Siku ambayo askari MP alipojitayarisha kumpiga risasi askari Sajenti kwa amri ya Mkuu wa Kambi ya Mgambo JKT

Siku ambayo askari MP alipojitayarisha kumpiga risasi askari Sajenti kwa amri ya Mkuu wa Kambi ya Mgambo JKT

Wakati mwingine sheria za kijeshi zinahitaji reforms.....nchi nyingine kama ujerumani askari anahaki ya kutotii amri ya kamanda wake kama amejiridhisha kuwa amri hiyo ikitekelezwa itakiuka haki za kibinaadamu..
Kuna kipengele Cha kutii AMRI HALALI ndo hicho unakisema

Maana amri isiyo halali mwisho lazima italeta shida tu either kwa raia au hata mtu yule ambae sheria inatekekezwa kwake

Kwahiyo bado mulemule tu Kama hao ujerumani


Ukitekeleza amri ISIYO HALALI utawajika wewe mtekekezaji maana utetezi wa kwamba nilipewa amri hawezi kukutoa kwenye hatia
 
Wakati mwingine sheria za kijeshi zinahitaji reforms.....nchi nyingine kama ujerumani askari anahaki ya kutotii amri ya kamanda wake kama amejiridhisha kuwa amri hiyo ikitekelezwa itakiuka haki za kibinaadamu..
Hawataki yajirudie ya World War Two na Final Solution, kama hii sheria ingekuwepo before, holocaust isingetokea
 
Kama nia yako ni Kuzungumzia Suala zima la Ole Sabaya na Utetezi wake wa Kutumwa katika Oparesheni za Kikatili na Kiuhalifu na Hayati Rais Dkt. Magufuli, Makamu wa Rais ( sasa ) Dkt. Mpango na BOT Governor Wala hukuwa na haja ya Kufumba na Kuzunguka sana hivi.
Sio kila kitu kinakuwa juu ya Sabaya. Na kama uko interested na Sabaya nilishajieleza kwa muungwana mmoja hapo juu. Jitahidi kusoma.

Unajua Mkuu, tukiwa jeshini, tulikuwa tukiambiwa askari anapaswa kutii amri wakati wote, ili mradi iwe wazi ni amri halali.

Kwa hiyo Sabaya alijua wazi alikuwa anapewa amri isiyo halali, hivyo hakupaswa kutii. Lakini hata hivyo, inawezekana kabisa amri halali ya Magufuli ilikuwa ni Sabaya kwenda kuwakamata wale watu. Lakini unadhani aliambiwa utakapoenda kuwakamata uwapige na kuwaumiza? Hata hivyo bado kuna maswali kama, kwa nini Magufuli akamtumia Sabaya na sio vyombo halali vya usalama kama TISS na Polisi? Ni wazi basi Magufuli na Sabaya walijua wazi walikuwa wanafanya uhalifu.

Sasa Sabaya akijua alikuwa anatekeleza amri ya kihalifu, utetezi wake haupaswi kuwa alitumwa, kwa sababu anajua hupaswi kutii amri isiyo halali. Ukiwa mhasibu huwezi kujitetea niliiba fedha za kampuni kwa kuwa meneja wangu aliniambia niibe. Utetezezi wa Sabaya unapaswa kujikita kwamba alifanya vile kwa kuwa kwa alivyomjua Magufuli, asingetekeleza maisha yake yangekuwa hatarini.

Na labda Sabaya awe na ushahidi kwamba fulani aliamriwa kutekeleza jambo la kihalifu na Magufuli na alipokataa aliuwawa katika mazingira tatanishi. Na pia anaweza kuweka ushahidi ambao unamwonyesh kuwa Magufuli alikuwa anaua watu waliompinga. Hapo ndipo anaweza kujiokoa na hii kesi.
 
Luteni ndo cheo gani hicho? We utakua huna tofauti na mtu anayesema nna degree ya Bachelor.

Sent from my ALE-L21 using JamiiForums mobile app
Tanzania kuna watu wajinga lakini hamjui kama ni wajinga, kwa hiyo mnaishia kuwa wabishi na kuongea ujinga.

Sasa wewe unanikandia mimi eti Luteni ndio cheo gani, na unanipa mfano wa mtu kusema degree ya bachelor, sasa huo si wendawazimu? Acha kuropoka pale unapokuwa mjinga wa jambo, unajiabisha mbele za watu. Mie nimepitia jeshini ndio maana nikaweka hii thread. Wewe umewahi kwenda hata jeshi la mgambo? Watu kama wewe ndio mlimuudhi Mwakyembe akaishia kusema wewe darasa la saba unabishana na mimi wa digrii nne!

Kwa taarifa yako basi, kukusaidia kuondoa ujinga wako, Tanzania Luteni (Lieutenant) ni cheo jeshini cha mtu mwenye nyota mbili.

Na neno Luiteni linakuja kutumika tena kwa kanali, ambapo kuna Luteni Kanali kabla hujawa Kanali kamili.. Na pia kuna Luteni Generali kabla hujawa Generali kamili

Iko hivi;

Kuruta
Private
Koplo
Sajenti
Sameja
Sekandi Luteni
Luteni
Kepteni
Meja
Luteni Kanali
Kanali
Brigedia
Meja jenerali
Luteni jenerali
Jenerali
 
Tanzania kuna watu wajinga lakini hamjui kama ni wajinga, kwa hiyo mnaishia kuwa wabishi na kuongea ujinga.

Sasa wewe unanikandia mimi eti Luteni ndio cheo gani, na unanipa mfano wa mtu kusema degree ya bachelor, sasa huo si wendawazimu? Acha kuropoka pale unapokuwa mjinga wa jambo, unajiabisha mbele za watu. Mie nimepitia jeshini ndio maana nikaweka hii thread. Wewe umewahi kwenda hata jeshi la mgambo? Watu kama wewe ndio mlimuudhi Mwakyembe akaishia kusema wewe darasa la saba unabishana na mimi wa digrii nne!

Kwa taarifa yako basi, kukusaidia kuondoa ujinga wako, Tanzania Luteni (Lieutenant) ni cheo jeshini cha mtu mwenye nyota mbili.

Na neno Luiteni linakuja kutumika tena kwa kanali, ambapo kuna Luteni Kanali kabla hujawa Kanali kamili.. Na pia kuna Luteni Generali kabla hujawa Generali kamili

Iko hivi;

Kuruta
Private
Koplo
Sajenti
Sameja
Sekandi Luteni
Luteni
Kepteni
Meja
Luteni Kanali
Kanali
Brigedia
Meja jenerali
Luteni jenerali
Jenerali
We jamaa huna akili na huko jeshini sijui ulienda kufanya nini? hivi mtu anaweza kukuuliza mwanao anasoma la ngapi ukamwambia yuko "form" ilihali kuna form one mpk six.
Sa huo mfano ndo sawa na ujinga wako.
Jeshini kuna
2nd lieutenant
1st lieutenant
Lieutenant colonel
Lieutenant general.
Sa we unaposema lieutenant unamaanisha cheo gani kati ya hivyo?
Afu unajiona mwanajeshi wakati hujui hata ranks.


Sent from my ALE-L21 using JamiiForums mobile app
 
We jamaa huna akili na huko jeshini sijui ulienda kufanya nini? hivi mtu anaweza kukuuliza mwanao anasoma la ngapi ukamwambia yuko "form" ilihali kuna form one mpk six.
Sa huo mfano ndo sawa na ujinga wako.
Jeshini kuna
2nd lieutenant
1st lieutenant
Lieutenant colonel
Lieutenant general.
Sa we unaposema lieutenant unamaanisha cheo gani kati ya hivyo?
Afu unajiona mwanajeshi wakati hujui hata ranks.


Sent from my ALE-L21 using JamiiForums mobile app
Hivi akili yako ina nini?

Nimekuambia Lieutenant jeshini ni cheo cha nyota mbili, lakinini pia neno lieutenant linatumika kama prefix kwa kanali na jenerali.

Umewahi kuona mtu amevaa cheo chenye alama ya nyota mbili na ngao? Unamwitaje?

Na mtu mwenye nyota mbili, unamwitaje?

Usijifanye kujua wakati hujui
 
Tanzania kuna watu wajinga lakini hamjui kama ni wajinga, kwa hiyo mnaishia kuwa wabishi na kuongea ujinga.

Sasa wewe unanikandia mimi eti Luteni ndio cheo gani, na unanipa mfano wa mtu kusema degree ya bachelor, sasa huo si wendawazimu? Acha kuropoka pale unapokuwa mjinga wa jambo, unajiabisha mbele za watu. Mie nimepitia jeshini ndio maana nikaweka hii thread. Wewe umewahi kwenda hata jeshi la mgambo? Watu kama wewe ndio mlimuudhi Mwakyembe akaishia kusema wewe darasa la saba unabishana na mimi wa digrii nne!

Kwa taarifa yako basi, kukusaidia kuondoa ujinga wako, Tanzania Luteni (Lieutenant) ni cheo jeshini cha mtu mwenye nyota mbili.

Na neno Luiteni linakuja kutumika tena kwa kanali, ambapo kuna Luteni Kanali kabla hujawa Kanali kamili.. Na pia kuna Luteni Generali kabla hujawa Generali kamili

Iko hivi;

Kuruta
Private
Koplo
Sajenti
Sameja
Sekandi Luteni
Luteni
Kepteni
Meja
Luteni Kanali
Kanali
Brigedia
Meja jenerali
Luteni jenerali
Jenerali
Naomba elimu kidogo tofauti ya KURUTA na PRIVATE

Tafadhali
 
Hivi akili yako ina nini?

Nimekuambia Lieutenant jeshini ni cheo cha nyota mbili, lakinini pia neno lieutenant linatumika kama prefix kwa kanali na jenerali.

Umewahi kuona mtu amevaa cheo chenye alama ya nyota mbili na ngao? Unamwitaje?

Na mtu mwenye nyota mbili, unamwitaje?

Usijifanye kujua wakati hujui
We unachokiongea hukijui mtu mwenye nyota mbili ni first lieutenant na sio lieutenant kama unavyosema

Sent from my ALE-L21 using JamiiForums mobile app
 
Naomba elimu kidogo tofauti ya KURUTA na PRIVATE

Tafadhali
Unapoingia jeshini bado una maji magotini hujui hata kupiga mguu upande, wewe ni kuruta. Kwa JKT hupewi hata kombati, unavaa bukta na vesti.

Unapokuwa umamaliza mafunzo yote ya msingi ya jeshi lakini wewe ni askari bila cheo chochote, wewe ni private. Ukiona polisi au mwanajeshi hana kitu chochote begani, huyo ni private
 
We unachokiongea hukijui mtu mwenye nyota mbili ni first lieutenant na sio lieutenant kama unavyosema

Sent from my ALE-L21 using JamiiForums mobile app
Ahaa, kwa hiyo Lieutentant sio cheo kwa kuwa kuna first na second?

Sasa huo sio utaratibu wa JWTZ. Sisi nyota mbili tunaita Luteni, kama unatuletea mambo ya USA nenda USA kaongelee puani tuondolee shombo za kina Trump hapa.
 
Ahaa, kwa hiyo Lieutentant sio cheo kwa kuwa kuna first na second?

Sasa huo sio utaratibu wa JWTZ. Sisi nyota mbili tunaita Luteni, kama unatuletea mambo ya USA nenda USA kaongelee puani tuondolee shombo za kina Trump hapa.
We jamaa ni mbishi we unaongelea kimazoea au ki uhalisia?


Sent from my ALE-L21 using JamiiForums mobile app
 
We jamaa ni mbishi we unaongelea kimazoea au ki uhalisia?


Sent from my ALE-L21 using JamiiForums mobile app
Angalia hapa uniambie nani mbishi

1629103646034.png
 
Unapoingia jeshini bado una maji magotini hujui hata kupiga mguu upande, wewe ni kuruta. Kwa JKT hupewi hata kombati, unavaa bukta na vesti.

Unapokuwa umamaliza mafunzo yote ya msingi ya jeshi lakini wewe ni askari bila cheo chochote, wewe ni private. Ukiona polisi au mwanajeshi hana kitu chochote begani, huyo ni private
Anhaaa hapo sasa nimeeelewa
 
Ni jambo ambalo sintalisahau maishani mwangu, japo lilitokea zaidi ya miaka 20 iliyopita. Leo nimeamua kulisimulia kwa kuwa nadhani kwa sasa limefikia hatua ya kuwa "declassified" hata kama lilikuwa ni siri, ila sintataja majina ya wahusika.

Ilikua usiku mmoja katika kambi ya JKT Mgambo, katika sehemu moja ya starehe watu walikuwa wakinywa na kuburudika kwa vinywaji mbalimbali pamoja na bia, wakihudumiwa na wasichana warembo service girls. Katika sehemu hii, alikuwapo pia Mkuu wa Kambi, ama CO kama tulivyowaita mara nyingi.

Sasa tunajua kwamba pombe sio chai, na baada ya bia mbili au tatu watu hubadilika katika kufikiri kwao na hata kutenda. Katika harakati za kuhudumia watu, service girl moja alipokuwa akipita katikati ya meza za wateja wake, aliangusha chupa ya bia ya askari Luteni ikapasuka na bia kumwagika. Luteni (nimekumbushwa kwamba alikuwa Luteni mmoja bongebonge sio Sajenti na mtu aliekuwapo Mgambo) huyu alikuja juu kama vile amepoteza maji yake ya uzima! Alianza kumfokea yule service girl kwa uzembe kwa sauti ya juu.

Sasa Mkuu wa Kikosi alipoona hivyo alitoa amri kwa Luteni, "kamanda acha kelele! Service girl, mpe bia nyingine kamanda kufidia iliyovunjika"

Basi yule service girl alienda kumletea Luteni bia nyingine. Sasa jambo la ajabu ni kwamba yule Luteni alipoletewa bia kufidia iliyovunjia, bado akaendelea kumbwatukia yule service girl. Kitendo hiki kikamuudhi sana Mkuu wa Kikosi, akasema kwa hasira, "Kamanda, umerudishiwa bia yako na bado unapiga kelele, haya inuka nenda mahabusu sasa hivi"

Kwa ujasiri wa ajabu yule Luteni hakuinuka. Mkuu wa Kikosi akarudia tena, "Kamanda nakuamuru jipeleke mwenyewe mahabusu". Yule Luteni aliendelea kukaa pale kwenye kiti huku akigumia kwamba huo ulikuwa uonevu, kwa sababu bia yake ilivunjwa kwa uzembe.

Sasa Mkuu wa kikosi alikuwa na dereva wake MP nje ambaye alikuwa na SMG. Aliitwa ndani na Mkuu wa Kikosi akaambiwa "askari, koki silaha, mlenge sajenti". SMG ilitoa mlio wa vyuma kugongana wakati ikikokiwa, sauti ambayo wale wanaozijua bunduki watakuwa wanaifahamu vizuri. Ni mlio wa pekee sana.

Kisha Mkuu wa Kikosi akasema, "Kamanda, nakuamuru kwa mara ya mwisho inuka jipeleke mwenyewe mahabusu"

Watu wote pale ukumbini wakawa kimya, ungeweza hata kusikia kishindo cha sisimizi wakitembea!

Yule Luteni aligeuka akaona SMG imeelekezwa kwake, na akajiinua taratibu na kuanza kuondoka kwenda mahabusu huku akisema kwa chini chini hii sio sawa.

Baada ya Luteni kuondoka, kulikuwa bado na kimya cha kama sekunde 30 hivi, na Mkuu wa Kikosi akasema "tuendelee kuburudika na kufurahi"

Lilikuwa na gumzo lililotawala kikosini kwa muda mrefu, watu wakijiuliza hivi Luteni angekataa kuinuka Mkuu wa Kikosi angemwambia dereva mpige risasi? Dereva angetii? Mimi niliamini kwa dhati kwamba Mkuu wa Kikosi angetoa amri Luteni apigwe risasi na dereva angetii, kwa sababu tu ya Mkuu wa Kikosi kulinda heshima yake.

Lakini jambo moja lilikuwa wazi kwangu, kwamba wote Luteni na Mkuu wa kikosi walifikia hatua ile kutokana na kwamba walikuwa wamekunywa bia. Na kwa mara nyingine niliona wazi kwamba kweli pombe sio chai!
Nimekusoma in reference to Naneya aka Tisaya aka Panki one at Kisongo over!

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Ya kwako imeandikwa na mmarekani, sisi tunaita luteni usu, sio luteni wa pili na wa kwanza
We uache ubishi we sema tu kwamba kimazoea luteni wa kwanza mnamuita "luteni" bas tutakuelewa ila ki rasmi anaitwa luteni wa kwanza na kiukweli jeshini hakuna cheo kinachoitwa luteni bila kufuatiwa na neno lingine.

Sent from my ALE-L21 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom