubiri
Mkuu usifikiri watu wana inferioritycomplex hapana hata kidogo lakini ujue arusha kama haikuweza kuizidi mikoa mingine kama mwanza usitegemee leo hii arusha ikaizidi ka sababu kipindi cha nyuma jamii ya kanda ya ziwa ilikuwa nyuma kwenye sekta nyingi kama elimu na uenzi laini saizi mambo yako tofauti sana ukienda leo kiiini huko usukuma na kanda ya ziwa kwa uumla utakutana na nyumba kali sio za bati tu bali za msouth. Kwa hiyo construction industry kwa upande wa mwanza ni kubwa kuliko arusha ukitaka kujua angaliamji na senta za kanda ya ziwa zinavyobadilika kwa kasi kubwa.
 
Mkuu sio kweli ukisemacho... Morombo ipi unayosema ina lami hadi intel?
naomba kufahamu unaishi wapi
ila Morombo gadi dampo hadi intel kote ni lami mpya nzuri na ina taa za barabarani hadi kuonganisha na barabara ya east Africa
 
Mkuu usifikiri watu wana inferioritycomplex hapama hata kidogo lakini ujue arusha kama haikuweza kuizidi mikoa mingine kama mwanza usitegemee leo hii arusha ikaizidi ka sababu kipindi cha nyuma jamii ya kanda ya ziwa ilikuwa nyuma kwenye sekta nyingi kama elimu na uenzi laini saizi mammbo yako tofauti sana ukienda leo kiiini huko usukuma na kanda ya ziwa kwa uumla utakutana na nyumba kali sio za bati tu bali za msouth. Kwa hiyo construction industry kwa upande wa mwanza ni kubwa kuliko arusha ukitaka kujua angali mji na senta za kanda ya ziwa zinavyobadilika kwa kasi kubwa.
ukiangalia population statistics kama nilivosema Arusha ilikua ya 9 hadi leo imekua ya 3
nnachoongelea ni huduma especially Private sector facilities
kama ningekua naongelea population dar imeizidi mwanza na Arusha zote kwa pamoja mbali mno sheik💪
 
naomba kufahamu unaishi wapi
ila Morombo gadi dampo hadi intel kote ni lami mpya nzuri na ina taa za barabarani hadi kuonganisha na barabara ya east Africa
Ni kweli ukisemacho... Ila kwa njia ya gari za morombo mpaka intel, lami inaishia boston car wash, icho kipande mpaka unapita mizani mpaka round bado ni vumbi tu, japo tayar kuna kibao cha ujenzi!
 
Kwani Mwanza kuna lami gani za mitaani za kusafiri zaidi ya hizo dkk ukiacha barabara kuu ya Shy, Airport na Musoma?
Barabara ya kilimahewa to nyasaka.
Barabara ya sabasaba buswelu via kanyerere
Barabara ya kisesa usagara
Barabara ya nyakato busweru to kahama
Barabara ya iseni to sauti
Barabara ya mkuyuni butimba nk nk

Zipo barabara nyingi sana mwanza
 
Ukiondoa hali nzuri ya hewa, Arusha ni jiji la ovyo kabisa. Nyumba za ovyo zipo hadi ndani ya CBD, barabara ni nyembamba na hazina hadhi. Barabara nyingi hazina lami nenda makao mapya uone vumbi la ugoro. Arusha ndani ya miaka 60 ya uhuru inafaa kuitwa squalor of Africa
Ni barabara ipi makao mapya ina vumbi mkuu? Mimi sijaiona hata
 
Toa ujinga wako hapa unaongea kwa ushabiki 🤣🤣🤣
 
Ni miaka 10 tu imepita tangu mji huu maarufu kama Geneva of Africa utangazwe kuwa jiji.

Kutoka kuwa mji wa 9 kwa wingi wa watu hadi kuwa mji wa 3 kwa sensa ya mwaka 2012 na halmashauri ya jiji ya pili kwa wingi wa watu, lakini licha ya upya wake.

Lakini ndio jiji lenye hospitali nyingi za Private kwa uwiano wa watu kuliko mji wowote Tanzania.

Ndio wilaya inayoongoza kwa Ufaulu kwa matokeo ya shule za msingi na sekondari kwa miaka minne mfululizo.

Arusha pia ina hoteli 5 zenye hadhi ya kimataifa.

Arusha inahudumiwa na viwanja viwili vya ndege.

Arusha ndio mji wa pili kwa kuwa na largest foreign community nje ya Dar same as real estate licha ya kuwa na moderate population.

Bila kusahau leisure facilities, shopping centers, office za kimataifa na hali ya hewa ya kustaajabisha inayoufanya mji huu kupokea asilimia 80 ya wageni wote wanaotembelea nchi yetu.

Je, ni sahihi kusema Arusha ndio sehemu bora zaidi ya kuishi Tanzania.

View attachment 2038839

View attachment 2038840

View attachment 2038841

View attachment 2038842

View attachment 2038843
.

View attachment 2039251
Ni jiji chafu pamoja na kuwezeshwa na serikali pamoja na jumuiya ya Afrika mashari kutengeneza miundo mbinu ya kisasa lakini wapi.

Kama mji kamejiwekeza maeneo mawili tu mjini kati na clock tower karibu na makao makuu ya jumuiya na AICC tofauti na majiji kama Mwanza ya Mbeya ambayo wakazi wake ndio wameyafikisha hapo bila nguvu za ziada za serikali kuwekeza.

Majiji yaliyowezeshwa kwa makusudi na serikali ni Dar, Arusha na Dodoma
 
Hujakatazwa kusifia na wewe cha kwako.

Cha kwangu kama hakikidhi siwezi cfia,,,lakini wa kaskazini most of them ni kucficfia tu, mara oh moshi inastahili kuitwa jiji 🤣🤣🤣 mnalijuwa jiji ninyi!!! Na kahama iitweje?
 
Back
Top Bottom