Serikali kuwajadili waliokataa Ukuu wa Wilaya

Inaonyesha ni zaidi ya hilo bali wanawaondoa kijanja.. ujanja umefeli wamekasirika. Nafasi wana wakuwapatia wengine tayari
 
Kwa ni wasiteuliwe vijana wasio na ajila, wasomi ni wengi
 
Raisi siyo mjinga kuamua kuwatenganisha wale wezi,CWT kuna mpasuko mkubwa mpaka akaamua kutumia busara kufanya vile
Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na watu wengine wote wanaweza kupangiwa kazi yoyote na Raisi we unakataa kama nani?
 
Katiba Katiba Katiba....

Sasa ubovu wa katiba yetu unaanza kuwaumbua wenyewe .
 
Tatizo lao waliwekeza kwenye mitandao wakaona deal. Wangeweka mikakati ya kukataa kimyakimya huenda yasingekuwa haya. Tatizo wakaanza kupayuka kwenye makundi yao ya whatsapp. Hivyo vyeo walivyonavyo kama ndio vinawapa ujeuri watavisikia tu kwenye bomba na ukaguzi dhidi yao utawafuata.
 
Mh Rais imulikeni CWT!!! Kikichotokea nimrejesho kuwa ndani ya CWT Kuna ujujaji wa kutisha, pia napendekeza walimu wakatwe tsh 8000 kama CWT contribution!! Wasikatwe kulingana na ukubwa wa mshahara kama ilivyo sasa
Ukweli ni kuwa tabia na mienendo ya CWT haina tofauti na Ile ya CCM.Rushwa ,wizi,upendeleo ubadhilifu ndio kwao.Waliomo CWT hawataki kutoka kwakuwa Kuna ulaji mkubwa.Nafurahi kuwa siyo mwanachama wao
 
bora ya hao waliokataa uteuzi huo kuliko kukubali hali yakuwa mtu uwezo huo hana mfano alikuwepo mkuu wa wilaya kilombero huyu
huyu mama alikuwa mzigo mzito yani ajiwezi kabisa sasa katumbuliwa bodo ofisi ya aridhi nayo imeoza
 
Mbona habari hii kama ilikanushwa vile kwenye vyombo vya habari? au mimi sielewi yani nimecheck Clouds nimemuona huyo mteule akikana kuwa hajakataa uteuzi hizo ni propaganda za waandishi naombeni ufafanuzi.
 
...wastage of time and resources, kwwani hii ni vita ya mtukula kwamba mtu asipokwenda anachukuliwa hatua? Au walitaka wakaripoti, wasitimize wajibu wafukuzwe kwa aibu?
Humu jukwaani naona watoto ni wengi sana; hawaijui kabisa Serikali namna ambavyo huwa inafanya kazi.

Kama una akili timamu, naomba uchukue funzo kutoka kwenye swala hili halafu litakusaidi maisha yako yote hadi uzeeni utakapokuwa una miaka 90+
 
Haya maoni based kwenye hasira fulani hivi!
Watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria naamini rais wa sasa si kama aliyepita hatoruhusu wachukuliwe hatua ikiwa hakuna sheria inayotamka kumkatalia rais uteuzi ni kuvunja kifungu namba fulani cha sheria fulani ya mwaka fulani!
 
Ataharibu vipi?Hao watu wamejazwa viburi na fedha za WALIMU ambao wapo wapo tu
Maendeleo ya nchi yatapatikana kwa viongozi kupenda kuwa viongozi wa wananchi, mtu asilazimishwe kuwa kiongozi wa siasa wakati mwenyewe anayaona mapungufu yake. Cheo ni dhamana..........
 
Mh Rais imulikeni CWT!!! Kikichotokea nimrejesho kuwa ndani ya CWT Kuna ujujaji wa kutisha, pia napendekeza walimu wakatwe tsh 8000 kama CWT contribution!! Wasikatwe kulingana na ukubwa wa mshahara kama ilivyo sasa
Huko mbele ya safari nadhani kuna haja angalau tukapitisha hata
Tukiruhusu kila mtu afanye analoona linafaa Nchi itaenda kweli?
Tunatakiwa tuigawane nchi kila mtu kwenye mji wake awe ni Nchi kamili inayojitegemea. Yaani hawa watu nawatamani wangekuwa kwenye anga zangu lakini ubaya meno sina. Hatuwezi kuwa tunaishi holela tu namna hii utafikiri ni wanyama porini
 
Kwa hiyo kwako ipi bora?

Aende aharibu au akatae kwenda kuharibu?
Uteuzi wao umezingatia mambo kadhaa muhimu sana ikiwa ni pamoja na kuonekana kuwa wana rekodi ya kufanya vizuri sana au kutokuharibu kwenye sehemu walizopo sasa. Kwa nini itarajiwe kuwa watakwenda kuharibu walikoteuliwa ilhalii kwenye post ambazo si za uteuzi hawajawahi kuharibu?
 
Hao wala haina haja ya kutumia nguvu. Wahamishiwe kuwa wakufunzi chuo chochote cha ualimu grade A, au ofisi za TSC wilaya yoyote au wathibiti ubora wa shule (tena wale wa chini)

Mtumishi haruhusiwi kukataa uhamisho, hapo watakuwa wamewamaliza maana sifa ya kuwa kiongozi CWT ni uwe mwanachama na wakufunzi sio wanachama hivyo automatically watakuwa wameondoka CWT kirahisi tu.

Lakini kwenye uteuzi hapo wana hiari ya kukubali au kukataa
 
Siyo kila mtu anaweza kuwa DC
Uko sahihi kabisa. Ndiyo maana mamlaka za uteuzi zikawaona wao kuwa wanafaa kuwa ma-DC na siyo mimi au wewe. Vinginevyo kama mimi na wewe tungekuwa tunafaa na si wao, basi wao wasingeteuliwa ila mimi na wewe ndiyo tungekuwa kwenye list hiyo
 
Siasa ni kazi ya muda mfupi, heri ubaki kwenye ajira ya kudumu

Hili halipaswi kujadiliwa kuna watu wanaweza ku-cover hizo nafasi. Ila chawa hiyo ni wake up call kwao.
Ulikuwa ni mwalimu umeteuliwa kuwa DC. Ikitokea umetenguliwa u-DC, unarudi kuwa mwalimu; hufukuzwi kazi ya ualimu kisa ulikuwa DC halafu ukatenguliwa, hicho kitu hakipo
 
Sasa wao wameteuliwa na mpaka siku ya uapisho awajatoa sababu yoyote kama walikuwa awataki walitakiwa wamwambie aliewateua
 
Nadhani Kwa nchi za kidemokrasia hili lisingebebe vichwa cha habari.

Hutaki uteuzi anapewa mwingine anayehitaji hakuna haja kuwekeana vinyongo.

Sana sana wahusika walitakiwa washukuru na kukataa kwa heshima
Tatizo wahusika awajashukuru wala awajakataa
 
Kama hili Jambo limefika mezani kwa Jenista, CWT waandae uchaguzi na segerea wakae mkao wa kupokea wateja.
Naelewa unachoongea. Kile kimama huwa hakina vitisho ni kistaarabu sana, sijawahi kukiona kinatishia watu; watu ambao huwa hawatishi wanatisha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…