Siwezi kusahau haya manyanyaso ya mama wa kambo

Siwezi kusahau haya manyanyaso ya mama wa kambo

Sote tulifundishwa mada ya uandishi wa barua za kikazi. Hebu leo kamata graduate ye yote mwambie aandike barua siriazi ya kuomba kazi uone majanga yake. CV ndiyo kabisaaa!

➡️➡️➡️ Anyway. Binti Sayuni03 ana maumivu bado; na childhood trauma ni mbaya maana inaweza kuathiri mahusiano yake yote maishani yakiwemo yake na watoto pamoja na wenza wake. Kutokujithamini, kuhisi anaonewa katika kila jambo (inferiority complex), hasira na chuki zisizo na sababu, kutokuridhika na upendo hata apendwe vipi, kupenda kuhusiana na watu wa hovyo (bad boys), moyo kuwa sugu na kutojali, kutaka kupendwa na kila mtu, kuumizwa sana na maneno ya watu, hamu isiyoisha ya kutaka sana kufurahisha watu na matatizo mengine mengi.

Maumivu haya inabidi yachimbuliwe katika mizizi yake ili yaweze kung'olewa. Na hapo ndipo safari ya uponaji wa kweli itaweza kuanza. Hata kuja kuyasema tu hapa naamini huko aliko anajisikia unafuu kidogo. Inabidi sasa atafute mshauri nasaha/mwanasaikolojia mzuri ili wakae na kuchimbua mizizi ya hii trauma. Naamini atakuwa sawa; hasa ikifika mahali akawasamehe na kuwaachilia kabisa hao wazazi wake kwa tanuru la mateso walilompitisha. Mungu na Amsaidie 🙏🏿
😭😭😭hii ndiyo hali nayopitia kwa sasa, nahitaji mshauri kweli
 
Sad,sahau....usiwe Kama Mimi niliweka kinyongo na kikaja kunitesa mwenyewe...Kupitia njia ngumu ni sehemu ya maisha
Hakika namshukuru Mungu nimepitia huko nimejifunza kupambana na kusimama mwenyewe maana hakuna ndugu yeyote aliyekuwa nami kipindi hicho japo walikuwa wanajua yote hayo
 
Kama ulikuwa unafanya maujinga kakitia viboko kwa ajili ya kukutia adabu alikuwa anafanya viziri sema kuanza kukutukana matusi ya nguoni lilikuwa ni tatizo, mlezi au mzazi hutakiwi kumtamkia mtoto wake tusi hata kwa bahati mbaya.
Ni hapo sasa mkuu, alikuwa anakosea na kwenda mbali zaidi hadi kuniambia nina laana hii huwa inanitesa kwani kuna muda nafanya vitu, kama haviendi hadi nawazaga au ni kweli nilivyoambiwa nina laanq😭😭
 
Unavyoongea hivyo ni kama tumekuwa wote, aya endelea kunielezea
Si ninavyo kuelezea bali jinsi ulivyo jielezea ww, au sio ww uliye leta mada ya kujutia maisha yako ya nyuma?
Na kwenye maelezo yako sio ww ulie sema kuwa mama yako wa kambo alikuwa vizuri mpaka pale ulipo anza tabia za ajabu?
Hata ww una upande wa pili iwapo mtu atavuka mipaka yako ya uvumilivu.

Kama ww unavyo jutia makosa yako ya nyuma na hutaki kuhukumiwa kwa uliyo yafanya huko nyuma, hivyo hivyo huna haki ya kumuhukumu mama yako wa kambo kwa mama yako wa kambo kwa mambo ya nyuma msamehe maisha yaende mbele.
 
Si ninavyo kuelezea bali jinsi ulivyo jielezea ww, au sio ww uliye leta mada ya kujutia maisha yako ya nyuma?
Na kwenye maelezo yako sio ww ulie sema kuwa mama yako wa kambo alikuwa vizuri mpaka pale ulipo anza tabia za ajabu?
Hata ww una upande wa pili iwapo mtu atavuka mipaka yako ya uvumilivu.

Kama ww unavyo jutia makosa yako ya nyuma na hutaki kuhukumiwa kwa uliyo yafanya huko nyuma, hivyo hivyo huna haki ya kumuhukumu mama yako wa kambo kwa mama yako wa kambo kwa mambo ya nyuma msamehe maisha yaende mbele.
Hayo maisha mabaya nilipitia kwasababu yake, nilishamsamehe
 
Kiukweli nilikuwa nikimchukia baba yangu, lakini sioni faida ya kufanya, nimeamua tu niache hayo maana kuna leo na kesho, nyie “”single faza jaribuni kuoa au kuishi na wanawake watakaowapenda watoto wenu, siyo unaishi na mwanamke unajua kabisa hampendi mwanao ila kwasababu wewe anakupenda unaganda nae hii siyo sawa””

Single Daddy ni muhimu sana kuzingatia 👆.


Anyways, kama ningekuwa mwanaume basi ningetumia njia nyingi sana kumfahamu vizuri mwanamke anaenda kuishi na watoto ambao hajawazaa yeye.wababa/wamama jaribuni kuwasikiliza watoto wenu wanaoishi na mama/baba wa kambo wanakuwaga na mengi yakuzungumza.
 
Kiukweli nilikuwa nikimchukia baba yangu, lakini sioni faida ya kufanya, nimeamua tu niache hayo maana kuna leo na kesho, nyie “”single faza jaribuni kuoa au kuishi na wanawake watakaowapenda watoto wenu, siyo unaishi na mwanamke unajua kabisa hampendi mwanao ila kwasababu wewe anakupenda unaganda nae hii siyo sawa””

Single Daddy ni muhimu sana kuzingatia 👆.


Anyways, kama ningekuwa mwanaume basi ningetumia njia nyingi sana kumfahamu vizuri mwanamke anaenda kuishi na watoto ambao hajawazaa yeye.wababa/wamama jaribuni kuwasikiliza watoto wenu wanaoishi na mama/baba wa kambo wanakuwaga na mengi yakuzungumza.
Mimi huyu baba angu alikuwa kashikwa akili na mkewe kabisa, yaani unamwambia anasikitika tu na hafanyi kitu, anaona kabisa matusi kama hayo tunatukanwa lakini hafnyi kitu
 
Ni hapo sasa mkuu, alikuwa anakosea na kwenda mbali zaidi hadi kuniambia nina laana hii huwa inanitesa kwani kuna muda nafanya vitu, kama haviendi hadi nawazaga au ni kweli nilivyoambiwa nina laanq😭😭
Yaa maneno ya mzazi huwa yana umba hutakiwi kumtamkia laana mtoto hata kama atakuwa amekosea, mtoto akikosea inatakiwa kumtia bakora kumrudisha kwenye mstaari na sio kumtamkia maneno ya ajabu.
 
Mengi ya aliyofanya hata mama yako mzazi angefanya. Bond ya binti na baba yake huwa inakuwa kubwa kiasi cha kuanza kutiliwa shaka na mama. Wanawake wengi wanakuwa na wivu na huu uhusiano wa binti na baba yake.

Kama umeolewa na una mtoto wa kike hili utalishuhudia wazi. Akivunja ungo na kuota vimatiti uhusiano wa karibu haufi. Na binti anaongeza kiburi zaidi. Utaomba chochote utapewa na kupewa muda zaidi kuliko yeye. Hapo ndio utaanza kuona wivu wa mama kuelekea binti yake na kuanza kukuhisi unaliwa. Sio mama wa kambo tu hata mama mzazi
Binafsi nimekuwa na kulelewa na baba kwani mama yangu alifariki nikiwa nipo mdogo, nilipofika darasa la 6 baba alipata mwanamke wa kuishi nae, huyu nilitambulishwa kuwa atakuwa akiishi nasi.

Huyu mwanamke wa baba alikuwa mkarimu, mchapakazi, msafi, mchangamfu na ana stori nyingi sana, kabila lake alikuwa mngoni. Baada ya kuanza kuishi naye mwanzoni mambo yalikuwa mazuri tu, lakini baadae baada ya kufika secondary na kipindi hiki ndiyo kilikuwa kipindi cha ukuaji, kwahiyo vitabia vya ujeuri jeuri nilikuwa navyo hapo ndiyo tukaanza kukosana sasa.

Nakumbuka nilikuwa nikikosea mama huyu alikuwa ananipiga sana kama anataka kuua mtu, kama hakuna mtu wa kukugombelezea hapo naona anaweza hata kukuvunja kiungo, maana alikuwa akikasirika mishipa inamtoka na anakuwa na nguvu za ajabu, ikafika kipindi akaanza kuninenea maneno mabaya sana huyu mama, nikikumbuka hayo maneno sitamani hata kuonana nae.

Wakati haya yote yanatendeka baba angu alikuwa anaona lakini ni vile mapenzi yana nguvu kwahiyo aliacha mimi niteseke ili wasikosane na mkewe, ilifika kipindi tulikuwa hatuongei kabisa zaidi ya mwaka kipindi hiki nilikuwa nimeshamaliza kidato cha 4, kwahiyo nilikuwa naenda kwa ndugu nakaa alafu narudi nyumbani, sasa kuna siku tulipishana kauli na huyu mama akaanza kusema maneno mabaya mpaka kunitukana na kusema natembea na baba angu😭😭 hili alikuwa analiongea kama kitu cha kawaida sana, hakika aliniumiza sana, akaniambia nimeathirika mimi, akaniambia anaweza hata kuninyonga nisimchukulie poa😭😭 sasa sijui ni lini alinipima, kiukweli sikuweza kumvumilia tulijibishana hapo, na mzee alikuwepo akawa anaamualia maana huyu mama alitaka kunipiga.

Sasa mzee akaniambia niende kumuita mjumbe, nikaenda nikarudi mjumbe alikuwa bize nikaenda kumuita jirani yetu mama mmoja hivi ambaye pia ni shosti yake na mama, basi kufika pale akawa anasuluhisha lakini huyu mama alikuwa anasema hawezi kunisamehe, hasemi kikubwa nilichomkosea ila ndiyo hivyo tu anasema.

Mwisho wa siku, akaniambia amenisamehe basi tukashikana mikono ila mimi nikamuona usoni kama ameridhia kinafki tu, sikutaka mambo mengi nikawa sawa tu na mimi nikafurahia pale.

Sasa mimi nilikaa nyumbani kama siku mbili tatu nikaondoka nikaenda kwa ndugu zangu, nilivyokuwa huko mzee akanipigia simu akaniambia wamegombana na mkewe ameongea maneno ya hovyo, yeye mwenyewe anasema kamchoka mkewe, akaniambia walivyogombana akawa anasema hajanisamehe pale aliona aibu tu sababu ya yule mama jirani, aisee mimi nikamwambia watajua wenyewe, wamalizane wenyewe maana kugombana wamezoea wanashikianaga hadi mapanga na kesho unawakuta wako wanacheka kama hakuna kilichotokea.

Ikapita muda nikarudigi home, maisha mengine yakaendelea kama kawa japo hivyo hivyo kiunafki nafki tu, lakini hadi hii leo tunaongea tu, nilimsamehe kweli lakini moja kwa moja lakini sina amani na furaha ya kupafurahia nyumbani ndiyo maana huwa siendi mara kwa mara hadi nipigiwe simu waniulize mbona kimya siendi kuwasalimia ndiyo ntaenda.

Hivi, sisi wanawake tuna shida gani kwanini hatuwezi kuishi kwa upendo na watoto wa wanawake wenzetu, sasa nilichogundua japo sijafanya uchunguzi wa kina sana ila nimegundua huyu mama ana shida kidogo kwenye afya ya akili au kuna ugonjwa unamsumbua ndiyo unampelekea kupenda ukorofi na fujo hivyo maana alikuwa akitaka kunipiga anakuwa anataka kama kuning"ata sasa sijui kwanini, kingine ni chuki na roho mbaya pia.

Haya matukio na maisha niliyopitia hapo yameniachia alama na makovu makubwa nashindwa kupona kabisa kuna muda huwa nakaa namuuliza Mungu hivi kwanini umeruhusu nipitie maisha ya namna hii, kwanini umeruhusu mama angu aondoke mapema naimani angekuwepo mama angu nisingepitiaga yote haya na pengine ningekuwa na furahia background yangu.

Kiukweli nilikuwa nikimchukia baba yangu, lakini sioni faida ya kufanya, nimeamua tu niache hayo maana kuna leo na kesho, nyie single faza jaribuni kuoa au kuishi na wanawake watakaowapenda watoto wenu, siyo unaishi na mwanamke unajua kabisa hampendi mwanao ila kwasababu wewe anakupenda unaganda nae hii siyo sawa.

Mimi sina la zaidi ndugu zangu, asanteni kwa kusoma japo mimi siyo mwandishi mzuri, nadhani sijaandika kama inavyopaswa lakini atleast imeeleweka.
 
Yaa maneno ya mzazi huwa yana umba hutakiwi kumtamkia laana mtoto hata kama atakuwa amekosea, mtoto akikosea inatakiwa kumtia bakora kumrudisha kwenye mstaari na sio kumtamkia maneno ya ajabu.
Hakika mkuu maneno siyo mabaya hayafai kumtamkia mtoto
 
Huyu mwanamke wa baba alikuwa mkarimu, mchapakazi, msafi, mchangamfu na ana stori nyingi sana, kabila lake alikuwa mngoni. Baada ya kuanza kuishi naye mwanzoni mambo yalikuwa mazuri tu, lakini baadae baada ya kufika secondary na kipindi hiki ndiyo kilikuwa kipindi cha ukuaji, kwahiyo vitabia vya ujeuri jeuri nilikuwa navyo hapo ndiyo tukaanza kukosana sasa.
Mtoa mada anajifunga mwenyewe halafu anataka ahurumiwe.
 
Back
Top Bottom