#COVID19 Serikali isiwaache Wananchi katika mataa kwenye suala la Corona
Corona ipo duniani na Tanzania siyo kisiwa.

Nchi kuwa na Corona siyo aibu, maana kirusi hakijui mipaka ya kisiasa.

Serikali zilizo responsible duniani zinaendelea kutekeleza sera za kupambana na Covid na kamwe hazitangazi kuwa zimeshashinda vita tayari, bali zinakuwa cautious na zinaendelea na jitihada za kupambana na huu ugonjwa.

Siyo siri, sisi Tanzania kwa kiwango kikubwa tulinusurika na wimbi la kwanza la maambukizi yale. Mungu wetu alitusaidia na kwa kweli watanzania walijitahidi pia kuchukua hatua, kila sehemu kulikuwa na ndoo za kunawa mikono etc

Pamoja na mafanikio yale haikuwa sahihi na haiendelei kuwa sahihi serikali kukaa kimya na kuacha kila mtu aamini Korona haipo nchini, au kuuaminisha umma kuwa korona haipo kabisa. kufanya hivyo siyo sahihi hata kidogo

Lakini cha kushangaza zaidi ni pale serikali na vingozi wake walipoanza kudiscourage wananchi kuchukua hatua za kujikinga. Barakoa zilianza kufanyiwa mizaha etc

Serikali ilipaswa iendelee kuhimiza watu waendelee kuchukua hatua, na kuencourage watu kujilinda lakini siyo kudiscourage measures zote ambazo wananchi wanafanya.

Labda kitu kimoja ambacho serikali lazima ielewe ni kuwa sasa wananchi wameanza kuwa na wasiwasi kuwa Korona ipo nchini, lakini wanakosa uhakika wa kimamlaka kulichukulia kwa uzito stahili maana serikali imeamua kupiga kimya!

Mimi ningependa kuieleza serikali yetu kuwa ni higly irresponsible katika kipindi hiki dunia imeingia katika vita ya pili juu ya huu ugonjwa lakini yenyewe imekaa kimya tu inawaacha wananchi peke yao utafikiri kondoo wasio na mchungaji.

Tunataka kusikia kauli ya serikali, Je Corona ipo Tanzania?, Je serikali ina mpango gani au imeamua wenye kuugua waugue, wenye kufa wafe lakini yenyewe itakaa kimya tu?

Nchi jirani zetu baadhi zimeanza kuchukua hatua kali mipakani mwao kuhusu wanaoingia, je sisi mambo shwari tu hakuna ishu?

Sisi tukimuona rais wetu amekwenda tena Chato kipindi hiki tukiambiwa kuwa Corona imechachamaa huko duniani tunapata wasiwasi kuwa huenda yasemwayo mitaani kuwa ni kweli maana tunakumbuka kipindi kule rais alipokwenda kukaa huko Chato kwa zaidi ya miezi miwili kipindi Corona imechachamaa mwaka jana!. Je ngoma imerudi kama mwaka jana?

Tunataka serikali itupe majibu, tunataka kujua status ya hali ya Corona nchini, maana baadhi ya watu wanaoaga dunia kuna watu mitaani wamekuwa wakinong'ona kuwa Korona ipo na inang'ata

Wananchi tunataka majibu, tena majibu sahihi ya hili suala!

Afya sio mali ya serikali,usisubiri mpaka ikuambie kwamba ipo ndio uanzae kuchukua hatua, umeanza vizuri, corona ipo duniani na TZ ni sehemu ya dunia. Chukua tahadhari DIPOTIVO ipo.
 
Kuna rafiki yangu yupo morogoro amenipigia simu Leo kuniambia kuwa Corona ipo nichukue tahadhari

Mtaani kwao modeko wamezika mtu alikuwa na dalili zote za Corona alipokuwa hai.
Pana watu yafaa washatakiwe kwa kumisslead watu Ili wapotee Hali wao wamejificha majumbani kwao kukimbia corona,nani alikuambia sisi ni kisiwa.
 
Ninapowapendea WaTZ ni hapa tu, ubishi na ukweli anaujua!!

Tanzania si kisiwa kwamba usiingie, kasema alikuwa na dalili kama....!! Mtu anauliza hakuna magonjwa mengine!! [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Kuanzia Desemba 29 nilianza kupatwa natatizo la kuhara na homa kali sana, nilipokwenda kupata vipimo sikukutwa na chochote, sikuridhika nikaanza kutumia mseto na flagili, hali haikutengaa sana kidooogo kuhara kukawa kumepungua.

Nikaenda duka la dawa za binadamu, nikajaribu kutoa maelezo yangu kwa jinsi ninavyosikia, mhudumu aidha ukapime ujue nini kinakusumbua au utumie dawa za typhoid, nikachukua cipro - hali ya kuahirisha ikawa imekata japo homa ikifika jioni inakuwa kali sana na kukohoa.

Nikatumiatumia tangawizi na limao hali ya kukohoa ikapungua kwa asilimia karibu 90.

Nikapata tena vipimo sehemu nyingine nikakutwa na viral blood infection/mchafuko wa damu, nikaanza dozi hata sijaimaliza hadi sasa na ninajihisi kupona kabisa huku nikiendelea na tangawizi sometimes.

NOTE: BAADHI YA MARADHI YANA DALILI ZA KUFANANA.
 
kuwa ni kweli maana tunakumbuka kipindi kule rais alipokwenda kukaa huko Chato kwa zaidi ya miezi miwili kipindi Corona imechachamaa mwaka jana!. Je ngoma imerudi kama mwaka jana?

Tunataka serikali itupe majibu, tunataka kujua status ya hali ya Corona nchini, maana baadhi ya watu wanaoaga dunia kuna watu mitaani wamekuwa wakinong'ona kuwa Korona ipo na inang'ata

Wananchi tunataka majibu, tena majibu sahihi ya hili suala
Kilichonifurahisha kwenye story yako ni kuwa ukimuona ameenda Chato, basi, corona ipo. Huwezi kutafuta ka fomyula kentine⁉️⁉️⁉️⁉️🤓🤓🤓🤓🤓
 
Tunataka serikali itupe majibu, tunataka kujua status ya hali ya Corona nchini, maana baadhi ya watu wanaoaga dunia kuna watu mitaani wamekuwa wakinong'ona kuwa Korona ipo na inang'ata

Wananchi tunataka majibu, tena majibu sahihi ya hili suala!
Majibu haya hapa toka kwa wazungu wanafurika nchini wakijua corona hamna.cheki mandege yanavyoshusha watalii hawana cha barakoa wala nini. Mleta mada una matatizo ya akili wahi mirembe haraka.

 
Jan 1 2021: Kifo cha baba mdogo, upumuaji.

Jan 14 2021 Kifo cha babu, upumuaji.

Wote walisaidiwa na mashine kupumua nyakati za mwisho za uhai wao.

ALLAH awarehemu.
HAWANA MAJINA NI WASIOJULIKANA?
 
Kuna Daktari Mmoja Rafiki yangu nilimuuliza kwanini kuanzia Mwezi Desemba 2020 hadi Januari 2021 Vifo ni vingi akajibu tu niwaulize Wachina.
Mkuu umehesabu hadi vifo vya ajali nini?maana mwisho mwa mwaka ajali nyingi.
 
Kwani kuna tamko la serikali lilishawahi kutolewa rasmi kuwaambia wananchi wake wasichukue tahadhari?wewe kama una mashaka vaa tu barakoa au tumia sanitizer pale inapobidi,pia jaribu kiasi unachoweza kuepuka mikusanyiko isiyo na msingi au keep distance popote unapokuwa kwenye mkusanyiko,hilo sio kosa la jinai,swala la afya ya mtu binafsi liko mikononi mwako mwenyewe.Unajua kabisa gears zote zinazotumika kujikinga ili usipate maambukizi halafu unalalamika eti unasubiri serikali ikwambie,hata kama itakwambia juwa kuwa haitakununulia vifaa kinga au wewe kupata unafuu wowote wa hivyo vifaa....
 
COVID ipo na uzuri haichagui, hata hao wanaosema haipo inaendelea kuwafyeka tu Jamaa zao na wao hawana kinga wala exception kusema COVID haiwezi kuwafikia.
Ndio Maana wame ji isolate, Mbochi Tocha
jikinge Mwenyewe usiwangoje wakwambie
Mkuu kama kweli ipo na inauwa sana watu kwanini sasa tuwe tunabishana humu? yani mie nifiwe na ndugu na jamaa zangu huku nikijua kwa sababu ya corona halafu nije humu kabisa niseme hakuna corona? au naona kabisa eneo nalokaa watu wanaugua isivyo kawaida na wengine wanakufa halafu nije nipinge humu mashaka ya uwepo wa corona?

Hivi kweli nikifanya nakuwa na akili ya aina gani au kwa kumfaidisha nani?
 
We nunua tangawizi, mchaichai chemsha iive ukiipua mix limao na asali gonga nusu kikombe asubuhi na jioni na familia yako ongeza immunite kwa mbegu za tikiti pia zina zink ya kutosha.

Sometime warm you body by drinking hot water until you sweat.
Mengine iachie serikali itajua cha kufanya.
ushirikina huu
 
Corona ipo tena umepamba moto, watu wanakufa sana sisi tumeamua kuendekeza siasa. Uliza madaktari wa Muhimbili na Mloganzila wakupe picha kamili
Kwahiyo wagonjwa wakifikishwa hospitali hupimwa hadi corona na ndio hao madktari wanajua kuwa watu wanakufa sana kwa corona?
 
Ni maranyingi sana serikali hata Rais ameshasema kuhusu kuishi kwa tahadhari.
Wanaoongoza kusema hali ya maisha ni mbaya ndo hao wanatamani lock down,nchi tajiri zilitepeta kwenye lock down wakaamua kuachia.
Kikubwa ni kuishi kwa taahadhari na namna ya kujikinga imeshaelezwa na watu wote wanajua.
Tanzania kama taifa serikali imeruhusu njia za ziada za kujikinga na Covid kwa kujifukiza na kutumia dawa zingine za asili kama za NiMR.
 
Mimi na wewe kwa sababu tuna kielimu kidogo tunaweza kuamini kuwa korona ipo
Ila kuna wale raia ambao uelewa wao wa masuala haya ni mdogo, tangu Magufuli atangaze Korona haipo TZ huwaambii kitu kuhusu korona, wanajua haipo tu!. Na bahati mbaya serikali iliamua makusudi kudiscourage njia za kujikinga na korona kama njia maalum ya kurudisha "ukawaida" (Normalcy), hilo ni kosa kubwa, ilitakiwa ihamasishe jitihada za kujikinga badala ya kuzipiga vijembe
Nilienda kuangalia mechi ya simba na platnum kwa makusudi walifunga baadhi ya mageti yakabaki machache matokeo yake kukawa na msongamano mkubwa wa watu kuingia tukawa tunajiuliza kama serikali ipo makini kuzuia Corona kama inatengeneza mrundikano wa makusudi
 
Nilienda kuangalia mechi ya simba na platnum kwa makusudi walifunga baadhi ya mageti yakabaki machache matokeo yake kukawa na msongamano mkubwa wa watu kuingia tukawa tunajiuliza kama serikali ipo makini kuzuia Corona kama inatengeneza mrundikano wa makusudi
Kuna watu wanasema kuwa ishu ya Afya ni personal issue, kwamba wewe raia wewe mwenyewe chukua tahadhari!, ni sahihi kwa upande mmoja lakini siyo sahihi kwa upande mwingine kwa sababu kazi mojawapo ya serikali ni kuwa wakweli na kuupa umma information sahihi kuhusu hali ya situation ili hao raia wachukue tahadhari husika.

Ukisema korona ipo chukua tahari wewe mwenyewe ni sahihi, LAKINI SWALI LA MSINGI NI JE, WATANZANIA WANGAPI LEO HII WANAJUA, AU WANAAMINI KUWA KORONA IPO TANZANIA?

Serikali ilishatangaza ushindi dhidi ya Korona kitambo sana na ikaacha kutoa information zozote juu ya hali ya korona nchini na raia wengi wanaimini serikali yao kuwa korona haipo na hawachukui tahadhari yoyote.

Hapa ndo tunaitaka serikali itoke mafichoni iseme, Hapa Tanzania hii kitu ipo au haipo ili wale raia wanaoamini Tumeishinda Korona wasijiachie sana!
 
Jan 1 2021: Kifo cha baba mdogo, upumuaji.

Jan 14 2021 Kifo cha babu, upumuaji.

Wote walisaidiwa na mashine kupumua nyakati za mwisho za uhai wao.

ALLAH awarehemu.
Kama kusingekuwa na kinachoitwa corona basi pengine hivyo vifo hata usingekuja kuvizungumzia hapa ila kwa sababu kuna corona basi hayo matatizo ya kupumua na kuwekewa mashine za kuwasaidia kupumua yanaonekana kama ni mambo mapya yaliyokuja kipindi hiki cha corona.
 
Imeshangata family members au jirani zako wangapi?? Labda tuanzie hapo. Nadhani kila mtu aanzie kwa immediate family members na sio hadithi za sijui mtaani wanasema nini, kama mtaani ipo na familia zetu pia zipo huko huko mtaani so hawawezi ugua au kufa bila sisi kujua
Personally najua wawili Nancy kafiwa na mama mdogo wake na Witness mzee wake yuko hoi anajitibu hiyo Covid kwa mitishamba ingawa ana hali mbaya sana.

Hyo ni mifano miwili nayoweza thibitisha
 
Back
Top Bottom