Serikali inawabagua wanafunzi wa shule binafsi; ushahidi huu hapa

Serikali inawabagua wanafunzi wa shule binafsi; ushahidi huu hapa

Mbona hatujawahi kuona wanafunzi wa vigogo wanachaguliwa kwenda shule za kata au wao wanafaulu sana? Acha kutetea upumbavu mkuu. Watu kama nyie ndio mnasababisha serikali ya CCM igome kuboresha mazingira ya shule za kata badala yake inawabeba wanafunzi vilaza na kuwasombea sekondari kwa kigezo cha mazingira magumu halafu inaumbuka baadaye.

Huu upumbavu wanaofanya serikali kwa kuchagua wanafunzi kwa upendeleo wa kipuuzi ndio unaosababisha uwepo wa wanafunzi vilaza kwenye sekondari zetu hivyo kuongeza wingi wa illiterates na ujinga kwenye nchi

View attachment 2848433
hata hao wa kwenu ni vilaza waliokaririshwa majibu, wajinga ndio waliwao. Hao watoto wenu wakifika vyuoni wanapigwa mbaya sana na hao wa shule za serikali, mnajilisha upupo tu na kuliwa mapesa kwa ulimbukeni wenu
 
we

we bwege endelea kuwasomesha shule binafsi, ulivyowapeleka shule binafsi shule ya msingi ulikuwa una malengo waende shule teule? Serikali iko makini, km hutaki waende hiyo shule ya kata warudishwe huko binafsi. Na ukae ukijua wataenda kusoma vyuo vya serikali na hawatakuwa na mikopo. Kupanga ni kuchagua. Mnaopeleka watoto hizo shule za gharama ni mabwege tu mnaoliwa hela na wajanja, walimu wanaowafundisha huko private ni watanzania wale wale waliosoma vyuo vya serikali, tofauti ni gharama na kiinglishi cha kuongea mtaani siyo kiinglishi cha kitaaluma. Watanzania wakiwa na vijihela kidogo ni malimbukeni.
Sasa povu lote hili la nini wewe bwege? Shule za serikali sio zza CCM pekee bali ni za watu wote. Mbona kama unataka kunipangia maisha. Kwa hiyo wanafunzi wanaosoma shule binafsi sio raia hawapaswi kutendewa haki kama watanzania? Mijitu yenye akili za kipuuzi kama wewe ndio mnasababisha serikali isiboreshe huduma za jamii. Ningekuwa na uwezo majitu kama wewe ningewanywesha sumu; bora mfe tu!.
 
Kwahiyo suluhisho ni kutujazia watoto wote wa darasa moja kwenye shule moja tena darasa moja?? Inaonyesha hujaelewa kabisa nini kinajadiliwa..!! Ishu ipo hivi, Mwenye C huko private aende hizo za kutwa na mwenye C huko primary za serikali naye aende huko sekondari za kutwa..!! Lakini kumchukua mwenye A wa private kumpeleka sekondari ya kutwa halafu mweye C toka kayumba aende shule maalumu ndo upendeleo ulipo..!! Na ndo kinacholalamikiwa..!! Hakujatajwa uwezo wa mzazi kulipa mamilioni au kushindwa kulipa mamilioni huko private..!!! Na kwa taarifa yako, si kila aliyeko Kayumba maana yake ameshindwa kulipa ada za mamilioni huko private. Ni maamuzi na mitazamo ya shule zipi kila mmoja anaona zinafaa kuwapeleka watoto wake.
Na serikali sikivu itaendelea na huu utaratibu hadi akili ziwakae sawa. Mwaka 2000 pale Ilboru kulijaa watoto wa Green Acres na shule nyingine za kishua hadi ikashangaza. Naona serikali imeshtuka. Utaratibu huu ni mzuri kama wanavyofanya HESLB. Mtoto wa St Kayumba apewe kipaumbele. Nyie wa private pelekeni watoto wenu sekondari za private acheni kulialia.
 
Na serikali sikivu itaendelea na huu utaratibu hadi akili ziwakae sawa. Mwaka 2000 pale Ilboru kulijaa watoto wa Green Acres na shule nyingine za kishua hadi ikashangaza. Naona serikali imeshtuka. Utaratibu huu ni mzuri kama wanavyofanya HESLB. Mtoto wa St Kayumba apewe kipaumbele. Nyie wa private pelekeni watoto wenu sekondari za private acheni kulialia.
Mkuu usichanganye mada. Hapa tunaongelea selection ya form one 2024 lakini wewe umekimbia hadi HSLB. Unatafuta nini huko? Kuwa muelewa.

Wanafunzi huchaguliwa kwenda sekondari bora kulingana na ufaulu bora. Wewe unataka serikali yako ya kusadikika iendelee kuwachukua wanafunzi bora kutoka shule binafsi na kuwapeleka shule za kutwa za Kayumba badala ya kuwapeleka shule teule? Una akili kweli au akili zako umezisahau nyumbani?
 
Mkuu tumekuelewa na tumekufikia. Tunaomba sasa ujikite kwenye mada. Mbona unakuwa kama kuku anayetaka kutaga? Hutulii. Jikite kwenye hoja usizunguke tu kama kipepeo bila muelekeo.
 
SI mna Hela wapelekeni private
Rudia kusoma uzi uelewe hoja. Usikurupuke tu kama panya aliyekurupuliwa kutoka kwenye kibuyu. Majitu kama wewe mnaosapoti ujinga ndio mnasababisha serikali igome kuboresha huduma za jamii.
 
Mkuu usichanganye mada. Hapa tunaongelea selection ya form one 2024 lakini wewe umekimbia hadi HSLB. Unatafuta nini huko? Kuwa muelewa.

Wanafunzi huchaguliwa kwenda sekondari bora kulingana na ufaulu bora. Wewe unataka serikali yako ya kusadikika iendelee kuwachukua wanafunzi bora kutoka shule binafsi na kuwapeleka shule za kutwa za Kayumba badala ya kuwapeleka shule teule? Una akili kweli au akili zako umezisahau nyumbani?
Acha kunililia mimi sio babako.
 
Wangekuwa wanawachukua hata nusu yao ya wanafunzi waliofanya vizuri, kwa kuwa wametokea kwenye shule zenye mazingira bora kwa baada Taifa lingekuja kupata wataalamu walio bora zaidi. Lakini wao watakuwa wanawaza kuwa kwa kuwa hawa wanafunzi wametokea kwenye shule zenye mazingira bora hivyo basi mategemeo yao wanawataka waje kuzipandisha hadhi shule za kata.
Watasubiri sana. Wapambane na hali zao. Wasitegemee ubwete wa kuandaliwa wanafunzi halafu waje kuchukua ujiko wa bwerere hapo baadaye.
 
Nimeshangaa sana hawa jamaa. Kuna dogo kijijini kwetu amepata wastani wa C mbovu kabisa eti amepangiwa korogwe girls alafu wale madogo waliopiga A wamepangiwa shule za kata. Duh
EQUITY!!!
 
Mara nyingi Wanafunzi waliosoma Private huwa hawaripoti kwenye shule walizochaguliwa hivyo inafanya shule kongwe kuwa na wanafunzi wachache,hivyo kwa muktadha huo serikali imeona ni bora tuwapeleke wanaohitaji na watasoma huko.!
 
Mara nyingi Wanafunzi waliosoma Private huwa hawaripoti kwenye shule walizochaguliwa hivyo inafanya shule kongwe kuwa na wanafunzi wachache,hivyo kwa muktadha huo serikali imeona ni bora tuwapeleke wanaohitaji na watasoma huko.!
Huu ni upumbavu..

Iko hivi, watoto wanajengewa foundation, vile sekondari ni lugha mpya kwa masomo yote.
 
Unajua ni kigezo gani kilitumika kufanya selection? pengine kigezo kilichotumika ni average ya marks na sio A zote
 
Serikali hii ya CCM ina mambo ya ajabu sana. Ni aibu kwa serikali inayojinasibu kuzingatia usawa kufanya uhuni wa kiwango hiki. Sijawahi kuona serikali yenye ubaguzi mkubwa kwa wananchi wake hapa ulimwenguni kama serikali ya CCM.

Katika uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga kidato cha kwanza mwaka 2024, serikali imeonyesha ubaguzi wa waziwazi kati ya wanafunzi wa shule za kata na shule binafsi. Hii tabia ya kibaguzi haifai hata kidogo. Tukumbuke kwamba kuna wazazi wa watoto wanaosoma shule binafsi ambao wangependa watoto wao waendelee na masomo katika shule za umma. Inasikitisha serikali imeamua kukatisha ndoto hizo kwa makusudi.

Nitatoa mifano hai ili kuthibitisha hili ninalosema hapa. Nimechukua sampuli ya shule mbili kutoka kata moja (moja ya serikali na nyingine ya binafsi) ili kuuonyesha umma wa watanzania jinsi serikali ya CCM ilivyojaa ubaguzi wa kipuuzi uliopindukia. Lengo la kuchukua shule kutoka kata moja ni la kitafiti zaidi…..kwamba wanafunzi wote wanatoka eneo moja lenye mazingira yanayofanana; hivyo hakuna sababu ya kuwabagua.

Tazama matokeo ya shule hii binafsi jinsi wanafunzi wake walivyofanya vizuri: https://matokeo.necta.go.tz/results/2023/psle/results/shl_ps0206131.htm
View attachment 2848392

Linganisha matokeo hayo na haya ya shule ya kata: https://matokeo.necta.go.tz/results/2023/psle/results/shl_ps0206125.htm
View attachment 2848390
Utaona idadi ya A kwenye shule binafsi ni 58 huku shule ya kata wakiambulia 9 tu!

Sasa njoo kwenyye uchaguzi wa wanafunzi waliochaguliwa kwenda shule za sekondari mwaka 2024. Serikali imechagua wanafunzi 2 waliopata A tu kutoka shule binafsi kwenda shule teule. Wengine wote waliosalia wamerundikwa kwenye shule za kata za kutwa kama mnavyoona.

Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, 2024

Na pia wamechaguliwa wanafunzi 2 tu kutoka shule ya serikali iliyofanya vibaya na wanafunzi hao wamepata B mbili katika masomo yao. Haki iko wapi?

Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, 2024

Kama serikali ingekuwa inafuata haki, wanafunzi wote 58 kutoka shule binafsi wangechaguliwa kwenda shule teule. Lakini kwa kuwa ubinafsi na upendeleo umetawala ndani ya roho zao za kutu, wameamua kuchagua wanafunzi 2 tu ili kufunika kombe mwanaharamu apite. Serikali hii ina mambo ya kijinga sijapata kuona.
Binafsi sio muumini sana wa kukosoa wengine lakini, katika hili naomba niweke Sawa baadhi ya mambo machache kuhusu selection (kwa uelewa kiasi nilionao).
1. Si kweli kwamba kuna mwanafunzi kapata wastani wa B kaenda shule teule.( kama una ushahidi tuoneshe tafadhari)
2. Mwanafunzi apelekwi shule teule eti kwa sababu kapata wastani wa A, badala yake kuna factors nyingi sana mfano, A ya ngapi? Mtu kapata wastani wa A lakini A ya 98, lakini kuna mwengine kapata A ya 100, kama wapo kwenye kapu moja la uchaguzi, mwenye A ya 100 lazima achaguliwe.
Au watoto wamegongana wastani wote wana A ya 98 na wenye 99 na 100 wote wamechaguliwa kulingana na makundi yao, mwenye ufaulu mzuri zaidi katika somo la hisabati au Sayansi ana nafasi kubwa ya kuchaguliwa shule teule kwa kigezo hiki.
Kwahiyo, shule X inaweza kuwa na A moja tu, lakini mwanafunzi akachaguliwa shule teule, na shule ikawa Z wakawa na A zote na wasipelekwe shule teule kulingana na uzito wa hiyo A. Tafadhari mtoa mada naomba ujiridhishe katika hili.
3. Uwiano ni jambo la msingi ndio maana hata jinsia huzingatiwa, walemavu n.k hivyo basi, hakuna namna utakayokwepa kuweka some standards kulingana na makundi mbalimbali. Ubaya ni pale tu unapoweka double standards kwa watu wa kundi moja.
Hivyo basi, nionavyo mimi unapoamua kuilamu Serikali au viongozi kutokana na maamuzi wanayoyafanya katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku, ni vyema tukawa na ushahidi usiokua na chembe ya mashaka hasa katika hili la selections.

Ahsante.
 
Hapa Tunachotakiwa kuilaumu serikali Ni kutokuboresha mazingira mazur gov schools
Lakini serikali ikishindwa kuboresha mazingira ya kusomea badala yake ikaboresha mazingira ya selection ya wanafunzi wa shule ya kata wewe unaona ni haki mkuu?
 
Back
Top Bottom