Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

1689262193028.png

1689262226657.png
 
Jiwe...
''Waingereza walipoja kuitawala Tanganyika (kama Tanzania inavyojulikana) baada ya kuondoka Wajerumani baada ya Vita Kuu ya Kwanza, Wajerumani walikuwa wameshafanya kazi ya kutosha ya kuiweka Tanganyika ndani ya mamlaka mbalimbali za Kikristo.

Tanganyika ilikuwa imegawanywa katika mamlaka mbalimbali za Kikristo kutoka nchi tofauti za Ulaya.
Kanisa Katoliki ambalo ndilo lenye nguvu zaidi, lilikuwa tayari limeshajikita Tanganyika.

White Fathers walikuwa wapo Tabora, Karema, Kigoma, Mbeya, Mwanza na Bukoba; Holy Ghost Fathers walikuwa Morogoro na Kilimanjaro; Benedictine Fathers walikwepo Peramiho na Ndanda; Capuchin Fathers walikuwepo Dar es Salaam; Consolata Fathers walikuwepo Iringa na Meru; Passionist Fathers walikuwa Dodoma; Pallotine Fathers walikuwa Mbulu; Maryknoll Fathers walikuwapo Musoma; na Rosmillian Fathers walikuwa Iringa.''

(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes)
Haya mashirika yapo mpaka leo.
Nimeipenda hiyo holly ghost father's nataman ungeielezea kiundan
 
Hayo ni mashirika ya kitume,je yalikua chini ya east africa association ya kipindi hicho kabla ya kuvunjika?
Holly ghost father's ni kanisa la kitume???


Kwa nin wamechagua jina lenye maana mbaya au nimeshindwa kutafsir kiusahih
 
White fathers walikuja kueneza injili na si vinginevyo
Nanta...
Ni kweli usemayo lakini ukisoma historia yao muasisi wa White Fathers anasema madhumuni ya kuja Afrika ni kueneza Injili na kuitoa Afrika gizani.

Anazungumza kuhusu, "Dark Continent."

Soma historia ya White Fathers utaongeza maarifa yako.
 
Huu sasa ni upuuzi, kuna watu wanatetea rasili mali za nchi, wengine wamekomalia udini.
 
Nanta...
Ni kweli usemayo lakini ukisoma historia yao muasisi wa White Fathers anasema madhumuni ya kuja Afrika ni kueneza Injili na kuitoa Afrika gizani.

Anazungumza kuhusu, "Dark Continent."

Soma historia ya White Fathers utaongeza maarifa yako.

Ndio walivyoamini hivyo,sidhani kama ilikua kosa lao kuamini na kufanya hivyo mana ndio utume wao,kama vile wewe unavyoamini na kuupigania uislamu,youre no different from them,tofauti ni kwamba wewe unaongozwa na chuki ila wao wanaongozwa na upendo na mfumo ulio imara ndio mana kila siku wanaendelea kustawi na kuenea.
 
Elimu dunia nayo ni muhimu sana kwa viongozi wetu wa dini la sivyo ndio kama haya.
 
Hilo li dua feki hata halitishi, mlipomsomea muislam mwenzenu JK Albadili alipata madhara gani?

We shehe ubwabwa kama hujui kusoma na kuandika acha wenye akili wakufunze uone upuuzi wa Waarab tuone ka utaukubali. Suala sio dini ni uozo wa mkataba!
 
TAMKO LA SHEIKH WA MKOA MWANZA KUHUSU MJADALA WA BANDARI

Utangulizi

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja kumekuwa na mjadala kuhusu uwekezaji na uendeshaji wa bandari zetu na kampuni kutoka Dubai. Mjadala ulianzishwa na wanasiasa na wanasheria lakini baadae ukachukua sura mpya na ya hatari ambayo nchi yetu haijawahi kushuhudia.

Hoja na mwelekeo wake

Wakati mjadala ulipoanza, hoja kubwa ilikuwa Wazanzibari wawili wanauza bandari za Tanganyika. Baada ya muda si mrefu, mjadala ukachukua sura mpya na kusisitizwa kuwa ni waarabu ndio waliouziwa nchi. Wakati mjadala unaendelea, ulihama kutoka sura ya kisiasa na kuingia udini.

Sote tumeshuhudia viongozi mbalimbali waandamizi wa dini ya kikristo walivyokuwa mstari wa mbele kupinga suala hili na wengine wamediriki kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa dini ya kikristo kumkejeli Rais Samia.

Baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wamedai kuwa Rais Samia amevunja Katiba na kwa maana hiyo anastahili kuondolewa madarakani. Mmoja wao ameenda mbali zaidi kwa kutishia kufanyike Mapinduzi ya kumuondoa Rais Samia madarakani. Jambo la ajabu ni kuwa mpaka sasa hakuna hata mtu mmoja ambaye ameupinga mkataba wa bandari kwa hoja za kiuchumi.

Wote waliozungumza na hasa viongozi wa dini ya kikristo wamezungumza kwa jazba na kumshambulia Rais Samia bila sababu za msingi. Kama viongozi hawa wana uchungu na wananchi, tuliwatarajia kupaza sauti zao wakati wa utawala uliopita ambao tumeshuhudia watu wengi kupoteza maisha yao bila maelezo. Pia tumeshuhudia serikali iliyopita imeingia kwenye miradi mikubwa kinyume cha utaratibu. Sote ni mashahidi, hakuna kiongozi hata mmoja wa kiislamu aliyeushambulia uongozi uliopita.

Wito

Mimi ninaamini kuwa mjadala huu umetawaliwa na UDINI na una lengo la kumtoa Rais Samia madarakani kabla ya muda wake. Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia.

Sheikh Hassan Kabeke ………………………………..

Sheikh wa Mkoa, MWANZA

Tarehe 6 Julai 2023
Huyu si ndiye sheikh masheikh wenzie, mwaipopo, majini walimtukana mno kuwa ni sheikh uchwara, mhuni, tapeli, mchawi, mwizi, fuska, na kadhalika? Walimwanika hadharani kweli kweli huyu.
Dini nyingine bwana!
 
CCM sio chama perfect wana mazuri na mabaya lakini kwa tabia hizi wanazozionesha Chadema ni hatari sana kwa nchi hii, maana tabia ya mtoto unamuona bado akiwa mdogo. CCM wanavumilia wanatukanwa lakini dola wanashika wao wangeweza kufanya mambo ya ajabu ila wameachia watu kuongea.

Sasa hawa wenzetu Chadema, hawana power, hawajashika hata u mayor tu lakini wewe toa maoni yako tofauti na wanavyotaka kusikia utatukanwa wewe, kahongwa , michawa na block unapigwa... Sasa kweli nyinyi mkija kushika nchi hii si itakuwa balaa. Maana mwenyekiti wenu tu hakuna wa kumgusa ukitaka ku challenge nafasi yake tu utapata habari yako, mtu zaidi ya miaka 20 mwenyekiti utasema karithi. JPM Mungu angempa umri alikuwa anafukia hichi chama na aliweza maana walifyata mikia, Rais Samia alidhani kuwa mkarimu ataweka mambo mazuri lakini nikiri kosa kubwa alifanya angeshika palepale JPM alipoachia. JPM alijuwa hawa hawana nia njema na nchi hii na sasa tumeanza kuwaona. Hawataki kupingwa wala hawakubali kuwa kuna watu wanapenda CCM.

Angalizo kwa wapenda amani, tupinge mabaya bila matusi ila tuepuke hichi chama CDM kama ukoma hawa hawafai hata kuwepo kwenye siasa za nchi ni watu wabaya tena wabaya kupitiliza. Jini ulijualo.... utamalizia.

CCM zibeni masikio kwa muda tokemezeni hichi chama haraka warudisheni kwenye mapango yao before is too late, usifanye mazoea sana na mbwa...
 
Back
Top Bottom