Sakata la Zumaridi na namna alivyokamatwa na polisi ni kichefuchefu, sheria haikuzingatiwa

Sakata la Zumaridi na namna alivyokamatwa na polisi ni kichefuchefu, sheria haikuzingatiwa

Mhalifu hawi mhalifu hadi pale itakapothibitika!

Sakata la mfalme Zumaridi (Kiongozi wa kanisa la Zumaridi huko Mwanza) Linaacha midomo wazi kwa wapenda haki na utii wa sheria!

Sipo hapa kumtetea Mfalme Zumaridi, Bali nashangaa namna ya uharamu wa ukamtaji!

Taratibu za ukamataji kwa mujibu wa sheria ziko wazi kabisa lakini mamlaka zimekuwa zikionesha kufeli Mara kwa Mara kutekeleza sheria hiyo jambo ambalo limekuwa likitweza utu wa watu wasio na hatia.

MFANO! mambo kama haya yalitokea huko mtwara hadi kufedhehesha uongozi wa polisi ambayo yalianza hihivi kwa kufumbafumba mambo,

Mfano 2. Ni huko ARUSHA Kuna taarifa ya askali mzalendo kulalamika kutaka kuuwawa na polisi wenzake kwa mambo Yale Yale kama ya mtwara na serikali iko kimya.

SASA NI HILI SAKATA LA TATU LINALOTIA KICHEFCHEFU

Ni TUKIO LA zumalidi Siku ya kwanza inaripotiwa kwamba polisi waliruka ukuta/geti ili kuingia kwa Zumalidi! Kitendo hiki kilitakiwa kulaaniwa na kila mtu! (Waliruka kwa Zumalidi kesho wataruka kwako)

Kama kulikuwa na ulazima wa kufika pale kwanini hawakufuata utaratibu wa upekuzi unavyotaka? Kwanini hawa kumshirikisha mwenyekiti wa mtaa/mjumbe? Kwanini waliruka ukuta kama jambazi! (VIPI KAMA ZUMARIDI ANGEJIBU MASHAMBULIZI KWA KUFYATUA RISASI KWA POLISI ALIYEVAA KIRAIA ALIPORUKA UKUTA?) Ina maana wangejibu kwamba walikuwa kwenye mapambano na majambazi au?

Kwa utaratibu walio utumia polisi hauna tofauti na utarabu wa kijambazi! Na hili linachangia sana siku hizi RAIA kutokutofautisha kati ya jambazi na polisi.

Tukiachana na mbinu ya ukamataji!

Riport ya polisi ina ukakasi mkubwa juu ya mtuhumiwa Zumaridi!

Kosa walilo utaarifu Umma kwamba anasafilisha BINADAMU 149, kosa hilo Linatia aibu nyingine!

Hivi tangu lini watu wanaokusanyika kusali pamoja imekuwa kosa la jinai?

Mbona jumuiya na taasisi kibao tunawaona wanakusanyika na kukesha na haijawahi kutajwa kuwa ni kosa?

Zumalidi kasafirisha binadamu kutoka wapi kwenda wapi kwa lengo gani? Kuna jinai gani pale?

Hapo taifa juzi wakatoliki walikusanyika mbona haikutamkwa kuwa ni usafirishaji wa binadamu?

Kina mwingira na wachungaji kibao Tanzania kila kutwa wanakusanya watu na haisemwi ni usafirishaji,

INAKUWAJE JAMBO LILE LILE LIWE HALALI KWA MWAMPOSA LAKINI LIWE HARAMU KWA ZUMARIDI?

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Nawashauri TAKUKURU WAINGILIE KATI!
Haiwezekani sheria zipo wazi, kwanini zisingefuatwa kama kweli ZUMALIDI anamakosa makubwa hivyo!

Mimi kwa utashi wangu nahisi sakata la Zumaridi lina maslahi binafisi!

TUKIRUHUSU HAYA YA UKIUKWAJI WA SHERIA HAKUNA ATAKAYEBAKI SALAMA!

Itakuwa mtu akikosana na polisi wanakuja kuluka ukuta! Na majambazi nao watatumia mwanya huohuo kufanya uharifu!
Pole sana muumini wa Zumaridi. Kikubwa huyo Zumaridi ana mapungufu makubwa sana ktk utendaji wake. Kwanza Polisi walipoingia mara ya kwanza hakupaswa wale watu wake wa mapepo wawatishie polisi, wewe nadhani uliona hao watu wake wenye majini walivyokuwa wanaruka kama vile wana weza kupambana na serikali. Pia kingine ujue mwanza kuna watu wanakuwa na biashara za viungo vya binaadamu kwenye mambo ya madini na uvuvi, jua kabisa polisi na vyombo vya usalama wana information za kutosha juu ya Zumaridi, kaa utulie mkuu wangu. Mimi simhukumu kwa sababu sina information ila kwa kitendo cha wafuasi wake wenye majini kuwatishia askari tena mmoja yule bonge alitoa bastola kidogo aanze kuitumia lakini akairudisha mfukoni. Asipoangalia Zumaridi atapotea kabisa ktk ulimwengu huu, maana onyo la kwanza alipewa kwa kufungiwa, alipaswa aufate utaratibu wa kibali na kuendesha ibaada zake kwa mujibu wa vibali.
 
Pole sana muumini wa Zumaridi. Kikubwa huyo Zumaridi ana mapungufu makubwa sana ktk utendaji wake. Kwanza Polisi walipoingia mara ya kwanza hakupaswa wale watu wake wa mapepo wawatishie polisi, wewe nadhani uliona hao watu wake wenye majini walivyokuwa wanaruka kama vile wana weza kupambana na serikali. Pia kingine ujue mwanza kuna watu wanakuwa na biashara za viungo vya binaadamu kwenye mambo ya madini na uvuvi, jua kabisa polisi na vyombo vya usalama wana information za kutosha juu ya Zumaridi, kaa utulie mkuu wangu. Mimi simhukumu kwa sababu sina information ila kwa kitendo cha wafuasi wake wenye majini kuwatishia askari tena mmoja yule bonge alitoa bastola kidogo aanze kuitumia lakini akairudisha mfukoni. Asipoangalia Zumaridi atapotea kabisa ktk ulimwengu huu, maana onyo la kwanza alipewa kwa kufungiwa, alipaswa aufate utaratibu wa kibali na kuendesha ibaada zake kwa mujibu wa vibali.
Kwahiyo polisi utaratibu walioufanya uko sawa?
Kwanini wamvamie?
Hao mabaunsa wa zumaridi wapole Sana walitakiwa wawatandike Askari wajifunze utaratibu.
Wameenda kizembe Sana eboo
 
Nakubaliana nawe kwa maana ya ukiukwaji wa sheria ila mfalme wako anakashfu imani za watu wengine kitu ambacho kinaweza sababisha uvunjifu wa amani
Kwani huyo mfalme ni dini gani?
Yaani anatumia kitabu gani kuendesha ibada?
 
Hivi kanisa lake limesajiliwa?Katiba yake umeiona?
Au mpaka yatokee kama ya "kibwetere" kuteketeza waumini ndani ndo muanze kulalama tena.. eti serikali ilikuwa wapi!

WAACHE WAFANYE KAZI YAO!
 
Kwa kudanganya

Kwa kukusanya watoto wa wenyewe akawafuga kama mbuzi

Kuhubiri upumbavu

Kujipatia kipato kinyume na sheria

Kuwatumikisha watu na kuwafanya mabwege

Kujifananisha na Mungu

Soma Katiba utajifunza mengi

Usisahau kusoma Vitabu Vitakatifu pia

Kadanganya nini?
Watoto kawakusanya au wameenda na wazazi wao Kama wanavyooenda kwenye nyumba zingine za ibada?
Kuhubiri kipumbavu ndio kupoje tofauti na wahubiri wengine wote?
Kuna mtu ameporwa au waumini hupeleka sadaka na matoleo Yao Kama ilivyo kwa madehebu mengine?
Mungu yupi unamjua anaejifananisha nae maana miungu ni wengi wajuaje nae ni mungu kwa Imani yake? Kwani lazima mungu wake awe ndio yule wako na wenu? Tangu lini watu wapangiwe Aina ya mungu wa kumuabudu?
Kwahiyo kosa lake hajasoma katiba? Watanzania wangapi hawajaisoma?
Kila mmoja apaswa kusoma vitabu vitakatifu? Ni vipi haswa? Kwanini viwe vitakatifu kwa kila mmoja wakati Imani sio moja?
Ikiwa zumaridi Hana vibali vya kuendesha ibada hiyo yaweza kuwa kosa kisheria za nchi, lakini mengine ni wivu wenu tu hamna tofauti nae.
Masuala ya Imani hayawezi fanana kwa watu wote kwani Safari ya Imani haiko uniform kwa watu wote.
 
dmkali mwanangu... kwa hili la huyu Mchungaji na Unguli wako hapa JF unajidhalilisha bure tu. Ungekuwa wewe ndie RPC wa Mwanza ukatuma Vijana wakaishia kurekodiwa na kufanyiwa ule ujinga na yale mazombie ungwfanyaje?

Kumbuka tayari kuna watoto hawaendi kuanza Form I wamefungiwa ili wawe Zombies.

Naaaamini wengi wetu tungekuwa Askari baada ya zile fujo za Mara ya kwanza next time kwenda kuwakamata ingetokea nini?

Polisi wamefanya kazi nzuri mnooooooo. Sitaki kusema mleta mada ni miongoni mwa hao misukule, lkn niseme amejishushia heshima kusapoti ule ujima wanaofanyiwa hao mnaita mazombie, ile siyo kuabudu bali ni watu wamefanyiwa dhuluma ya akili
Kosa labda ni hao watoto kutokwenda shule kwa sababu wazazi wao wamewapeleka hapo lakini mengine yote ni wivu wenu tu.
Kwani utaratibu wa ibada lazima mfanane?
Muelimisheni azingatie sheria za nchi kwa watoto kwisha habari
 
Tofautisha cult na kanisa ninvitu viwili tofauti. Kuna kitu serikali inataka kufanya ili kuzuia Mambo Kama ya Jim Jones na David Koreish kutokea Tanzania. Ila watu hawajaielewa Sana.

Cult nyingi huanza kwa kuwa na makambi na kukusanya watu sehemu moja baadae ndio hutokea.

Kasome historia ya cult ya Jim Jones na David Koreish ndio utaelewa. Walianza hivi hivi lakini mwishowe maafa yalikuwa mabaya.
Kwani Kuna tofauti gani Kati ya cult na hiyo unaita kanisa?
Huko kanisani hamkusanyiki na kufanya mambo yenu ya Imani?
Acheni wivu
 
Mkuuu nawewe ni mfuasi wa huyu mtu?? Au ni Miongoni mwa wale Zombies wa juzi waliorekodiwa?

Tuweke utani pembeni sisi watu Weusi tumepoteza dira kwenye masuala mazima ya kuabudu kwa sasa tunfanya mazingaombwe tu.
Hujawaona wazungu wanaombea silaha za urusi zisiwadhuru Ukraine?
 
Hata Jim Jones alitetewa hivi hivi Tena alijenga Hadi mji lakini mwishowe alichokifanya dunia haitasahau. Tuchukue hatua mapema kabla halijatokea la kutokea. Watu wanafanywa mazombie wewe unatetea be human kidogo wale nao Ni binadamu wanahitaji kulindwa.
Walifuatwa majumbani kwao?
Wanaenda sababu ya shida zao, ingefaa Sana Kama mngewatatulia shida zao ili wasiende huko mnakosema kubaya
 
Kwahiyo polisi utaratibu walioufanya uko sawa?
Kwanini wamvamie?
Hao mabaunsa wa zumaridi wapole Sana walitakiwa wawatandike Askari wajifunze utaratibu.
Wameenda kizembe Sana eboo
Je wewe una uhakika hawakuwa na kibali? Msipende kuteta vitu usivyovifahamu. Kwa ufupi hayo mapepo yake nadhani yalishaanza kutoka maana keshapata kichapo cha kutosha na wigi hana tena. Unajua wakichapwa waislamu huwa wakristo mnashangilia, rejea mwebe yanga, sasa kwa huyu kushushiwa tu kichapo kidogo inakuwa nongwa.
 
Mwenye picha za mfalme zumarid aweke maana mleta uzi kashindwa kabisa kuweka
 
Mkuu take time google Sheria ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu afu uje fasta ufute Uzi wako...!
Mimi kosa ninalo liona ni kuwa Polisi walikwenda kizembe ...Yale Mamisukule yangeweza hata kuwaua!
 
Kwa kudanganya

Kwa kukusanya watoto wa wenyewe akawafuga kama mbuzi

Kuhubiri upumbavu

Kujipatia kipato kinyume na sheria

Kuwatumikisha watu na kuwafanya mabwege

Kujifananisha na Mungu

Soma Katiba utajifunza mengi

Usisahau kusoma Vitabu Vitakatifu pia
mbona Mungu mwenyewe amepoa tu jamani?

Hiki unachoeleza hapa kina utofauti gani na wale wanaomtetea Mungu wao kwa Mapanga na Mitutu?
 
Kadanganya nini?
Watoto kawakusanya au wameenda na wazazi wao Kama wanavyooenda kwenye nyumba zingine za ibada?
Kuhubiri kipumbavu ndio kupoje tofauti na wahubiri wengine wote?
Kuna mtu ameporwa au waumini hupeleka sadaka na matoleo Yao Kama ilivyo kwa madehebu mengine?
Mungu yupi unamjua anaejifananisha nae maana miungu ni wengi wajuaje nae ni mungu kwa Imani yake? Kwani lazima mungu wake awe ndio yule wako na wenu? Tangu lini watu wapangiwe Aina ya mungu wa kumuabudu?
Kwahiyo kosa lake hajasoma katiba? Watanzania wangapi hawajaisoma?
Kila mmoja apaswa kusoma vitabu vitakatifu? Ni vipi haswa? Kwanini viwe vitakatifu kwa kila mmoja wakati Imani sio moja?
Ikiwa zumaridi Hana vibali vya kuendesha ibada hiyo yaweza kuwa kosa kisheria za nchi, lakini mengine ni wivu wenu tu hamna tofauti nae.
Masuala ya Imani hayawezi fanana kwa watu wote kwani Safari ya Imani haiko uniform kwa watu wote.
Kuna michango ya watu humu inatia Kichefuchefu.

Watu wanataka tufanane mawazo. Hata kama mawazo yao ni ya kipumbavu.
 
Mhalifu hawi mhalifu hadi pale itakapothibitika!

Sakata la mfalme Zumaridi (Kiongozi wa kanisa la Zumaridi huko Mwanza) Linaacha midomo wazi kwa wapenda haki na utii wa sheria!

Sipo hapa kumtetea Mfalme Zumaridi, Bali nashangaa namna ya uharamu wa ukamtaji!

Taratibu za ukamataji kwa mujibu wa sheria ziko wazi kabisa lakini mamlaka zimekuwa zikionesha kufeli Mara kwa Mara kutekeleza sheria hiyo jambo ambalo limekuwa likitweza utu wa watu wasio na hatia.

MFANO! mambo kama haya yalitokea huko mtwara hadi kufedhehesha uongozi wa polisi ambayo yalianza hihivi kwa kufumbafumba mambo,

Mfano 2. Ni huko ARUSHA Kuna taarifa ya askali mzalendo kulalamika kutaka kuuwawa na polisi wenzake kwa mambo Yale Yale kama ya mtwara na serikali iko kimya.

SASA NI HILI SAKATA LA TATU LINALOTIA KICHEFCHEFU

Ni TUKIO LA zumalidi Siku ya kwanza inaripotiwa kwamba polisi waliruka ukuta/geti ili kuingia kwa Zumalidi! Kitendo hiki kilitakiwa kulaaniwa na kila mtu! (Waliruka kwa Zumalidi kesho wataruka kwako)

Kama kulikuwa na ulazima wa kufika pale kwanini hawakufuata utaratibu wa upekuzi unavyotaka? Kwanini hawa kumshirikisha mwenyekiti wa mtaa/mjumbe? Kwanini waliruka ukuta kama jambazi! (VIPI KAMA ZUMARIDI ANGEJIBU MASHAMBULIZI KWA KUFYATUA RISASI KWA POLISI ALIYEVAA KIRAIA ALIPORUKA UKUTA?) Ina maana wangejibu kwamba walikuwa kwenye mapambano na majambazi au?

Kwa utaratibu walio utumia polisi hauna tofauti na utarabu wa kijambazi! Na hili linachangia sana siku hizi RAIA kutokutofautisha kati ya jambazi na polisi.

Tukiachana na mbinu ya ukamataji!

Riport ya polisi ina ukakasi mkubwa juu ya mtuhumiwa Zumaridi!

Kosa walilo utaarifu Umma kwamba anasafilisha BINADAMU 149, kosa hilo Linatia aibu nyingine!

Hivi tangu lini watu wanaokusanyika kusali pamoja imekuwa kosa la jinai?

Mbona jumuiya na taasisi kibao tunawaona wanakusanyika na kukesha na haijawahi kutajwa kuwa ni kosa?

Zumalidi kasafirisha binadamu kutoka wapi kwenda wapi kwa lengo gani? Kuna jinai gani pale?

Hapo taifa juzi wakatoliki walikusanyika mbona haikutamkwa kuwa ni usafirishaji wa binadamu?

Kina mwingira na wachungaji kibao Tanzania kila kutwa wanakusanya watu na haisemwi ni usafirishaji,

INAKUWAJE JAMBO LILE LILE LIWE HALALI KWA MWAMPOSA LAKINI LIWE HARAMU KWA ZUMARIDI?

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Nawashauri TAKUKURU WAINGILIE KATI!
Haiwezekani sheria zipo wazi, kwanini zisingefuatwa kama kweli ZUMALIDI anamakosa makubwa hivyo!

Mimi kwa utashi wangu nahisi sakata la Zumaridi lina maslahi binafisi!

TUKIRUHUSU HAYA YA UKIUKWAJI WA SHERIA HAKUNA ATAKAYEBAKI SALAMA!

Itakuwa mtu akikosana na polisi wanakuja kuluka ukuta! Na majambazi nao watatumia mwanya huohuo kufanya uharifu!
Umetaja watu wawili

1.Zumaridi
2.Zumalidi.

Yupi ni yupi na yupi si yupi?
 
Back
Top Bottom