#COVID19 Serikali isiwaache Wananchi katika mataa kwenye suala la Corona
Mabibi na mabwana kupeana ulio ukweli hata kama ni mchungu vipi ni jambo la msingi sana.

Haisaidii kuukimbia ukweli.

Kwa hakika hali ya ugonjwa huu ni mbaya sana labda kuliko hata maelezo. Niko Kagera kwa mazishi ya kigogo wa mahakama kuu Mwanza.

Nakutana na misiba zaidi. Itoshe kuonyesha hali hii:

"Bwana Tumsiime mmiliki wa zile shule maarufu Dar kafiwa na mama mkwe na pia shemeji yake ndani ya siku 2 tu."

Pole nyingi ziwafikie yeye na familia yake.

Alianza shemeji, akaenda kuzika na kurejea Dar. Juzi tena, mama mkwe aliyekuwa msibani kwa mwanaye naye kafariki. Amelazimika kurejea kwa mazishi tena.

Changamoto zile zile, watanzania wale wale.

Kwani mengine yapi ni mageni wapi?

View attachment 1703411

Ukweli mchungu, watu wanakufa sana na ugonjwa huu.

Maswali yangu ya msingi kwenye vita hivi nikidhani tuko sote, yamekuwa haya hapa:

View attachment 1703412

Sijapata majibu yake popote.

Ni wazi kuwa kudhani kuwa vita hivi vingepiganwa katika umoja wetu kama taifa, kama ilivyo kwingine, hakupo.

Basi wala isiwe taabu.

Rasmi sasa hapa tulipo ni kila mtu na lwake. Kila mtu ikiwamo serikali, sasa na apigane kivyake.

Kila mtu na achukue njia yake. Kila mtu achukue mzigo wake. Tuachane njia panda.

Kama binadamu mwenye kuwajibika na familia yangu, nami ninachukua njia yangu japo nikiwa nimechelewa sana.

Tusijuane.
Jana uzi wangu ulipigwa pini! Nilikuwa nahusisha uhusika wa vifo na viongozi wanatuhamasisha hakuna korona ilihali wao wanajificha na wengi tuna taarifa wamepokea chanjo! . Mod aliogopa lakini ukweli ndio huo. Hii ni masacre! tupende tusipende. Nimezika kaka yangu! Mimi na familia yangu yote ni wagonjwa tumeenda hospitali tumerudishwa nyumbani! Tuende wapi??
 
Mimi huwa nawaza watoto wa shule ingawa wao "changamoto" haiwasumbui sana.
 
Jana uzi wangu ulipigwa pini! Nilikuwa nahusisha uhusika wa vifo na viongozi wanatuhamasisha hakuna korona ilihali wao wanajificha na wengi tuna taarifa wamepokea chanjo! . Mod aliogopa lakini ukweli ndio huo. Hii ni masacre! tupende tusipende. Nimezika kaka yangu! Mimi na familia yangu yote ni wagonjwa tumeenda hospitali tumerudishwa nyumbani! Tuende wapi??
Pole sana ndugu yangu. Mzee laizer amazika ndugu watatu ndani ya juma lilopita, alianza mkewe, akafuata mamamkwe, akifuatiwa na shemejiye mjane wa marehemu kakaye.
 
Pole sana ndugu yangu. Mzee laizer amazika ndugu watatu ndani ya juma lilopita, alianza mkewe, akafuata mamamkwe, akifuatiwa na shemejiye mjane wa marehemu kakaye.
Umeipata hii ya wahadhiri wa SUA?
Dr Delphina-7/2/2021
Dr Mamiro Mume wa Delphina- 9/2/2021
Mama yake Delphina- 14th January 2021
Shangazi yake Delphina16 Jan 2021
Baba yake Delphina 23 Jan 2021
Shemegi yake Delphina- 16/1/2021
Dereva wake Delphina-10/2/2021
Wote walifariki katika kipindi kifupi.
Hizi Mbwa zinazojiita wanasiasa hawaniambii lolote sasa hivi. The suffering is beyond repair.
 
Jana uzi wangu ulipigwa pini! Nilikuwa nahusisha uhusika wa vifo na viongozi wanatuhamasisha hakuna korona ilihali wao wanajificha na wengi tuna taarifa wamepokea chanjo! . Mod aliogopa lakini ukweli ndio huo. Hii ni masacre! tupende tusipende. Nimezika kaka yangu! Mimi na familia yangu yote ni wagonjwa tumeenda hospitali tumerudishwa nyumbani! Tuende wapi??
Pole sana ndugu, tuna ombwe la uongozi, mbaya zaidi wanaiona hali na vifo vya watu ila hawajali! Huwa naangalia wakienda kuwazika wabunge na wengine wenye vyadhifa, ndipo napokumbuka machoni kama watu.. . ila mioyo yao ni bora Simba mwenye njaa[emoji706]
 
Hakuna kuzuia ndege kuja kwetu HAPANA, TUSIKUBALI.

Uamuzi sahihi ni Dunia kutusaidia kumwonfoa muuaji. Haiwezekani Dunia ikae kimya ikimwangalia kichaa mmoja akiangamiza mamilioni ya watu. Siyo sahihi. Dunia ibebe jukumu lake la msingi laf kuifanya Dunia mahali salama.
Ndio maana nasema nijuu yake na serikali kwa ujumla kubadilika haraka au watatuingiza katika doa jeusi katika history ya nchi kuja kujisafisha tena itachukuwa miaka. sisi tuna history nzuri miaka yote hatujawahi kuwa hivi tulivyo sasa.

Kama nilivyosema Corona sio ugonjwa wa Tanzania tu huu ni ugonjwa wa dunia na ukishakuwa wa dunia maamuzi ni ya dunia sio ya mtu au nchi moja moja.

Kama kuna kipindupindu basi usafi ni lazima kwa kila mtu sio unasema mimi kwangu kusafi ila jirani hakufai kawaida anapigwa fine na kushtakiwa kwa kuwa unahatarisha mtaa mzima na wakazi wote sio wewe tu na ndivyo ilivyo corona.

issue yake ya kuponda chanjo sasa kwa data watu wamethibitisha kuna mafanikio yanaonekana. hatuwezi kudharau science ndio msingi wa kila kitu hata Mungu alisema soma, na science iko katika dini.
 
Hakuna kuzuia ndege kuja kwetu HAPANA, TUSIKUBALI.

Uamuzi sahihi ni Dunia kutusaidia kumwonfoa muuaji. Haiwezekani Dunia ikae kimya ikimwangalia kichaa mmoja akiangamiza mamilioni ya watu. Siyo sahihi. Dunia ibebe jukumu lake la msingi laf kuifanya Dunia mahali salama.
Senseless opinion
 
Nimeona matamko ya Wamarekani, Waingereza na sasa wajapan. Juzi waangola wametuonesha kuwa na afrika siye hatukaribishwi na yeyote.

Isipokuwa Tanzania na Burundi nchi zote zimekubali kupokea chanjo ya Covid19.

Ni Tanzania tu ambapo takwimu za vifo na wagonjwa wa covid19 haziwekwi wazi.

Ni Tanzania tu ambapo Rais anasimama majukwaani na kutangaza kuwa hakuna corona.

Ni Tanzania tu ambapo taarifa kuhusu korona ni classified!

Ni Tanzania tu ambapo raia wanakufa kwa korona lakini hakuna anayeruhusiwa kusema.

Ndugu wamekufa, watu ni wagonjwa, maisha ni jehanam tuende wapi?

Tujadili
 
Back
Top Bottom