Serikali toeni hizo Combination za Dini hii siyo nchi ya kidini

Serikali toeni hizo Combination za Dini hii siyo nchi ya kidini

Aliyepanga haya masomo yafundishwe shule na mengine yasifundishwe shuleni nani?
Tatizo lenu tz hamna akili ya kuona madhara kufundishwa dini siyo kuwa muadilifu ...shuleni wanafunzi wangefundishwa uadilifu tu ...dini zifundishwe sehemu stahiki maana dini zipo nyingi tena zinapingana zenyewe kwa zenyewe ...waafrica tutazidi kuwa watumwa wa wazungu na waarabu milele daima kama tutaendekeza upumbavu ...kesho na kesho kutwa mashoga nayo yata anzisha dini yao ya ushoga na kutaka ifundishwe serikali..kesho na kesho kutwa freemason nao hivyo hivyo ....[emoji117][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90]
 
Hii nchi nahisi imelaaniwa kwa kutokuwa na viongozi wasio na akili kwa kweli. Hivi somo la dini za Watu zisizo tuhusu sie Watanzania zinamsaidia nini mtoto au hata Tanzania tu? Yani viongozi wetu maka leo hii hawajuwi kuwaití dini hihi za Watu ndizo zinafanya Watoto wetu kiwa wajinga? Kama picha hapo juu inavyojionyesha, wenzao wako bizę kwenye sayansi się wanetu wanakariri Qur'an na kujifunza ujinga na wengine wanahubiri vitu wasivyovijuwa kwenye vituo vya madaladala. Kwa kweli CCM has failed this nation.
Ccm ni mafiiiiiiii
 
Shinikizo hapa ni msukumo wa kiislam kuwepo na masomo yao katika mtaala wa taifa, hilo la kikristo limewekwa tu kubalanzi mambo. Wakristo hawana haja ya mtaala huo kwa kuwa ni wengi katika madhehebu yenye imani tofauti japo ni wamoja katika kristo. Haileti mantiki kujumuisha masomo ya dini katika mitihani ya taifa. Hayo masomo kila dini na dhehebu wanavyo vyuo vyao wakafundishane imani zao huo huko. Wengine hatuamini upuuzi huo katika taifa ambalo haliongozwi kwa misingi ya dini
 
Hapo ilikuwa inatafutwa namna ya kuingiza hiyo Islamic knowledge iingie kwenye mfumo rasmi huko kwingine ni geresha tu Prof Mkenda anafanya haya kumfurahisha Samia maana haya malalamiko ya kobaz yamekuwepo muda mrefu kuhusiana na Islamic knowledge kutojumuishwa ktk ku calculate Division.
 
Hapo nia ya serikali miaka ijayo ni kutaka mashehe wawe na vyeti vya serikali....taratibu itaanzishwa shehe lazma awe na ISLAMIC KNOWLEDGE ya serikali
 
Hivi hakuna vyuo vikuu vitoavyo elimu za dini huko ulimwengu wa Kwanza na hapa kwetu Africa?
Tuwaandae vijana wanataka bobea huko mimi naona hizi Tahusisi mpya ni jambo jema sana
 
Hujajibu swali madrasa ina fanya kazi gani? Unajua kwamba kila elimu ni muhimu kwa mlengo wa jamii husika?
Vipi kama elimu ya uchawi na yenyewe ikiwekwa kwenye mtahala wa elimu? Unajua maana ya katiba ya nchi kutokufungamanisha masuala ya kidini katika nchi?

Tatizo lenu tz hamna akili ya kuona madhara kufundishwa dini siyo kuwa muadilifu ...shuleni wanafunzi wangefundishwa uadilifu tu ...dini zifundishwe sehemu stahiki maana dini zipo nyingi tena zinapingana zenyewe kwa zenyewe ...waafrica tutazidi kuwa watumwa wa wazungu na waarabu milele daima kama tutaendekeza upumbavu ...kesho na kesho kutwa mashoga nayo yata anzisha dini yao ya ushoga na kutaka ifundishwe serikali..kesho na kesho kutwa freemason nao hivyo hivyo ....[emoji117][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90][emoji90]
Hivi unajua hata hyo elmu ya darasani tumeletewa?
 
Nimeona wameongeza combi nyingi sana kwenye kwenye elimu ya advance jambo zuri ila lina ubaya wake pia

Niende kwenye mada nchi yetu sio ya kidini yaani haifungamani na dini yeyote ile sasa serikali kwanini imeweke masomo ya dini ya kiislam na kikristo kwenye mtaahala ni kurudisha nyuma taifa letu na kuleta mkanganyiko hizo elimu zitolewee miskitini na makanisani full stop visiweke kwenye mifumo rasimi ya kiserikali

Naandika haya najua madhara ya serikali kuanza kuweka vitu vya kidini kwenye mifumo rasmi ya serikali

Sasa mfano wakristo wana madhebu mengi mno walokole waroman wapentecoste ...haya waislam kuna shia kuna suni ....mtaafundishaje maana haya madhehebu huwa yanatofautiana kwenye mambo mbali mbali kama sio kuleta fujo na mikanganyiko

Hao walimu watalipwa na nani yaani serikali ilipe walimu wa dini kama kweli ndo tumefikia huku tena katika elimu ya advance watoto narudia wasome hizo elimu huko makanisani au misikitini na madrassa ....

Naamini raisi ajae ataliangalia hili labda huyu wa sasa kaona sawa.....tunaomba rais atakae kuja atoe haya madude sijui divinity/ukristo sijui islamic knowledge hayana umuhimu wa taifa ambalo liko nyuma kisayansi na kiteknlogy mnazidi kulipoteza taifa kuleta mambo imani kwenye ulimwengu wa elimu serious zinahitaji fact sio imani .... fact ni muhimu kuliko imani ndo maana wazungu wanatupita maana wanaamini katika fact sio imani......sasa sisi imani ndo tunataka kabisa iwe elimu rasmi ni uzwazwa...

TANZANIA SIO NCHI YA KIDINI NA HAIRUSIWA HATA KUONESHA DALILI HIZO NI HATARI MNO KUWEKA MASWALA YA DINI SERIKALI

Eti necta nao wako busy watunge mitihani sijui yesu alifanya nini mara sijui mtume alifanya nini ...

Tuiheshimu tanzania hasa tanganyika mambo ya dini hatutaki toeni....kama upande wa pili znz watapenda muwakeeni ila tanganyika haiwezi jengwa kamwe na mifumo hii mnayoleta TANGANYIKA TUNATAKA WATOTO WAWE BUSY NA ELIMU DUNIA ZAIDI.....

SIJUI MAKAMBA SIJUI MAKONDA SIJUI RIDHIWAN AU YEYOTE ATAYEKUJA KUWA RAIS BAADa ya mama samia atoe haya madini kwenye elimu rasmi hayana tija kwa taifa ... taifa linahitaji sana kuendelea upande wa elimu dunia...... sio elimu ahera

Mambo ya mzee ruksa yanarudi sasa. Hayo masomo ya dini hayalengi Wakristo.
 
Hakuna masomo yoyote ya kidini yaliyowekwa kwenye combinations isipokuwa wewe una roho mbaya na husda. Yaani umeona lugha ya Kiarabu imo kwenye cobinations ndiyo shida ilipoanzia. Mbona Kichina, Kifaransa na Kiingereza vimo lakini siyo shida? Kama shida yako ni Kiarabu basi acha kutumia lugha ya Kiswahili kwani nacho ni krioli ya lugha ya Kiarabu na lugha za Kibantu za wenyeji wa pwani ya Afrika Mashariki.
 
Nchi ina watu wengi ,hatuwezi kusikiliza wapumbavu kama mtoa mada ...Ule mpango wa Dp world uliishia wapi ...Watu mil 60 tusikilize wapumbavu wachache kama wewe.
 
Back
Top Bottom