Serikali yamrejeshea Pascal Mayalla Press card yake iliyozuiliwa kwa takriban miaka 3 ataanza kuonekana Saba Saba!

Mimi najua Ccm haina ukabila ndio maana imejidhatiti kila kanda bara na visiwani.

Kimsingi mimi sio muumini wa siasa za kikabila, bali hizi ni siasa chafu za ccm inapozidiwa hoja. Kwa taarifa yako ccm kuenea nchi nzima sio kwa sababu haijali ukabila, bali ni sababu za kihistoria kuwa ilifaidi mfumo wa chama kimoja. Na wakati huo wa mfumo wa chama kimoja, ccm ilitembea kwa nguvu za serikali, sio zaidi ya hapo. Ila kinachoendelea chini ya awamu hii ya tano kwa upendeleo wa wazi kanda ya ziwa, hilo wala halihitaji mjadala.
 
 
Ndiyo atulize mshono sasa
 
Hizo ni dhana za kusadikika,sema umeingia kwenye siasa hivi karibuni tu. Hata Mwl Nyerere alikuwa anapakaziwa uongo kama huo kuwa anapendelea watu wa kanda ya ziwa wakati sio kweli.
 
"Press Card" ni nini? Hebu mtusaidie sisi wa St. Kayumba.

Yaani mwandishi ukishahitimu masomo yako bado utahitaji kibali cha kuzurura mitaani kukusanya habari na kuhoji watu?

Wajuzi tupeni shule!,

Je, wale waandishi wa milardayo na misago ambao huwa wanawahoji kina Shilole, Jux, Kingwendu na Jikeshupa wanazo hizo "Press Card"?
 
Usicheze kabisa na hii gavamenti, ukiwa ageinsti nayo wanakutingishaaa weeeee mpaka useme poooh,Halafu wanakupa maelekezo nini unatakiwa kufanya....yaani hii gavamenti hapa slovakia noma sana[emoji41]
 
Kumbeee!!!!
Ndio maana alikuwa na makala za uongo na kweli.
Kusifia na kuvuka mpaka, makosa dhahiri anayashobokea.
Ilibidi lazima apasi mtihani na mizania ya kusifu na kuabudu!
Pole Paskali!
 
Hizo ni dhana za kusadikika,sema umeingia kwenye siasa hivi karibuni tu. Hata Mwl Nyerere alikuwa anapakaziwa uongo kama huo kuwa anapendelea watu wa kanda ya ziwa wakati sio kweli.

Ninajua siasa kwa kiwango cha kuridhisha, huenda ni kweli sijui sana, ila kama ni kiwango cha kuijua siasa, basi ninakuzidi ww tena kwa mbali. Nyerere alikuwa na mapungufu yake, lakini hilo la kupendelea kanda ya ziwa haikuwahi kutokea. Rudi kwa anayekufundisha propaganda akuwekee hilo vizuri. Kwamba safari hii kuna upendeleo wa wazi kanda ya ziwa, hilo wala sina shaka nalo, na wala sijakuambia ili ukubali au ukatae, lakini habari ndio hiyo.
 
Hizo ni dhana za kusadikika,sema umeingia kwenye siasa hivi karibuni tu. Hata Mwl Nyerere alikuwa anapakaziwa uongo kama huo kuwa anapendelea watu wa kanda ya ziwa wakati sio kweli.
Mwalimu hajawahi kupakaziwa suala la ukabila, ila miaka ya mwanzoni mwa utawala wake alipakaziwa kuwa anawapendelea Wakatoliki.
 
Wewe ni mtu uliekariri mambo. Wakati David Musuguli ni Cdf ulikuwepo? Wakati akina Butiku wapo ikulu ulikuwepo? Unajua wenye akili ndogo kama wewe walikuwa wanasemaje?
 
Congratulions Pascal...hongera Sana...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…