#COVID19 Serikali isiwaache Wananchi katika mataa kwenye suala la Corona
mkuu tengua kauli yako utawala wa magufuli auna uwezo wa kusema Nani afe Nani asife. waliochukua hatua zote lakini bado watu wao wanafaliki
ZINGATIA. akuna mbadala wa kukwepa kifo
Eeenh, mawazo ya watu wengine yanasikitisha.

Kwa hiyo watu wajiachie tu, wasichukue tahadhari wanazoelekezwa na serikali na wataalam wao, kwa vile "hawawezi kukwepa kifo?

Unaelewa kweli ulichoandika hapo?
 
Kuna watanzania wengi sana wa uelewa mdogo hata ujaribu kuwaelewesha unaona bora ukae kimya tu.

Jana nikamuuliza kijana mmoja kaka italetwa chanjo ya corona utachanja akajibu hatachanja sababu rais ashasema hazifai.

Juzijuzi nikiwa natembea nikasiki wamama wakisema, itabidi wazae tu sababu Rais anasema haya madawa ya uzazi hayafai.

Walisikia aliposema wasichana walichanjwa kinga saratani ya kizazi kumbe walikuwa wakizuia mimba hivo alikataza eti.

Hata kuvaa tu barakoa mpaka wamsikie rais akitamka. Aliposema tu walipima mapapai wakakuta yana korona haaa watu waliona ni ujinga tu kupoma korona
Hata humu tu kuna uelewa mdogo kuhusu anachosema mkuu. Hata kama hawaelewi alitania au alisema wakati gani wamejipanga tu kutetea hadi shingo zinakakamaa.

Hawa wanaotetea na kujipendekeza kulikopitiliza ndio wanaharibu nchi yetu.
Yaani hawataki kusikia mawazo mbadala.

Ona walisaidia sana kuua upinzani kama sauti mbadala eti wanasaidia azma ya mkuu kumbe hata hawkumuelewa.

Waimba pambio wamegeuka wapembe wa mganga wakitafsisri asichomaanisha mganga.
Tupaaze sauti kuwakemea hawa watu la sivo tutaweza kutumbukia shimoni
Umesahau na lile kundi ambalo wana uelewa ila wametanguliza sana siasa mbele,hili kundi lilifanya makosa sana kipindi cha kampeni mwaka jana kwa kuungana na hao wasio na uelewa walisambaza sana maambukizi ya corona kipindi kile wakafanya hata Mkuu kujisifu kwamba hao waliyokuwa wanamkosoa nao wamekubaliana nae kwamba hakuna corona,cha ajabu nao wakaja na utetezi wa kijinga et kipindi kile corona ilipungua
 
Anataka nini !? Mbona hajapendekeza solution...
Kwa bahati mbaya wakosoaji wengi bongo hawakosoi ili hilo jambo lipatiwe solution,mfano sasa hivi solution hapo utaambiwa ni serikali kukiri kuwepo corona nchini kupima na kutoa takwimu na kuwaambia watu wachukue tahadhari. Ila mie nakwambia hata hayo yakifanyika bado lawama zitaendelea kuwepo kama ilivyokuwa mwaka jana mwanzoni ambapo hayo mambo yalikuwepo ila bado wakosoaji waliendelea kukosoa kwamba ilionekana bado hayo mambo hayatoshi na wengine walibeza kuwa hatuwezi kuondoa corona kwa kunawa mikono. Ajabu kampeni zilipoanza hakukua na ukosoaji tena hadi sasa ndio yameanza tena.
 
Mabibi na mabwana kwa mwendelezo huu:

IMG_20210213_164514_304.jpg


Sisi wazee na wenye magonjwa mengine ni muda wetu sasa kuanza kupaza sauti zetu na kuifahamisha serikali na wote wanaojifanya kutusemea kuwa sasa inatosha!

Sisi kama binadamu hatuoni ni sawa kutelekezewa gonjwa hili. Kwamba nyie haliwahusu au nyie mna mazingira wezeshi zaidi au nyie hata mmeshapata chanjo nk haiwahalalishii nyie kuona sisi kufa ni sawa ila nyie.

Ubinafsi wenu unatuelekeza kubaya. Ni wazi kuwa ubinafsi huo utakuwa unatuelekeza kwenye makabiliano ambayo kwa hakika ni kwa ajili ya kupigania uwezekano wetu nasi wa kuweza kuishi. Yaani our right to survive.

Ya "survival of the fittest" si katika jamii ambako kodi inakusanywa kwa wote.

Tutakufa tukipambana ikibidi na nyie kama hiyo itatupa nasi fursa ya kuishi dhidi yenu nyie mliokwisha ridhia sisi kujifia kibudu.

Kama hatua ya kwanza tutaanza kuhoji kikamilifu uhalali wa sisi kulipa kodi wakati kodi hiyo haina manufaa na sisi katika wakati wetu wa uhitaji.

Ninawasilisha.
 
Kwani kuna mtu kasema huna haki ya kuishi?

Mbona unvaongea kama umekatwa kichwa?
 
Huna haki ya kuishi kwa sababu wakati wahuni na mabumunda wanachukua nchi kwa njia za hila na za kihuni wewe uliishia kukenua meno!Sasa hivi ni wakati wako wewe kulipa uzembe uliofanya,na utalipa kupitia kifo.
Camooon meeen!!!
 
Huna haki ya kuishi kwa sababu wakati wahuni na mabumunda wanachukua nchi kwa njia za hila na za kihuni wewe uliishia kukenua meno!Sasa hivi ni wakati wako wewe kulipa uzembe uliofanya,na utalipa kupitia kifo.
Duh; hata kama ni kulipia uzembe malipo yamekuwa ya gharama kubwa kupitiliza. Adhabu hailingani na kosa.
 
Camooon meeen!!!
Ukweli lazima usemwe. Nitasema kweli dhaima, fitina kwangu mwiko. Watu wanapukutika kama Nzige waliopigwa dawa kwa sababu ya Irresponsible Government!

Kungekuwa na mkono wa serekali katika kuzuia/kudhibiti gonjwa hili nina imani vifo vingepungua sana tofauti na sasa hivi ambapo kila mtu anajiamulia kiholela cha kufanya.Hakuna mkono wa serekali kwa sababu serekali hii haikutokana na kibali cha wananchi.
 
Hili sio la kulaumu utawala ( serikali hii tu ), misingi katika sector ya afya kabla ya JPM haikuwa mizuri ( ni kitu endelevu kinaendelea kuboreshwa siku hadi siku ), capacity ya miundombinu na pesa kutokana na mlipuko wa gonjwa hili havijaendana na sio kwamba serikali imetelekeza watu wake.

Serikali imetoa maelekezo na kwa kadri ya uwezo wake ikijumuisha utaalamu, vifaa tiba, na pesa. Sie kama Taifa ni lazima tukubali na tuelewa hali harisi ya taifa letu, Tusitake kuishi kama USA au QUTAR au U.K. Kuna mambo mengine twendeni na uharisia, tofauti na hapa tutaishia pingana pasipo na majibu.

Idadi ya vifo, haina takwimu sahihi, na pia wanao kufa hatuwezi sema wote ni Corona, kumezuka tabia ya kila kifo watu kuhusisha na covid 19. Jiulize kabla ya COVID 19 kwa siku walikuwa wanakufa watu wangapi na baada ya COVID 19 wanakufa watu wangapi ??

Tuchukue taadhari sie wenyewe zaidi kwanza, maana ni afya zetu na uhai wetu. Kabla ya kuanza tafuta kasoro za serikali.

Janga la Corona halina cha kufanya na serikali zilizopita. Janga la Corona lina mambo ya msingi sana serikali zote duniani zinawajibika kuyafanya sasa.

Serikali yetu kwa mujibu wa katiba haina dini wala haifuati imani za kishirikina. Nchi yetu ni ya kidemokrasia inayopaswa kuendeshwa kwa masikilizano na si kwa matakwa ya mtu mmoja.

Serikali hii haitutendei haki sisi wazee na wenye magonjwa mengine kwa kututelekezea gonjwa. Tunayo haki ya kuishi kama ilivyo kwa mlipa kodi yeyote:


Wewe huoni hivyo jombi?
 
Huna haki ya kuishi kwa sababu wakati wahuni na mabumunda wanachukua nchi kwa njia za hila na za kihuni wewe uliishia kukenua meno!Sasa hivi ni wakati wako wewe kulipa uzembe uliofanya,na utalipa kupitia kifo.
Ungetoka nje wakati ule hata wewe ungesha RIP. Wale Askari walilipwa US$500 kwa siku kuhakikisha Kayafa anaapishwa.
 
Huna haki ya kuishi kwa sababu wakati wahuni na mabumunda wanachukua nchi kwa njia za hila na za kihuni wewe uliishia kukenua meno!Sasa hivi ni wakati wako wewe kulipa uzembe uliofanya,na utalipa kupitia kifo.

Mkuu ninakuelewa ila:

Ninayo haki ya kuishi. Nimepambana na udhalimu wa wapora nchi hawa si kuanzia leo:


Ninapambana nao leo na nitapambana kesho na hadi siku yangu ya mwisho duniani.

Sina popote nilipowahi kukenua jino kwa ajili yao, achilia mbali ya unayoita meno. Sina popote ambapo nina mchango wowote kwao kwenye dhuluma zao.

Kimsingi tuhuma zako za kweli zimeelekezwa to a very wrong person.
 
Janga la Corona halina cha kufanya na serikali zilizopita. Janga la Corona lina mambo ya msingi sana serikali zote duniani zinawajibika kuyafanya sasa.

Serikali yetu kwa mujibu wa katiba haina dini wala haifuati imani za kishirikina. Nchi yetu ni ya kidemokrasia inayopaswa kuendeshwa kwa masikilizano na si kwa matakwa ya mtu mmoja.

Serikali hii haitutendei haki sisi wazee na wenye magonjwa mengine kwa kututelekezea gonjwa. Tunayo haki ya kuishi kama ilivyo kwa mlipa kodi yeyote:


Wewe huoni hivyo jombi?
Mkuu mie nakuelewa vizuri sana. Siangalii serikali katika negative pekee ( katika yale iliyo shindwa ), naangalia pia katika yale iliyoweza kuyafanya pia na yakawa na faida kwa jamii. Swala la afya nchi nyingi za africa zimekuwa nyuma, na zimekuwa zinategemea zaidi misaada katika sector ya afya hata katika janga la corona nchi nyingi hazina uwezo wa kukabiliana nalo wenyewe hadi pale ambapo wame wezeshwa misaada. Kwa nchi yetu imepata fund ya kutosha ?
 
Tunaaminishwa kuwa si jukumu la serikali kuongeza vituo vya kupimia covid na walioathirika kupata matibabu stahiki.

Badala ya kusubiri Serikali Kwanini sisi wananchi tusianze kuonyesha tunachohitaji? Kwanini wananchi tusijitolee kusaidia Hospitali ambazo tayari zipo uwezo wa kutoa huduma? Kwanini kila kitu tusubiri serikali?
 
Duh; hata kama ni kulipia uzembe malipo yamekuwa ya gharama kubwa kupitiliza. Adhabu hailingani na kosa.
Niliwahi sema hivi hapa JF:

Gharama ya watu kupuuza siasa katika nchi si tu ni kubwa mno na hailipki kwa masikini na matajiri,bali hakuna hata tajiri anaeweza kuimudu.

Mfano, safari hii hata matajiri wakiwemo kina MO, wameonja adha ya siasa na wanasiasa baada ya kutekwa.

Na sasa changamoto ya upumuaji na madhara yake inayochangiwa na maamuzi mabovu ya wanasiasa wetu hata matajiri hawako salama.
 
mkuu tengua kauli yako utawala wa magufuli auna uwezo wa kusema Nani afe Nani asife. waliochukua hatua zote lakini bado watu wao wanafaliki
ZINGATIA. akuna mbadala wa kukwepa kifo
Kwel jf kuna wato
mkuu tengua kauli yako utawala wa magufuli auna uwezo wa kusema Nani afe Nani asife. waliochukua hatua zote lakini bado watu wao wanafaliki
ZINGATIA. akuna mbadala wa kukwepa kifo
Kwel jf kuna wat mko na akili sana asante mkuu kwa. Kuona hil
 
Ungetoka nje wakati ule hata wewe ungesha RIP. Wale Askari walilipwa US$500 kwa siku kuhakikisha Kayafa anaapishwa.

Mapambano si ujinga. Mapambano ni strategies:


Labda jombi ndiyo kawasili tokea sayari nyingine.
 
Back
Top Bottom