Serikali: Wahanga vyeti feki kulipwa mafao yao

Serikali: Wahanga vyeti feki kulipwa mafao yao

Mtu akiwa na cheti feki ukweli ni kwamba inabatilisha hata ajira aliyoipata kwa kutumia vyeti hivyo. Katika jambo hili nasimama na JPM.

Mambo ya kugushi nyaraka ni kinyume cha sheria. Kwa hiyo basi ile kutokushtakiwa na kuhukumiwa ilikuwa ni huruma tosha kutoka serikalini. Sasa suala la kuwalipa waliogushi vyeti linatoka wapi wakati ajira zao zilikuwa batili!?

Katika baadhi ya mambo nilimuelewa sana JPM. Alikuwa jasiri, mwenye uthubutu wa kuchukua hatua na kufichua uozo. Sasa msimamo wa serikali umeshabadilika na kutaka kuwapa shavu wakosaji!?

RIP Magufuli.

Serikali hiyohiyo ndio iliajiri wenye vyeti feki, serikali hiyohiyo ndio ikawafukuza na kuwanyima haki zao, serikali hiyo hiyo leo hii inataka kuwalipa mafao yao kwa kugundua ilifanya makosa.
 
Mkuu muhalifu hastahili kulipwa chochote, kitugani ambacho huelewi hapo.
Labda kama tulidanganywa kwamba watu walighushi vyeti na imejulikana waliingia kihalali.

Kwa namna yoyote kama nikweli walighushi vyeti kuwalipa makato sijui mafao vyovyote, kuwalipa niwadekeza wahalifu.
Boss, Jambo lolote likifanyika kisiasa linatulizwa kisiasa na ndicho kilichofanyika.

Nchi tulizidiwa, tukafikiria shortcut ya kubana matumizi tukaja na drs la saba na vyeti feki. Hawa vyeti feki ni watu ambao tupo nao muda na wengi tuliwaajiri wakiwa drs la 7 na kuwalazimisha kujiendeleza wakiwa watu wazima ndipo wengi wakafanya ujanja ujanja na tuliendelea nao sababu tuliwahitaji sio kwamba hawakufahamika.(Serikali kutoa maagizo kwa mtu mwenye miaka 45 akasome elimu ya form four ilijua kuna watakaolazimisha na baada ya kulazimisha ilinyamaza, haikusitisha mkataba sababu utendaji haukuwa mbaya, uzoefu uliwabeba)

Sababu kuu ya kuwaondoa ilikuwa tunahitaji fedha na hatukua na tatizo na vyeti vyao sababu walifahamika.

Kilichokuwa kinaendelea ilikuwa ni kusubiri wastaafu na kuajiri kwa vigezo vipya vya elimu kuanzia form four tofauti na zamani ilivyokuwa drs la saba ila sasa tuna marejesho ya mikopo ya biashara, tuna miradi mikubwa tunafanyaje ili kuwa na fedha?

Tukaamua bana hawa wafanyakazi waondolewe, drs la saba wote na waliofoji vyeti ili tupate pesa. Ila yale maeneo nyeti yasiguswe sababu hatutaweza kupata mbadala, haya maeneo mengine wacha yabaki na mapengo tukiwa na fedha tutaajiri. Tangazo likatoka watu wakafukuzwa.

Sasa ukifukuza watu kisiasa kwa kuacha wengine kuna madhara yake na usipoyatibu lazima yatakutafuna. Yataibuka kila mwaka na utalazimika tu kuyatatua sababu uliadhibu bila usawa.

JPM akaanza, akarekebisha kwa kurudisha drs la saba na inasemekana alikuwa na mpango wa kuwarekebishia wa vyeti feki ila MUNGU hakumpa huo muda akamwita. Samia akamaliza kwa kuwapa 5% na huu mjadala utaisha.
 
Boss, Jambo lolote likifanyika kisiasa linatulizwa kisiasa na ndicho kilichofanyika.

Nchi tulizidiwa, tukafikiria shortcut ya kubana matumizi tukaja na drs la saba na vyeti feki. Hawa vyeti feki ni watu ambao tupo nao muda na wengi tuliwaajiri wakiwa drs la 7 na kuwalazimisha kujiendeleza wakiwa watu wazima ndipo wengi wakafanya ujanja ujanja na tuliendelea nao sababu tuliwahitaji sio kwamba hawakufahamika.(Serikali kutoa maagizo kwa mtu mwenye miaka 45 akasome elimu ya form four ilijua kuna watakaolazimisha na baada ya kulazimisha ilinyamaza, haikusitisha mkataba sababu utendaji haukuwa mbaya, uzoefu uliwabeba)

Sababu kuu ya kuwaondoa ilikuwa tunahitaji fedha na hatukua na tatizo na vyeti vyao sababu walifahamika.

Kilichokuwa kinaendelea ilikuwa ni kusubiri wastaafu na kuajiri kwa vigezo vipya vya elimu kuanzia form four tofauti na zamani ilivyokuwa drs la saba ila sasa tuna marejesho ya mikopo ya biashara, tuna miradi mikubwa tunafanyaje ili kuwa na fedha?

Tukaamua bana hawa wafanyakazi waondolewe, drs la saba wote na waliofoji vyeti ili tupate pesa. Ila yale maeneo nyeti yasiguswe sababu hatutaweza kupata mbadala, haya maeneo mengine wacha yabaki na mapengo tukiwa na fedha tutaajiri. Tangazo likatoka watu wakafukuzwa.

Sasa ukifukuza watu kisiasa kwa kuacha wengine kuna madhara yake na usipoyatibu lazima yatakutafuna. Yataibuka kila mwaka na utalazimika tu kuyatatua sababu uliadhibu bila usawa.

JPM akaanza, akarekebisha kwa kurudisha drs la saba na inasemekana alikuwa na mpango wa kuwarekebishia wa vyeti feki ila MUNGU hakumpa huo muda akamwita. Samia akamaliza kwa kuwapa 5% na huu mjadala utaisha.
Hapo watanzania watakwelewa kidogo. Hapa bwana hatakama serikali ilikosa pesa waliliendea kwa nguvu na kusababisha taharuki katika familia na kuwachonganisha na marafiki, ndugu, na jamii. Hili tatizo lilikuwa la kitaifa. Wangetafuta namna ya kupata hela ili wasisumbue familia za watu.

Kwa kweli huu unyama na ukatili ni laana hata mungu hakuachi.

Mfano Familia ambayo imekumbana na vyeti feki hapo hapo wakaambiwa nyumba inavyunjwa, Happ hapo mtoto kafukuzwa chuo alama zake hazistahili asome hapo ukiwa ni mzazi, kaka, Dada, mjomba, shangazi, rafiki utajisikia je? Ukiwa na ubinadamu lazima umwonee huruma huyu mtu.

Sio kuwafokea mweleweshe akwelewe. Wapigaji serikali wapo wengi kuliko wanavyojua. Tena walioiandaa hiki kituko wanaweza kuwa ndio wezi wakubwa. Walifanyaoazi wakawa wanalipwa kuandaa uhakiki was kuwashusha wenzao kaburini.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Hapo watanzania watakwelewa kidogo. Hapa bwana hatakama serikali ilikosa pesa waliliendea kwa nguvu na kusababisha taharuki katika familia na kuwachonganisha na marafiki, ndugu, na jamii. Hili tatizo lilikuwa la kitaifa. Wangetafuta namna ya kupata hela ili wasisumbue familia za watu.

Kwa kweli huu unyama na ukatili ni laana hata mungu hakuachi.

Mfano Familia ambayo imekumbana na vyeti feki hapo hapo wakaambiwa nyumba inavyunjwa, Happ hapo mtoto kafukuzwa chuo alama zake hazistahili asome hapo ukiwa ni mzazi, kaka, Dada, mjomba, shangazi, rafiki utajisikia je? Ukiwa na ubinadamu lazima umwonee huruma huyu mtu.

Sio kuwafokea mweleweshe akwelewe. Wapigaji serikali wapo wengi kuliko wanavyojua. Tena walioiandaa hiki kituko wanaweza kuwa ndio wezi wakubwa. Walifanyaoazi wakawa wanalipwa kuandaa uhakiki was kuwashusha wenzao kaburini.
Mkuu tuna changamoto ya mifumo ya usahili hivyo mambo haya yanapotokea inakuwa ni kama kengele.

Pia, Watu kama JPM ni muhimu sana katika nchi sababu wana ujasiri wa kugusa bila kuogopa kufukunyua makosa yake(Watu wanaojilipua). Unadhani baada ya hili ni wangapi watapeleka vyeti feki serikalini?
 
Hawalipwi mafao, wanapewa makato ile 5% ya mshahara waliyokuwa wanakatwa kwenye mshahara. Serikali imekuwa na msimamo tofauti na hili hitimisho lako.
Chochote walichokuwa wakilipwa au kukatwa katika mishahara yao kilikuwa ni batili, kwa kuwa hata mikataba yao ya kazi ilikuwa pia ni batili, "null and void ab initio"

Kwa hiyo hata hiyo unayosema ni makato ya 5% bado ni batili. Hawa washukuru huruma ya serikali kwa kutowafungulia mashtaka ya kugushi nyaraka na kijipatia kipato kwa njia ambayo si halali. Hili kundi la wahalifu kama wengine ambao walipaswa kushitakiwa na jamuhuri.
 
Hawa hawastahili kulipwa chochote ilibidi wawe jela kwanza. Umeghushi nyaraka muhimu sana serikali nadhani iyo ingekua kesi bila ya dhamana ili iwe funzo kwa wengine.
 
Chochote walichokuwa wakilipwa au kukatwa katika mishahara yao kilikuwa ni batili, kwa kuwa hata mikataba yao ya kazi ilikuwa pia ni batili, "null and void ab initio"

Kwa hiyo hata hiyo unayosema ni makato ya 5% bado ni batili. Hawa washukuru huruma ya serikali kwa kutowafungulia mashtaka ya kugushi nyaraka na kijipatia kipato kwa njia ambayo si halali. Hili kundi la wahalifu kama wengine ambao walipaswa kushitakiwa na jamuhuri.
Ukiamua kuadhibu wahalifu ndani ya serikali siasa weka pembeni na sio jambo jepesi. Samia yupo sahihi, hili suala linakwenda kuisha.
 
WATALIPWA LINI ? MAANA HII POROJO NI YA MUDA MREFU SANA , mnawadanganya watu wanajipa matumaini huku mkijua kumbe ni uongo mtupu !
 
Watumishi wa Serikali katika Kada mbalimbali ambao waliondolewa kazini kutokana na tuhuma za kuwa na vyeti feki vya taaluma. Serikali imeagiza mchakato wa kuwalipa mafao yao uanze mara moja.

Siku ya leo Mawaziri wawili watafanya mkutano na waandishi wa habari Kuhusu michango ya pensheni waliyokatwa Watumishi waliondolewa kazini baada ya zoezi maalumu la Uhakiki wa vyeti .

Mkutano huo utaongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menijementi ya Umma na Utawala Bora. Mhe.Jenista Mhagama

Pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.

Mkutano utaanza saa tatu kamili asubuhi katika ukumbi wa PSSSF Tower ghorofa ya Nne Dodoma.
Rais Samia ni mtu siyo sawa na yule mwingine 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20221026-130749.png
    Screenshot_20221026-130749.png
    157.7 KB · Views: 5
Watumishi wa Serikali katika Kada mbalimbali ambao waliondolewa kazini kutokana na tuhuma za kuwa na vyeti feki vya taaluma. Serikali imeagiza mchakato wa kuwalipa mafao yao uanze mara moja.

Na kwanini walifanya sabotage? Kutumia vyeti ambavyo sio halali

Badala ya kuhakikisha vijana wanajiajiri kwa kuwapa mitaji unaenda kutupa mamilioni ya fedha kwa watu waliogushi vyeti! Stupid!
Kwa makusudi kabisa, Serikali inaamua kuwachafua wananchi klwake walioitumikia serikali kwa kuwaita WATUMISHI WA VYETI FEKI. Mwaka 2017 wapo walioondolewa kazini kwa sababu ya kuwa na vyeti vya kughushi na waapo walioondolewa kazini kwa kuambiwa kuwa walikuwa na elimu ya darasa la saba (elimu chini ya KIDATO CHA NNE). Idadi ya walioondoshwa kwa kuwa na elimu chini ya kidato cha 4 ni wengi kuliko walioghushi vyeti, ila sasa wote wanawekwa kapu moja, VYETI BANDIA, ni uonevu aisee.
 
Waziri Profesa Joyce Ndalichako amesema mifuko ya Hifadhi ya Jamii PSSSF na NSSF itarejesha michango ya wafanyakazi iliyopokelewa bila kuhusisha michango ya mwajiri

Marejesho ya michango yataanza kufanyika Novemba 1, 2022, ambapo mtumishi husika atatakiwa kwenda kwa aliyekuwa mwajiri wake akiwa na passport size 2, nakala ya taarifa za benki (Bank Statement) ya akaunti iliyo hai na nakala ya kitambulisho cha Taifa au mpiga kura au leseni ya udereva

Ndalichako amesema Rais Samia ameridhia watumishi 14,516 kulipwa michango yao waliyoipoteza kutokana uhakiki wa vyeti uliofanywa na Serikali April 2016 hadi 2017

====================

Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia kuwa watumishi wote walioondolewa kazini kwa kughushi vyeti warejeshewe michango yao waliyochangia kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Watumishi hao ni wale walioondolewa katika utumishi wa umma katika shughuli maalum la uhakiki wa vyeti lililoendeshwa na Serikali kwa kushirikiana na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) katika kipindi cha kuanzia Oktoba 2016 hadi Aprili mwaka 2017.

Kufuatia uhakiki huo, watumishi wasiopungua 14,516 walibainika kuwa na vyeti vya kughushi na waliondolewa katika utumishi wa umma.

Hayo yamesemwa leo Jumatano Oktoba 26, 2022 na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako wakati akizungumzia kuhusu uamuzi huo.

“Kufuatilia maelekezo hayo, mifuko ya Hifadhi ya Jamii PSSSF na NSSF itarejesha michango ya wafanyakazi iliyowasilishwa kwenye mifuko hiyo bila kuhusisha michango ya mwajiri,”amesema.

Amesema marejesho ya michango hiyo itaanza kufanyika kuanzia Novemba Mosi mwaka 2022, ambapo mtumishi husika atatakiwa kwenda kwa aliyekuwa mwajiri wake akiwa na picha mbili za passport size.

Vingine anavyotakiwa kwenda navyo ni nakala ya taarifa za benki (Bank Statement) ya akaunti iliyo hai na nakala ya kitambulisho cha Taifa au mpiga kura au leseni ya udereva.

Amesema pia mtumishi atatakiwa kujaza hati ya ridhaa kwa aliyekuwa mwajiri wake.

MWANANCHI
 
punguza hasira hamna mkamilifu Duniani hata ww c mkamilifu hiyo ni haki Yao ww mtu ametumikia Taifa Kwa muda WA miaka 40,Leo hii uje umfukuze bila kumpa hata kianzio SI haki kabsa huenda atamhusika naye hajakamilika chukulia mwalimu ambaye amekutoa ujinga na cheti chake feki,mm SI halalishi ila busara ingetumika
 
Serikali inafanya vyema kuwafurahisha hawa watu, lakini inazidi kuchukiwa kwa maisha magumu sana kwa wananchi wa kawaida,

Serikali inawafanya kazi pengine wasiofika hata milioni moja,

Inafanya kuwafurahisha hao mbali kwamba walikuwa wafoji vyetu, wagonjwa walikuwa wakifanyiwa oppression za hovyo kwa hovyo enzi hizo za madakitar form four felia,

Serikali imewasahau kabisa mamilioni ya watanzania wasio wafanya kazi kwa kuwasababishia maisha magumu na kukumbatia waliokuwa wakilitia hasara taifa letu
 
Hivi kweli unaandika kusapot. Wezi? Nchi hii ya Ajabu sana. Tena Magufuli aliwaonea huruma hawa majizi.

Tunasomesha Watoto wetu kwa gharama kubwa wanakosa Ajira. Kwa sababu kuna watu wanafanyakazi kwa kutumia vyeti feki.

Siungi mkono hoja ya SERIKALI kuwalipa wezi fedha tena ilitakiwa warudishe fedha zote za walipa kodi walizolipwa kwa miaka yote.
 
Kati ya Serikali na wao nani mwizi hapo??

Hawajaiibia tu Serikali pia wamesababisha watu wenye sifa kukosa hizo nafasi.

Hawa hawakustahili kulipwa, walipaswa washtakiwe kwa ulaghai au kughushi nyalaka ( wataalamu wa sheria wanaweza kufafanua zaidi)
Wengine walionewa kabisa , mfano ;kuna mtu cheti cha O level kina jina Aisha Juma Mandamo halafu A level na shahada kina jina Asha Juma Mandamo halafu anaambiwa amegushi cheti ni halali hiyo ?
 
Watumishi wa Serikali katika Kada mbalimbali ambao waliondolewa kazini kutokana na tuhuma za kuwa na vyeti feki vya taaluma. Serikali imeagiza mchakato wa kuwalipa mafao yao uanze mara moja.

Siku ya leo Mawaziri wawili watafanya mkutano na waandishi wa habari Kuhusu michango ya pensheni waliyokatwa Watumishi waliondolewa kazini baada ya zoezi maalumu la Uhakiki wa vyeti .

Mkutano huo utaongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menijementi ya Umma na Utawala Bora. Mhe.Jenista Mhagama

Pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.

Mkutano utaanza saa tatu kamili asubuhi katika ukumbi wa PSSSF Tower ghorofa ya Nne Dodoma.
Samia Ni chaguo la Mungu, magufuli aliwasibu wengi na hakuwa na utu kabisa
 
Hivi kweli unaandika kusapot. Wezi? Nchi hii ya Ajabu sana. Tena Magufuli aliwaonea huruma hawa majizi.

Tunasomesha Watoto wetu kwa gharama kubwa wanakosa Ajira. Kwa sababu kuna watu wanafanyakazi kwa kutumia vyeti feki.

Siungi mkono hoja ya SERIKALI kuwalipa wezi fedha tena ilitakiwa warudishe fedha zote za walipa kodi walizolipwa kwa miaka yote.
Jiwe alikuwa shetani kabisa,huwezi kudhulumu jasho la mtu
 
Back
Top Bottom