Serikali inawabagua wanafunzi wa shule binafsi; ushahidi huu hapa

Serikali inawabagua wanafunzi wa shule binafsi; ushahidi huu hapa

Huwezi kulinganisha ufaulu wa Kagera na Mtwara au Lindi na Mbeya au Katavi na Kilimanjaro.
Huwezi kuweka mizani sawa hata siku moja. Kata ya Umasaini iwe sawa na kata ya Dsm! Nooo!!

Mimi si mmoja wao. Ni fikra zangu zinanifikirisha hivyo
Wamezingatia EQUITY !!!
 
Na mimi nitaelezea uzoefu wangu katika swala hili la selection kwa kidato cha kwanza. Jambo hili naweza kusema kwamba halijaanza leo, linaweza kuwa limeanzia tangu miaka ya 2008 na litaendelea. Kwanini nasema hivi? Sababu ni hii mimi mwenyewe nilikumbwa na kadhia hii hii japo nilisoma shule ya serikali. Matokeo yetu ya shule ya msingi yalikuwa mazuri mno kwani shule yetu ilikuwa inafahamika kwa kufaulisha vizuri. Lakini lilipokuja swala la selection za kidato cha kwanza hadi waalimu pale shuleni walibaki kushangaa. Kwani kwa ufaulu nilioupata na kupelekwa shule ya kata nilipofika kule nilishangaa. Nilitegemea kupelekwa shule ya mkoa kama si wilaya. Kwani kuna wanafunzi waliokuwa na ufaulu kama wangu wa shule nyingine na walipelekwa shule za mkoa au wilaya. Na kibaya zaidi aliyefaulu kwa ufaulu wa juu zaidi pale shuleni kwetu aliishia kupelekwa Azania wakati mdada aliyemfuata ndiye aliyepelekwa Shule ya Vipaji yaani Kilakala. Kwa kweli ilikuwa ni sintofahamu sanaa. Kwahiyo nataka kusema hili swala kwa sasa hv ndo linaanza kuonekana ukubwa wake. Lakini lilianzia miaka ya nyuma kabisa. Kuwa na amani, muhimize kijana wako asome kwa bidii katika shule aliyochaguliwa atafaulu, au laa ukiona haujaridhika baadae umuhamishie shule nyingine ya serikali utakayoona ina uhafadhali kuliko hiyo. Shule za Kata zimekuwa zikitazamika vibaya katika jamii zetu kutokana na miundombino pamoja na vitendea kazi vya kufundishia lakini pia na aina ya wanafunzi wapelekwao huko. Wengi wao wanakuwa ni wale wasindikizaji hili linazidi kuzifanya shule hizi kuzidi kudharaulika lakini, wewe kama mzazi lisikuvunje moyo mpambanie mwanao na atafanikiwa. Mimi nilifaulu vizuri kuliko hata baadhi ya waliopelekwaga shule za mkoa na wilaya sijisifii lakini natoa ushuhuda.
Mkuu umetoa ushuhuda na ushauri mujarab! 👍👏🙏
 
Mtoto aliepata B ya akisoma kayumba
Uwezi mfananisha na mtoto aliepata A akisoma Private school

Ni watoto wawili wenye uwezo tofauti ukizingatia vema mazingira ya usomaji

Kingine, Watoto wengi toka private wanaochaguliwa shule teule, hawaendi

Wanaenda zao feza, Marian, n.k

Nadhan serikali pia imezingatia hilo
 
Acha wa kwangu wabaki huko nje kuliko nije kuilamu sirekali hii ya ccm ukiongeza na wale wenyeviti chupukizi naamini hakuna mwenye huruma na hii nchi uzalendo haupo asikwambie mtu hilo!

Kinachoniudhi ni watoto wao wala hawasomi hizo za kata na wala hawahangaiki na ajira mitaani yaani kama vile kuna mkataba wa kikundi flani tu kuitawala Tanzania wengine hawawezi kuongoza!
 
Kwa hiyo kumbe selection haifuati ufaulu bali inafuata uwiano kama vile Tanganyika inavyowiana na Zanzibar? Hii kali aisee!

Hebu tufafanulie kidogo mkuu huenda unakuwemo kwenye selection board. Huwa mnachagua kwa kutumia muongozo kutoka juu bila kuzingatia ufaulu?
Mkuu unapaswa kuzingatia pia mazingira ya usomaji Kati ya private na kayumba
 
Mazingira ya kujifunzia kwa maana ya walimu, vitabu n.k

Serikali inatambua kuwa shule zake zina mazingira mabovu.
Kwa hiyo ndio maana serikali inaamua KUBORESHA mazingira ya shule zake kwa kufanya upendeleo kwenye selection?
 
Kuna mdau aliandika humu, hakuna kitu hata kimoja ambacho serikali inafanya kwa ufasaha na usahihi. Ni kuunga unga tu mradi pakuche
Halafu matokeo yake hawahawa wenye uwezo mdogo ndio wanaokuwa watumishi wa serekali, hii ndio inapekelekea mambo ya serekali kuendeshwa kwa maguvu na akili kidogo, huku kukiwa na ufanisi duni.

Na wengi wa hao vilaza hutokea kuwa makada wa ccm, Hadi uzee wao unakuta wanategemea Hila tu maana wamelelewa kwa njia ya mbeleko. Wengi wa watu wenye akili huru ni adui waccm, ndio sababu ya huo upendeleo kwa vilaza.
 
Serikali hii ya CCM ina mambo ya ajabu sana. Ni aibu kwa serikali inayojinasibu kuzingatia usawa kufanya uhuni wa kiwango hiki. Sijawahi kuona serikali yenye ubaguzi mkubwa kwa wananchi wake hapa ulimwenguni kama serikali ya CCM.

Katika uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga kidato cha kwanza mwaka 2024, serikali imeonyesha ubaguzi wa waziwazi kati ya wanafunzi wa shule za kata na shule binafsi. Hii tabia ya kibaguzi haifai hata kidogo. Tukumbuke kwamba kuna wazazi wa watoto wanaosoma shule binafsi ambao wangependa watoto wao waendelee na masomo katika shule za umma. Inasikitisha serikali imeamua kukatisha ndoto hizo kwa makusudi.

Nitatoa mifano hai ili kuthibitisha hili ninalosema hapa. Nimechukua sampuli ya shule mbili kutoka kata moja (moja ya serikali na nyingine ya binafsi) ili kuuonyesha umma wa watanzania jinsi serikali ya CCM ilivyojaa ubaguzi wa kipuuzi uliopindukia. Lengo la kuchukua shule kutoka kata moja ni la kitafiti zaidi…..kwamba wanafunzi wote wanatoka eneo moja lenye mazingira yanayofanana; hivyo hakuna sababu ya kuwabagua.

Tazama matokeo ya shule hii binafsi jinsi wanafunzi wake walivyofanya vizuri: https://matokeo.necta.go.tz/results/2023/psle/results/shl_ps0206131.htm
View attachment 2848392

Linganisha matokeo hayo na haya ya shule ya kata: https://matokeo.necta.go.tz/results/2023/psle/results/shl_ps0206125.htm
View attachment 2848390
Utaona idadi ya A kwenye shule binafsi ni 58 huku shule ya kata wakiambulia 9 tu!

Sasa njoo kwenyye uchaguzi wa wanafunzi waliochaguliwa kwenda shule za sekondari mwaka 2024. Serikali imechagua wanafunzi 2 waliopata A tu kutoka shule binafsi kwenda shule teule. Wengine wote waliosalia wamerundikwa kwenye shule za kata za kutwa kama mnavyoona.

Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, 2024

Na pia wamechaguliwa wanafunzi 2 tu kutoka shule ya serikali iliyofanya vibaya na wanafunzi hao wamepata B mbili katika masomo yao. Haki iko wapi?

Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, 2024

Kama serikali ingekuwa inafuata haki, wanafunzi wote 58 kutoka shule binafsi wangechaguliwa kwenda shule teule. Lakini kwa kuwa ubinafsi na upendeleo umetawala ndani ya roho zao za kutu, wameamua kuchagua wanafunzi 2 tu ili kufunika kombe mwanaharamu apite. Serikali hii ina mambo ya kijinga sijapata kuona.
Inawakatisha sana tamaa, Tunazalisha wakandarasi wanaojenga kituo cha mwendokasi katika ya Jangwani na wanaona sawa maana walibebwa na hawajui kitu.
 
Halafu matokeo yake hawahawa wenye uwezo mdogo ndio wanaokuwa watumishi wa serekali, hii ndio inapekelekea mambo ya serekali kuendeshwa kwa maguvu na akili kidogo, huku kukiwa na ufanisi duni.

Na wengi wa hao vilaza hutokea kuwa makada wa ccm, Hadi uzee wao unakuta wanategemea Hila tu maana wamelelewa kwa njia ya mbeleko. Wengi wa watu wenye akili huru ni adui waccm, ndio sababu ya huo upendeleo kwa vilaza.
Hao wenye D shule za Kata Form four wanapiga division 4 wanaingie ile chuo kikuu kipo Moshi kina wakurya wengi sijui kinaitwa sisipii .
 
Halafu matokeo yake hawahawa wenye uwezo mdogo ndio wanaokuwa watumishi wa serekali, hii ndio inapekelekea mambo ya serekali kuendeshwa kwa maguvu na akili kidogo, huku kukiwa na ufanisi duni.

Na wengi wa hao vilaza hutokea kuwa makada wa ccm, Hadi uzee wao unakuta wanategemea Hila tu maana wamelelewa kwa njia ya mbeleko. Wengi wa watu wenye akili huru ni adui waccm, ndio sababu ya huo upendeleo kwa vilaza.
1703098606707.png
 
MarksGrade
00 - 10F
11 - 20D
21 - 30C
31 - 40B
41 - 50A
nimewaza labda wanaangalia wastani;

mwenye 50,50,50,40,40(atachukuliwa ana A tatu, B mbili) ana wastani mkubwa kuliko mwenye 41,41,41,41,41(atachukuliwa ana A tano)

ni mfano tu, ila inaonesha inawezekana.
 
Serikali hii ya CCM ina mambo ya ajabu sana. Ni aibu kwa serikali inayojinasibu kuzingatia usawa kufanya uhuni wa kiwango hiki. Sijawahi kuona serikali yenye ubaguzi mkubwa kwa wananchi wake hapa ulimwenguni kama serikali ya CCM.

Katika uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga kidato cha kwanza mwaka 2024, serikali imeonyesha ubaguzi wa waziwazi kati ya wanafunzi wa shule za kata na shule binafsi. Hii tabia ya kibaguzi haifai hata kidogo. Tukumbuke kwamba kuna wazazi wa watoto wanaosoma shule binafsi ambao wangependa watoto wao waendelee na masomo katika shule za umma. Inasikitisha serikali imeamua kukatisha ndoto hizo kwa makusudi.

Nitatoa mifano hai ili kuthibitisha hili ninalosema hapa. Nimechukua sampuli ya shule mbili kutoka kata moja (moja ya serikali na nyingine ya binafsi) ili kuuonyesha umma wa watanzania jinsi serikali ya CCM ilivyojaa ubaguzi wa kipuuzi uliopindukia. Lengo la kuchukua shule kutoka kata moja ni la kitafiti zaidi…..kwamba wanafunzi wote wanatoka eneo moja lenye mazingira yanayofanana; hivyo hakuna sababu ya kuwabagua.

Tazama matokeo ya shule hii binafsi jinsi wanafunzi wake walivyofanya vizuri: https://matokeo.necta.go.tz/results/2023/psle/results/shl_ps0206131.htm
View attachment 2848392

Linganisha matokeo hayo na haya ya shule ya kata: https://matokeo.necta.go.tz/results/2023/psle/results/shl_ps0206125.htm
View attachment 2848390
Utaona idadi ya A kwenye shule binafsi ni 58 huku shule ya kata wakiambulia 9 tu!

Sasa njoo kwenyye uchaguzi wa wanafunzi waliochaguliwa kwenda shule za sekondari mwaka 2024. Serikali imechagua wanafunzi 2 waliopata A tu kutoka shule binafsi kwenda shule teule. Wengine wote waliosalia wamerundikwa kwenye shule za kata za kutwa kama mnavyoona.

Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, 2024

Na pia wamechaguliwa wanafunzi 2 tu kutoka shule ya serikali iliyofanya vibaya na wanafunzi hao wamepata B mbili katika masomo yao. Haki iko wapi?

Uchaguzi wa Wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, 2024

Kama serikali ingekuwa inafuata haki, wanafunzi wote 58 kutoka shule binafsi wangechaguliwa kwenda shule teule. Lakini kwa kuwa ubinafsi na upendeleo umetawala ndani ya roho zao za kutu, wameamua kuchagua wanafunzi 2 tu ili kufunika kombe mwanaharamu apite. Serikali hii ina mambo ya kijinga sijapata kuona.
CCM inahofia uwekezaji makini kwenye elimu kwamba watakuja kuanguka kwenye chaguzi.

Wanaogopa sana jamii iliyoelimika na kujitambua ndo maana kila mara inacheza na mitaala ya elimu ambapo tunaishia kupata wasomi wanaokariri bila kutumia ubongo wao vyema
 
Kwa hiyo unataka kusema nini kuhusu selection inayofanywa na serikali ya CCM?
Selection ipo Sawa

Nakupa mfano

John kapata math 41 "A" English 42 " A" wastan hapo ni 42

ISSA kapata Math 48 "A" English 38 "B" wastan hapo ni "43"

Hapo John na ISSA nan kamzid mwenzake ufaulu?
 
Mfumo wa elimu wa Tanzania ni outdated na elimu inayotolewa na mfumo huo ni ya dark ages ndo maana nchi haiendi mbele.Hakuna shule ya serikali inayotoa elimu bora bila kujali ikoje na ipo wapi,hata malalamiko yako nayaona hayana msingi kwa sababu anaesoma kata au hiyo spesho wote wapo chini ya mfumo uleule uliofeli. Shule za kata, bweni, teule, spesho kote ni full ujinga uleule,we unapelekeshwa na majina ya shule.
Mkuu umekasirika sana...
Umeandika mambo mengi in a very summarized form..

Kuujadili mfumo wa Elimu wa nchi hii, inabidi kwanza uwe huna kazi ya kufanya, alafu ulipwe pesa nyingi sana.

Though.. it's all said in JKs Nyerere Vision. Elimu Ya Kujitegemea. Education For Self Reliance.
 
Hizo shule teule ni chache mpendwa! Ukisema utumie vigezo unavyovisema wewe maanake kwanza hazitatosha kwa hiyo uwiano ni mhimu ili kila upande upate! Kinachofanyika shule za private zina nafasi zao za kwenda huko hivyo hivyo na shule za umma zina idadi yao! Kutokana shule za private ni wengi wanafaulu ndo maan wanagawana wawili wawili mkuu! Shule za umma wanaofaulu kwa ufaulu wa juu ni wachache ndo maana wale wanaofaulu kwa kiwango hata cha B wanabahatika maana nafasi zao wengi hawafaulu kwaviwango vya juu!!


Sio kila kitu kuilaumu serikali mambo mengine tunapaswa kuipongeza
Uko sahihi lakini lazima serikali ifanye juhudi za kuboresha shule za umma ili kiwango cha ufaulu kilingine na wale wa private kwani kwa sasa tofauti ni kubwa mno.Waone private wanafanya investment gani mpaka wanafaulu kwa rate kama ile

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom