Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

CCM sio chama perfect wana mazuri na mabaya lakini kwa tabia hizi wanazozionesha Chadema ni hatari sana kwa nchi hii, maana tabia ya mtoto unamuona bado akiwa mdogo. CCM wanavumilia wanatukanwa lakini dola wanashika wao wangeweza kufanya mambo ya ajabu ila wameachia watu kuongea.

Sasa hawa wenzetu Chadema, hawana power, hawajashika hata u mayor tu lakini wewe toa maoni yako tofauti na wanavyotaka kusikia utatukanwa wewe, kahongwa , michawa na block unapigwa... Sasa kweli nyinyi mkija kushika nchi hii si itakuwa balaa. Maana mwenyekiti wenu tu hakuna wa kumgusa ukitaka ku challenge nafasi yake tu utapata habari yako, mtu zaidi ya miaka 20 mwenyekiti utasema karithi. JPM Mungu angempa umri alikuwa anafukia hichi chama na aliweza maana walifyata mikia, Rais Samia alidhani kuwa mkarimu ataweka mambo mazuri lakini nikiri kosa kubwa alifanya angeshika palepale JPM alipoachia. JPM alijuwa hawa hawana nia njema na nchi hii na sasa tumeanza kuwaona. Hawataki kupingwa wala hawakubali kuwa kuna watu wanapenda CCM.

Angalizo kwa wapenda amani, tupinge mabaya bila matusi ila tuepuke hichi chama CDM kama ukoma hawa hawafai hata kuwepo kwenye siasa za nchi ni watu wabaya tena wabaya kupitiliza. Jini ulijualo.... utamalizia.

CCM zibeni masikio kwa muda tokemezeni hichi chama haraka warudisheni kwenye mapango yao before is too late, usifanye mazoea sana na mbwa...

Umeongea pumba na kupoteza bando. unajua yanayotendeka au unakalia kusoma habari za michezo
 
Umeongea pumba na kupoteza bando. unajua yanayotendeka au unakalia kusoma habari za michezo
Unafanya yaleyale niliyosema hamtaki mtu mwingine kuwa na maono mengine ndio maana nasema nyinyi kamwe hamtashika nchi JPM hata bungeni tu aliwasafisha.
 
Ubaguzi ni upi na wakiarabu ni upi?

Kama wewe ni Mwafrika achana na biashara za Kiarabu na kuwabagua waafrika wenzako .
Umedhihirisha wewe ni mbaguzi, na ni mdini vile vile, mimi ni muislamu na Mwenyezi Mungu ametutaka tupendane na sio kuwekeana chuki, eti nimchukie mwarabu halafu nimpende only mwafrika😄, unachekesha sana,, ni kwamba huna imani ndio maana unawachukia waarabu, kwa taarifa yako nawapenda binaadam wote bila kujali rangi ya mtu, udini na ukabila. Ilaa ilaa nachukia matendo maovu
Leo hii ikitokea ajali au janga lolote linalowahusu watanzania maskini weusi hakuna Mhindi Wala muarabu anayekusaidia wewe mmatumbi zaidi ya mmatumbi mwenzako .
Usome Uislamu vizuri upate kujua, waarabu ni ndugu zetu, siwezi kuona mwarabu anaonewa au kutukanwa na mkristo mtu ambae hana undugu na waislamu halafu nimuangalie tu, never never. Tena ondoa akilini hilo mzee

Miaka mingi watu wa Kigoma , Tabora , Lindi Mtwara hawakua na Barabara zinazopitika Kwa uhakika lakini Waarabu na Wazungu walikuwapo na wapo miaka yote . Wanaangalia kwao na maslahi yao. Rasilimali za Nchi yetu ni Kwa ajili za Vizazi vya waafrika na sio wageni ndio maana mwenyzezi Mungu alituwekea waafrika kama akina Karume na wakawatoa hao wageni waovu na mashetani.

Huko kanisani ndivyo mnafundishwa kuchukia waarabu kiasi hicho? Huko makanisani mnafundishwa kuchukia wazanzibari kiasi hicho? Kisa waislamu!! Sikiliza bwana, tena watu kama wewe na wenye vimelea vya ubaguzi, udini na ukabila na kuchochea chuki dhidi ya waarabu na Uisilamu kwa ujumla, dawa yenu mkamatwe na kuswekwa ndani, ili iwe fundisho kwa wengine. Uisilamu ni dini iliyokamilika, usome vizuri upate kujua.
Shetani hajawahi kuuza mtu lakini Wazungu na Waarabu waliuza watu . Tunasimuliwa habari za shetani kama tunavyosimuliwa habari za Waarabu na Wazungu . Likini shetani hajawahi KUONEKANA akimuuza binadamu kama walivyofanya hao watu waovu wa mashariki na magharibu .
Kwangu Mimi hao ndio mashetani wanaotajwa.
Tunawakaribisha mashetani .

Elimu elimu elimu,
Utajiri wao usiondoe utu wetu Sisi waafrika na nchi yetu.
Wanawachanganyia dini na siasa bila kuangalia matendo yao ndio maana mnawaona kuwa ni watu wazuri kumbe ni mashetani wakubwa.

Hakuna mwafrika anaweza kupewa ardhi yenye mafuta Dubai .
Wazungu wametumia mabavu kupata mafuta Huko lakini sio ridhaa yao.


Kule Sudani weusi walijidanganya kuwa wako sawa na Waarabu lakini walipojaribu kushika madaraka ndio wakagundua kuwa wao ni Daraja la watumwa.

Kama unabisa vunja muungano Utaona Jinsi dini isivyo na nafasi kwenye kutawala maana watu wa dini Moja watabaguaja katika kushika madaraka. Utaona kuwa umoja unaousema ni kwasababu Kuna watu wa dini nyingine.

Ni lazima Tuthamini kile Mungu alichotupa Sisi watu weusi.
Mungu ametupa Rasilimali nyingi zaidi yao. Kuonyesha kuwa alitupenda kuliko wao wanaotaka kutununua na kutufanya watumwa.
Watoto wa Mfalme ni sisi waafrika na wao wanapaswa kuja Kununua na kuondoka sio kutufanya watumwa.
Wabaki na mafuta yao mana tunanunua na hawatupi Bure na hatuwaombi mana tukiamia waafrika tutachimba ya kwetu.
Ni viongozi wa hovyo TU ndio wanawaona Waarabu kama malaika na kuona kuwa wao ni Bora kuliko Sisi.

KILA KITU MWANADAMU ANAFUNDISHWA MAANA ELIMU ILILETWA ILI KILA MTU AIPATE AITUMIE KUENDESHA MAISHA YAKE NA KUONDOKANA NA UTUMWA NA UNYANYASAJI.
WAAFRIKA TUNA WASOMI WENGI TUWATUMIE SIO KUBAGIANA KWA ITIKADO ZA KIDINI.

DINI NI ELIMU PIA TUIFUATE KAMA INAVYOTUTAKA KUTENDA SIO KUTUMIA DINI KUWANYONYA NA KUWAFANYA WENGINE WATUMWA

Maneno meeengi, in short jirekebishe na auache ubaguzi, udini na ukabila
 
Umedhihirisha wewe ni mbaguzi, na ni mdini vile vile, mimi ni muislamu na Mwenyezi Mungu ametutaka tupendane na sio kuwekeana chuki, eti nimchukie mwarabu halafu nimpende only mwafrika[emoji1], unachekesha sana,, ni kwamba huna imani ndio maana unawachukia waarabu, kwa taarifa yako nawapenda binaadam wote bila kujali rangi ya mtu, udini na ukabila. Ilaa ilaa nachukia matendo maovu

Usome Uislamu vizuri upate kujua, waarabu ni ndugu zetu, siwezi kuona mwarabu anaonewa au kutukanwa na mkristo mtu ambae hana undugu na waislamu halafu nimuangalie tu, never never. Tena ondoa akilini hilo mzee



Huko kanisani ndivyo mnafundishwa kuchukia waarabu kiasi hicho? Huko makanisani mnafundishwa kuchukia wazanzibari kiasi hicho? Kisa waislamu!! Sikiliza bwana, tena watu kama wewe na wenye vimelea vya ubaguzi, udini na ukabila na kuchochea chuki dhidi ya waarabu na Uisilamu kwa ujumla, dawa yenu mkamatwe na kuswekwa ndani, ili iwe fundisho kwa wengine. Uisilamu ni dini iliyokamilika, usome vizuri upate kujua.


Elimu elimu elimu,


Maneno meeengi, in short jirekebishe na auache ubaguzi, udini na ukabila
Wewe ndiye mdini na umejipambanua wazi kuwa huwezi kumsaidia mkristo Badala ya Mwarabu ámbaye ni muislam mwenzako.

Sina upumbavu huo Wa kuwa mtumwa Wa Matajiri Toka nje.
Hapo unachokinyenyekea ni utajiri Wa Waarabu na SIO Dini.
Dini Kila mmoja Ana madili yake na Mungu wake. Wapo Waarabu wanaotumia Dini kujilimbikizia Mali bila na kuwanyanyasa watu kama mbwa.
Nimeweka wazi kuwa sitakubali kamwe nchi Yetu kuuzwa Kwa wageni Kwa Sababu tu ya Dini .
Sijapiga uislam Wala uarabu lakini napinga MTU yeyote anayegawa Mali za nchi Kwa kushindwa kusimamia watu aliowateua mwenyewe.
Wangeanza kuuza bandari za ndugu Wa Waarabu kule Zanzibar kabla ya zile za bara zenye mchanganyiko Wa wasio na Dini Wala nasaba za Kiarabu Kama tunaangalia udini na uarabu.

Tujifunze Kule Sudani ambapo wote ni Waislam lakini weusi wananyanyaswa kwenye bara lao na nchi Yao ya asili.

Zanzibar hawataki chama kingine kitawale na hawataki usultani wakati watanzibar wote ni Waislam.
Muungano ndio unawapa jeuri ya kuwaonea Wakristo kuwa SIO ndugu zao lakini Amini na kuambia Siku Muungano ukivunjika watanzibar watabaguaja Kwa rangi Kwa misingi ya Uarabu na Uafrika Kama wataanza kuchanganya mambo ya siasa Dini ,maendeleo na kutegemea Waarabu nje ya Zanzibar ndio wawaamulie kuhusu maendeleo ya nchi Yao.

Karume hakuwa mkristo lakini aliifanya Mapinduzi Kupinga dhulma za Waarabu. Hakupinga Dini ya kiislam.

Mimi sipingi kamwe uislam .
Na Karne hii hakuna mkristo anayehangaika Kupinga uislam. Wakristo na watu Wote wanaojitambua hawana muda Wa kuchanganya masuala ya Dini na uchumi ,watu Wanapinga kugawanywa Kwa rasilimali za nchi Yao Kwa Wageni bila kujali Dini . Wachina hawana Dini tulizo nazo lakini wameshika miradi mingi Kwa mikataba ya muda mfupi na ya kueleweka.

Huu mkataba uachwe haraka mana umejikita kwenye udini na Uarabu . Utaharakisha Amani na usalama Wa nchi.
Dubai ni mawakala Wa Marekani miaka mingi . Tanzania hatufungamani na nchi yoyote . Kuwakaribisha Wamarekani kupitia mgongo Wa Dubai ni kuhatarisha Amani ya ukanda Wa Bahari ya Hindi Kwa kupora Madini ya Urenium na kumiliki mafuta na gesi.

Dunia imejaa Matajiri Wanaowaza kulimbikiza Mali na Sio kuwasaidia WAAFRIKA. WAAFRIKA wakiamka Hawa watakua wamehamia Mars .
 
Mohamed,hayo yote unayosema nayajua.
Kifo cha EAMWS ( taasisi iliyoanzishwa na Aga Khan mShia ambae nyie mnawaona apostate) kilitokana na wao kukataliwa na Karume ambae hakuwa mkristu kwa kuiona kuwa ni taasisi ya waarabu na wahindi. Aga Khan (muasisi wa EAMWS) muislamu hajawahi kuzuiwa kujenga Chuo Kikuu Tanzania.

Upendo ni mmisheni kutaifisha mamia ya shule za wamisheni ili kila raia aweze kupata elimu anayostahili. Upendo ni mmisheni kuchukua chuo kilichojengwa kwa fedha za umma na kuipa bure taasisi ya kiislamu ili wakigeuze kuwa Chuo Kikuu cha Kiislamu. Vyote hivi huvioni kwa sababu chuki za kidini ziko kwenye DNA yako.

Waislamu walipewa eneo la kujenga Chuo Kikuu chao Chang'ombe lakini hamkuweza kukiendeleza mpaka mwishoni mkaamua kukiuza kwa mfanyabiashara mmoja wa kiislamu. OIC haijawahi kuzuiwa kuanzisha Chuo Kikuu Tanzania. Kilichopigiwa kelele na Nyerere ni Zanzibar kujiunga kinyemela na OIC. Sasa kama rushwa ya kujiunga ili kuwa ni kujengewa Chuo Kikuu ndio kwanza nasikia. Na kama walikuwa na nia ya dhati ya kujenga hicho Chuo Kikuu kitu gani kinacho wazuia hadi leo?

Hawa maprofesa, madaktari na wasomi kibao wa kiislamu walipatikanaje wakati unasema wizara ya elimu haikutaka wapate elimu? Badala ya kujiangalia wenyewe na kujiuliza kwa nini vijana wenu hawafanyi vizuri kama vijana wa dini nyingine, unashinda kutafuta mchawi. Na kwa vile sio waislamu wote ambao hawafanyi vizuri ingekuwa busara zaidi kujifunza kutoka wale wanaofanya vizuri pamoa na wale wa dini nyingine wanaofanya vizuri.

Hizo shule za FEZA, Al-Muntazir ni za wakristu? Shule gani ya kiislamu iliyohujumiwa kwa sababu tu ni ya kiislamu na sio kwa sababu ya matendo ya uongozi wake? Au unazungumzia ile shule iliyomdhulumu maksi binti maskini wa kiislamu na kuwapa wale wenye uwezo wa kifedha? Ulitaka isiadhibiwe kwa sababu ilikuwa inamilikiwa na kuendeshwa na waislamu? Seriously!

Hilo la kufuta historia ya mchango wa waislamu tumeijadili sana humu ndani na imekuwa debunked. Tofauti na unavyotaka mchango wa wazazi wako wa Gerezani wapewe kipaumbele, ukweli ni kuwa watu kutoka dini na makabila yote walipigania uhuru bila kujali dini au kabila zao. Hao wakina Sykes, walipigania kama wazalendo wa kitanganyika na sio waislamu. Hawakupigania uhuru ili kuigeuza Tanganyika iwe Caliphate bali iwe nchi ambayo watoto wao na wa wakina Julius John, Dennis na wengine waweze kuishi pamoja kwa upendo na kuheshimiana katika nchi yao ya Tanganyika. Kitu ambacho kwa kiasi kikubwa walifanikiwa na kitaendelea kufanikiwa pamoja na juhudi zako wewe na wenzako za kupanda mbegu za chuki katika jamii yetu.

Mwenyewe unajua kuwa hamna jipya tunaloweza kujadiliana kuhusu mchango wa waislamu katika jamii yetu. Ushahidi mwingi uliouweka uligundulika kuwa ni fake au ulikuwa wa kupotosha. Mimi sikatai kuwa waislamu kama wakina Sykes, Aziz, Mwapachu walitoa mchango mkubwa katika juhudi za ukombozi wa nchi hii. Ninachokataa ni wewe kutaka mchango wao upewe nafasi kubwa kuliko wa wakina Julius na John kwa sababu tu ni waislamu.

Ninakataa kuwa mchango wao haukupewa uzito uliostahili kwa sababu ya dini yao kwa sababu mchango wa wakristu wengi tu kama wakina Vedastus Kyaruzi, Dennis Phombeah, John mwakangale, John Rupia, Mwanjisi na wengine wengi tu nao haujapewa heshima inayostahili. Nyerere pamoja na kuwa mkatoliki lakini aliwatia kizuizini wakristu wengi na kuwafungulia wengi kesi za uhaini. Kumgeuza mdini ni kutomtendea haki. Nyerere ana mengi ya kukoselewa lakini sio kwenye masuala ya ubaguzi hasa wa dini.

Amandla...

Nguruvi3 JokaKuu Mag3
Unamnukuu Mohamed Said bila kumpa heshima yake.


Wengi ya uliowataja kwa mara ya kwanza kwenye historia ya Tanganyika kawataja Mohamed Said.
 
Ubaguzi ni upi na wakiarabu ni upi?

Kama wewe ni Mwafrika achana na biashara za Kiarabu na kuwabagua waafrika wenzako .
Leo hii ikitokea ajali au janga lolote linalowahusu watanzania maskini weusi hakuna Mhindi Wala muarabu anayekusaidia wewe mmatumbi zaidi ya mmatumbi mwenzako . Miaka mingi watu wa Kigoma , Tabora , Lindi Mtwara hawakua na Barabara zinazopitika Kwa uhakika lakini Waarabu na Wazungu walikuwapo na wapo miaka yote . Wanaangalia kwao na maslahi yao. Rasilimali za Nchi yetu ni Kwa ajili za Vizazi vya waafrika na sio wageni ndio maana mwenyzezi Mungu alituwekea waafrika kama akina Karume na wakawatoa hao wageni waovu na mashetani.

Shetani hajawahi kuuza mtu lakini Wazungu na Waarabu waliuza watu . Tunasimuliwa habari za shetani kama tunavyosimuliwa habari za Waarabu na Wazungu . Likini shetani hajawahi KUONEKANA akimuuza binadamu kama walivyofanya hao watu waovu wa mashariki na magharibu .
Kwangu Mimi hao ndio mashetani wanaotajwa.
Tunawakaribisha mashetani .

Utajiri wao usiondoe utu wetu Sisi waafrika na nchi yetu.
Wanawachanganyia dini na siasa bila kuangalia matendo yao ndio maana mnawaona kuwa ni watu wazuri kumbe ni mashetani wakubwa.

Hakuna mwafrika anaweza kupewa ardhi yenye mafuta Dubai .
Wazungu wametumia mabavu kupata mafuta Huko lakini sio ridhaa yao.


Kule Sudani weusi walijidanganya kuwa wako sawa na Waarabu lakini walipojaribu kushika madaraka ndio wakagundua kuwa wao ni Daraja la watumwa.

Kama unabisa vunja muungano Utaona Jinsi dini isivyo na nafasi kwenye kutawala maana watu wa dini Moja watabaguaja katika kushika madaraka. Utaona kuwa umoja unaousema ni kwasababu Kuna watu wa dini nyingine.

Ni lazima Tuthamini kile Mungu alichotupa Sisi watu weusi.
Mungu ametupa Rasilimali nyingi zaidi yao. Kuonyesha kuwa alitupenda kuliko wao wanaotaka kutununua na kutufanya watumwa.
Watoto wa Mfalme ni sisi waafrika na wao wanapaswa kuja Kununua na kuondoka sio kutufanya watumwa.
Wabaki na mafuta yao mana tunanunua na hawatupi Bure na hatuwaombi mana tukiamia waafrika tutachimba ya kwetu.
Ni viongozi wa hovyo TU ndio wanawaona Waarabu kama malaika na kuona kuwa wao ni Bora kuliko Sisi.

KILA KITU MWANADAMU ANAFUNDISHWA MAANA ELIMU ILILETWA ILI KILA MTU AIPATE AITUMIE KUENDESHA MAISHA YAKE NA KUONDOKANA NA UTUMWA NA UNYANYASAJI.
WAAFRIKA TUNA WASOMI WENGI TUWATUMIE SIO KUBAGIANA KWA ITIKADO ZA KIDINI.

DINI NI ELIMU PIA TUIFUATE KAMA INAVYOTUTAKA KUTENDA SIO KUTUMIA DINI KUWANYONYA NA KUWAFANYA WENGINE WATUMWA
1689729319791.png

 
Sema wafuasi wa bakwata wakiibuka kuongelea mambo ya kitaifa huwa wanatema upupu kuliko hata watoto wa primary school.

Tatizo nini ?
[emoji3526][emoji23][emoji38][emoji38][emoji23][emoji23][emoji3526][emoji16][emoji4][emoji6][emoji6][emoji3526][emoji23][emoji38][emoji38]
 
Mohamed Said salam sheikh
Naanza kwa tahadhari kwamba unapoleta jambo ni vema ukajiridhisha na uthabiti wake.



Mag3 Fundi Mchundo JokaKuu Pascal Mayalla

Mbona umesahaukuwaiota kina pascal Mayala, Mzee Mwanakijiji, Yericko Nyerere, Mushi nani sijuwi. Waje kukusaidia?

Hao uliowataja pamoja na wewe bado, hamumuingii Mohamed Said. Unafikiri tumesahau alivyowahenyesha mpaka mkasema mtaenda kuandika kitabu chenu cha kumpinga? Kiko wapi?


Matokeo yake Yericko Nyerere akafanya plagiarism mtindo mmoja, sema akamkuta Alama Mohamed Said muungwana hakutaka kumsasambuwa, Mzee Mwanakijiji akaenda kuandika article hayohayo, plagiarism mwanzo mwisho.

Bado hamjaelimika. Ikiwa ma profesa wenu kina Issa Shivji wanaenda kupiga goti kwa Mohamed Said kuchota elimu, itakuwa nyinyi?
 
Unamnukuu Mohamed Said bila kumpa heshima yake.


Wengi ya uliowataja kwa mara ya kwanza kwenye historia ya Tanganyika kawataja Mohamed Said.
Haiendi hivyo. Ninachopaswa kufanya ni kusema ni wapi nimetoa hayo niliyoandika na si vinginevyo. Kwa vile hii nilikuwa siandiki academic paper silazimiki kufanya hivyo. Vile vile siwezi vile vile kusema nani alikuwa wa kwanza kuwataja bila kufanya utafiti wa kutosha.

Amandla...
 
Tatizo la wengi wanaotetea mkataba upitishwe ni kwamba wanawapinga watoa hoja na sio hoja zinazoletwa
 
Mbona umesahaukuwaiota kina pascal Mayala, Mzee Mwanakijiji, Yericko Nyerere, Mushi nani sijuwi. Waje kukusaidia?

Hao uliowataja pamoja na wewe bado, hamumuingii Mohamed Said. Unafikiri tumesahau alivyowahenyesha mpaka mkasema mtaenda kuandika kitabu chenu cha kumpinga? Kiko wapi?


Matokeo yake Yericko Nyerere akafanya plagiarism mtindo mmoja, sema akamkuta Alama Mohamed Said muungwana hakutaka kumsasambuwa, Mzee Mwanakijiji akaenda kuandika article hayohayo, plagiarism mwanzo mwisho.

Bado hamjaelimika. Ikiwa ma profesa wenu kina Issa Shivji wanaenda kupiga goti kwa Mohamed Said kuchota elimu, itakuwa nyinyi?
Faiza siku hizi umezidisha uongo. Lini nimewahi kusema kuwa nitaandika kitabu kushindana na Mohammed Said? Hebu weka hilo bandiko ambamo mimi au Nguruvi3 tumesalimu amri kwa Mohammed? Moja tu.

Hilo la Issa Shivji kumpigia magoti ni lako na wala halituhusu.

Amandla...
Nguruvi3
 
Faiza siku hizi umezidisha uongo. Lini nimewahi kusema kuwa nitaandika kitabu kushindana na Mohammed Said? Hebu weka hilo bandiko ambamo mimi au Nguruvi3 tumesalimu amri kwa Mohammed? Moja tu.

Hilo la Issa Shivji kumpigia magoti ni lako na wala halituhusu.

Amandla...
Nguruvi3
Mlikuwa wengi wengi tu tu siyo peke yako.

Wewe pia piga goti uulize upewe elimu. Unaijuwa historia ya Uhuru wa Tanganyika ilianzia wapi? Hiyo unayoijuwa wewe utueleze na chanzo chako, thubutu kama hujarudi mule mule tu.

Huna ujanja huo.
 
Mlikuwa wengi wengi tu tu siyo peke yako.

Wewe pia piga goti uulize upewe elimu. Unaijuwa historia ya Uhuru wa Tanganyika ilianzia wapi? Hiyo unayoijuwa wewe utueleze na chanzo chako, thubutu kama hujarudi mule mule tu.

Huna ujanja huo.
Faiza, sina haja ya kurudia rudia niliyoandika. Mimi na Mohammed Said tumejadiliana masuala mengi tu na sio historia ya Tanganyika peke yake. Nadhani mwisho wa siku tumekubali kuwa yeye hawezi kunibadili kama vile mimi nisivyoweza kumbadili.

Hii ni tofauti na mtu kama wewe ambae unaamini kuwa sehemu yote tunayoijua sasa kama Tanganyika ilikuwa chini ya Sultan wa Zanzibar. Mtu kama wewe ni vuvuzela maana unarudia tu bila kufikiri yale yanayosemwa na wale unaowaabudu. Mbaya zaidi ni muongo.

Amandla...
 
Faiza, sina haja ya kurudia rudia niliyoandika. Mimi na Mohammed Said tumejadiliana masuala mengi tu na sio historia ya Tanganyika peke yake. Nadhani mwisho wa siku tumekubali kuwa yeye hawezi kunibadili kama vile mimi nisivyoweza kumbadili.

Hii ni tofauti na mtu kama wewe ambae unaamini kuwa sehemu yote tunayoijua sasa kama Tanganyika ilikuwa chini ya Sultan wa Zanzibar. Mtu kama wewe ni vuvuzela maana unarudia tu bila kufikiri yale yanayosemwa na wale unaowaabudu. Mbaya zaidi ni muongo.

Amandla...
huna jipya, nimekuuliza swali dogo umeshindwa kulijibu.

Wewe unakijuwa nini kwenye historia ya uhuru wa Tanganyika cha kuweza kubadili mawazo ya mtu?

Mengine hayo nakuona unabwabwaja na kuhororoja bila mpango.
 
huna jipya, nimekuuliza swali dogo umeshindwa kulijibu.

Wewe unakijuwa nini kwenye historia ya uhuru wa Tanganyika cha kuweza kubadili mawazo ya mtu?

Mengine hayo nakuona unabwabwaja na kuhororoja bila mpango.
Faiza, ndio maana kujibishana na wewe ni kupoteza muda. Nitakujibu ukiniambia Chifu Mkwanyivika Munyigumba Mwamunyinga wa Wahehe alianza lini kumtumikia Sayyid Barghash bin Said al-Busaid aliyekuwa Sultan wa Zanzibar?

Amandla...
 
Faiza, ndio maana kujibishana na wewe ni kupoteza muda. Nitakujibu ukiniambia Chifu Mkwanyivika Munyigumba Mwamunyinga wa Wahehe alianza lini kumtumikia Sayyid Barghash bin Said al-Busaid aliyekuwa Sultan wa Zanzibar?

Amandla...
Hakuna "Chifu" aliyemtumikia Sultani, nijuavyo Sultani ndiye anawatumikia raia zake.

Kwanza hata jina "chifu" halikuwepo wakati wa utawala wa Masultani, kumbuka hilo.

Hakuna reality kwenye swali lako.
 
TAMKO LA SHEIKH WA MKOA MWANZA KUHUSU MJADALA WA BANDARI

Utangulizi

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja kumekuwa na mjadala kuhusu uwekezaji na uendeshaji wa bandari zetu na kampuni kutoka Dubai. Mjadala ulianzishwa na wanasiasa na wanasheria lakini baadae ukachukua sura mpya na ya hatari ambayo nchi yetu haijawahi kushuhudia.

Hoja na mwelekeo wake

Wakati mjadala ulipoanza, hoja kubwa ilikuwa Wazanzibari wawili wanauza bandari za Tanganyika. Baada ya muda si mrefu, mjadala ukachukua sura mpya na kusisitizwa kuwa ni waarabu ndio waliouziwa nchi. Wakati mjadala unaendelea, ulihama kutoka sura ya kisiasa na kuingia udini.

Sote tumeshuhudia viongozi mbalimbali waandamizi wa dini ya kikristo walivyokuwa mstari wa mbele kupinga suala hili na wengine wamediriki kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa dini ya kikristo kumkejeli Rais Samia.

Baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wamedai kuwa Rais Samia amevunja Katiba na kwa maana hiyo anastahili kuondolewa madarakani. Mmoja wao ameenda mbali zaidi kwa kutishia kufanyike Mapinduzi ya kumuondoa Rais Samia madarakani. Jambo la ajabu ni kuwa mpaka sasa hakuna hata mtu mmoja ambaye ameupinga mkataba wa bandari kwa hoja za kiuchumi.

Wote waliozungumza na hasa viongozi wa dini ya kikristo wamezungumza kwa jazba na kumshambulia Rais Samia bila sababu za msingi. Kama viongozi hawa wana uchungu na wananchi, tuliwatarajia kupaza sauti zao wakati wa utawala uliopita ambao tumeshuhudia watu wengi kupoteza maisha yao bila maelezo. Pia tumeshuhudia serikali iliyopita imeingia kwenye miradi mikubwa kinyume cha utaratibu. Sote ni mashahidi, hakuna kiongozi hata mmoja wa kiislamu aliyeushambulia uongozi uliopita.

Wito

Mimi ninaamini kuwa mjadala huu umetawaliwa na UDINI na una lengo la kumtoa Rais Samia madarakani kabla ya muda wake. Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia.

Sheikh Hassan Kabeke ………………………………..

Sheikh wa Mkoa, MWANZA

Tarehe 6 Julai 2023
Bila maelezo Mengi.. hata Kwa Magufuli Kuna baadhi ya maamuzi viongizi WA kikristo walisimama kukemea hadharani pasipo unafki

Kwa huu mkataba hiyo inferiority complex yenu isitufanye tukaonekana tunao udini.. hapana

Na kama huyo shekh amaetamka hayo Mambo kweli ameonyesha udhaifu mkubwa kama kiongozi Kwa kufikiria jambo hili kidini..

Ukifatilia hoja za watanzania Ni kuhusu namna ambavyo mkataba umekaa kinyonyaji.. tunataka tuingie mkataba ambao wakizingua na Sisi tunawazungua yani Kwa kifupi

Nampa Sheikh mfano atakao uelewa Zaidi.. kama ilivyo ndoa ya kiislamu Talaka Ni ruksa
 
Hakuna "Chifu" aliyemtumikia Sultani, nijuavyo Sultani ndiye anawatumikia raia zake.

Kwanza hata jina "chifu" halikuwepo wakati wa utawala wa Masultani, kumbuka hilo.

Hakuna reality kwenye swali lako.
Faiza, wewe ni muongo au haujaelimika au vyote viwili. Nitajaribu kukuelimisha ingawa najua hauwezi kuelewa. Sultani au absolute Mfalme/ Malkia hajawahi kuwatumikia watu wake. Ndio maana watu hao wanaoitwa "subjects" wake na sio raia wake. Mifano hai tunaiona Saudi Arabia, Brunei, Eswatini, Morocco n.k. ambako neno la mfalme ni la mwisho.

Kama unasema hakuna Chifu aliyemtumikia Sultani utasemaje Sultani alitawala sehemu yote iliyokuja kujulikana kama Tanganyika? Ukweli ni kuwa Sultani wa Zanzibar hajawahi kutawala sehemu yote hiyo isipokuwa miji michache iliyokuwa katika pwani ya sehemu hiyo na michache iliyokuwa mwambao. Sehemu kubwa ya sehemu hiyo ilikuwa chini ya utawala wa viongozi wa kiafrika wa kiasili ambao kwa kiingereza waliitwa "chiefs" au machifu kwa kiswahili. Viongozi hao waliitwa majina mengine ( Mangi, Mtemi, Kabaka n.k.) kwa lugha za makabila yao.

Baadhi ya viongozi hao ndio walioingia mikataba ya maghumashi na Karl Peters. Karl Peters alifanya hivyo kwa sababu alitambua kuwa walikuwa viongozi huru na hawakuwajibika kwa huyo Sultani wako. Kuonyesha jinsi Sultani wako alivyokuwa hana nguvu, hakuhusishwa hata kwenye makubaliano ya Heligoland na Zanzibar! Najua hata hiyo Treaty hauijui.

Amandla...
 
Faiza, wewe ni muongo au haujaelimika au vyote viwili. Nitajaribu kukuelimisha ingawa najua hauwezi kuelewa. Sultani au absolute Mfalme/ Malkia hajawahi kuwatumikia watu wake. Ndio maana watu hao wanaoitwa "subjects" wake na sio raia wake. Mifano hai tunaiona Saudi Arabia, Brunei, Eswatini, Morocco n.k. ambako neno la mfalme ni la mwisho.

Kama unasema hakuna Chifu aliyemtumikia Sultani utasemaje Sultani alitawala sehemu yote iliyokuja kujulikana kama Tanganyika? Ukweli ni kuwa Sultani wa Zanzibar hajawahi kutawala sehemu yote hiyo isipokuwa miji michache iliyokuwa katika pwani ya sehemu hiyo na michache iliyokuwa mwambao. Sehemu kubwa ya sehemu hiyo ilikuwa chini ya utawala wa viongozi wa kiafrika wa kiasili ambao kwa kiingereza waliitwa "chiefs" au machifu kwa kiswahili. Viongozi hao waliitwa majina mengine ( Mangi, Mtemi, Kabaka n.k.) kwa lugha za makabila yao.

Baadhi ya viongozi hao ndio walioingia mikataba ya maghumashi na Karl Peters. Karl Peters alifanya hivyo kwa sababu alitambua kuwa walikuwa viongozi huru na hawakuwajibika kwa huyo Sultani wako. Kuonyesha jinsi Sultani wako alivyokuwa hana nguvu, hakuhusishwa hata kwenye makubaliano ya Heligoland na Zanzibar! Najua hata hiyo Treaty hauijui.

Amandla...
Tatizo huuelewi Usultani wala Ufalme.

Na huelewi kuwa hakukuwepo hata neno "chifu" kwenye utawala sultani. Hata hao "machifu" wenyewe walikuwa hawalijuwi neno "chifu" mpaka alipokuja Muingereza.

Rudi kafanye homework kabla hujaja kulumbana na mimi..

Naona hoja ya neno "chifu" ilikukwida umekuja na kubwabwaja na kuhororoja mpaka povu. sasa mimi tu linakutoka povu, wewe ndiyo wa kumuelimisha Alama Mohamed Said kuhusu historia ya Tanganyika?

Usianzishe vichekesho.
 
Back
Top Bottom