Simpendi Rais Samia ila yawezekana Akitokea mtu akaniambia alichofanya cha maana Tangu aingie Madarakani naweza kubadili mawazo nikampenda

Simpendi Rais Samia ila yawezekana Akitokea mtu akaniambia alichofanya cha maana Tangu aingie Madarakani naweza kubadili mawazo nikampenda

Kwanza ikumbukwe ya kuwa Rais samia mama wa shoka ,chuma cha Reli,jasiri muongoza njia,Simba wa vita,shujaa wa Afrika,Nuru ya wanyonge,mtetezi wa Afrika na waafrika, Sauti ya wanyonge alipokea na kuchukua nchi katika wakati mgumu sana,wakati wa mdororo wa uchumi Duniani kwote uliokuwa umetokana na ugonjwa wa Corona ulioikumba Dunia na kupelekea kufungwa kwa shughuli nyingi za uzalishaji kuanzia viwandani hadi hadi katika Biashara mbalimbali,.Makampuni na Taasisi mbalimbali zilifunga biashara zao na kupunguza wafanyakazi. Hali hii pia ilipelekea na kusababisha biashara za kimataifa kupungua,mfumuko wa bei kwa baadhi ya bidhaa kutokana na uhaba wake katika kupatikana,ukosefu wa ajira,kushuka na kupungua kwa wawekezaji na watalii ambao ni chanzo pia cha mapato na fedha za kigeni, lakini pia ukosefu wa masoko kwa bidhaa tulizokuwa tunategemea kuuza nchi za nje.

Ndani ya muda mfupi pia vita vya ukrein navyo vikaripuka na kuanza ambavyo navyo vilipelekea mfumuko mfumuko wa bei wa bidhaa muhimu na Tegemezi katika uchumi wetu na watanzania.bidhaa hizo ni pamoja na nishati ya mafuta ,unga wa ngano pamoja na pembejeo hasa mbolea ambayo ni tegemeo kwa watanzania hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa asilimia kubwa ya watanzania ni wakulima na wanategemea kilimo katika kuendesha maisha yao.

Mama wa watu mwenye moyo wa upendo,huruma ,upole, unyenyekevu na uzalendo mkubwa kwa Taifa letu alianza kwa ujasiri,ushupavu na umadhubuti wa hali ya juu sana alianza safari ya kuufufua uchumi wetu kwa hatua mbalimbali kama ifuatavyo.

Kwanza alianza kuvutia wawekezaji na watalii kufika hapa nchini, katika hatua hii alifanya pia ubunifu wa kipekee kuwahi kutokea hapa nchini wa kuja na wazo la kuitangaza nchi yetu pamoja na vivutio tulivyo navyo hapa nchini maarufu kama Royal Tour. Kwa uhodari na umaridadi wa hali ya juu sana akafanikiwa kuyafikia makampuni makubwa ya kitalii, wawekezaji pamoja na wafanya biashara wakubwa kutoka katika kila pembe ya Dunia.

Haraka sana watanzania tukaanza kushuhudia mafuriko ya watalii kuwahi kushuhudiwa hapa nchini Tangia kuimbwa kwa Dunia pamoja na wawekezaji mbalimbali. Tukaanza kuona pia biashara mbalimbali zikifunguliwa na wafanyabishara mbalimbali wa ndani na nje ya nchi mpaka kupelekea kupanda kwa mapato kufikia Trilioni mbili kwa mwezi. Rais samia alianza pia kuimarisha Diplomasia nyeti na mahusiano yetu na Taasisi na mataifa mbalimbali makubwa kiuchumi na kiteknolojia kama vile Marekani,china ,Ufaransa n.k. ni katika ziara hizo za kufufua mahusiano ya kimataifa ilipelekea Tanzania kusamehewa Deni la Billion 31 na nchi ya nchi.

Rais samia na serikali yake pia alianza kufufua matumaini kwa watumishi wa umma na vijana ili wafanye kazi kwa bidii, juhudi,maarifa na kujituma katika kutoa huduma bora kwa watanzania.kwa hapa alianza kuwaboreshea maslahi yao,kupandisha mishahara kwa 23%, kuwapandisha madaraja na kuwapa stahiki zao n.k. lakini vilevile kwa upande wa vijana ametoa maelfu ya ajira zikiongozwa na secta ya Afya na Elimu ili kuongeza ufanisi katika utoaji huduma kwa watanzania.

Lakini wakati wa mfumuko wa bei ya mafuta na mbolea katika kukabiliana nao Rais Samia alitoa Ruzuku ya Billion mia moja kila mwezi pamoja na Ruzuku ya Billion mia moja hamsini katika mbolea hali iliyopelekea kushuka kwa bei ya mbolea sokoni,mfano mbolea ya DAP iliyokuwa ikiuzwa shilingi lakini na Arobaini ikaanza kupatikana kwa Elfu 70 Tu. Hali hii ilichochea kuongezeka kwa uzalishaji na kuinua kipato kwa kaya nyingi na hivyo kuondoa umasikini kwa kaya nyingi ,hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa kilimo ndio secta iliyoajili Watanzania wengi hapa nchini.

Ni Rais samia na Serikali yake amejenga vituo vya afya kila kona ya Taifa letu ikiwepo vya miezi michache iliyopita wakati wa Mh Innocent Bashungwa vituo takribani 234 nchini kwote kwa fedha zetu wenyewe. Kujenga shule na vyumba vya madarasa zaidi ya elfu ishirini vilivyoweka historia yakipekee kwa wanafunzi wote kuanza kuripoti kwa wakati mmoja pasipo kuchelewa kwa wanafunzi wanaokuwa wamefaulu masomo yao ya kujiunga kidato cha kwanza tofauti na ilivyokuwa awali ambapo wengine walisalia majumbani kwa uhaba wa vyumba vya madarasa.

Ni Rais Samia na serikali yake yupo katika hatua za mwisho kujenga barabara mbalimbali nchini ikiwepo kilometers 237.9 za barabara za njia nne kutoka igawa Mbeya hadi Tunduma mkoani Songwe. Huku mradi wa mwalimu Nyerere ikiwa mwishoni na kuanza uzalishaji umeme mapema mwakani ,pamoja na ukamilishaji wa mradi wa reli ya kisasa kabisa. Lakini ni wakati wa Rais samia ambapo ameimulika kigoma na kuitoa gizani tangia uhuru.

Ni wakati wa Rais samia ambapo sasa Elimu ni bure hadi kidato cha sita pamoja na kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wenye sifa.lakini kwa sasa fedha ya kujikimu kwa wanafunzi wa Elimu ya juu ni elfu kumi ,hali iliyopelekea wanafunzi kusoma kwa raha na furaha.lakini kwa sasa hata watoto wanaotoka familia za kipato cha chini wanauhakika wa kutimiza ndoto zao na kufikia malengo yao kwa kuwa Rais Samia a Amebeba mzigo wa ada na gharama zingine zote.

Ngoja nipumzike kidogo nakuja kuendelea baadaye kidogo kuelezea kazi za mh Rais samia .
Khaaaaa unaandika babu....
 
Ngoja waje [mention]chawa wa mama [/mention] na bibi mdogo [mention]FaizaFoxy [/mention] wakurarue vizuriiii
 
Magufuli ameacha Mamiradi kibao ikiwa haijakamilika kama Mama angekua na roho mbaya angeipiga chini yote akaanzisha ya kwake,, lakini Mama kakomaa nayo mwanzo mwisho na ndio maana halisi ya "Kazi iendelee" 2025 tutakapo mchagua tena ndio atatuonyesha yalio yake,, sina shaka na Mama Samia

Anaupiga mwingi,,, tatizo team Msoga
 
Kwakweli ameboresha sana sekta ya kilimo,ametuheshimisha na Kwa Sasa kilimo ni biashara na mi ajira.bei nzuri za mazao + ruzuku za pembejeo
 
Ukihitaji salamu njoo unieleweshe kwanza,tofauti na hapo utaula wa chuya!.

Hii nchi kila mtu yuko huru ili mradi asivunje utaratibu na sheria za nchi tulizojiwekea kwa utaratibu pendekezwa toka kwenye Katiba.

Kumpenda au kumchukia mtu ni hiari au matakwa ya mtu.

Mimi binafsi simpendi na si mkubali Rais Samia Suluhu Hassan kwasababu naona kama kwenye huu uongozi wake ndiyo amekuwa Rais wa ajabu kuliko waliomtangulia.

Binafsi pia nilikuwa simkubali Rais Magufuli lakini naona kidogo yeye alikuwa na uafadhali kwa raia wa Tanzania kuliko huyu Samia.

Sasa nahitaji mtu anayeweza kunieleza kwa facts aliyoyafanya Rais Samia tangu amekuwa Rais pengine naweza kumpenda kuanzia leo.


Mnakaribishwa wadau wa siasa
Yaani humuoni amevaa hijab?
 
Kwakweli ameboresha sana sekta ya kilimo,ametuheshimisha na Kwa Sasa kilimo ni biashara na mi ajira.bei nzuri za mazao + ruzuku za pembejeo
SIDHANI KAMA UNA AKILI TIMAMU
 
Magufuli ameacha Mamiradi kibao ikiwa haijakamilika kama Mama angekua na roho mbaya angeipiga chini yote akaanzisha ya kwake,, lakini Mama kakomaa nayo mwanzo mwisho na ndio maana halisi ya "Kazi iendelee" 2025 tutakapo mchagua tena ndio atatuonyesha yalio yake,, sina shaka na Mama Samia

Anaupiga mwingi,,, tatizo team Msoga
HIYO MIRADI ALIYOIKAMILISHA NI IPI?
 
Kwa Sisi wengine KUPENDA ni Amri ya Mungu wa Mbinguni aliyoyupa. Hamna mbadala wake. "MPENDE BWANA Mungu Wako na ya pili inafanana na hii Mpende Jirani yako.
Jirani wa nyooooooooko
 
Back
Top Bottom