Pre GE2025 Shabiby: Mkipewa Uwaziri mnaanza kuweka mipango ya kuwa Rais

Pre GE2025 Shabiby: Mkipewa Uwaziri mnaanza kuweka mipango ya kuwa Rais

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Akiwa Jimboni kwake Gairo Mkoani Morogoro, Mbunge Mheshimiwa Shabibi amewatonya wananchi juu ya mawaziri watumbuliwa.

Akiongea kwa mtindo au style ya kumsifu waziri wa Maji Juma Aweso alisema " Mheshimiwa Aweso wewe ni mchapa kazi Usiye na makuu wa kutamani makubwa, mwenzio mmoja aliyetenguliwa alishaandaa baraza lake la mawaziri , Ma RC, Ma DC, Ma DED na alibakiza nafasi chache za ubalozi" Alisema Waziri Aweso sio mtu wa kujikweza.

Hìi ina maana mmoja wa watumbuliwa alishajiandaa kuwa Rais tutake tusitake.
Kwenye nchi inayoheshimu misingi ya demokrasia na utawala bora hilo sio kosa, ni utaratibu wa kuweka bidhaa sokoni wanunuzi ndio wanaochagua bidhaa bora ya kununua
 
Shabibi ana hasira sana na Kipara!

Inawezekana kipara alikuwa anawakera watu wengi sana.

Hizo takataka zilizotumbuliwa ndio jpm alizipiga chini ila chura kiziwi akazirusisha eti anafungua nchi.
 
Ingependeza asaidie mamlaka kuwabaini wote waliopangwa kwenye uongozi wa huyo mtumbuliwa na wote waliopangwa wachunguzwe kama walikuwa wanafahamu ama laa kama walikuwa wanafahamu basi hatua kali za kinidhamu na kimaadili zichukuliwe dhidi yao

haha wakifanyiziwa utashangaa na kurudi hapa kulalamika tena, humo kwenye hilo baraza wamo akina tundu lisu wenu &co., waziri na tundu lisu ni wamoja ….
 
Mkumbuke pia kijana alikuwa Waziri wa Nishati.

Nchi hii usimuamini kila mtu maana wengi wetu ni wanafiki.
 
Kumanufesti kabla hujawa?
Mkuu alikuwa anapractice ile law of attraction ili law hiyo ije kumanifest hapo baadae.


Wataalamu mbalimbali wanasema kwamba ili law of attraction ifanye kazi vizuri ni vyema uka act kama yule mtu ambaye unataka kuwa hapo baadae.
 
Mkuu alikuwa anapractice ile law of attraction ili law hiyo ije kumanifest hapo baadae.


Wataalamu mbalimbali wanasema kwamba ili law of attraction ifanye kazi vizuri ni vyema uka act kama yule mtu ambaye unataka kuwa hapo baadae.
Ndio uanze na kuwapanga kabisa physically? wakati Ile inakua km unamediteti huko kwenye subconscious mind ndio mambo yanajipanga sio unaonyesha wazi wazi kabla hujawa
 
Akiwa Jimboni kwake Gairo Mkoani Morogoro, Mbunge Mheshimiwa Shabibi amewatonya wananchi juu ya mawaziri watumbuliwa.

Akiongea kwa mtindo au style ya kumsifu waziri wa Maji Juma Aweso alisema " Mheshimiwa Aweso wewe ni mchapa kazi Usiye na makuu wa kutamani makubwa, mwenzio mmoja aliyetenguliwa alishaandaa baraza lake la mawaziri , Ma RC, Ma DC, Ma DED na alibakiza nafasi chache za ubalozi" Alisema Waziri Aweso sio mtu wa kujikweza.

Hìi ina maana mmoja wa watumbuliwa alishajiandaa kuwa Rais tutake tusitake.
Story ya uongo alijuaje
 
Back
Top Bottom