Serikali: Wahanga vyeti feki kulipwa mafao yao

Serikali: Wahanga vyeti feki kulipwa mafao yao

Watumishi wa Serikali katika Kada mbalimbali ambao waliondolewa kazini kutokana na tuhuma za kuwa na vyeti feki vya taaluma. Serikali imeagiza mchakato wa kuwalipa mafao yao uanze mara moja.

Siku ya leo Mawaziri wawili watafanya mkutano na waandishi wa habari Kuhusu michango ya pensheni waliyokatwa Watumishi waliondolewa kazini baada ya zoezi maalumu la Uhakiki wa vyeti .

Mkutano huo utaongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menijementi ya Umma na Utawala Bora. Mhe.Jenista Mhagama

Pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.

Mkutano utaanza saa tatu kamili asubuhi katika ukumbi wa PSSSF Tower ghorofa ya Nne Dodoma.
Je Poo makonda na yeye atalipwa stahiki zake??
 
Kuingiza watu wasio na maarifa sahihi hasa kwenye kazi za kitaaluma inashusha sana ufanisi kwa sababu huyo mtu anakuwa hana au ana weledi wa kiwango cha chini, nafikri kabla ya kuwaondoa wangewaachia wakuu wao wa kazi wafanye tathmini ili kujua kama huyo mtu alikuwa na maarifa sahihi kwa kazi aliyokuwa anafanya na alikuwa anaongeza tija kwenye eneo lake, pia kuna watu kama madereva ambao kwa kweli kulikuwa hakuna haja ya kuwaondoa kwa sababu ujuzi wao na uzoefu waliokwisha upata katika udereva ulikuwa hauwezi kuathiriwa kwa namna yoyote na kukosa vyeti sahihi.​
Tupe na ufafanuzi wa kujenge kibanda Cha mlinzi kwa milion 11 halafu ana cheti OG. Mwizi ni mwizi tu.
 
Tupe na ufafanuzi wa kujenge kibanda Cha mlinzi kwa milion 11 halafu ana cheti OG. Mwizi ni mwizi tu.
Halafu jambo jingine, hawa watu walifanya kazi mwaka mmoja wakiwa kwenye uangalizi, wakaonekana kumudu kazi na kuthibitishwa kazini. Kwa maana nyingine, hao watu walimudu kazi zao ndo maana wakathibitishwa kazini. Kwa hiyo hili pia lipo kwa upande wa serikali kuweza kujisahihisha, ndo maana hailazimiki kuchukua hatua kali sana dhidi yao kama wengine wanavyoshawishi.....​
 
Watapewa michango yao tu, sio ya mwajiri wala sio pension.

Wengi wameliwa vichwa wakiwa na mshahara chini ya m1 na wakiwa kazini pungufu ya miaka 15 na ikumbukwe walianza kazi na mishara midogo sana pungufu ya laki.

Watapata hela pungufu ya milion 6
hiyo m6 ni nyingi sana bwashe kama waliostaafu kiuhalali na wakiwa wakilipwa 1.3m bado wamepewa m8 tu.hayo matasisi hasa LIPPF lilidhulumu sana pesa ya watumishi.
 
Wizi ni wizi tu usitake kuupaka mafuta! Kitendo cha kuchukua vyeti si vyako kwenda navyo chuo au sehemu ya kazi ukavitumia isivyo halali ni uharifu! Huu uzuzu upo hapa kwetu tu nchi za watu wenye akili huwezi kukuta upumbavu kama huu! Ushawahi kujiuliza vijana wangapi waliohitimu vyuo wapo mtaani kwa miaka mingi bila ajira? Unachukuaje hela ya walipa kodi kwenda kumlipa mtu mwizi wakati kipindi chote alichokuwa anafanya kazi na vyeti vyake feki alikuwa anapokea mshahara isivyo halali! Au ndio wale mnaoendeshwa na mihemko na busara za kipumbavu?
Sazingine unaweza kukosa cha kuandika. Ama unaweza ukatukana ukaonekana mjinga kumbe ni mambo ya kuudhi kwa kiwango Cha juu sana.

Yani mtu ameghushi vyeti badala yakuchukuliwa hatua za kisheria eti analipwa hahahaa.
Labda kama Kuna jambo jingiane ambalo hatulifahamu,vinginevyo kunamtu anatengenezewa jungu alafu alaumiwe baadae naaonekane hafai kwenye nafasiyake.

Haiingii sio akilini tu,haiingii hata kwenye ujinga.
 
Lowasa ana busara sana. Nasimama na mtazamo wake kuhusu hili suala. Inasemekana hata JPM alitaka kulegeza msimamo na kuwalipa kidogo ila akapumzika.

Raisi ni mlezi wa raia wote, na raia wanafanya makosa. Raisi anategemewa na wafanyakazi, wafungwa, wakulima wa korosho, omba omba, matajiri, masikini.

Woote hawa wanamuhutaji raisi hata wanapokuwa na makosa. Anapoadhibu ni ubinadamu kuhakikisha kuwa adhabu inalenga kurekebisha na sio kutengeneza wategemezi wapya kwa kutoa adhabu kubwa mpaka anayeadhibiwa asiweze tena kusimama yeye na wanaomtegemea.
Huruma tayari ilisha tolewa baada ya kuamua kutowapeleka kwenye vyombo vya Sheria, "that's more than enough!"
Napia hawakutakiwa kurudisha pesa walizopata kama mishahara kwa njia ya udanganyifu.

Kuanza kuwalipa mafao nikuhalalisha uhalifu wao.
 
Sazingine unaweza kukosa cha kuandika. Ama unaweza ukatukana ukaonekana mjinga kumbe ni mambo ya kuudhi kwa kiwango Cha juu sana.

Yani mtu ameghushi vyeti badala yakuchukuliwa hatua za kisheria eti analipwa hahahaa.
Labda kama Kuna jambo jingiane ambalo hatulifahamu,vinginevyo kunamtu anatengenezewa jungu alafu alaumiwe baadae naaonekane hafai kwenye nafasiyake.

Haiingii sio akilini tu,haiingii hata kwenye ujinga.
Tatizo la watawala wameshindwa kusimamia vitu vya msingi kama kupanda kwa gharama za maisha wamebakiza kuokoteza sifa kwa watu waharifu!
Yaani kwa nchi zingine hii ni jinai kubwa kwa usalama wa nchi na watu wake!
Ila kwa vile alifanya JPM wanataka kufanya tofauti ili aonekane alikuwa wrong!
Mpumbavu huwezi kuacha upumbavu hata umtwange kwenye kinu na baadae upime kiasi cha upumbavu utaukuta ni ule ule!
 
Hatimaye vibaka watanashati kulipwa mafao yao.
Only in Tanzania 🤣🤣🤣🤣
Mimi nashauri kwa kasi anayoenda nayo Mama ya kufungua nchi na HAZINA,sheria ya forgery ifutwe tu,mtu ambaye ata hakukanyaga shuleni,achonge Cheti na apewe ajira na ata ikiwezekana awe Rais au Waziri ili Taifa liendelee kwa kasi chini ya Watumishi mbumbumbu!
 
Hatimaye vibaka watanashati kulipwa mafao yao.
Only in Tanzania 🤣🤣🤣🤣
Mimi nashauri kwa kasi anayoenda nayo Mama ya kufungua nchi na HAZINA,sheria ya forgery ifutwe tu,mtu ambaye ata hakukanyaga shuleni,achonge Cheti na apewe ajira na ata ikiwezekana awe Rais au Waziri ili Taifa liendelee kwa kasi chini ya Watumishi mbumbumbu!
Lengo ni kuonesha JPM alikosea hakuna kingine!
 
Huruma tayari ilisha tolewa baada ya kuamua kutowapeleka kwenye vyombo vya Sheria, "that's more than enough!"
Napia hawakutakiwa kurudisha pesa walizopata kama mishahara kwa njia ya udanganyifu.

Kuanza kuwalipa mafao nikuhalalisha uhalifu wao.
Hawalipwi mafao, wanapewa makato ile 5% ya mshahara waliyokuwa wanakatwa kwenye mshahara. Serikali imekuwa na msimamo tofauti na hili hitimisho lako.
 
Watumishi wa Serikali katika Kada mbalimbali ambao waliondolewa kazini kutokana na tuhuma za kuwa na vyeti feki vya taaluma. Serikali imeagiza mchakato wa kuwalipa mafao yao uanze mara moja.

Siku ya leo Mawaziri wawili watafanya mkutano na waandishi wa habari Kuhusu michango ya pensheni waliyokatwa Watumishi waliondolewa kazini baada ya zoezi maalumu la Uhakiki wa vyeti .

Mkutano huo utaongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menijementi ya Umma na Utawala Bora. Mhe.Jenista Mhagama

Pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.

Mkutano utaanza saa tatu kamili asubuhi katika ukumbi wa PSSSF Tower ghorofa ya Nne Dodoma.
Mbona hili siyo jipya maana maagizo yalihatolewa kitambo kwamba walipwe michango yao?
 
Kumbe hadi leo hawakulipwa ! kwahiyo alichokua anatuambia Mchengerwa ilikuwa porojo siyo ?
 
Namuona anko magu alivyo nuna huko akhera baada ya kupata habari hii. Hee he laiti ningekukuwa hai wangelima kwa meno.
 
Hawalipwi mafao, wanapewa makato ile 5% ya mshahara waliyokuwa wanakatwa kwenye mshahara. Serikali imekuwa na msimamo tofauti na hili hitimisho lako.
Mkuu muhalifu hastahili kulipwa chochote, kitugani ambacho huelewi hapo.
Labda kama tulidanganywa kwamba watu walighushi vyeti na imejulikana waliingia kihalali.

Kwa namna yoyote kama nikweli walighushi vyeti kuwalipa makato sijui mafao vyovyote, kuwalipa niwadekeza wahalifu.
 
Back
Top Bottom