Single mothers ni athari na madhara yanayotokana na kampeni ya usawa

Single mothers ni athari na madhara yanayotokana na kampeni ya usawa

Siku vijana wa siku hizi hawapendi kubeba misalaba yao,sipo humu kumtetea mtu kisa ni jinsia moja ni upuuzi. Nina Single mother wawili ambao ni ndugu zangu na wasaidia kwa baadhi ya vitu na najua visa vyao.

Kiasili na kiumbaji mwanaume ni Mlezi na Mlinzi ,ukishindwa kufanya hivyo ww kiasilia sio mwanaume kamili na mwanaume HASUSI (hizi tabia za kike) majukumu yake,umefanya ngono haijalishi mlikutana vipi na alikufanya nini, ila kile kiumbe ni msalaba wako hauwezi kukimbia.

Mimi sitetei upumbavu kama wewe na husijipe nafasi ya malaika eti wanaume hawakosei, ila single mother wanakosea hilo na kukatalia, kwani sisi ni binaadam na kukosea ni asili yetu.

Eti ni mtetea mtu kisa mwanaume mwenzangu, mimi upumbavu huo sifanyi (mimi sio oya oya) na sina akili ya kushikiwa kwani nina uwezo wa kuchanganua na kujua yupi yuko sawa na yupi hayuko sawa.

Wanaume hatuwezi kukikimbia hiki kikombe cha mamtatizo ya Single mother,kwani ktk asilimia 100 ya tatizo basi yetu wanaume inaweza kuwa 40+.

MWANAUME KAMILI HASUSI MAJUKUMU YAKE KWANI KUSUSA NI TABIA ZA KIKE KWANI HAWA WAMEUMBWA KUSUSA NA KUDEKA.Umetia mimba mwanamke kakukera mnaachana unabeba msalaba (mtoto) wako kama MWANAUME wa kulea na kumtunza wanao.

Eti ni mtetea mtu kisa jinsia moja,mimi Us*nge huo sifanyi labda ww na kama ukikosea na kuchana kama MWANAUME.
Mkuu nimesoma mara mbili mbili hii comment yako nikabaki najiuliza ni wewe kweli, natamani wanaume wote mngekuwa realistic and sincere kiasi hiki labda tungejua wapi pa kuanzia ili kusolve haya matatizo yote kwenye jamii, sisi wengine tukiongea mnatuita feminists lakini tunachofanya ni kujaribu kuonesha kwamba hii mentality ya wanaume kujiona kuwa wakifanya maovu ni sawa ndio inafanya jamii izidi kuharibika
 
Na unakuta kilichomtoa kwenye muungano wa ndoa ni hiyo hiyo biashara ya mihogo baada ya kupata faida mfululizo ya 15K per day akajiona naye anaweza akamletea mumewe kiburi kwamba asimwambie kitu kama biashara na yeye anayo asimbabaishe amuache.

Kuna mmoja alinipigia story yake anauza matunda kwenye basin namna ndoa yake ilivyoenda mrama hata unajiuliza kama anajitambua
Alikaza ubongo akajikuta yupo single again 😂
 
Hapo nyuma kampeni na uhamasishaji ulikuwa mkubwa sana, na wengine walisikika wakisema, "Wanawake Tunaweza." Sasa, athari zake zimeanza kuonekana: wanawake wenye watoto wasiokuwa na baba wamekuwa wengi kadri muda unavyosonga mbele.

Sijui itakuwaje baada ya miaka 20 ijayo. Mbaya zaidi, hawa mama wasio na waume wanajiona wana haki ya kusaidiwa, na ukimsaidia, usitegemee shukrani; msaidie tu. Miaka ijayo, tutakuwa na kiwango kikubwa cha hawa mama wasio na waume wenye tatizo la afya ya akili.

View attachment 2964040
Asikudanganye nyuma kuna mtu na watu wenyewe ni waume za watu, wasijefanye wapo peke yao
 
Humu kuna watu wana Mentality kama hawa Wadau..... And in so far as that Fact - Nachelea Kusema Safari bado ni Ndefu....
1713196643795.png
 
Kwanini mwanamke anakuwa Single ?

Kwahio akifiwa akamfufue mme wake ?; Akiachwa kama hatakwi tena au kama anapigwa au akikimbiwa afanye nini atengeneze Robot linalofanana na aliyemwacha ?

Umeona verse nilizokuakea ? Ni kwamba mwanaume anamdanganya mtu kwamba wanajenga mahusiano alafu mwisho wa siku anamtelekeza inakuwaje....; Yule First Love wake waliyokutana Chuoni mapenzi yakichacha afanye nini aende akawe third wheel kwenye relation mpya ya mtu wake ?

Bibi zetu walikuwa hawana Choice mtu anapigwa mwingine mpaka anauliwa alikuwa hana pa kukimbilia sasa hivi wana choice ukiwafanyia ndivyo sivyo wanasepa (hii sio maadili wala nini things have changed) na kilichobadilika ni options kwa mwanamke zamani angekufa kwenye ndoa sasa hivi ana uwezo wa kutoka / kuondoka (Na je hilo wewe unaona ni baya) kwa wao kupata option ya kuweza kuondoka kwenye ndoa ambayo ni hatari kwao na watoto ? (Au unataka kuniambia ndoa zote ni Rosy hazina matatizo wala Abuse )?
🤝
 
Back
Top Bottom