Ishu wala siyo Usukuma bana.
Wasukuma hawako monolithic.
Tatizo kubwa lililopo, kwa mtazamo wangu, ni la kikatiba.
Tukiondokana na urais wa kifalme [imperial presidency], nadhani hali itakuwa bora zaidi ya ilivyo sasa.
Haya mambo hayajaanza jana wala leo.
Hivi unakumbuka Mchungaji Mtikila alikamatwa na kufungwa mara ngapi? Na Mtikila hajawahi kuwepo kwenye utawala wa Magufuli.
Unakumbuka hata mke wa Dkt. Slaa aliwahi kupigwa virungu na kutolewa ngeu na polisi?
..kwanza niombe msamaha hapo kwenye usukuma.
..nilikuwa natania tu, you did not have to explain yourself. Samahani kama nimekukwaza.
..ni kweli haya mambo hayakuanza na Magufuli au ktk awamu hii.
..nakumbuka Mrema alipigwa mabomu kwelikweli alipokwenda Moshi / Kilimanjaro. Na RPC alikuwa Omari Mahita ambaye baadae alipandishwa cheo na kuwa IGP.
..ni kweli Mchungaji Mtikila alifungwa. Pia Mchungaji Kamara Kusupa alifungwa. Juma Duni na wenzake walikuwa na kesi ya uhaini. Halafu kulitokea mauaji ya Unguja na Pemba. Hiyo ni kwa uchache tu.
..What is the difference btn now and then?
..Mimi nadhani MKAPA na KIKWETE walikuwa smart enough in keeping their distance na UKATILI waliokuwa wakifanyiwa WAPINZANI.
..Kwa mfano, mauaji ya Mwembechai na Pemba aliyebebeshwa lawama ni Waziri Mkuu Sumaye, na siyo Amiri jeshi mkuu Mkapa.
..MAGUFULI sijui kwasababu ni TOUGH GUY, or his rhetoric, UKATILI unaonekana kama vile ni kwa MAAGIZO yake yeye binafsi.
..Pamoja na kuonyesha kwamba ni mtu wa SALA / MAOMBI bado hajaweza kuondokana na imani / hisia kwamba mambo haya mabaya hayana baraka na maelekezo yake.
..He has to do something very drastic kubadilisha hisia hizo otherwise anaweza kuharibu LEGACY yake na kuchafua taswira ya nchi kimataifa.