Mwananchi B
JF-Expert Member
- May 23, 2013
- 1,885
- 4,131
Mwendo wa kula tu kimasihara
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Halafu sasa hapo Kenya hata tochi hakuna, na kwa gari za abiria speed limit ni 100Kmh., unatembea kutoka Nairobi to Mombasa bila hata shida., ila jamaa wanazingatia sana sheria, hutaona dereva amezidi speed 100. Shida ni hawa Madereva wetu wasipoona police barabarani wanashangilia, hapo mnaweza kudhani mnapaa.Duuh, tuna safari ndefu sana kama watu wenyewe ndo kama wewe. Hilo kosa liko wapi!? Wanaoruhusu usafiri 24hr wanapitia changamoto zipi ambazo unahisi zitatukuta nasi? Kenya and Uganda wana utaratibu huo wa 24hrs na bado sisi tuliokuwa tunasafiri mchana tuliwazidi kwa matukio ya ajali.
Hii dunia ni yetu ama unadhani ni ya ng'ombeKwani hii dunia ni yetu??? (In majanaba markuba's voice)
Hapo inabidi polisi iweke tochi za usiku vinginevyo madereva watatumaliza pamoja na kusafirisha mirungi .Samahani nje ya mada!! Hivi usiku Kuna tochi zatrafic!?
We inabidi nikukutanishe na jb una kitu maana picha umelimaliza kibabe kama mel gibson 😄[emoji1787][emoji1787][emoji1787] kuna siku nilipanda IT kutoka Dar, tukafika msamvu dereva akapakia abiria wengine wawili wote wa kiume safari ikaendelea na story nyingi.
Hapo mdada nipo peke yangu. Tulivyofika Mikumi wakatokea abiria wengine wawili nao wanaume tupu. Dereva akaingia tamaa walitaja pesa nyingi akawapakia hivyo hivyo kwa kubanana.
Mimi sikuwa na muda nao si nimekaa zangu mbele kwa dereva.
Shuhuli ilianzia tulivyozianza zile kona za Iyovi wale majamaa yaliyopakiwa Msamvu yakaanza lugha tusizozielewa. Muda huo dereva yupo speed, mbele katikati tukaona wale wakaka waliokuwa wanaongea kilugha wamechomoa MAPANGA yamenolewa kote kote yanang’aa.
Wanamwambia dereva paki gari pembeni, dereva anatetemeka panga liko shingoni mimi muda sielewi kitu nilikumbuka kusema Mungu nisaidie.
Lakini cha kushangaza wale wakaka wengine wao wametulia, nikaangalia kwenye kioo mmoja wa wale majamaa wengine anamuonyesha ishara dereva lakini sijaielewa.
Dereva akapaki gari tukashuka wote, wale majambazi wanaitaka gari na walishachorewa ramani na watu wao. Kabla hawajachukua gari tukashangaa wale wakaka wengine wanachomoa silaha za kazi [emoji23][emoji23][emoji23] woiiiih!!
Nikasema hii movie ya Damme leo naiona live.
Wakawaambia nyie wangese aliewaambia gari inaibiwa kijinga namna hii nani? Haya tupa mapanga chini kabla hatujamwaga ubongo wenu. Wakatupa zile panga yule mwenzie akazichukua, tukaambiwa we sister na suka ingiieni kwenye gari. Wale majambazi wa mapanga wakaomba basi bro tusameheane usiku saa hizi porini hapa tupeni lift mkatuache hata Ruaha Mbuyuni [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Wale majambazi wa bunduki mmoja akamuuliza dereva, “Oya suka hawa maboya wamekulipa nauli yako?” Dereva akasema hawajanilipa, akaulizwa unawadai shingapi? Akajibu, tulikubaliana elfu 60,000 wote wawili. Wakaambiwa leteni pesa hizo wakatoa lakini kwa manung’uniko. Akaambiwa oya mwanangu suka chukua pesa zako. Na nyie maboya mnabaki hapa mtajua wenyewe mnatoka vipi.
Safari ikaendelea ila hatujui hawa kina Van Damme na mwenzie Dolph tunamalizana nao vipi??
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
We inabidi nikukutanishe na jb una kitu maana picha umelimaliza kibabe kama mel gibson [emoji1]
Sema wewe wasinge kugusa 😄[emoji1787][emoji1787][emoji1787] wenzio tulikua tunacheza na kifo ooho! Usifanye masihara
Maabudu mashetani yasijeona fursa ya kufanya marejesho yao sasa. Nasikia nabii mdogo asiye na jina rejesho lake kwa mwezi ni damu ya watu sita. Mungu yehova awakemeeKuruhusu usafiri kwa saa 24 ni kutengeneza bomu ajali zitakuwa nyingi
Punguza uoga. Watakuja na mechanism nzuri.Kosa kubwa sana
Usiku watapelekeana motoEwaaaa.... hapa sasa ligi zitapendeza
Wamesha weka mipango, sio kwamba wameamka tu na kuruhusu.Kuruhusu usafiri kwa saa 24 ni kutengeneza bomu ajali zitakuwa nyingi
Sio kutembea usiku, usafiri utakuwa masaa ishirini na nne. Ina maana muda wowote basi linaondoka.Jumanne Sagini Wewe utapanda hayo mabasi ya kutembea usiku?
Mungu atunusuruSerikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeruhusu Mabasi ya abiria kufanya usafirishaji wa Saa 24, baaada ya kujiridhisha kiusalama, mwamko wa wananchi, huduma za mawasiliano pamoja na miundombinu ya usafirishaji.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Nchi, Jumanne Sagini wakati anaongea na Baraza la Taifa la Usalama Barabarani na kusema kuwa wamefikia maamuzi hayo baada ya Serikali kuimarisha shughuli za uchumi wa wananchi wake wa maeneo ya mjini na Vijijini.
Akiongeza kuwa wamezingatia maoni ya Wadau mbalimbali wakiwemo Wabunge, wamiliki wa mabasi, madereva wa mabasi, wasafiri, Wafanyabiashara na Wananchi kwa ujumla.
Aidha, Serikali imetoa maagizo kwa wadau wote wa usafirishaji kuzingatia Sheria, Kanuni na utaratibu wa leseni zao.
Pia madereva wametakiwa kuthibitishwa na LATRA, ambayo itatoa ratiba za safari kwa saa 24, TANROADS kuhakikisha ubora wa miundombinu, Serikali za Mitaa kuhakikisha zinasimamia usalama wa abiria kwenye huduma wanazosimamia pamoja na Jeshi la Polisi kusimamia Usalama wa watu na mali zao.
Umemsikia Mkurugenzi wa LATRA?. Wamesema watatoka utaratibu wa jinsi ya kusafiri.Madereva wa Tz mchana kweupe wanashindwa kufuata mwongozo wa taa za barabarani mpaka awepo askari wa usalama barabarani (trafiki), kweli watafuata sheria za barabarani usiku wa giza, hapa tunajipangia kuongeza takwimu za ajali mbaya za barabarani.
Ila watanzania tupo very negative. Tunawaza mabaya tu. Mbona mabasi yameruhisiwa kusafiri saa tisa usiku na hakuna shida. Tuangalir mambo chanya sio hasi pekee.Yaandaliwe kabisa maeneo ya kufanyia mazishi