Sina chuki na Wakenya ila nimejifunza haya katika kufanya nao kazi

Sina chuki na Wakenya ila nimejifunza haya katika kufanya nao kazi

Nimefanya kazi sehemu mbili na Wakenya pamoja na Waganda usemacho kweli.

Waganda wapo smart sana na hawana majigambo na wanajua sana,ila Wakenya Daah wabinafsi halafu kama husipokuwa makini wanaweza kukuangushia jumba bovu ambalo uhusiki nalo kabisa,wengi wapo shallow ila lugha inawabeba ila technical weupe.

Uongo,wewe hujafanya kazi na waganda labda ulifanya kazi na waganga.Waganda kujisikia ni jadi yao kabisa na majigambo kama yote na hawatakagi shobo na wabongo.Roho mbaya hawana
 
Wanafanana na ndugu zetu fulani hapa Tanzania. Na wao mtu Kama ni mkikuyu akafanya Jambo kubwa yaani wakikuyu watajisifu kuwa wao Wana akili Sana kuliko wakenya wengine i.e wakalenjin,kamba, taita,jaluo, kisii etc.
Yaani mie siku nilipodharau kuwa English sio chochote ni pale fomu wani tumefika,Kuna waliotoka English medium na mie Swahili medium, yaani iyo2 English waliyozaliwa nayo nikawa nawapelekesha mbaya Sana.
Kuna jamaa akasomea Uganda alidisco second year na English alikuwa anajua.
Watanzania tuko poa sema we're undervalued ourselves
Braza nikuambie kitu tofautisha lugha kama grammer ya kuuza na lugha katika academics ni tofouti kabisa.Mfano unaposoma masomo kama Engineering au Chemistry unafikiri swali likiulizwa wanangalia weledi wa kujieleza? ni point tu na formular mimi mwenyewe nilisoma na Mganda UDSM miaka ileee hakika ali disco mwaka wa pili mimi mbongo nikapeta tofautisha hapo.
Wakenya mnawaita wazuri ila kwa masomo ya sayansi watanzania wako vizuri sana.Na ndio maana shule utitiri wa english mediums ulivyoanza Tanzania chunguza tuliona wakenya wana akili sana.Sio kweli ukweli ni kwamba wako vizuri kwa lugha si wongo.
 
mkuu nakubaliana na wewe kwny 1,2 na 3 zingine sina uhakika lkn pia umesahau kuwapa sifa yao nyingine ambayo mimi naiona ni sifa kuu ya msingi inayotutofautisha na sisi TZ, wenzetu wanauthubutu mkubwa klko sisi bado tumelala. Basi na tuwape credit ktk hili la uthubutu.
Mkuu usifananishe Wa tz wote hawako saw a,kuna kabila wanaitwa chaga,huyu ni jamii moja na Kikuyu.
 
1. Wako tayari kukukandamiza hata km huna kosa , hawawezi kukutetea kwa bosi/ mkuu, they are always on management side.

2. Wanapenda kujua habari za wenzao ila zakwao hawataki zijukikane
3. Wanaroho mbaya ya uchoyo
4. Mbali na kingereza, hawako smart sana kama inavyofikiriwa

5. Wanapenda mambo ya kulinganisha hasa mambo ya kimaendeleo.

6. Wakenya wakiume walipata nafasi kidogo ni waxhafu sana kwa dada zetu
7. They like show off, wanapenda kujionesha kua wao wema na wanafanya kazi

Prove me wrong from your work place
....=wahindi + Wanaijeria?!!!

Tanzania nchi BORA NA YA MFANO WA KUIGWA.....

CCM imezidi kutufanya tuwe bora hivi ijapokuwa wengi wetu HATUUTAKI UKWELI HUO....

HASTA LA VICTORIA EL COMANDANTE JULIUS K .NYERERE amen!!

#SiempreCCM
 
Wewe hujui vizuri mataifa ya EAC yalivyo. Kenya ndio nchi pekee inayoweza ikakaa na sisi watanzania bila kutubagua kihivyo labda mmoja mmoja tu. Ila Mataifa mengine yote yaliyobaki EAC hayatupendi wa Tz kweli na hayana shobo na Tanzania. Shida mkenya kama jambo la serius anakua serious tofauti na sisi kila kitu tuna take easy.
 
Watanzania wana asili ya "kujitosheleza"...si vyakula si nyumba za kuishi ...si mifugo ya kufuga na mashamba......


Hizo nchi nyingine hayo HAKUNA.....

Kongole apewe Baba wa taifa hayati JKN👍

-Alivunja uchifu wa kiutawala na kimamlaka
-Aliwachanganya pamoja wanafunzi
wa sehemu tofauti

TANZANIA NI TAIFA LA KIPEKEE KABISA....UNAWEZA KUITA UJINGA NA KUCHELEWA...ILA NDIO SALAMA YETU NA NDANI MWAKE KUNA URAHISI NA MAZURI MENGI MNO ZAIDI YA HUKO TUNAKOONA WATU WAMECHANGAMKA AMA KUENDELEA SANA💪

#SiempreJMT👊
#NchiKwanza😍
 
hata huwa nashangaa unakuta mwanaume mzima anakaa na kusema wakenya hiki wakenya kile,hawa jamaa wanapenda wajinga wajinga ili wawadanganye.
Umenikumbusha Lisu, mpaka leo huwa anaona Kenya ni sawa na Mbinguni,

Hata kwenye kampeni za mwaka jana utasikia baada ya maneno mawili tu kenya vile, kenya hivi. Nina damu nyingi sana ya wakenya,

Yani yule angeshinda urais ikulu nagehamishia nairobi.

Mbali na wazungu watu wanaoabudiwa na chadema ni wakenya.
 
ukweli ni kwamba wakenya wametuacha sana.
Wamekuacha kwenye kipi?
Screenshot_20210827-151228_Telegram.jpg
 

Attachments

  • Screenshot_20210828-165845_Twitter.jpg
    Screenshot_20210828-165845_Twitter.jpg
    56 KB · Views: 6
1. Wako tayari kukukandamiza hata km huna kosa , hawawezi kukutetea kwa bosi/ mkuu, they are always on management side.

2. Wanapenda kujua habari za wenzao ila zakwao hawataki zijukikane
3. Wanaroho mbaya ya uchoyo
4. Mbali na kingereza, hawako smart sana kama inavyofikiriwa

5. Wanapenda mambo ya kulinganisha hasa mambo ya kimaendeleo.

6. Wakenya wakiume walipata nafasi kidogo ni waxhafu sana kwa dada zetu
7. They like show off, wanapenda kujionesha kua wao wema na wanafanya kazi

Prove me wrong from your work place
Mambo haya huhitaji utulivu na uwezo wa kuchanganua mambo kwa mapana. Mimi nina haya:

1. Si mara ya kwanza mimi kusikia waTz tukiwalaumu waKE kwa mienendo yao. Lakini, kwanini tumekuwa watu wa kulaumu tu, hakuna namna ya kujibu mashambulizi? Ukiona tunabaki kulaumu tuu, ujue kuna shida upande wetu pia. Tusipokubali kujitathmini, au kukiri udhaifu wetu tutabaki hivihivi.

2. Mengi uliyoongea ni tabia za jamii nyingi sema tunazidiana kutokana na mazingira tuliyokulia. Sisi Tz, hatukukaa na mkoloni. Wenzetu waliishi nao, hivyo, uchumi wa kibepari na tabia zao wamezibeba sana(uninafsi, hila, ari ya kufanya kazi n.k). Wakenya wanafahamu maana ya kazi, na wanajua kama huna kazi unakufa au unaishia uchizi. Tz hatupo hivyo, mbongo ni mpole siku anaomba kazi tu, baada ya hapo utajuta kumuajiri. Mbongo hata ofisi au biashara yake binafsi anaifanyia upuuzi. Hatupendi kujifunza zaidi, kile ulichotoka nacho darasani tu ndicho hicho utakufa nacho. So, ile hali ya kupigana na kufanya lolote ili maisha yaende sisi hatuna sana, Wakenya wanalo kwa kiasi fulani.

3. Kutokana na maisha ya kikoloni, maisha magumu, yamewafanya Wakenya kuwa na ujanjaujanja ili waweze kukabiliana na mazingira yao. Kwa kulinganisha, kwao wasomi ni wengi, hawana rasilimali za kutosha kama sisi pia, hivyo, ushindani ni mkubwa sana. Ndiyo maana utaona wanatuzidi maeneo kadhaa japo wengi hawaamini hili ,pengine kwa kutokujua ama kwa uzalendo usio na tija. Tazama sekta ya habari tu, wao tuliwatangulia kuwa na TV binafsi. ITV yetu ni bibi kwa TV nyingi za binafsi za Kenya, lakini, tazama vyombo vya Kenya na TZ. Kama mfuatiliaji utaona tofauti kubwa.

Kiufupi , hizo tabia unaweza kuzitazama kwa ubaya ama uzuri. Sisi tunapowasema hivyo Wakenya, tuna uzuri gani? Sisi ndiyo wachamungu sana? Sisi hatuna majungu? Je, mkaka wa kiTz ndiyo atawaacha salama wadada wa Kikenya akipata fursa? Usishangae, hayo niliyosema hapo juu ndiyo yanaingia hadi huku kwenye relationship. Si ajabu kumuapproach mdada wa Kikikuyu ikawa na tofauti fulani na huyu wa kibongo maana tuna tofautishwa sana na exposure. Hii inaweza kulinganishwa hata hapa Tz, katika mahusiano, kuna wadada wa mikoa /kabila fulani hawapo sawa na wa kabila fulani. Kuna ambao ukiwa nao wanajitambua, hujiloweki tu kirahisi, lazima kuwe na returns. Ndugu,huenda sisi ni hatari zaidi sema tu sababu ya kukosa exposure na uelewa, hatuna ujanjaujanja kama wenzetu. Mkenya anaweza asiwe na ujuzi kiviiile kwa kazi anayoifanya, lakini ile aggressiveness inaweza kumpa kazi na akakubalika kuliko mbongo na PhD yake.

Note
Siwasifii Wakenya, bali ninakerwa na tabia ya kuwalalamikia wakati maisha ya kidunia ni kama Yanga na Simba. Hakuna atakaekuombea heri. Hakuna atakaekuonea huruma. So, turekebishe tabia na mienendo yetu na sisi siku moja tulalamikiwe kwa kuwazidi wengine. Kuwatukana, kuwasema vibaya hakusaidiii lolote zaidi ya kujiangamiza zaidi.

Mjadala ni mpana na hauna jibu moja, itategemea sana mtazamo wa mtu juu ya kibaya na kizuri ni kipi kwake. Haya hapa ni maoni yangu,kadiri ninavyofahamu hali ya mambo.

Good day
 
Sasa kazi ktk hizo ofisi tulifanya wote..........? au ndio ule ubishi wako wa Koffi na Yanga unataka kuuhamishia huku.
EA nzima Waganda ndio wanaongoza kwa kutokua na interaction na raia wengine wote wa EA ukikutana nao.Give or take.Nenda EAC office Arusha utajionea.
 
Braza nikuambie kitu tofautisha lugha kama grammer ya kuuza na lugha katika academics ni tofouti kabisa.Mfano unaposoma masomo kama Engineering au Chemistry unafikiri swali likiulizwa wanangalia weledi wa kujieleza? ni point tu na formular mimi mwenyewe nilisoma na Mganda UDSM miaka ileee hakika ali disco mwaka wa pili mimi mbongo nikapeta tofautisha hapo.
Wakenya mnawaita wazuri ila kwa masomo ya sayansi watanzania wako vizuri sana.Na ndio maana shule utitiri wa english mediums ulivyoanza Tanzania chunguza tuliona wakenya wana akili sana.Sio kweli ukweli ni kwamba wako vizuri kwa lugha si wongo.
Yes kwa lugha na si pengine.
Ila pia sie hatujiamini sijui lugha unayaotaka kujua sijui ni ya kupigia story na umbeya.
Kiukweli hao jamaa hawana kitu.
Mfano nimeshawahi pata tempo ya kufundisha physics advanced level,shule ya private so wakenya kibao. Nakuambia Ile fizikia walikuwa hawawezi kuigusa labda olevo. Na hapo wanalalamika kuwa hii kitu tz ime complicate labda Mambo mengine yangepelekwa kwa chuo. Ila olevo sawa.
Muda huo napiga pindi concepts natembea na up yangu na tokea Nina miaka 8 sijawahi ichungulia physics sema nafurahi dents walikubali kwa uongozi kuwa jamaa anaijua fizikia nikafurahi msuli yatima.
 
Huyu ni mtazamo wa mtu mvivu, mwenye chuki, hizi ni tabia za watu wengi uwe mkenya au mtanzania hakuna binadam aliye kamili, wewe unaonekana upo katika nafasi ya chini kulingana na auwezo wako mdogo ndo maana mtu akiwa anaishi maisha yake ya kawaida unaona ni show off, Majority ya watanzania wakishona mtu amefanikiwa lzm watampa jina baya, mara mwizi, fisadi au hata jambaz ili mradi wapate faraka katika umaskini wao ,futailia chuki kubwa inayojemgwa hata kwa makabila yanayooneka yamefanikiwa hapa Tanzania utaona jinsi walivyojaa chuki.,ndugu hutokaa ufanikiwe kwa kuendekeza chuki na wivu kwa wenye mafanikio
 
Back
Top Bottom