Sasa imekuwa wazi, kanda ya ziwa ina watanzania asilimia 25 tu

Sasa imekuwa wazi, kanda ya ziwa ina watanzania asilimia 25 tu

Hoja za kipuuzi kabisa.

Ukienda Mwanza sasa hivi, hasa jijini Mwanza, miongoni mwa wafanyabiashara, hasa wakubwa na wa kati, wapo wa makabila mengi, wakiwemo wachaga, wameru, mpaka wakenya. Sasa muingilioni wa kikanda unaousema sijui ni upi.

Sioni utofauti wowote wa Kanda ya Ziwa na Kanda nyingine. Na wala Kanda hazikugawanywa kwa kufuata makabila au desturi za wahusika.

Ebu niambie muingiliano wa watu wa Iringa na Rukwa kidesturi, au watu wa Ruvuma na Lindi, jadi wawe kwenye Kanda moja. Au niambie desturi za watu wa Kagera zinazoshabiahiana na za watu wa Shinyanga. Au watu wa Tabora Vs Kigoma.

Leo hii, mbao zilizojaa Mwanza, Shinyanga, Tabora, zinatoka Iringa na Mbeya. Hayo ni maingiliano ya kibiashara. Kwa hiyo tuseme na Mbeya na Iringa ni Kanda ya Ziwa? Mahindi yanayoliwa Mwanza na Shinyanga, zaidi yanatoka Singida, maharage na viazi mviringo vinatoka Arusha, kwa hiyo hii mikoa ya Arusha na Singida, nayo ni Kanda ya Ziwa kwa sababu ina muingiliano mkubwa wa kibiashara na mikoa ya Kanda ya Ziwa?

Tatizo anataka kulazimisha kwamba Kanda ya Ziwa ni wasukuma pekee. Wasukuma wapo Geita , Simiyu na Mwanza. Ila Kagera na Mara ni makabila tofauti.
 
Kwa taarifa yako .Kanda ya ziwa itabaki kuwa mwamuzi wa mwisho wa kisiasa hapa nchini [emoji116][emoji116]
Kanda ya mashariki
Dar -5.3
pwani -2.0
Morogoro -3.1
Jumla =10.1
Kanda ya kaskazini
Arusha -2.3
Kilimanjaro -1.8
manyara -1.8
Tanga-2.6
Jumla=8.5 milioni
Kanda ya nyanda za juu
Mbeya-2.3
Songwe -1.1
ruvuma-1.8
Njombe -0.8
Iringa -1.1
Rukwa-1.5
Jumla =8.6
Kanda ya kati
Dodoma -3.0
Singida -2.0
Jumla =5 milioni
Kanda ya magharibi
Kigoma -2.4
Tabora -3.3
Katavi-1.1
Jumla =6.8
Kanda ya kusini
Mtwara -1.6
Lindi -1.1
Jumla =2.7 milioni
NIMEKUTAJIA KANDA ZOTE HAMNA ILIYO NA 10 MILION + .. isipokuwa Kanda ya ziwa pekee

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa hivyo tunaenda kuwaiga Kenya ambapo Mt Kenya ndio huamua Rais?
 
Co
Nitakusahidi kukusogeza karibu kiuelewa japo kichwa chako ni kigumu.Kwa taaarifa yako ukisikia kanda ya ziwa elewa ni tofauti na kanda zote nchi hii na itakuchukua muda kuelewa inawezekana sababu ikawa ujawahi kuishi au kufika kabisa.Kwa kukusaidia tu watu wakanda ya ziwa sio watu wakukutanishwa na biashara tu wewe toka kanda yoyote ile nenda kanda ya ziwa kafanye biashara na utafanya bila shida ila kuna kitu kitakuwa nje ya co- relation ya hawa watu na kama hauamini fanya research utaniambia na hii co-relation sasa imenea mpaka tabora,kigoma na katavi.

Kuna co relation gani Kati ya msukuma na mkurya au muha au mfipa?
 
Ongeza na mkurya, mjita , mkerewe na mzanaki.
Kwa maoni yangu watu wa mwanza na mara wako karibu zaidi kuliko watu wa mwanza na kagera maana Wahaya wengi wamejitenga sana kwa umachinoo mwingi.Hata migodini utawakuta wakurya na wasukuma wanashirkiana kuliko wahaya na wasukuima au wakurya.
 
Mgombea yoyote mwenye akili timamu hawezi ignore 15 milion .... akaenda Kanda zenye watu 8 milion kama kaskazini,na nyanda ya kusini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa maoni yangu watu wa mwanza na mara wako karibu zaidi kuliko watu wa mwanza na kagera maana Wahaya wengi wamejitenga sana kwa umachinoo mwingi.Hata migodini utawakuta wakurya na wasukuma wanashirkiana kuliko wahaya na wasukuima au wakurya.
Mwanza imejengwa asilimia kubwa na watu wa kutoka Mara ,,,,,,,Kagera wengi wako kahama .hasa waangaza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
una elimu ya kuokoteza
Kama umegundua hili una akili mno mkuu hukutakiwa kuwemo hapa afrika nadhani Mana mwenzako Elon musk aliondoka afrika Yuko USA anafanya wonders. Na Ni kweli elimu yangu nimeunganishaunganisha. Mwenzako Elon hajaenda havard Ila anaaajili walioenda havard.
Kamata tunda kwa pongezi
 
Ngome ndio Nini?. Hakuna Cha ngome ya CCM Wala nini?
Mimi ndo nakwambia upinzani walichukua majimbo 2010 tu ila miaka ya nyuma yote walichukua CCM niambie unaweza kusema mwanza ni ngome ya wapinzani kisa walichukua majimbo kipindi kile.
 
Nitakusahidi kukusogeza karibu kiuelewa japo kichwa chako ni kigumu.Kwa taaarifa yako ukisikia kanda ya ziwa elewa ni tofauti na kanda zote nchi hii na itakuchukua muda kuelewa inawezekana sababu ikawa ujawahi kuishi au kufika kabisa.Kwa kukusaidia tu watu wakanda ya ziwa sio watu wakukutanishwa na biashara tu wewe toka kanda yoyote ile nenda kanda ya ziwa kafanye biashara na utafanya bila shida ila kuna kitu kitakuwa nje ya co- relation ya hawa watu na kama hauamini fanya research utaniambia na hii co-relation sasa imenea mpaka tabora,kigoma na katavi.

Porojo nyingi hoja hakuna
 
[emoji12][emoji12][emoji28][emoji28]we unachekesha aisee ..toka Lini shinyanga Iko Kanda ya magharibi...kwanza Kanda ya magharibi haipo official......tabora na kigoma wanapata huduma zao za kikanda mwanza ...nzega na igunga hiz wilaya ni Kanda ya ziwa 90 percent kutokana na sukuma culture na ukaribu wake na shinyanga....
Kigoma wanapata huduma zao za kiafya ,na kifedha Kanda ya ziwa . mwanza

Sent using Jamii Forums mobile app

Acha ubishi wa kikabila. Unalazimisha nchi nzima iwe Kanda ya ziwa? Yani serikali inatambua Kanda ya magharibi unasema siyo rasmi? Mkaguzi wa Elimu Kanda ya Magharibi anasimamia mikoa ya Shinyanga, Tabora na Kigoma, Sasa nashangaa wewe unayesema Kanda ya magharibi siyo rasmi.o. Kanda ya magharibi ipo rasmi ndio maana Kuna JaJi mfawidhi wa Kanda ya magharibi. Hayo ya igunga na nzega kuwa ya ziwa ni imagination yako tu.
 
Mimi ndo nakwambia upinzani walichukua majimbo 2010 tu ila miaka ya nyuma yote walichukua CCM niambie unaweza kusema mwanza ni ngome ya wapinzani kisa walichukua majimbo kipindi kile.

Mwanza labda misungwi na Kwimba (ingawa diallo alishasema waliiba kura). Ila Magu, Nyamagan, Ukerewe, Sengerema na Ilemela Ni 50 kwa 50.
 
Acha ubishi wa kikabila. Unalazimisha nchi nzima iwe Kanda ya ziwa? Yani serikali inatambua Kanda ya magharibi unasema siyo rasmi? Mkaguzi wa Elimu Kanda ya Magharibi anasimamia mikoa ya Shinyanga, Tabora na Kigoma, Sasa nashangaa wewe unayesema Kanda ya magharibi siyo rasmi.o. Kanda ya magharibi ipo rasmi ndio maana Kuna JaJi mfawidhi wa Kanda ya magharibi. Hayo ya igunga na nzega kuwa ya ziwa ni imagination yako tu.
Ukisema mkaguzi wa elimu Kanda ya magharibi anasimamia shinyanga..Mimi nitakuletea BOT Kanda ya ziwa inasimamia mikoa ya tabora na kigoma ...
Hospital ya Kanda bugando inahudumia mikoa ya kigoma na tabora.
Sijui umenipata hapo
Multinational franchise za coca-cola,Pepsi ,TBL na Serengeti Kanda ya ziwa zinahudumia mikoa ya tabora na kigoma ..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom