Nyabhera,
Samahani kwa kukosea jina lako na kuondoa shida hii nitaliandika kwa kirefu siku zote.
Wewe unaweza kuwa na tafsiri yako ya suala hili ambayo iko kinyume na yangu.
Mimi nina paper nzima nimeandika nakuwekea hapo chini kipande:
''Wamisionari hawa walipotia mguu pwani ya Afrika ya Mashariki, nia yao hasa ilikuwa kuufuta Uislam.
Wakazi wa pwani hii iliyokuwa ikijulikana kama Zanj waliuona Ukrsto kwa mara ya kwanza kabisa mwaka 1498 Wareno walipofika sehemu hizo.
Mwaka 1567 wamishionari wa Augustinian waliingia Afrika ya Mashariki kupambana na Uislam ili Ukristo uwe dini ya dunia nzima.
Kadinali Lavigirie alianzisha The White Fathers, taasisi ya Kanisa Katoliki kwa kusudi maalum la kuupiga vita Uislam Wakati huo huo Church Missionary Society (CMS) ilikuwa imejitwisha kazi ya kuondoa ulimwengu kutokana na Uislam, ujinga na giza.
Hadi hii leo White Fathers wapo Tanzania wapo Tanzania wakiendelea kufanya kazi iliyowaleta Tanganyika zaidi ya miaka mia iliyopita.
Wajerumani walipofika Tanganyika waliwakuta Waislam wanafahamu kuandika, kusoma na walikuwa wameelimika katika hesabu.
Mmishionari Ludwig Krapf alipofika kwa Chifu Kimweri wa Usambaa mwaka 1848 alimkuta yeye na wanae wote wanajua kusoma.
Herufi walizokuwa wakitumia zilikuwa za Kiarabu.''
Wamishionari wamekuja kuwastaarabisha watu Pwani ya Afrika ya Mashariki wakawakuta watu tayari wamestaarabika kwa miaka mingi sana.
Hili halikuwafurahisha.
Ukristo ni dini mpya Tanzania kwa kuwa uliingizwa katika karne ya kumi na nane na wamisionari. Kanisa na Mwafrika Mkristo ni matokeo ya...
mohamedsaidsalum.blogspot.com