Serikali yaruhusu Mabasi ya abiria kusafiri kwa saa 24

Halafu sasa hapo Kenya hata tochi hakuna, na kwa gari za abiria speed limit ni 100Kmh., unatembea kutoka Nairobi to Mombasa bila hata shida., ila jamaa wanazingatia sana sheria, hutaona dereva amezidi speed 100. Shida ni hawa Madereva wetu wasipoona police barabarani wanashangilia, hapo mnaweza kudhani mnapaa.
 
Safari za usiku zinahitaji utulivu sana wa akili. Kuna watu wa malori huko barabarani muda wa kuanzia saba-hadi kumi alfajiri wengi wao huwa na fatigue hivyo kupunguza umakini.
Binafsi sipendi safari za kuzidi sita usiku.
Kwa uendeshaji wetu napenda barabara yenye askari wengi wa barabarani
 
Safari za usiku zilisimamishwa na Lyatonga akiwa waziri mambo ya ndani kwa kukurupuka bila tafiti, kabla ya hapo mabasi yote ya mikoani yalikuwa yanaanza Safari saa 12 jioni, wapo wanaoona mchana ajali za mabasi hasa kupasuka matairi ni kubwa kuliko usiku,
Changamoto ya usiku ni usingizi wa madreva, Jambo ambalo ni uzembe
 
We inabidi nikukutanishe na jb una kitu maana picha umelimaliza kibabe kama mel gibson 😄
 
Hongera kwa uamuzi huu!

Fikiria ATM isingekuwa saa 24!!!

Tumechelewa sana,ni vyema uchumi uzunguke kwa saa 24.(kama ATM za benki)

Mauzo ya mafuta saa 24,wanaouza chakula na shughuli mbalimbali watakuwa wapo saa 24.uchumi na ajira itaongezeka.

Usafiri usiku ni sawa na mwenye kiwanda awe na uzalishaji wa bidhaa mara 2 kwani bidhaa zitazalishwa mchana na usiku.

Mataifa yaliyotuzidi kiuchumi wana itaratibu huu wa shughuli za uchumi kuwa saa 24

Wananchi wakubali na waelewe utaratibu ulikuwepo na maisha yaliendelea kama kawaida!!
 
Mungu atunusuru
 
Madereva wa Tz mchana kweupe wanashindwa kufuata mwongozo wa taa za barabarani mpaka awepo askari wa usalama barabarani (trafiki), kweli watafuata sheria za barabarani usiku wa giza, hapa tunajipangia kuongeza takwimu za ajali mbaya za barabarani.
Umemsikia Mkurugenzi wa LATRA?. Wamesema watatoka utaratibu wa jinsi ya kusafiri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…