Uchaguzi 2020 Serikali ya Marekani yaonya "Vitisho na mabavu dhidi ya upinzani si dalili nzuri ya Uchaguzi Huru Tanzania Oktoba 2020"

Uchaguzi 2020 Serikali ya Marekani yaonya "Vitisho na mabavu dhidi ya upinzani si dalili nzuri ya Uchaguzi Huru Tanzania Oktoba 2020"

Jumuia za kimataifa zinatakiwa kuziingilia nchi zote zenye Utawala wa kikomunisti na kidikteta na kuwafurusha watawala waliokosa malezi Bora utotoni ambayo yanapelekea uvunjifu wa amani na kuipa dunia gharama kubwa Sana za kuhudumia wakimbizi ili kuokoa pesa hizo zikatumike kwenye project zingine duniani, watawala wa kiafrica wanachojua ni kuzalisha wakimbizi duniani na sio kuhudumia wakimbizi wanaachiwa mzigo wengine.
Hawa watu waliokosa malezi Bora utotoni ndio uisumbua dunia.
 
Mkuu mimi nilikuuliza hayo kutokana na hoja yako hii.

watu wameshindiliwa risasi, maiti ndani ya viroba zimeokotwa ufukweni, watu wametekwa, wamepotezwa, wamefungwa, wamefilisiwa...kwa hiyo wanaokandamizwa wakae tu kimya waseme hewala baba?!!

Nilikuuliza yote hayo kwasababu kwanza nilitaka utambue kuwa matendo ya utekaji, risasi, mauaji n.k hapa nchini hayakuanza leo yalikuwepo tangu muda mrefu na si serikali hii tu yanatokea. Pili nilitaka tu tuweke kumbukumbu sawa sawa kuhusu hawa tunao waita watetezi wa demokrasia na haki za binadamu
swali je wameanza kufanya utetezi wakati huu tu? kwasababu matukio maovu yapo tangu siku nyingi au hawakuwa wanayaona ama hayakuwa na maana kwao kunyooshea vidole na matamko Kama wanavyofanya sasa?

Haya matamko yao wanayo yatoa kila siku ni ya kinafiki yenye lengo fulani nyuma ya pazia huku wakijificha kwenye kivuli cha haki za binadamu.
Angalia hiyo tweet hapo eti ofisi ya CHADEMA imepigwa Bomu!! Hivi kweli kabisa ofisi ya CHADEMA tena ya Kanda ipigwe bomu, yani mtu kabisa abebe bomu akalipue ofisi ya CHADEMA ya Kanda? Vitu vya ajabu kabisa hivi.

Alafu hao ccm ni wapumbavu kiasi gani hadi wafanye matukio Kama hayo ambayo wanajua kabisa yatawachafua alafu wakafanye kwa makusudi kabisaa? Siamini Kama ni wajinga kiasi hiki, alafu mara mbili mfululizo tukio la Arusha bado halijapoa wanatupiwa zigo la lawana na kupakwa matope alafu leo tena waende kuchoma nyingine mbeya? Kama ni hivyo basi huyu anae ratibu haya matukio ni mpumbavu wa kiwango Cha lami.

Kwa haraka haraka tutasema kuna masilahi yao yameguswa ndio mana wamekuwa wepesi sana kutoa matamko.

1 Unakumbuka tamko lao kuhusu shambulio la kigaidi masaki bila hata kushirikisha vyombo vya ndani kana kwamba wao ndio watawala wa nchi hii?

2 Unakumbuka matamko yao wakilazimisha Tanzania Kuna Ebola tena wakataja na hospital ya temeke Kuna mtu kafa kwa Ebola?

3 Unakumbuka matamko lukuki wakati wa Corona?

Uhalali wa wao kufanya vitu kama hivi wanaupata wapi?

Upouliza kuwa tutajibu nini kwa MUNGU hapa maana yake ni kwamba unatoa tuhuma kuwa wauaji ni hawa walio madarakani.
Sasa hebu lete tukio moja lenye ushahidi usio shaka kuwa muuwaji ni fulani (namaanisha ushahidi na sio fulani alisema au alitoa tuhuma kuwa wauaji ni serikali), unaweza kuleta ushahidi wa angalau tukio moja?

Kama ni kweli hawa watawala ndio wanaua sasa wale polisi, wanachama wa ccm na viongozi wa serikali kule kibiti waliokuwa wakiuawa kila kukichwa nani alikuwa anawaua? Kama muuaji wetu ni serikali inamaana walikuwa wanauana wenyewe kwa wenyewe?

Kuna tamko lolote kutoka ccm lililohusisha au kutuhumu upinzani kuhusika na mauaji yale?

Kuhusu hoja yako ya kununua upinzani kwa pesa za walipa kodi, hili nalo pia ni jambo la kufikirika mkuu halina ushahidi, au una ushahidi wa mmoja wapo aliye nunuliwa utuwekee hapa?
Unadhani kwamba hawa watu hawawezi kuhama kwa utashi wao tu, kwanini hutaki kuamini kuwa huo ni uchaguzi wao binafsi?
Unataka kuniambia kuwa wote waliopo CHADEMA wameridhika kabisa na kila kitu na kwamba kamwe hawawezi kuhama kwa maamuzi yao?
Kwahiyo na hawa wanao hama kutoka ccm kwenda CHADEMA vipi nao wamenunuliwa au ni maamuzi yao tu kwa kuto ridhishwa ndani ya ccm?
Kuna watu wamehama kutoka CHADEMA kwenda ACT mfano ni yule mbunge wa ubungo vipi nae ACT walimnunua sh ngapi?
sasa hivi vyombo vya habari vimepigwa kofuli.

bunge live lilifungwa na wabunge wa upinzani kila kukicha kufukuzwa bungeni, kupigwa hadi kuvunjwa viungo nk.

Kodi za wananchi kutumika kununua wapinzani mfano arumeru, ushahidi ukatupwa na wanunuzi wakapandishwa vyeo.

mtu mmoja anaamua mipango yote ya serikali ikiwemo bajeti ambazo zinatakiwa zipangwe na kuamuliwa bungeni.

watu wanateuliwa na kutenguliwa hovyo bila kufuata sheria na taratibu zilizowekwe.

watu wapo magerezani miaka na miaka hawafikishwi mahakaman ili wajitetee na kama wana makosa waHukumiwe kwa mujibu wa sheria....madhila ni mengi mkuu....yaan uchochozi ni wapinzani, risasi wapigwe upinzani, ofisi zichomwe za upinzani, mikutano ya kisiasa wazuiliwe kufanya wapinzani, mali ziharibiwe ni za wapinzani mfano mali za mbowe.. nyumba zibomolwe ni za wapinzani, tume huru hakuna, maonevu ya jeshi la polisi ni kwa wapinzani...yan yote hayo hakuna hata moja anafanyiwa ccm ni upinzani tu....dah!! Mkuu acha USA, the hegi na dunia watusaidie tu sababu hatuna namna..kodi zetu wenyewe zinatumika kutuminya kila
kona tufanyeje sasa? hivi unafikiri wanaojilipuaga kule mashariki ya kati wanapenda sana kufa? Mkuu paka mkimbize atakimbia lakini akifika kwenye kuta nne hana pa kwenda tena ndo utauona mziki wake
 
Kama mtu anaendesha gari kwenye barabara nzuri ya Lami, hawezi kusimama ghafla barabarani na kuanza kushangaa kwa nini Tairi za gari lake yanazunguka vizuri; akifanya namna hiyo, kila mtu atamshangaa kwani ataleta foleni kwenye barabara au watu watasimama ili kumsaidia;LAKINI kama atasimama kwa sababu TAIRI LIMEPATA PANCHA au limepasuka, kila mwenye NIA njema ataguswa kutoa mchango wake ama kuziba pancha, au kumpatia tairi la spea; Sasa hivi tupo kwenye Uchaguzi ni lazima tuangalie,Je Gari/tairi letu lina pancha au linatembea vizuri bila matatizo? Kama mtu atakuwa kwenye shida au atakuwa anakwenda kutumbukia kwenye shimo ni lazima Jumuiya zote za Kimataifa kutusaidia kuepukana na hujuma za maadui ama wa Ndani au wa Nje? Sisi Tanzania tunao akili timamu na tunapaswa kujiangalia wenyewe bila kuingiliwa na watu wasiojua mila na desturi zetu; Tupo Imara na tunaijua Nchi yetu vizuri isipokuwa kama tairi/gari limepata pancha;tunapaswa kuziba pancha na kuendelea na safari; tusiwakaribishe watu kutushangaa kwa kuangalia gari /tairi letu kuwa halina pancha ila tunalishangaa
 
Ila hawasemi,
Afrika inasumbuliwa na utumwa wa fikra, wafuasi wa upinzani wanafurahia kuona tunaingiliwa Mambo ambayo inapaswa tujisimamie wenyewe
acha tuingiliwe bana, miafrika ndivyo tulivyo hatujitambui bila kulazimiswa. yan wananchi tuonewe halafu tukae tu kimya ina maana mnataka mpaka mtunyee mdomoni au?
ni kweli tunasumbuliwa na utumwa wa fikra maana tumejaa ubinafsi, roho mbaya kati yetu, hatupendi uhuru wala demokrasia..ni wapenda giza giza tu. acha watuingilie maana tunashindwa kujitawala wenyewe.
 
sasa hivi vyombo vya habari vimepigwa kofuli.

bunge live lilifungwa na wabunge wa upinzani kila kukicha kufukuzwa bungeni, kupigwa hadi kuvunjwa viungo nk.

Kodi za wananchi kutumika kununua wapinzani mfano arumeru, ushahidi ukatupwa na wanunuzi wakapandishwa vyeo.

mtu mmoja anaamua mipango yote ya serikali ikiwemo bajeti ambazo zinatakiwa zipangwe na kuamuliwa bungeni.

watu wanateuliwa na kutenguliwa hovyo bila kufuata sheria na taratibu zilizowekwe.

watu wapo magerezani miaka na miaka hawafikishwi mahakaman ili wajitetee na kama wana makosa waHukumiwe kwa mujibu wa sheria....madhila ni mengi mkuu....yaan uchochozi ni wapinzani, risasi wapigwe upinzani, ofisi zichomwe za upinzani, mikutano ya kisiasa wazuiliwe kufanya wapinzani, mali ziharibiwe ni za wapinzani mfano mali za mbowe.. nyumba zibomolwe ni za wapinzani, tume huru hakuna, maonevu ya jeshi la polisi ni kwa wapinzani...yan yote hayo hakuna hata moja anafanyiwa ccm ni upinzani tu....dah!! Mkuu acha USA, the hegi na dunia watusaidie tu sababu hatuna namna..kodi zetu wenyewe zinatumika kutuminya kila
kona tufanyeje sasa? hivi unafikiri wanaojilipuaga kule mashariki ya kati wanapenda sana kufa? Mkuu paka mkimbize atakimbia lakini akifika kwenye kuta nne hana pa kwenda tena ndo utauona mziki wake
Sasa mbona mkuu unakuwa hueleweki unavamia tu kila hoja bila utaratibu.
Hapo nimekuuliza maswali umejibu lipi ? Naona unarudia yale yale niliyokwisha kukujibu.
Haya mkuu mimi naishia hapa we wasubiri USA waje wakuletee democrasia.
 
ni mchakato!
Kwa mtu wa kawaida mwenye uelewa wa kujadili JF, unawezaje kuamini kwamba kuna mtu anaitwa Lissu ni maarufu na ana uwezo kuliko wewe? Huoni hiyo ni kasoro kichwani mwako.

Binadamu, kimaumbile ana tabia ya kujiamini kabla ya kuamini mtu mwingine. Leo hii unaamini Lissu atakukomboa baada ya kushitaki US? bora uishi zizini na nguruwe tu!
 
Jumuia za kimataifa zinatakiwa kuziingilia nchi zote zenye Utawala wa kikomunisti na kidikteta na kuwafurusha watawala waliokosa malezi Bora utotoni ambayo yanapelekea uvunjifu wa amani na kuipa dunia gharama kubwa Sana za kuhudumia wakimbizi ili kuokoa pesa hizo zikatumike kwenye project zingine duniani, watawala wa kiafrica wanachojua ni kuzalisha wakimbizi duniani na sio kuhudumia wakimbizi wanaachiwa mzigo wengine.
Hawa watu waliokosa malezi Bora utotoni ndio uisumbua dunia.
kabisa. tupaze sauti hadi watusikie waje kutusaidia..tumeonewa vya kutosha.
 
Sasa mbona mkuu unakuwa hueleweki unavamia tu kila hoja bila utaratibu.
Hapo nimekuuliza maswali umejibu lipi ? Naona unarudia yale yale niliyokwisha kukujibu.
Haya mkuu mimi naishia hapa we wasubiri USA waje wakuletee democrasia.
kwani wakituletea demokrasia ni vibaya mkuu? kwa hiyo mkuu wewe hutaki demokrasia?
 
Ila hawasemi,
Afrika inasumbuliwa na utumwa wa fikra, wafuasi wa upinzani wanafurahia kuona tunaingiliwa Mambo ambayo inapaswa tujisimamie wenyewe
Si uliona wakijikusanya ubalozi wa EU eti wanashitaki juu ya uchaguzi? Ni aibu kuwa na watu wa aina hii ktk siasa.

Kila anayejitambua akiingia ktk vyama hivi anatoka. Leo hii hatuwasikii akina Baregu, Safari, wote wamewaachia upuuzi wao. Ni vigumu kumshauri mtu aliyekulia maisha ya 'misheni tauni'. Hata ndani ya familia hatuwezi!
 
Si uliona wakijikusanya ubalozi wa EU eti wanashitaki juu ya uchaguzi? Ni aibu kuwa na watu wa aina hii ktk siasa.

Kila anayejitambua akiingia ktk vyama hivi anatoka. Leo hii hatuwasikii akina Baregu, Safari, wote wamewaachia upuuzi wao. Ni vigumu kumshauri mtu aliyekulia maisha ya 'misheni tauni'. Hata ndani ya familia hatuwezi!
ndiyo demokrasia Mkuu, mtu anakusanyika anapoona patamfaa mradi havunji sheria na haingilia uhuru wa mtu mwingine kinyume cha sheria. wewe ni nani hadi upangie wenzako pakukusanyika? wewe hujakusanyika huko EU na hakuna anayekuuliza sasa wewe wanaokusanyika wanakuwashia nini? kwan nchi ni ya kwako peke yako mkuu?!!!
 
USA linaendelea kuwa taifa kubwa na la hovyo sana dunia, kila siku kutoa matamko ya siyo kuwa na kichwa wala miguu.

Walionya na kutoa tamko la kuhusu corona kiko wapi? Watuache nani huwa anaingila mambo yao wao ya ndani? Ukitaka kujua USA wakati mwengine ni wajinga angalia aina ya rais waliye naye wakati huu.
Tendeni haki kwa kukamata walio muuwa mawazo, Ben Saanane, waliompiga Lissu risasi, walionvunja Mbowe miguu, waliomvuja Ester Bulaya mikono, waliomvunja halima Mdee mikono, waliochoma ofisi za Chadema Arusha na Lindi. Baada ya hapo waambie USA kuwa tuna usawa na amani
 
Kwa mtu wa kawaida mwenye uelewa wa kujadili JF, unawezaje kuamini kwamba kuna mtu anaitwa Lissu ni maarufu na ana uwezo kuliko wewe? Huoni hiyo ni kasoro kichwani mwako.

Binadamu, kimaumbile ana tabia ya kujiamini kabla ya kuamini mtu mwingine. Leo hii unaamini Lissu atakukomboa baada ya kushitaki US? bora uishi zizini na nguruwe tu!
nikiishi zizi la nguruwe nitanenepa kwa kula kitimoto daily, so poa poa tu..

kama kawaida yenu, MATAGA mlichobaki nacho sasa baada ya Lissu kuwashika kunako ni matusi tu... hoja kwishnei!
 
USA linaendelea kuwa taifa kubwa na la hovyo sana dunia, kila siku kutoa matamko ya siyo kuwa na kichwa wala miguu.

Walionya na kutoa tamko la kuhusu corona kiko wapi? Watuache nani huwa anaingila mambo yao wao ya ndani? Ukitaka kujua USA wakati mwengine ni wajinga angalia aina ya rais waliye naye wakati huu.
Wakuache uwe unawabambikia kesi unawapiga risasi unawapora ushindi wakurugenziccm kufocha form kama kule ubungo?
 
Naona hii ndio inamdangaya huyu mwanasheria msomi na kumpa kiburi na dharau iliyo pitiliza. Mpaka kukejeli vyombo vya ulinzi na usalama na wakuu wake kwa maana hiyo watendaji wote, kudharau na kukebehi kazi na maendeleo ya awamu ya tano. Kudharau wananchi wote waliochagua serikali ya CCM kwamba hawana akili. Lakini kubwa zaidi ni kumdharau Rais na Amiri jeshi mkuu. Na amini tabia hizi za ajabu na ambazo si za heshima, wala asili wala utamaduni wetu zina mwisho wake.
Wewe ndiyo ulitumwa kwenda kumpiga risasi? Mtu ana uchungu wa mabaya mliomtendea mnadai anamdharau Rais? Lisu hamdharau Rais bali husema mapungufu yake kwa uwazi ndipo nyinyi wanafaika wa mfumo kandamizi mnaenda kumchochea awahujumu chadema muendelee kutafuna pesa za kutokomeza upinzani Tanzania
 
Marekani kwa Sasa wanakurupuka kwenye kutoa matamko yao. Ndio maana wenye akili tunawaona wapuuzi tuu kama wapuuzi wengine. Rejea tamko juu ya kilichoitwa Kushambuliwa na kuvunjwa vunjwa miguu kwa Mbowe.

Kama intelligence yao ilishindwa kujua kuwa Mbowe hakushambuliwa bali aliteleza tuu na kupata mshituko wa Kifundo Cha Mguu, wanatudhihirishiaje kuwa ofisi za Chadema- Arusha zimechomwa na watu wa Serikali na si Wana Chadema wenyewe Kama sehemu ya kutafuta public Attention?
Hugo Chavez alikuwa anawaletea dharau nadhani unajua kilichomkuta,endeleeni kuleta nyodo zenu
 
Waambie USA wamkamate Bush kwanza wampeleke the Hague. Acheni kuwa mandondocha wa nashoga.
Waanze kuwakamata waonevu wanawabambikia kesi kuwapiga risasi wapinzani kwanza ndipo waende huko
 
Back
Top Bottom