Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Sheria 15 za mpira za kipindi cha utotoni;

1. Mkubwa hachezi na akicheza mnaingia wawili.

2.Mwenye mpira hatolewi hata akicheza vibaya.

3.Inaruhusiwa kubadili kipa kama penati imetokea na baada ya penati. anaruhusiwa kurudi wa mwanzo.

4.Yule mtaalam wa soka hakosi namba hata siku moja.

5. Dogo mnene lazima awe golikipa.

6.Mwenye mpira ataamua nani asicheze.

7.Penati itatokea tu pale mchezaji akiumia sana na kutoka damu.

8.Mechi itaisha kama kila mchezaji atakuwa amechoka.

9. Hakuna free kick, refa wala offside.

10. Ukichaguliwa mwishoni ujue uwezo wako mdogo kuliko wote uwanjani.

11.Mtaalam wa timu akipewa kazi na wazazi wake lazima mumsaidie ndo mwende kucheza.

12.Ukiumia kidonda kinawekwa mchanga.

13.Kipa anaruhusiwa kudaka popote.

14. Wale ambao wamekosa namba kazi yao ni kufata mipira ikitoka.

15. Mwenye mpira akikasirika mechi ndo inakuwa imeisha.
Daah wengine hatujapitia izi mambo kabisa.
 
bdeb12bb63300d046f76c667e0d0972c.jpg
hahaha enzi.
 
Habari za Muda huu wadauu Kwa wale Ambao
Tuliowahi kucheza cha Ndimu Uswahilini
Tukumbushane zle Sheria Zetu za Cha Ndimu

1.Mwenye Mpira lazma Acheze Hata kama hajui

2.Wale Ambao Waliokuwa Hawajui Kucheza kazi yao ilikuwa kuokota Mipiraa

3.Mabonge Ndo Makipa

4.Mwenye Mpira Akikasirika tu Basi Na Mpira umeishaa

5.Kuchimba ilikuwa kitu cha Kawaida Mnoo

6.Mpaka Mpira ukiisha Idadi Ya Magoli Inafikia hata 15

7.Kuna watu Hata Wakichelewa Lazma Namba wapate !

8.Magoli ya Miti Tena Mianz / Wavu NETI !

Tuongezee nyingineee Ambazo unazikumbukaaaa
 
SHERIA 11 ZA MPIRA WA UTOTONI
Kati ya hizi ulipenda ipi hasa,
1 Mwenye Mpira Lazima Acheze Hata Kama Hajui Kucheza

2 Dogo Mnene Lazima Awe Golikipa

3 Mwenye Mpira Ataamua Nani Acheze Na Nani Asicheze

4 Kama Hujashiriki Kufuma Mpira Inawezekana Usipate Namba

5 Idadi Ya Wachezaji Inategemeana Na Uwanja

6 Mwenye Mpira Akikasirika Apoapo Mpira Utamarizika

7 Inaruhusiwa Kubadilisha Golikipa Kama Ikitokea Penat Na Kisha Ataendelea Kukaa Yule Yule

8 Mechi Itaisha Pale Giza Linapoingia

9 Wale Ambao Wamekosa Namba Kazi Yao Kuokota Mpira Ukitoka

10 Hakuna Mapumziko Wala Offsaid

11 Huruhusiwi Kuvaa Viatu

Mwenye nyongeza karibu
 
Kama mwenye mpira kapewa kazi na mam yake wote mnamsaidia ili nae aende pamoja nanyi kwenye gemu
 
Mpira unarusha kwa mkono mmoja au unajirushia mwenyewe
 
Ukicheza rafu sana wanakuziria mechi mpaka uombe samahani kwamba utacheza rafu tena au utoke nje
 
Back
Top Bottom