Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Habari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania, kwa kweli sijawahi kuona nchi yenye amani na usalama wa hali ya juu kama Zambia.

Kwa wale wenzangu waliowahi kuikanyaga nchi hii bila shaka wataleta ushuhuda wa hiki ninachoongea. Zambia ndio nchi ambayo unaweza kununua kitu njiani huku basi linakwenda, cha ajabu kama ulitangulia kumpa muuzaji hela kubwa, basi muuzaj atalikimbilia hilo basi hadi ahakikishe amekurudishia chenji yako, kitu ambacho kwa nchi nyingi including Tanzania hakipo. Yani ukinunua kitu ukatangulia kutoa hela na basi likaanza kwenda, basi uhesabu ushapigwa, maana muuzaji hatokupa chenji yako, badala yake atakimbia zake akijua hauna uwezo wa kutoka ndani ya basi linalotembea ili umkimbize yeye.

Hiyo tisa, kumi ni pale unapofika Lusaka katika ile stand yao kuu inayoitwa Kaunda bus terminal. Aisee pale utakuta wale jamaa wanaochenji hela wakiwa na maburungutu ya dola za mia mia, hamsini hamsini nk wameziweka mezani kwa ajili ya kuwachenjia wasafiri mbali mbali wanaoshukia pale kutoka nchi mbali mbali. Lile soko liko wazi masaa 24, na hakuna anaeingia kuwasumbua au kuwaibia wale wanao anika madola yao hadharani kwa ajili ya chenji. Kwa Tanzania ukiwa na sh laki 1 ukienda kariakoo kununua kitu, basi muda wa kulipa inabidi usogee kona kidogo ndo uchomoe hela, tena kimagutu magutu unaangalia huku na kule ili usije fatwa na vibaka. Kwa Zambia hiyo haipo.

Kuna siku nilishuka pale na mzigo wa maana, kwa vile nina mjomba wangu anaishi pale ikabidi na mimi nichukue hata wiki moja ili niuze mzigo wangu mdogo mdogo. Aisee nilishangaa kuona jamaa amekuja na zaidi ya dola 2500 tena kaziweka mfukoni tu, hana wasi wasi wowote mpaka pale town lilipo duka la mjomba wangu, akanipa changu na mimi nikamkabidhi mizigo yake akaita gari akapakia akaondoka.

Mimi mcheche ukanishika nikifikiri labda kuna watu wametuona kwahiyo wanaweza kuja kutupora yale madola aliyoniachia jamaa, mjomba wangu akacheka na kuniambia kuwa hapa watu huwa wanatembea mpaka na dola elf 7 town, itakuwa mimi wa dola elf 2 bwana.

Ki ukweli style ya maisha ya pale niliipenda sana haswa kwa upande wa usalama, sema ndo hivyo sehemu ambayo haukuanzia maisha ukisema uende kuanza tena itachukua muda kutoka.

Hizi nchi zetu zingine usalama ni zero, mpaka inafika kipindi wengi wetu tunakuwa tunatembea na kadi za bank tu mifukoni, ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kutokea wakati wowote. Mpaka sasa sijajua ni mbinu gani wanayotumia hawa jamaa kudhibiti wizi na ujambazi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Lusaka na Zambia yote kwa ujumla.
Hiyo Nchi ina watu wachache sana kulinganisha na ukubwa wa Nchi yao na uwezo wa serikali yao kuwahudumia ni mkubwa so lazima wawe na kaunafuu la maisha kiasi fulani..

Shule zao za msingi ,walimu Wanamiliki magari kitambo sana wakati huku kwetu wameanza kujikongoja miaka hii ya Leo..

Zambia watu mil.16 ,Tzn mol.60
 
Mimi nimeishia hapo kwa mjomba Mbagala kibonde maji.

Tuweke mzani sawa, umetembea nchi ngapi kaka kiasi useme zambia ndio nchi yenye amani na usalama zaidi? (uliyoandika humo nimesadiki ila ningependa kujua nchi ulizotembelea ila niweze kufanya tathmini)
Nimeshatembea nchi zaidi ya 5, ila kati ya hizo nchi nimeona Zambia ndio nchi yenye amani na usalama zaidi kwa sababu
1) Zambia ndio nchi pekee ukiingia town iwe sokoni, kwenye mall au stand ya mabasi utakutana na watu wanaochenji pesa tena wengi wao ni wageni kutona Nigeria, Congo nk. Wachenji hela hawa utawakuta wamekaa mstari mfano wa wauza samaki pale feri. Kila mtu utakuta kaweka maburungutu ya usd (yani dola za kimarekani) mia mia, hamsini hamsini na ishirini ishiri.
Kifupi kwa hesabu ya haraka haraka kila meza moja au mfuko wa mchenji hela mmoja huwa haukosi dola elfu 3, elfu 5 na kuendelea. Sasa fikiria kama ukipiga vamizi la meza 10 utaondoka na dola elf ngapi? Na ukizichenj kwa hela ya Tanzania utapata bei gani. Pia watu wanauza vitu vyao nje nje tena vya thamani kubwa, ila hakuna anaelalamika kuvamiwa wala kuibiwa. Zambia nimeshakaa takriban miezi 3 na pia huwa napita nikirudi Tanzania kutokea South. So nina uhakika na ninachokisema.
Nafikiri umesoma na michango ya watu wengine humu na kushuhudia mwenyew jinsi watu waliofanikiwa kupita, au kuishi nchi ile wanavyokubaliana na kile nilichoandika.
 
Kwa nnachoamini kila nchi ina kitu chakr ambacho imebalikiwa, wao yawezekan wamebarikiwa ilo lakin in other hand yawezekan huo ushuhuda wako hauna uhakika 100% kwasababu hujaweka wazi ni kwa muda gani umekaa uko kwajil ya utafiti huo na malengo ya utafiti wako yalikuwa ni yapi na je majibu uliyoyapata tunaweza kuyathibitisha vipi katika muktadha wa tafiti. Lakin kwa Tanzania niseme tu wazi hali ya usalama imeimarika sana kwa siku za hivi karibuni matukio kam uliyoyatolea mfano hapo kariakoo kuna baadhi ya maeneo matukio hayo hayapo kabisa.

Kwaiyo huwezi kutumia eneo mmoja kujustify kwamba Tanzania hakuna usalama ndugu yangu. Labda ungesema hali ya usalama nchini bado inakumbwa na changamoto ivyo mamlaka ziongeze nguvu ili kuhakikisha usalama unakuwepo kwa 100%.
Mkuu soma post namb #144 utapata majibu yako. Watanzania hatuwafikii hata robo ya uaminifu na usalama hawa jamaa. Labda tatizo lao, au ulemavu wao mkubwa ni pombe tu. Hawa jamaa wanakunywa pombe zaidi ya nchi zote zilizounda umoja wa nchi za East Africa.
 
Kingine kinacho fanya waheshimu hela ya mtu ni hofu ya kulogwa. Kama ujuavyo Zambia ni road kuu ya kupitisha mizigo na biashara kwenda KONGO.
Huko nyuma wakongo wengi walikuwa wanatapeliwa sana pesa na mizigo yao wakaamua kutoa fundisho kwa kuloga.
😂😂🤣🤣🤣
 
Hiyo Nchi ina watu wachache sana kulinganisha na ukubwa wa Nchi yao na uwezo wa serikali yao kuwahudumia ni mkubwa so lazima wawe na kaunafuu la maisha kiasi fulani..

Shule zao za msingi ,walimu Wanamiliki magari kitambo sana wakati huku kwetu wameanza kujikongoja miaka hii ya Leo..

Zambia watu mil.16 ,Tzn mol.60
Watu mil 16 nchi nzima?
Kulikuwa na ulazima kutolea mfano walimu😂
 
Kwa haraka haraka kuwa pale siku 5 niligundua hivi:, chakula anachukula mvuta Guta wa Zambia mwalimu wa Tanzania hawezi kukila mfulilizo kwa wiki nzima unless akubaliane kusave laki ama elfu 80 kwa mwezi.
2) wanawake wa Zambia uwatenganishi na vazi la kanga/kitenge.
Wanapenda sana kujifunga kanga na vitenge no matter kavaaje utamkuta kajifunga kitenge/kanga.
Ya ulichosema kina ukweli mkubwa. Kingine hawa jamaa wanapiga sana mkojo wa mjusi, yani katika nchi zinazoongoza kwa ulevi barani Afrika Zambia haikosi kwenye tatu bora.
 
Hilo wengi hawalijui kwa sababu ya kukua kwenye mazingira magumu ya dhulma na uongo

Ukiwa muongo lazima utakuwa tapeli tu huwa vinaendana sana

Ila ukiwa muaminifu utaendelea haraka kwani utapata madili hata kama sio moja ya biashara zako

Unauza duka mtu anakuletea Dili la kumuuzia kiwanja kisa uaminifu tu
Dah ndugu unayoongea yana ukweli mtupu. Bila uaminifu lazima maisha yaje yakupige chenga, maana hata ukibahatika kupata matumizi yako yatakuwa ya hovyo hovyo kama akili yako. Ila ukiwa mwaminifu basi na maisha yatakuwa mazuri kwa kuridhika na kile kidogo au kikubwa unachokipata.
 
Hujakosea kabisa kuhusu Zambia
Hata askari polisi wao si washenzi kama wa kwetu. Askari ni waadilifu, wanatumia akili.
Hali ya hewa pia ni nzuri. Ni nchi fulani naipenda sana, ukiongeza na Namibia, Seychelles, Botswana na Cape Verde.
Ya hizo nchi ulizozitaja pia usalama ni mzuri ukilinganisha na nchi zetu za East Africa zilizojaa vibaka.
 
Hiyo Nchi ina watu wachache sana kulinganisha na ukubwa wa Nchi yao na uwezo wa serikali yao kuwahudumia ni mkubwa so lazima wawe na kaunafuu la maisha kiasi fulani..

Shule zao za msingi ,walimu Wanamiliki magari kitambo sana wakati huku kwetu wameanza kujikongoja miaka hii ya Leo..

Zambia watu mil.16 ,Tzn mol.60
Mkuu mi nafikiri uaminifu wao hausianiani na idadi ya watu wala swala la kuhudumiwa na serikali. Kama ingekuwa kuhudumiwa na serikali ndio mwarobaini wa uaminifu basi Kaburu ingeongoza kwa hilo, maana wao wanapewa huduma za bure, lkn swala la uaminifu kwao ni zero.
 
Inamaana huko hakuna wezi kabisa au Sheria zao ni Kali kwanini kuwe na utulivu hivo na ikiwa watu ni wengi pia?
Wezi wanaweza kuwa wapo, lkn ni wachache mno ukilinganisha na wale ambao sio wezi. Yani ni kama
a) wezi 5%.
b) wasiokuwa wezi 95%.
Nafikiria na sheria zao zimechangia pia kuleta uaminifu ndan ya nchi hizi.
 
Mkuu mi nafikiri uaminifu wao hausianiani na idadi ya watu wala swala la kuhudumiwa na serikali. Kama ingekuwa kuhudumiwa na serikali ndio mwarobaini wa uaminifu basi Kaburu ingeongoza kwa hilo, maana wao wanapewa huduma za bure, lkn swala la uaminifu kwao ni zero.
Sijaweka idadi ya watu kwamba ndio kigezo cha uaminifu bali kuonyesha kwamba wako wachache hivyo serikali ina nafasi kubwa ya kuwahudumia ikilinganishwa ndio matajiri wa kopa Dunia nzima hapo sijataja mali zingine.
 
Back
Top Bottom