#COVID19 Serikali isiwaache Wananchi katika mataa kwenye suala la Corona
Kwenye suala la Ulinzi wa mwili hapo Mungu sidhani kama ataweza maana kama ingewezekana najua kwa imani aliyo nayo Rais angesema hata walinzi hataki amemwachia Mungu. Maana atakaye ikoa nafsi yake ataipoteza.
Kwani Corona inaingia kwenye mwili au kwenye nini?
 
Pamoja na kuonfoa hofu katika jamii, suala la maambukizi mapya, 2nd wave ya covid 19 bado limekuwa tishio kubwa.

Madaktari bingwa na wanasayansi waliobobea wameluwa kimya utafikiri wamewekewa maji baridi.
Kama kuna kada itaokoa wananchi na janga hili ni utaalam wa kidaktari na afya ya jamii.

Cha ajabu sasa hivi waongeleaji wakubwa wa ugonjwa utokanso na maambukizi ya covid19 ni wanasiasa na watu wa dini, makasisi, maaskofu na mashekhe.
Mara tusivae barakoa, mara tumepona Mungu ameponya, mara tuvae tena barakoa!
Hii ni ajabu sana kwa Tanzania.
Hivi hatuna Dkt Fauci wa Tanzania?
 
Kama kweli nyie ni wapenda ukweli amkeni usiku wa manane muone buguruni palivyojaa watu wakihangaika, huyu anaemda Kariakoo,huyu Ubungo ,yule G mboto. Kwa ujumla ni mshikemshike. Watu wako busy kusaka maisha yao.

Ninyi mpo mitandaoni, mnakesha kueneza kile ambacho hakipo. Maana hata kama kuna uwepo wa Covid 19 sio kwa kiasi mnachokieneza kwenye mitandao.

Mbaya zaidi wengine mpo Usa,Uk na Sweden. Mnaishi kwa migongo ya kodi za wazungu. Lakini kila siku ni kueneza uongo kuhusu Tanzania. Kama hali ni mbaya kiasi hiki, hivi hapa bongo tutaishi?

Huko mikoani watu wako busy wanalima,wanafanya biashara. Ninyi mmebakiza kupiga propaganda za uongo kama kwamba sasa watu wanadondoka kama mdondo.

Kweli tatizo lipo maana Tanzania sio kisiwa, lakini mnaeneza uongo mwingi kuliko uhalisia.

Kumbukeni Mungu ni muweza, na anawalinda Watanzania. Hata kama mlitaka kushudia maelfu wanakufa kwa siku,Mungu atawalinda.
 
Nadhani kuna kitu hakipo sawa, ingawa changamoto ya ukimya iliyopo itawamaliza kimya kimya.

Tumeusiwa kutokuongea bila data, ila hii kada ya afya pia wanaondoka mno kutokana na covid. Nadhani hawachukui tahadhali za kutosha wanapowahudumia wagonjwa wao.
 
Pamoja na kuonfoa hofu katika jamii, suala la maambukizi mapya, 2nd wave ya covid 19 bado limekuwa tishio kubwa...
Kwa hiyo wewe unataka waseme nini? Madaktrai unawategemea wako chini ya mkono wa Mungu unayemdharau. Na usipotubu upumbavu wako wa kumdharau Mungu, shauri lako. Endelea kukufuru. Sisi tunajua wave ya kwanza ya COVID 19 Mungu alituponya na madaktari walishuhudia hili. Leo wewe unajifanya mungu mpumbavu.

Ni mpumbavu kwa kuwa hata maelekezo ya rais huwezi ku yelewa. Wapi amesema usivae barakoa? Mbona wewe juha sana? Kama hrauwezi kuelewa ama kwa ushetani wako unabadilsha statement za Magufuli ili kumfurahisha shetani, huwezi kumwelewa Fauci na ndiyo sababu unamshangilia.
 
Kwa hiyo wewe unataka waseme nini? Madaktrai unawategemea wako chini ya mkono wa Mungu unayemdharau. Na usipotubu upumbavu wako wa kumdharau Mungu, shauri lako. Endelea kukufuru...
Utanisamehe ndugu yangu.

Unachosema ndio upotoshaji wa hali ya juu katika gonjwa hili.

Kwa hiyo mtu akiambukizwa aende kanisani au msikitini kusali na kuswali?
Huu ni ujinga uliopitiliza.

Na hao madktari bingwa tumetumia fedha nyingi za kodi zetu kuwasomesha. Mbona hatuwasikii katika suala la Public Health katika hili, misingi ambayo ni ya kisayansi.
 
Utanisamehe ndugu yangu.
Unachosema ndio upotoshaji wa hali ya juu katika gonjwa hili....
pale politics onapo zidi professiinalsm. ndicho konachotokea sasa. Hata madaktaru bingwa wameshindwa kuwa na msimano kabisa. wote wanasifu na kuabudu.. taaluma wameweka mfuko wa nyuma.

kisa mtu mmoja tu. ambae hana taaluma hiyo. kwa umoja wao MAT wanashindwa nn?
 
Nadhani kuna kitu hakipo sawa, ingawa changamoto ya ukimya iliyopo itawamaliza kimya kimya.

Tumeusiwa kutokuongea bila data, ila hii kada ya afya pia wanaondoka mno kutokana na covid. Nadhani hawachukui tahadhali za kutosha wanapowahudumia wagonjwa wao.
and maybe wana uhaba wa vifaa. so wanafanya kazi kwa mazingira yale yale.
ndio maana wanakuwa exposed, lakin wapi watapeleka malalamiko haya? maana kila mahali ni siasa
 
Corona ipo duniani na Tanzania siyo kisiwa.

Nchi kuwa na Corona siyo aibu, maana kirusi mpaka serihakijui mipaka ya kisiasa...
Hivi Ni kweli hujasikia serikali ikihimiza watu kuchukua tahadhari? Hata kule kuambiwa tumia barakoa uliyoshona mwenyewe ni tahadhari kubwa Sana dhidi ya Corona, je hujawahi kusikia?
 
Kama kweli nyie ni wapenda ukweli amkeni usiku wa manane muone buguruni palivyojaa watu wakihangaika, huyu anaemda Kariakoo,huyu Ubungo ,yule G mboto. Kwa ujumla ni mshikemshike. Watu wako busy kusaka maisha yao...
Ni kweli kabisa! Akifariki mtu tu tayari ni kosa kana kwamba kabla ya Corona watu walikuwa hawafi!

Kabla ya Corona changamoto za kupumua zilikuwepo na zilishika nafasi ya pili Tanzania na duniani kwa ujumla kwa kusababisha vifo. Takwimu hizi kazionesha naibu waziri wa afya Jana asubuhi wakati akihojiwa na watangazaji wa Wasafi Redio.

Leo hii mtu akifa kwa changamoto ya upumuaji wahuni akiwemo zytow wanasema Ni corona!! Ili mradi tu mabwaana wao mabeberu wafurahi!!!
 
Corona ipo duniani na Tanzania siyo kisiwa.

Nchi kuwa na Corona siyo aibu, maana kirusi hakijui mipaka ya kisiasa.

Serikali zilizo responsible duniani zinaendelea kutekeleza sera za kupambana na Covid na kamwe hazitangazi kuwa zimeshashinda vita tayari, bali zinakuwa cautious na zinaendelea na jitihada za kupambana na huu ugonjwa.

Siyo siri, sisi Tanzania kwa kiwango kikubwa tulinusurika na wimbi la kwanza la maambukizi yale. Mungu wetu alitusaidia na kwa kweli watanzania walijitahidi pia kuchukua hatua, kila sehemu kulikuwa na ndoo za kunawa mikono etc

Pamoja na mafanikio yale haikuwa sahihi na haiendelei kuwa sahihi serikali kukaa kimya na kuacha kila mtu aamini Korona haipo nchini, au kuuaminisha umma kuwa korona haipo kabisa. kufanya hivyo siyo sahihi hata kidogo

Lakini cha kushangaza zaidi ni pale serikali na vingozi wake walipoanza kudiscourage wananchi kuchukua hatua za kujikinga. Barakoa zilianza kufanyiwa mizaha etc

Serikali ilipaswa iendelee kuhimiza watu waendelee kuchukua hatua, na kuencourage watu kujilinda lakini siyo kudiscourage measures zote ambazo wananchi wanafanya.

Labda kitu kimoja ambacho serikali lazima ielewe ni kuwa sasa wananchi wameanza kuwa na wasiwasi kuwa Korona ipo nchini, lakini wanakosa uhakika wa kimamlaka kulichukulia kwa uzito stahili maana serikali imeamua kupiga kimya!

Mimi ningependa kuieleza serikali yetu kuwa ni higly irresponsible katika kipindi hiki dunia imeingia katika vita ya pili juu ya huu ugonjwa lakini yenyewe imekaa kimya tu inawaacha wananchi peke yao utafikiri kondoo wasio na mchungaji.

Tunataka kusikia kauli ya serikali. Je, Corona ipo Tanzania? Je, serikali ina mpango gani au imeamua wenye kuugua waugue, wenye kufa wafe lakini yenyewe itakaa kimya tu?

Nchi jirani zetu baadhi zimeanza kuchukua hatua kali mipakani mwao kuhusu wanaoingia, je sisi mambo shwari tu hakuna ishu?

Sisi tukimuona rais wetu amekwenda tena Chato kipindi hiki tukiambiwa kuwa Corona imechachamaa huko duniani tunapata wasiwasi kuwa huenda yasemwayo mitaani kuwa ni kweli maana tunakumbuka kipindi kule rais alipokwenda kukaa huko Chato kwa zaidi ya miezi miwili kipindi Corona imechachamaa mwaka jana! Je, ngoma imerudi kama mwaka jana?

Tunataka serikali itupe majibu, tunataka kujua status ya hali ya Corona nchini, maana baadhi ya watu wanaoaga dunia kuna watu mitaani wamekuwa wakinong'ona kuwa Korona ipo na inang'ata.

Wananchi tunataka majibu, tena majibu sahihi ya hili suala!
Lazima tuji ulize maswali. Rais Magufuli pamoja na team yake ikulu lazima wanafahamu vizuri sana kuhusu ugonjwa huu wa corona, athari zake na njia za kuji kinga. Wao kusema kwamba hatuhitaji lockdown wala chanjo zinazo tolewa nchi zingine na ku ongezea haya kwa kusema kwamba tumtegemee Mungu kutusaidia ni njia moja ya kusema kwamba

1. Tuna fahamu kuhusu Janga hili vizuri ila tatizo hili halipo Tanzania

2. Takwimu za waathirika wa ugonjwa huu nchini hazipo

3. Takwimu za waathirika wa ugonjwa huu nchini zipo ila hatutaki kutangaza

4. Waathirika wa Corona wapo nchini ila tatizo limefanyiwa kazi na kwa uhakika watanzania walio wengi wata nusurika..

- Kama kweli kuna waathirika wa Corona Tanzania, ni lazima wahusika serikalini wanafahamu kwamba huwezi kusema Mungu atasaidia bila kuchukua hatua zingine kulinda watanzania wote. Yanayotokea sasa hivi yame kusudiwa
 
pale politics onapo zidi professiinalsm. ndicho konachotokea sasa.
hata madaktaru bingwa wameshindwa kuwa na msimano kabisa. wote wanasifu na kuabudu.. taaluma wameweka mfuko wa nyuma.

kisa mtu mmoja tu. ambae hana taaluma hiyo. kwa umoja wao MAT wanashindwa nn?
Hivi ulimsikia naibu waziri wa afya alipokuwa anazungumza na watangazaji wa Wasafi Redio? Je alikuwa anaongea Siasa au sayansi ya tiba? Hoja zake zimesimama kisayansi na dunia inajifanya kuwa haijamsikia kumbe imekosa namna ya kujibu hoja zake!!
 
and maybe wana uhaba wa vifaa. so wanafanya kazi kwa mazingira yale yale.
ndio maana wanakuwa exposed, lakin wapi watapeleka malalamiko haya? maana kila mahali ni siasa
Exactly, wana vifaa duni vya kujikinga wakati wa kufanya utabibu
 
Back
Top Bottom