Siku ya Wanawake Duniani; Nini kifanyike katika kulinda mahusiano?

Ni kweli mkuu asilimia kubwa siye ndo chanzo
 
Wanaume kama ilivyo Kwa wanawake, hatupendi stress za rejareja. Hatupendi makelele ( hapa namaanisha mjifunze kyfikisha malalamuko, mapendekekezo au kukosoa Kwa staha). Mwanaume anaeweza kutulia na mtu yeyote anaempa utulivu, hata kama Hana kingine Cha ziada, ili tu anaonyesha kumheshimu na kumkosoa Kwa staha.

Pia kutuelewa kwamba tunavurugwa na mambo mengi kama ilivyo kwenu pia. Inahitaji kumwelewa mtu wako wakati Gani umwambie jambo Gani akakusikiliza.

Ya mwisho, hauwezi kumchunga binadam. Onyesha kumwamini na yeye ajue unamwamini hata kama unaona viashiria na chembechembe za ugaidi ( kuchepuka). Tulizana ukikusanya ushahudi wako huku ukitumia diplomasia kuigiza uko sawa. Kutufuatilia sana na wasiwasi uliopitiliza hua inafanya mpoteze point kirahisi sana. Kuna wakati jambo halihusiani kabisa na mambo ya mahusiano mtu anataka akufuatilie Kila kitu na kuongea Kwa kujiamini huku akiwa Hana uhakika. Kwa ufupi wanaume hatupendi kelele.

Niwatakie maadhimisho mema Mama zetu, Dada zetu, Binti zetu, malkia wake zetu, na wanawake wote Kwa ujumla.
 
Amina,tuache kelele
 
Maana kiukweli dunia hii imeshatawaliwa na pesa ,yaan utu wa binadamu umezongwa na kitu pesa.Mwanaume hataki kuhudumia ila anataka kisafi
Hii haina jibu moja kwa kila mtu,au kwa kila aina ya matatizo,ni kujadiliana nyie wana ndoa,au mlio kwenye uhusiano
 
Ndio, wanawake huwa hampendi kuona mwanamke mwenzako kakuzidi (mna wivu)

Sasa hiyo ndio silaha wanaume tunaitumia mkileta ngendembwe...
Ha ha haa
 
Wa manzense kweli
Na huo ndio ukweli wakikuletea pointi sijui za heshima sijui utulivu ,tulizo hivi vyote utakuta mwamba anapata kwa mke wake bado anatoka nje so hizo point ni za ku justify matendo yao ila real reason ndio hio

We unadhani king Solomon kwenye Bible alikuwa hapati heshima ,kutiiwa [emoji3]
 
Ni ngumu sawa kumuhudumia mwanamke ambaye humuamini unahisi kama ana kucheat ili kupunguza maumivu bora usimuhudumie kabisa

Demu akiwa loyal tunahudumia tu hamna tatizo
 
Solomon alitisha sana
 
Ni ngumu sawa kumuhudumia mwanamke ambaye humuamini unahisi kama ana kucheat ili kupunguza maumivu bora usimuhudumie kabisa

Demu akiwa loyal tunahudumia tu hamna tatizo
Ubaguzi huo mkuu..ha ha haa
 
Amina,tuache kelele

Oh! SI maanishi msiongee au mnyamaze. Mkosoe Kwa staha. Yaani mkiweza kuigiza kutuheshimu kidogo tu? Mtapunguza matatizo mengi sana.

Kuna wakati unataka kufanya ujinga ila ulikumbuka mwenzako, unajiuliza hivi kwanini nimtendee hivi mwenzangu wakati hastahili na ananiheshimu? Unajikuta taratibu unabadili gia angani.

Haya mambo yanahitaji HEKIMA sana.
Kuna wale wanawake wananyenyekea, wavumilivu, wasikivu na wanapenda mbali sana kujitolea kutekeleza majukumu yao, lakini Bado wanaambulia kero na maumivu yasiyo kifani. Hao tuwaombee sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…