ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
Wanataka vya Bure na Kodi hawalipi,iwe Ili vya Bure lipeni Kodi harafu Serikali itenge Bajeti za kuendeshea shule Ili zinunue hayo mahitaji.Huko wananchi wake wanafanya kazi na kulipa kodi, Tz hata kodi hawataki kulipa wanadai ni wanyonge
Mmmmh!! Laki nne ni vitu gani hivyo?Mkuu sio fagio tu,kumpeleka mtoto advance ili apokelewe vitu walivyoorodhesha at least uwe na laki nne ndio pesa ya chini kabisa
Kwani walimu wamejipangia au ni kwa mjibu wa mahitaji ya watoto watakao kuwepo shule?Walimu wavae majoho ya wazazi. Watoto wao je
Mafagio ya Nini wakati hizi.shule nyingine hazina upuuzi huo zinafaulisha vizuri.Elimu ya TZ ni rahisi sana, yani unaambiwa fagio tu nalo hutaki kupeleka unalalamika.Tuache ujinga
Hiyo ya kumletea mtoto chuki upo sahihi kabisa. Kuna jamaa yangu mwanae alimueleza jinsi asivyo na amani Shuleni kwa madai kuwa kuna mwalimu anamchukia tu yeye bila sababu na amekuwa anaona kama vile ni yeye tu anayenyanyasika darasani kwao.Pole Sana, wahusika wapo humu, hope suala lako litashughulikiwa, sema umekosea kutaja mkoa uliotoka coz ni rahisi kwa walimu kumtambua mwanao. Na kuanza kumletea chuki.
Mafagio ya Nini?Sasa watakaa sehemu chafu?Mafagio ya Nini wakati hizi.shule nyingine hazina upuuzi huo zinafaulisha vizuri.
Kwa tuliosoma high za government tunajua upuuzi wao, wanajazana vitu vidogo dogo lakini unakuta walimu hamna wa.kutosha.Mafagio ya Nini?Sasa watakaa sehemu chafu?
Sawa,Sasa Hilo la ukosefu wa walimu na mafagio linaingilianaje ?Kwa tuliosoma high za government tunajua upuuzi wao, wanajazana vitu vidogo dogo lakini unakuta walimu hamna wa.kutosha.
Kuna mwanafunzi katoka Na kasoma Songea O level, kapangwa Kagera Advance.Kwanza imekuaje Mwanao Kapangwa Dodoma na ametoka Mtwara?
Nijuavyo kuanzia mwaka huu, ili kuepuka usumbufu serikali inampanga mwanafunzi kwenye kanda aliyosomea O-level na hilo limefanyika kweli...
Kuna kanda Ya ziwa, Kanda ya kati, kusini, kaskazini Pwani n.k,
Labda uniambie mwanao Kasomea Maeneo ya karibu ila Kwa sasa ndio mmetokea mtwara..
Kwa tuliopitia manyanyaso mashuleni, tunasema "ahsante kwa kutoka salama" vinginevyo unakimbia shule na hugeuki nyuma wala hurudi tenaaa.Hiyo ya kumletea mtoto chuki upo sahihi kabisa. Kuna jamaa yangu mwanae alimueleza jinsi asivyo na amani Shuleni kwa madai kuwa kuna mwalimu anamchukia tu yeye bila sababu na amekuwa anaona kama vile ni yeye tu anayenyanyasika darasani kwao.
Mwanzo mzazi huyo alipuuza na hakumzingatia sana huyo mwanae. Lakini bado mtoto alionyesha kulalamika kila mara. Sasa jamaa siku moja alikwenda shuleni hapo kupeleka risit za ada na kwa kuwa alishaambiwa jina la huyo mwalimu akadadisi akamuona. Alipomuona ndipo akili ikachanganya kidogo kwavile muonekano wa huyo mwalimu ni kijana sana halafu kama mjanjamjanja hivi na jamaa mtoto wake ni wa kike mwili mkubwa.
Sasa jamaa kwa kukurupa akamuona mkuu wa Shule akamtaarifu kuwa mwanae analalamika kunyanyaswa na mwalimu fulani. Mkuu wa Shule akamuahidi kulifanyia kazi, kimsingi alionyesha kulipokea hasa. Baada ya hapo mtoto akawa anamuambia baba yake kuwa sasahivi ana amani sana na yule mwalimu alijirekebisha kabisa.
Sasa baada ya binti kumaliza la saba ndipo akamuambia baba yake kuwa alijutia sana kitendo cha kumueleza maana kilichoendelea kwake pale Shuleni ni Mungu tu ndie anajua maana ni walimu wote walionyesha kumchukia sana hadi mkuu mwenyewe wa shule na walimu wakawa wanamsimanga indirect kwa wenzao . Binti anasema ni heri ilitokea wakati yupo la saba kwani ingetokea akiwa la 5-6 angekimbia hiyo shule bila kuaga.
Hiyo Shule inaitwa Green Belt ipo Mbezi.
Kimsingi kuna yanayoendelea mashuleni huko ambayo sio mazuri. Taaluma ya ualimu mbali na kuhitaji watu wenye elimu nzuri lakini pia inahitaji walimu wenye Utu/ubinaadam , upendo na maadili.
LipaHabari Watanzania,
Nawasalimu kwa jina la muungano..
Nina kero yangu haswa kwa shule za advance wanaopokea kidato cha tano Walimu wakuu wanachukua maamuzi ya kukataa kumpokea Mtoto ikiwa tu hajamaliza michango na vifaa vingine kama vile vya usafi ukiangalia umbali uliotoka na Mtoto ni mbali sana.
Mfano mimi mwanangu kapangiwa Kibaigwa Girls iliyopo Dodoma, Mwalimu mkuu na makamo Mkuu wa shule wamenigomea kumpokea Mtoto kisa nimelipia nusu ya pesa za michango na sijakamilisha vifaa vya usafi ukizingatia nimetokea mkoa wa Mtwara
Sijui cha kufanya, naomba waziri husika kufuatilia hili jambo, wazazi tunashindwa kuwapeleka shule mapema watoto kutokana na hizi changamoti.
Naomba kuwasilisha
🤝
Mtwara wameuza ufuta bei nzuri tu na Kwa sasa wanauza mbaazi kilo Moja tsh 2000Heb share hivo vitu vinavyofika laki nne,
Wote tumesoma siku hizi, wew peleka michango mtoto apokelewe, kwa hio unataka vyoo vya mtoto wako visafishwe kwa fagio ya nani?
Halafu akumbuke elimu ya advance ni chini ya miaka 2,ukimdisturb mtoto kidogo tu akatoks ktk reli kurecover huchukua muda sana,inataka utulivu wa akili,hivyo unavyofanya harakati walimu wakimmaki kuwa babaake alileta harakati unaweza kumfanya mtoto asiwe comfortable shuleni,wazazi vumilieni hakuna elimu ya bure kabisa na vifaa vingi unavoambiwa ununie ni kwa matumizi ya mtoto wako, kaongee vzr na mwlm wake uone mtamsaidiaje siyo kuleta harakati!!Jaman elimu bure ni ada tu !! Ila mahitaji ya mtoto ni wewe mwenyewe mzazi na CCM walivyo wajanja wakasema elimu bure , wazazi msibweteke kusomesha bado ni gharama aseee
Angalau kama una mtoto anaenda kidato cha tano andaa 500k umekosa sana 350k iwepo na kama huna hela weka mambo ya msingi mbele kwanza.
Mfano sare za shule (mashati) atumie alizomalizia kidato cha nne , suruali au sketi apate moja na ya kushindia !! Viatu Pair moja anaweza kuanzia !! Shoe polish ndogo counter book sio lazima aende na Quire 4 aende na ndogo ! Bananeni hivyo hivyo dogo akasome ! Huku akiondoka na wewe unacheki mazingira jinsi ya kumwinua !
Mnavyolalamika hivi dogo akienda ndo imeisha hiyo mtoto anaishi kwa tabu vibaya mno ! Hatukatai kukosa kupo ila ukishapata mtoto na mradi ulimtafuta ukiwa kwenye furaha zako huo ni wajibu sio hiyari tena!
-mzazi mtarajiwa [emoji23]